Thursday, June 7, 2012

OKWI ANA THAMANI YA Tshs BILIONI 1


Emmanuel Okwi katika uzi wa Klabu yake ya Simba Sports

KLABU ya Simba imesema iko tayari kumruhusu mshambuliaji wake wa kimataifa toka Uganda, Emmanuel Okwi kwenda kucheza soka la kulipwa Ulaya, lakini hilo litawezekana iwapo klabu itakayomuhitaji itakubali kulipa ada ya uhamisho ya Pauni 500,000 (Sh1.3 Bilioni).

Okwi aliyetoa mchango mkubwa na kuiwezesha Simba kutwaa ubingwa wa Bara msimu huu, amepata ofa ya kwenda kufanya majaribio katika nchi tatu, Uingereza, Serbia na Austria.

Akiongea jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Simba, Ismail Rage alisema kimsingi klabu yake imekubali maombi kutoka nchi hizo ili nyota huyo aende kufanya majaribio.

"Kwa kuzingatia sera ya klabu, tumekubali maombi hayo na tuko tayari kumruhusu Okwi kwenda kufanya majaribio wakati wowote atakapohitajika kufanya hivyo," alisema Rage.

"Kumekuwa na maneno mengi kuhusu Okwi, hapa napenda kutoa ufafanuzi sahihi kwamba, tumepokea maombi ya mawakala kutoka Uingereza, Serbia na Austria akihitajika kwenda kufanya majaribio," aliongeza.

Rage alisisitiza kuwa, klabu yake haina kinyongo na mchezaji huyo kwenda kucheza Ulaya, lakini kwa ada ya uhamisho inayokwenda sambamba na kiwango cha mchezaji huyo, ambacho ni Sh1.3 Bilioni.

Wolfgang Strainwender, wakala raia wa Austria ndiye ameonyesha kumuhitaji haraka Okwi baada ya kumwona kwenye mchezo kati ya Uganda na Angola uliokwisha kwa sare ya bao 1-1, huku bao la Uganda likitumbukizwa wavuni na Okwi, alifafanua Rage.

"Wakala wa Uingereza na Serbia hawajasema wanamuhitaji haraka kiasi gani. Nadhani kufikia kesho jioni tutakuwa kwenye nafasi ya kufahamu ni lini atakwenda Austria," alisema Rage.




Okwi akimwaga udambwidambwi na klabu yake ya Simba Sports

Okwi akiwa katika uzi wa Timu yake ya Taifa Uganda "The Cranes"

Wakati huohuo, Rage alisema kikosi chake kinatarajia kuondoka jijini Dar es Salaam, Juni 15 kikiwa na wachezaji 25 kuelekea mkoani Shinyanga kwa ajili ya kucheza mechi ya kujipima nguvu dhidi ya Toto Africans.

Alisema baada ya mechi hiyo msafara wa Simba utakwenda Mwanza ambako pia utacheza mechi nyingine ya kujipima nguvu Juni 17.

"Nichukue fursa hii pia kuwaambia wale wanaotaka kujua Simba imemsajili nani na kumwacha nani, kufikia Juni 15 watafahamu kila kitu kwani kikosi chetu kitakuwa na sura mpya," aliongeza Rage

Tuesday, June 5, 2012

FAHAMU KWA UNDANI NCHI, MIJI, VIWANJA MICHUANO YA EURO 2012


POLAND
City
Stadium
Capacity
ChorzówSilesia Stadium50,000
WarsawNational Stadium55,000
PoznańMunicipal Stadium46,000
WrocławStadium in Maślice44,000
GdańskBaltic Arena44,000
KrakówWisła Stadium35,000

Ukraine

City
Stadium
Capacity
KyivNSK Olimpiyskyi73,000
DonetskShakhtar Stadium50,000
KharkivMetalist Stadium42,000
LvivUkraina Stadium32,000
OdesaChornomorets Stadium34,362
DnipropetrovskDnipro Stadium34,000

HAZARD ATUA CHELSEA


Eden Hazard

Klabu ya soka ya England ya Chelsea imetangaza katika tovuti yake kwamba hatimaye imekubaliana na klabu ya Lille ya Ufaransa kwamba mchezaji wa kimataifa ya Ubelgiji, Eden Hazard, atajiunga na klabu hiyo ya Stamford Bridge msimu ujao. Mchezaji huyo, mwenye umri wa miaka 21, tayari afya yake imekaguliwa na klabu ya Chelsea, na imeonekana hana tatizo lolote.

