| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| | | |
| |
Wednesday, February 8, 2012
NUSU FAINALI KOMBELA MATAIFA YA AFRIKA NYASI KUCHIMBIKA LEO
GHANA "BLACK STARS"
Wachezaji wa Ghana wakishangilia katika moja ya mechi zao
IVORY Coast na Ghana zinapewa nafasi kubwa ya kukutana katika hatua ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika wakati zitakapopambana na Mali na Zambia leo katika mechi za hatua za nusu fainali za mashindano hayo zinazosubiriwa kwa hamu.
Ivory Coast mpaka sasa imeshinda mechi zote nne ilizocheza katika fainali hizo za Afrika bila ya kuruhusu hata bao moja, ambapo hivi sasa inataka kufika fainali na kutwaa ubingwa ambao haijaupata kwa miaka 20, huku Ghana ikitafuta ubingwa huo kwa mara ya tano baada ya miaka miwili iliyopita kushindwa kutwaa ubingwa huo baada ya kufungwa na Misri katika mechi ya fainali.

Kikosi cha Zambia
Lakini Ghana kama inataka kuingia fainali na kutwaa ubingwa huo inabidi iifunge kwanza Zambia katika mechi ya leo ya nusu fainali katika mechi inayotarajiwa kuwa kali kwa sababu Zambia pia imeonyesha soka la kuvutia ikitaka kucheza fainali mjini Libreville kwa ajili ya kumbukumbu ya wachezaji wenzao 25 na viongozi baada ya miaka 19.
Kwa upande wa Ivory Coast wapinzani wake ni Mali, ambao pia nao wanataka kucheza fainali baada ya kufanya kazi kubwa ya kuwatoa wenyeji Gabon katika hatua ya robo fainali.
Ingawa mpaka sasa Ivory Coast imefunga mabao nane bila kufungwa, lakini imeshindwa kuonyesha soka la kiwango cha juu kama ilivyotarajiwa kwa sababu ni timu inayoundwa na wachezaji bora wanaofanya vizuri katika ligi kubwa za Ulaya.
Ivory Coast ikiongozwa na nahodha wake Didier Drogba, Yaya Toure na Gervinho inapewa nafasi kubwa ya kufanya vizuri katika mechi ya leo, ingawa inatarajiwa itapata pia upinzani mkubwa kutoka kwa Mali.
"Jambo la msingi ni kutinga fainali kwa sababu tumeshindwa kufanya hivyo mara tatu katika fainali hizi za Afrika," alisema Yaya Toure akimaanisha kwamba walishindwa kufanya vizuri katika fainali za Afrika za mwaka 2006, 2008 na 2010.
Alisema: "Tuna wachezaji wazuri na washambuliaji, lakini tunatakiwa tupambane ili tuweze kushinda fainali hizi."
Kikosi cha Ivory Coast
Didier Drogba anatazamiwa kuongoza mashambulizi ya Ivory Coast dhidi ya Mali leo.
Naye kocha wa Mali, Alain Giresse alisema: "Wachezaji wote katika kikosi changu wana kiwango cha juu, tunawapenda na kuwaheshimu. Wote hawa wameshacheza fainali za Afrika zilizopita hivyo wana uzoefu."
Kwa upande wa mechi ya Ghana dhidi ya Zambia, kiungo wa Ghana, Anthony Annan ambaye mama yake alifariki alhamisi iliyopita aliamua kubaki kambini pamoja na wenzake ili kukisaidia kikosi cha Ghana kiweze kuibuka na ushindi kwa sababu mara ya mwisho Ghana ilitwaa ubingwa wa Afrika mwala 1982.
Kikosi cha Mali
Frederic Kanoute ataiongoza Mali dhidi ya Ivory Coast
Ghana waliingia hatua hiyo ya nusu fainali baada ya kuichapa Tunisia, huku Zambia wakiingia hatua ya nusu fainali baada ya kuichapa Sudan.
