Wednesday, October 19, 2011

Kisa cha Muisraeli aliebadilishwa na wapalestina 1000



Tangu kutekwa kwake mapema Juni 25, 2006, Gilad Shalit aligeuka kuwa ndio turufu kubwa ya kundi la Hamas katika makabiliano yake na Israel.

Kijana huyo aliyekuwa na umri wa miaka 19 alivushwa hadi Gaza baada ya shambulio la Hamas. Israel iliapa kumkomboa bila ridhaa na kuanzisha mashambulio ya kijeshi dhidi ya Gaza.

Lakini hawakufanikiwa kumkomboa. Hamas siku zote ilikua na sharti moja tu - kwamba wafungwa takriban 1500 wa Kipalestinina waachiliwe kutoka jela - wengi wakiwemo waliohusika na mashambulizi mabaya ya mauaji dhidi ya raia wa kawaida.

Na akizungumza mwaka 2007 baba yake Gilad Noam Shalit alikiri kwamba hilo lingekuwa vigumu kwa Israeli kulikubali.

Juhudi za upatanishi ziliongozwa na maafisa wa Ujerumani na Misri.

Masharti ya kimsingi yakabainika wazi na hayatofautiani na mpango huu unaotekelezwa sasa wa kubadilishana wafungwa. Lakini juhudi hizi hazikufua dafu.

Na sababu moja ilikua waziri mkuu wa Israel wakati huo Ehud Olmert alikuwa dhaifu kisiasa hadi kwamba hakuwa na ubavu wa kulazimisha makubaliano.

Lakini kampeni ya kushinikiza Gilad aachiliwe huru ikiongozwa na wazazi wake ilizidi kupata msukumo.

Mapema mwaka 2009 Israeli ilianzisha mashambulio makubwa katika Gaza kwa lengo la kumkomboa Gilad Shalit lakini haikufanikiwa.

Baadae makubaliano yalifikiwa kwa kuachiliwa wafungwa 20 wanawake wa Kipalestina kwa kubadilishana na video ya Gilad ambayo ilithibitisha kuwa yuko hai.

Gilad alionekana amekonda sana ingawa alikuwa na hali nzuri ya afya.

Picha hizo zilisaidia kumfanya awe nembo kubwa zaidi nchini Israel ambayo siku zote imefanya juhudi kubwa za kuhakikisha kwamba inawarudisha wanajeshi wake waliotekwa, hata kama wamerejea maiti.

Lakini msemaji wa waziri mkuu mpya , Benjamin Netanyahu, bado hakutaka kufikiria wazo lolote la kutoa ridhaa kwa kundi la Hamas.

Familia ya Gilad iliimarisha kampeni yake ya kufikiwa makubaliano ya kubadilishana wafungwa wakiungwa mkono na vyombo vya habari vya Israeli na kuendeleza shinikizo kwa kuandamana kutoka nyumbani kwao hadi makao ya Bw Netanyahu.

Hamas nayo haikuonyesha ishara yoyote ya kubadili msimamo wake.

Hatimae ni wazi kabisa kwamba kitu kilichoshawishi serikali ya Israeli na Hamas kwamba makubaliano yangezinufaisha pande zote mbili ni mageuzi makubwa ya kisiasa yaliyotokea Mashariki ya kati mwaka huu.

Pande zote mbili zilikabiliwa na changamoto mpya na zilihitaji angalau kwa sasa kuimarisha umaarufu wao ambao wangeupata kwa kubadilishana wafungwa.

MUISRAELI 1 ANA THAMANI YA WAPALESTINA 1000

Makundi ya watu wenye furaha nchini Israel na Palestina wamekuwa wakisheherekea mpango wa kihistoria wa kubadilishana wafungwa.

Israel iliwaachiliwa huru mamia ya wafungwa wa Kipalestina, ikiruhusu wengi wao kurudi katika eneo la Gaza na Ukingo wa Magharibi wa mto Jordan, na badala yake kukabidhiwa askari wa Kiisrael Gilad Shalit.

Sajini Shalit aliyekuwa amezuiliwa katika eneo la Gaza kwa zaidi ya miaka mitano, alipokelewa kishujaa alipowasili nyumbani kwake.

Shalit mwenye umri wa miaka 25, hatimaye alilala nyumbani kwao na familia yake kwa mara ya kwanza tangu kuachiliwa huru.