Walipochukua ubingwa wa ligi ya klabu bingwa, nilijiuliza, "Kwa nini sio Chelsea?", alisema Hazard.

"Kulikuwa na mvutano kati ya Chelsea na Manchester united, lakini binafsi naona Chelsea ndio mradi bora zaidi. Ni klabu cha ajabu."


Eden Hazard

Inaarifiwa kwamba Chelsea wameamua kutoa pauni milioni 32 kumpata kijana huyo, na ambaye akizungumza na kituo cha redio cha nchini Ufaransa, RMC, aliongezea: "Chelsea ni timu changa, na nitakuwa na nafasi bora zaidi ya kucheza."
"Ikiwa nitajitahidi kucheza vyema nikiwa Chelsea, huenda nikapata nafasi katika timu."






Hazard awapo uwanjani shughuli yake ni pevu kama inavyoonekana pichani amekusanya Vijiji

Hazard alikuwepo katika kikosi kilichoshinda ligi wakati Lille ilipopata ubingwa mwaka 2010-11 na katika msimu wake wa mwisho, alifanikiwa kufunga magoli 21 katika mechi 48.

Katika mechi yake ya mwisho dhidi ya Nancy mwezi uliopita, alifanikiwa kupata hat-trick (magoli matatu) wakati timu yake ilipocheza dhidi ya Nancy.

Lakini alishindwa kuvuma wakati Ubelgiji iliposhindwa na England katika mechi ya kirafiki Jumamosi iliyopita.

Hiyo ilikuwa ni mara yake ya 28 kuichezea timu yake ya taifa ya Ubelgiji.

Hazard sasa ni mchezaji wa pili kusajiliwa Chelsea tangu dirisha la usajili la mwezi Januari, wa kwanza akiwa ni mchezaji wa kimataifa wa Ujerumani, Marko Marinas.

Monday, June 4, 2012

IVORY COAST ILIVYOIBANJUA STARS 2-0

IVORY COAST 2-0 TANZANIA



 

RATIBA MICHUANO YA ULAYA (EUROPEAN CHAMPIONSHIPS FIXTURES 2012)

European Championships | FIXTURES


All times CAT (SA, GMT+2)East Africa(Tanzania) + saa moja. mfano 18:00=19:00

Friday 08 June 2012
Poland v Greece Warsaw National Stadium 18:00
Russia v Czech Republic Wroclaw Municipal Stadium 20:45

Saturday 09 June 2012
NetherlandsvDenmark Metalist Stadium 18:00
GermanyvPortugal Arena Lviv 20:45

Sunday 10 June 2012
SpainvItaly Arena Gdansk 18:00
IrelandvCroatia Poznan Municipal Stadium 20:45

Monday 11 June 2012
FrancevEngland Donbass Arena 18:00
UkrainevSweden Olympic Stadium 20:45

Tuesday 12 June 2012
GreecevCzech Republic Wroclaw Municipal Stadium 18:00
PolandvRussia Warsaw National Stadium 20:45

Wednesday 13 June 2012
DenmarkvPortugal Arena Lviv 18:00
NetherlandsvGermany Metalist Stadium 20:45

Thursday 14 June 2012
ItalyvCroatia Poznan Municipal Stadium 18:00
SpainvIreland Arena Gdansk 20:45

Friday 15 June 2012
UkrainevFrance Donbass Arena 18:00
SwedenvEngland Olympic Stadium 20:45

Saturday 16 June 2012
Czech RepublicvPoland Wroclaw Municipal Stadium 20:45
GreecevRussia Warsaw National Stadium 20:45