Zambia wana sababu ya kushinda mechi hiyo na kwenda Libreville itakapochezwa mechi ya fainali Jumapili ijayo, ambako kuna kumbukumbu ya wechezaji wenzao 18 na viongozi saba kufariki kwa ajali ya ndege mwaka 1993
"Hatuna wasiwasi wa kuifunga Ghana, tunataka kuifunga Ghana ili tucheze fainali, nina furaha timu yangu kucheza nusu fainali ya Fainali za Mataifa ya Afrika, tuna furaha na hatua tuliyofikia, naamini tutacheza kwa asilimia 100 kuhakikisha tunashinda, hatutaki kukata tamaa wala kujutia baadaye," alisema kocha wa Zambia, Herve Renard.
Yanga kulipa kisasi kwa Mtibwa leo?

MABINGWA wa soka nchini, Yanga leo wanaweza kuwakaba vizuri kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Bara, mahasimu wao wakubwa Simba lakini hilo likiwezekana tu, iwapo watazoa pointi zote tatu mbele ya Mtibwa Sugar katika mechi itakayopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Vinara Simba, mwishoni mwa wiki iliyopita walishindwa kuvuna pointi zaidi kufuatia kushitushwa na kipigo wasichokitarajia cha bao 1-0 toka timu iliyokuwa ikiburuza mkia, Villa Squad ya Dar es Salaam.
Kama Yanga watatumia vizuri fursa ya kutereza huko kwa mahasimu wao na kushinda mechi dhidi ya Mtibwa, itapanda mpaka nafasi ya pili na kufikisha pointi 34, ambazo ndizo zinazoipa jeuri ya kukaa kileleni Simba.
Kinyume na matokeo hayo, Yanga itajikuta ikiiruhusu Simba kujikandamiza zaidi kileleni, huku pia ikitoa mwanya kwa Azam FC kukoleza mbio za kupanda kileleni.
Yanga itashuka dimbani kusaka ushindi utakaosindikizwa na sababu kuu mbili, kwanza kulipa kisasi cha kufungwa bao 1-0 katika mchezo wao wa kwanza, na pili kuhakikisha inapata pointi tatu za kupunguza kasi ya Simba.
Matokeo mazuri kwa Yanga yanahitajika ili kuwajenga vizuri kisaikolojia wachezaji wake kabla ya mechi ngumu ya Ligi ya Mabingwa Soka Afrika dhidi ya Zamalek ya Misri Februali 18 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Kocha wa Yanga, Kostadin Papic huenda akamuanzisha kipa namba moja wa timu hiyo, Yaw Berko ambaye taarifa za furaha zinadai kuwa ameshapona baada ya kuwa majeruhi tangu kumalizika michuano ya Kombe la Mapinduzi.
"Wachezaji wote akiwemo Yaw Berko wako katika hali nzuri, isipokuwa Nurdin Bakar ambaye anatarajia kuondolewa bandeji ngumu (POP) baada ya wiki mbili zijazo," alisema Louis Sendeu, Afisa habari wa Yanga.
Kazi ngumu itakuwa kwa Mtibwa itakayokuwa ikicheza mechi ya kwanza ugenini baada ya kufungwa mechi mbili mfululizo kwenye uwanja wao wa nyumbani dhidi ya JKT Oljoro ya Arusha na Coastal Union ya Tanga.
Ikiwa na pointi 22 katika nafasi ya tano kwenye msimamo, Mtibwa itakuwa na kila sababu ya kushinda mechi ya leo ili 'kuganga' majeraha hayo ya vipigo na pia kurejesha imani kwa mashabiki wake.
Vichapo hivyo vilipelekea kutimuliwa kwa kocha msaidizi wa muda mrefu wa timu hiyo, Mecky Mexime aliyedaiwa kuwa kiini cha kufanya vibaya katika mechi hizo mbili za vipigo.
Msemaji wa Mtibwa Sugar, Thobias Kifaru alitamba timu yake kuiduwaza Yanga na kuondoka na pointi zote tatu katika mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka.