Babake Shalit amesema mwanawe ana matatizo ya kutangamana na watu kutokana na kuzuiliwa kifungo cha upweke cha miaka mingi, kwa hivyo hangeweza kuhutubia waliojitokeza kumkaribisha.

Alisema anaeleewa machungu yanayozikumba familia ambazo zimepoteza wapendwa wao waliouawa na Wapalestina walioachiliwa huru wakati wa kubadilishana wafungwa.
Ghilad Shalit awasili Israel
Waziri wa ulinzi,waziri mkuu Netanyahu na baba yake Ghilad Shalit wakimkaribisha Shilat

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu wa viongozi wa kundi la kiislamu la Hamas walioafikiana kuhusu kubadilishanaji kwa wafungwa hao, walisifu hatua hiyo kama thibitisho la sera zao.

Lakini waandishi wa habari wamesema kubadilishana kwa wafungwa huenda kusiwe na athari kubwa katika mazungumzo ya amani ya Mashariki ya Kati.

Wakati hayo yakijiri, zaidi ya watu laki moja walijumuika katika ukumbi maalum mjini Gaza kusherehekea kuachiliwa huru kwa nusu ya zaidi ya Wapalestina 1000.

Mji wa gaza uko chini ya kundi la Hamas na kiongozi wa kundi hilo Khaled Meshal alisema limepata ushindi mkubwa kufuatia hatua hiyo.

Tuesday, October 18, 2011

Kim Kardashian kusherehekea siku yake ya kuzaliwa 21 october 2011

CAT HOUSE   photo | Kim Kardashian
Kim Kardashian katika vazi la chui

Mwanamitindo Kim Kardashian atasherehekea siku yake ya kuzaliwa siku ya tarehe 21 october 2011, kama atafanikiwa kusherehekea siku hiyo mwanamitindo huyo atakuwa anatimiza miaka 31. Tayari ameshaanza kupokea salamu za pongezi kutoka sehemu mbalimbali maalum kwa siku yake hiyo ya kuzaliwa. Happy Birthday Kim Kardashian. 

Wednesday, October 12, 2011

JE,unaweza kusoma neno hili kwa mara ya kwanza?

http://groups.yahoo.com/group/babes_in_blue

Ili usome vizuri neno hili fumba macho yako kwa 80% uangalie kwa mbaaali....nimetishaaaa

KASA HATARINI KUTOWEKA DUNIANI MAYAI YAKE DILI

Aibu kubwa duniani inafanyika huko pwani ya Costa Rica ambapo maisha na kizazi cha viumbe wa baharini aina ya kasa hatarini kupotea kutokana na watu wa maeneo hayo kufanya biashara ya kuuza mayai ya kasa kwa kasi kubwa.
Picha zifuatazo zinaonesha watu katika shughuli ya kukusanya mayai ya kasa katika pwani ya Costa Rica na kwenda kuyauza.
http://groups.yahoo.com/group/babes_in_blue/
Kasa katika pwani ya Costa Rica

http://groups.yahoo.com/group/babes_in_blue/
Mwanamama akikusanya mayai ya Kasa mbele yake bila huruma kwenda kuyauza

http://groups.yahoo.com/group/babes_in_blue/
Safari kuelekea sokoni kuuza mayai ya kasa

http://groups.yahoo.com/group/babes_in_blue/
Kazi ya kukusanya mayai ikiendelea

http://groups.yahoo.com/group/babes_in_blue/

http://groups.yahoo.com/group/babes_in_blue/

http://groups.yahoo.com/group/babes_in_blue/
Hakuna mtu kubaki nyumbani kazi ni moja tu

http://groups.yahoo.com/group/babes_in_blue/
http://groups.yahoo.com/group/babes_in_blue/
Oyaa picha hiyo nomaaa

http://groups.yahoo.com/group/babes_in_blue/

PICHA YA LEO

    Mpishi katika Hotel moja ya nyota tano nchini Italia akifanya mambo.

PICHA AMBAZO HUJAWAHI KUZIONA POPOTE





Bruce Lee na Chuck Norris

Cheguevara na Fidel Castro

Copacabanna Beach,Rio De Jeneiro.BRAZIL

Meli ya Titanic ikiwa chini ya Bahari

Familia ya OSAMA,Osama amezungushiwa kiduara chekundu