Suarez, Forlan waonesha viwango.
Tuesday, July 26, 2011
MANCINI ANA MATUMAINI YA KUMNASA SERGIO AGUERO
Meneja wa Man City Roberto Mancini amefunguka na kusema kuwa ana matumaini makubwa ya kumnasa Sergio Aguero kutoka Atletico Madrid mwishoni mwa wiki hii. Man C inafungua milango ya maongezi na Atletico Madrid kwa kuwa Srgio amekuwa ni mmoja kati ya wachezaji anaowahitaji katika kikosi chake.
"Nafikiri kati ya siku nne au tano kabla ya mechi inayofuata,na inaweza kuwa wiki hii tukamaliza mazungumzo"Alioneza Mancini.
"Aguero amecheza Copa America, kama tukikubalina nataka nizungumze nae mwenyewe kwasababu nataka nijue maoni yake(kuhusu kucheza Manchester City)" Alifunguka zaidi kocha huyo wa Manchester City.
Sergio Aguero
Pamoja na upinzani uliopo kutoka kwa Real Madrid na Juventus ambao nao wanatajwa kumuwania Sergio lakini Mancini ana matumaini ya kushinda kinyang'anyiro hicho mwishoni mwa mwezi huu."Sielewi kwa sasa lakini ninachojua Atletico walikuwa na maongezi na Sergio kabla ya mwisho wa wiki" alisema Mancini."Nafikiri kati ya siku nne au tano kabla ya mechi inayofuata,na inaweza kuwa wiki hii tukamaliza mazungumzo"Alioneza Mancini.
"Aguero amecheza Copa America, kama tukikubalina nataka nizungumze nae mwenyewe kwasababu nataka nijue maoni yake(kuhusu kucheza Manchester City)" Alifunguka zaidi kocha huyo wa Manchester City.
ASTON VILLA YAKUBALI KUTOA DAU KUMNYAKA N'ZOGBIA TOKA WIGAN
Charles N'zogbia
Aston Villa imefungua milango ya maongezi na Wigan Athletic juu ya kumsajili Charles N'zogbia mwenye umri wa miaka 25 na imekubali kulipa ada ya uhamisho ya paundi za uingereza 9.5 milioni. Meneja wa Villa Alex Mc Leish ameridhishwa na kiwango cha N'zogbia na timu yake imeamua kufanya mazungumzo rasmi na Wigan ili kumsajili mchezaji huyo. Habari kutoka ndani ya klabu ya Villa zinasema pesa ipo ya usajili baada ya kumuuza Ashley Young kwenda Man United na Stewart Downing kwenda Liverpool zote za uingereza, kabla ya kusaini mkataba mrefu ndani ya Villa N'zogbia anatarajiwa kwanza kufanyiwa vipimo vya afya.
FERGUSON ASEMA AMERIDHIKA NA WACHEZAJI KWA SASA
Kocha wa Manchester United Sir Alex Ferguson anasema hatomsajili mchezaji yoyote hadi pale watakapokabiliana na majirani zao Manchester City katika uwanja wa Wembley.
Sir Alex Ferguson
Tayari ameshamsajili Ashley Young, Phil Jones na mlinda mlango David de Gea.Monday, July 25, 2011
AMY WINEHOUSE AFARIKI DUNIA
Mwimbaji maarufu mwanamke wa Uingereza, Amy Winehouse, amekutwa amekufa katika fleti yake mjini London.
Amy amefariki akiwa na umri wa mika 27 tu.
Amy Winehouse alishinda tuzo kadha kwa albamu yake ya pili, Back to Black, ambayo ilitolewa mwaka 2006.
Sababu ya kifo chake haijajulikana.
Lakini mwimbaji huyo amekuwa akipambana na uraibu wa ulevi na mihadarati kwa muda.
Mara nyingi alitokeza kwenye tamasha akiwa amelewa.
Amy amefariki akiwa na umri wa mika 27 tu.
Amy Winehouse alishinda tuzo kadha kwa albamu yake ya pili, Back to Black, ambayo ilitolewa mwaka 2006.
Sababu ya kifo chake haijajulikana.
Lakini mwimbaji huyo amekuwa akipambana na uraibu wa ulevi na mihadarati kwa muda.
Mara nyingi alitokeza kwenye tamasha akiwa amelewa.
BALLOTELI ATOLEWA UWANJANI BAADA YA KUFANYA MZAHA KWA TIMU PINZANI
Mchezaji wa Manchester City Mario Balotelli alitolewa nje katika kipindi cha kwanza katika mechi yao dhidi ya LA Galaxy kwa kutoonyesha heshima kwa wapinzani wake.
Kocha wa Manchester City Roberto Mancini alimpumzisha Balotelli kutokana na tukio hilo lakini wakati akitoka nje ya uwanja alionekana kujibizana na kocha wake.
Awali Balotelli alifunga bao kupitia mkwaju wa penalti katika mechi hio ya kirafiki iliomalizika kwa sare ya 1-1.
Man City Imepata ushindi wake wa tatu katika mechi zake za kujiandaa kwa msimu wa ligi kuu ya England.Katika uwanja huo mashabiki wa LA Galaxy walimzomea Balotteli kwa kitendo chake hicho.
Hii si mara ya kwanza kwa mchezaji huyo wa zamani wa Inter kujikuta katika matatizo na Kocha Mancini, ambaye pia alikuwa kocha wake nchini Italia.
Mancini na Balotelli
Mshambuliaji huyo wa Italia mwenye umri wa miaka 20 alikuwa karibu kufunga goli,lakini hakufunga na badala yake akapiga mpira kwa kisigino na kukosa goli.Kocha wa Manchester City Roberto Mancini alimpumzisha Balotelli kutokana na tukio hilo lakini wakati akitoka nje ya uwanja alionekana kujibizana na kocha wake.
Awali Balotelli alifunga bao kupitia mkwaju wa penalti katika mechi hio ya kirafiki iliomalizika kwa sare ya 1-1.
Man City Imepata ushindi wake wa tatu katika mechi zake za kujiandaa kwa msimu wa ligi kuu ya England.Katika uwanja huo mashabiki wa LA Galaxy walimzomea Balotteli kwa kitendo chake hicho.
Hii si mara ya kwanza kwa mchezaji huyo wa zamani wa Inter kujikuta katika matatizo na Kocha Mancini, ambaye pia alikuwa kocha wake nchini Italia.
Subscribe to:
Posts (Atom)