"Kikosi kiko shwari, wachezaji wana ari na moyo wa ushindani dhidi ya Yanga. Tumejipanga kushinda mechi hii pamoja na kufahamu kwamba tunacheza na timu ngumu," alisema Kifaru.
Tuesday, February 7, 2012
Mechi ya Yanga kuhamishiwa Sudan ni sawa na kuruka maji na kukanyaga matope
Wapiganaji wa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sudan
Sehemu ya uwanja ikiungua baada ya kutokea vurugu kati ya mechi ya Al-ahly dhidi ya Al-masry nchini Misri
Mechi ya Yanga na Zamalek kuhamishiwa Sudan kutoka Misri kutokana na vurugu zilizotokea Misri na kuua mashabiki uwanjani, Uamuzi huo ni sawa na kuruka maji na kukanyaga matope.
Kama timu zinahofia kucheza Misri kutokana na kuhofia usalama wao sidhani kama Sudan ni sehemu salama, kwani hivi sasa Sudan kuna vita vya wenyewe kwa wenyewe na mgogoro mkuu ukiwa ni mafuta yanayopatikana katika mipaka ya Sudan kusini na Khartoum,huku serikali mbili zikishutumiana kila moja ikimhofia mwenzake kuwasaidia waasi wanaosababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.
Hata hivyo, Sudan inaweza kuwa si sehemu salama sana kwani mwaka 2009 wakati wa mechi ya mwisho ya kufuzu kwa Kombe la Dunia 2010 iliyozikutanisha Misri na Algeria kulitokea vurugu na mamia ya mashabiki kujeruhi.
Liverpool yatoa yatoshana nguvu na Tottenham,kuivaa Man United Jumamosi
Bale wa Tottenham akijaribu kuwahadaa walinzi wa Liverpool
Liverpool imeshindwa kuutumia vyema uwanja wake wa nyumbani baada ya kutoka sare ya 0-0 na Tottenham Hotspur katika mchezo wa Ligi Kuu ya England.
Spurs wakicheza bila ya wachezaji wao wengi na pia bila ya meneja wao Harry Redknapp, walicheza kufa na kupona kuzuia mashambulizi ya Liverpool yaliyokuwa yakiongozwa na Andy Carroll.Paka akikatiza uwanjani katika mechi ya Liverpool na Spurs,ingekuwa bongo ungesikia shutuma za uchawi.
Luis Suarez aliingia muda mchache baada ya kuanza kwa kipindi cha pili na kupata nafasi nzuri, lakini kipa wa Spurs Brad Friedel aliudaka mpira.
Liverpool sasa wanasalia katika nafasi ya saba wakiwa na pointi 39 pointi moja nyuma ya Arsenal. Spurs wamefikisha pointi 50, pointi saba nyuma ya Man City wanaoongoza ligi, na pointi tano nyuma ya Man United waliopo katika nafasi ya pili na pointi 55.
Liverpool watapambana na United Jumamosi.
Paka akikatiza uwanjani
Monday, February 6, 2012
GHANA yawasambaratisha waarabu yaifuata MALI nusu fainali
Ghana "Black Stars"
Andrew Ayew,Johnson Ayew na wachezaji wengine wakishangilia goli lililopeleka msiba Tunisia
Ghana siku ya Jumapili ilifuzu kuingia nusu fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa kuishinda Tunisia magoli 2-1, katika muda wa ziada.
Kipindi cha kawaida cha dakika 90 kilipokwisha, timu hizo zilikuwa sare ya 1-1.
Nahodha wa Black Stars ya Ghana, John Mensah, alifunga bao la kwanza katika mechi hiyo, katika dakika ya tisa, kabla Sabeur Khalifa kuisawazishia Tunisia kabla ya kipindi cha kwanza kumalizika.
Bao la ushindi la Ghana lilifungwa na Andre 'Dede' Ayew.
