Wednesday, April 25, 2012

GARI LA KIFAHARI FERRARI ENZO LENYE THAMANI YA DOLA ZA KIMAREKANI 1.6 MILIONI LATELEKEZWA DUBAI


Polisi wa Dubai akiingalia Ferrari Enzo iliyotelekezwa Dubai na mtu aliyesadikiwa kuwa ni raia wa Uingereza, habari zaidi zinasema mshkaji huyo alifikia uamuzi wa kusepa na kuacha ndinga yenye mkwanja mrefu baada ya kushindwa kulipa kodi za ndani na kodi za askari wa usalama barabarani.


Ndinga hiyo iliyotelekezwa mwaka jana mwezi wa nane(8) na mchizi huyo, kwasasa serikali ya Dubai imeshatoa amri kwa jeshi la Polisi la nchi hiyo kulipiga mnada, wanahabari wanasema mnada huo haujawahi kutokea katika historia ya minada iliyowahi kufanywa na Polisi kutokana na ukweli kuwa ndinga hiyo ina ya Ferrari Enzo ina thamani ya kufa mtu,kiasi kinachofikia dola za kimarekani milioni 1.6


Habari zinasema kwa Dubai ni kitu cha kawaida kukuta magari ya biashara au ya thamani yakiwa yametelekezwa maeneo ya kuegeshea magari au maeneo ya viwanja vya ndege na wenye mali hizo kusepa kinyemela kukwepa kodi.

NIMEMFUMA MZUNGU HUYU BAGAMOYO

Mwanamama kazini..akimfanyia massage mzungu maeneo ya Bagamoyo
                                                                                                                              
Baada ya massage kazi ya kusuka ikaanza..ha ha ha haa mzungu anaona utaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaamu!

CHELSEA YATINGA FAINALI KLABU BINGWA BARANI ULAYA BAADA YA KUIADHIRI BARCELONA


Bousquets akifunga goli la kwanza la Barca

Klabu ya soka ya Chelsea ya Uingereza imefanikiwa kutinga fainali ya klabu bingwa barani Ulaya, licha ya nahodha John Terry kulimwa kadi nyekundu.

Mechi hiyo ilimalizika kwa sare ya 2-2, lakini Chelsea ikapata ushindi wa jumla ya magoli 3-2.

Andre Iniesta akitupia kambani goli la pili kwa Barca
Timu ya The Blues (Chelsea) ilionekana kuelemewa baada ya Sergio Busquets na Andres Iniesta kuiwezesha Barca kuongoza katika mchezo huo.

Lakini Ramires kwa umakridadi alifanikiwa kuichomoka ngome ya Barca na kutupia kambani bao safi la Chelsea kwa staili ya ku-chop katika mechi hiyo.



Ramires na golikipa Valdes wakishuhudia mpira uliopigwa na Ramires ukitinga wavuni

Barca walipata penalty, lakini Lionel Messi, licha ya maarifa yake na sifa nyingi katika ufundi wa penalty, lakini mkwaju huo ukagonga mwamba.


Messi akipiga penati iliyogonga mwamba

Muda wa majeruhi wa dakika tatu za nyongeza, Fernando Torres alionyesha utulivu wa hali ya juu sio tu kwa kushambulia ngome ya Barca ambayo kwa muda mrefu ilikuwa haiguswi, lakini vile vile kwa kumchenga hata kipa Valdes na kuukwamisha mpira wavuni kwa makini.

Mapema wiki hii, Torres alikuwa amenukuliwa akisema “sio siku zote timu bora hupata ushindi”, matamshi ambayo ni ndoto iliyotimia.


Torreeeeeees akimlamba chenga Valdes na kutupia kamba ya pili kwa Chelsea

Sasa vijana wa Chelsea wa Roberto di Matteo wanasubiri kufahamu kama watacheza na timu ya kocha wao wa zamani, Jose Mourinho, akiwa mkufunzi wa Real Madrid, au pengine watakutana na Bayern Munich, ambao uwanja wao ndio utakaotumiwa kuandaa fainali ya ligi ya klabu bingwa.


Nahodha John Terry akilimwa kadi nyekundu baada ya kumpiga teke Alexis Sanchez

Wachezaji wa Chelsea wakishangilia ushindi wa kutinga fainali baada ya kipyenga cha mwisho kupulizwa.

Drogba akimpoza machungu Leonel Messi

Real Madrid na Bayern zinapambana Leo, tarehe 25 Aprili 2012.

Tatizo la Chelsea ni kwamba katika fainali ya Jumamosi tarehe 19 Mei, sasa watazikosa huduma za nahodha John Terry, Ramires, Branislav Ivanovic na Raul Meireles mjini Munich, kutokana na kuadhibiwa kwa kucheza mchezo wa kuumizana katika nusu fainali.