Ghana 2-1 Tunisia
Black Stars sasa wana matumaini ya kuendelea katika mashindano hayo na kupata ubingwa baada ya subira ya miaka 30, na watakutana na Zambia katika nusu fainali itakayochezwa uwanja wa Bata, siku ya Jumatano, tarehe 8 Februari, na ikiwa ni nusu fainali ya kwanza.
Mali na Ivory Coast nao watapambana katika nusu fainali ya pili siku ya Jumatano, katika uwanja wa Libreville.
Mali vs Gabon
Bao la Eric Mouloungui lilikuwa limewatia matumaini wenyeji Gabon, ambao mwaka huu wamekuwa wakishirikiana na Equatorial Guinea kuandaa mashindano ya mwaka huu.
Lakini kutangulia sio kufika, na Tidiane Diabate aliweza kuisawazishia Mali, zikiwa zimesalia dakika tano tu kabla ya mechi kumalizika.
Kwa kushindwa kufungana katika muda wa ziada, ilikuwa ni pigo kubwa wakati wa mikwaju ya penalti, Pierre-Emerick Aubameyang aliposhindwa kuifungia Gabon bao.
Gabon hawajawahi kufuzu kufika nusu fainali za mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika.
Idhaa ya Kiswahili ya BBC, ikishirikiana na redio washirika, itakutangazia nusu fainali kati ya Mali na Ivory Coast kutoka mjini Libreville, Gabon, katika matangazo maalum ya Ulimwengu wa Soka.
Charles Hilary vile vile atakutangazia mechi ya fainali ya mashindano hayo.
WEBB aibeba Man United kutoa sare na Chelsea
Howard Webb refa alieibeba Man United
Meneja wa Chelsea, Andre Villas-Boas, amelalamika kuhusiana na uamuzi wa Howard Webb, baada ya timu yake ambayo ilikuwa ikiongoza magoli 3-0, hatimaye ilipotoka sare ya magoli 3-3 na Manchester United katika mechi ya Jumapili.
Chelsea, ikichezea uwanja wa nyumbani wa Stamford Bridge, ilionekana kuelekea kupata ushindi, lakini kufuatia uamuzi wa refa Webb, Wayne Rooney aliweza kufunga magoli mawili ya penalti, na mchezo kubadilika.Chelsea 3-3 Man United
"Penalti ya kwanza ilikuwa ni wazi, na hakuna la kusema, lakini ya pili, ni ya kutiliwa shaka kabisa", alielezea Villas-Boas.
"Sijui kama Howard Webb alikuwa katika nafasi muwafaka ya kuweza kuona vyema na kufanya uamuzi, lakini ni jambo la kutoridhisha kwa yeye kutoa penalti hiyo", alilalamika meneja wa Chelsea.
Villas-Boas aliongezea: "Sijui kama Howard alikuwa analipizia jambo fulani ambalo hakulifanya katika nusu ya kwanza, lakini uamuzi wake haukufaa".
Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson alisisitiza kwamba penalti zote mbili zilikuwa halali, na akielezea kwamba hata walistahili penalti zaidi, baada ya Gary Cahill kugongana na Danny Wellbeck katika kipindi cha kwanza.
"Tungeliweza kupata jumla ya nafasi nne za penalti", alisema.
Katika mchezo wa awali wa Jumapili, Papiss Demba Cisse, aliyesajiliwa na Newcastle, na akicheza mechi yake ya kwanza, aliweza kuifungia timu yake bao, na wakapata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Aston Villa.
Newcastle sasa imo katika nafasi ya tano katika ligi kuu ya Premier kufuatia ushindi huo.
Cisse alisajiliwa kwa pauni milioni 10.
Mapema mwenzake kutoka Senegal, Demba Ba, alikuwa ameiwezesha timu yake kupata bao la kwanza katika mechi hiyo, lakini Robbie Kean akaisawazishia Villa.
Subscribe to:
Posts (Atom)