Sunday 17 June 2012
DenmarkvGermany Arena Lviv 20:45
PortugalvNetherlands Metalist Stadium 20:45

Monday 18 June 2012
CroatiavSpain Arena Gdansk 20:45
ItalyvIreland Poznan Municipal Stadium 20:45

Tuesday 19 June 2012
EnglandvUkraine Donbass Arena 20:45
SwedenvFrance Olympic Stadium 20:45

MAKUNDI MICHUANO YA ULAYA 2012

European Championships | LOGS


Group A

Pos Team P W D L GF GA GD Pts
1 Czech Republic 0 0 0 0 0 0 0 0
2 Greece 0 0 0 0 0 0 0 0
3 Poland 0 0 0 0 0 0 0 0
4 Russia 0 0 0 0 0 0 0 0

Group B

Pos Team P W D L GF GA GD Pts
1 Denmark 0 0 0 0 0 0 0 0
2 Germany 0 0 0 0 0 0 0 0
3 Netherlands 0 0 0 0 0 0 0 0
4 Portugal 0 0 0 0 0 0 0 0

Group C

Pos Team P W D L GF GA GD Pts
1 Croatia 0 0 0 0 0 0 0 0
2 Italy 0 0 0 0 0 0 0 0
3 Ireland 0 0 0 0 0 0 0 0
4 Spain 0 0 0 0 0 0 0 0

Group D

Pos Team P W D L GF GA GD Pts
1 England 0 0 0 0 0 0 0 0
2 France 0 0 0 0 0 0 0 0
3 Sweden 0 0 0 0 0 0 0 0
4 Ukraine 0 0 0 0 0 0 0 0

DIRK KUYT ATIMKIA UTURUKI


Dirk Kuyt

Mchezaji wa safu ya mbele ya Uhalonza Dirk Kuyt ameitosa klabu ya Liverpool na kujiunga na Fenerbahce ya Uturuki kwa mkataba wa miaka mitatu. Mshambuliaji huyo anasepa Liverpool baada ya kukipiga kwa kipindi cha miaka sita.
Kuyt mwenye umri wa miaka 31 alihamia uwanja wa Anfield mnamo mwaka 2006 na kushiriki mara 250 akifunga jumla ya mabao 71.
Habari kutoka Liverpool iliyotolewa kufuatia hatua hio imesema kua Kila mmoja anamtakia Dirk kila la heri na kumshukuru kwa mchango wake.
Aliposajiliwa, Kuyt alisema wakati huo, Kwangu mimi, Liverpool ni ndoto iliyokamilika. Hapana cha kuilinganisha nayo klabu hii, yenye sifa na historia ya kujivunia, alisema.
Mechi yake ya kwanza kushiriki ilikua dhidi ya West Ham United mwezi Agosti mwaka 2006, alipoingia kuchukua mahala pa Peter Crouch ambapo upande wake uliondoka na ushindi wa 2-1.


Kuyt akifanya vitu vyake alipokuwa Liverpool

Bao lake la kwanza lilipatikana mwezi mmoja baadaye alipofunga bao la kwanza katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Newcastle.
Baadaye alipendwa na mashabiki wa Liverpool, kivutio kikiwa mchangon wake katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Everton kwenye uwanja wa Goodison Park mwaka 2007 kisha alipofunga 3- peke yake dhidi ya Manchester United, mahasimu wakuu wa klabu kutoka Anfield.
Kuyt ambaye ameshiriki mara 80 kwa Timu yake ya Taifa ya Uholanzi, pia alifunga dhidi ya AC Milan katika mchuano wa Ligi ya mabingwa mwezi Mayi mwaka 2007.
Msimu uliopita mshambuliaji huyo alipata shida kupata nafasi katika kikosi kikuu, akishiriki mara 22 pekee na kuletwa kama mchezaji wa ziada mara tano katika mechi tisa za mwisho wa msimu.
Kwa wakati huu mchezaji huyo aliyesajiliwa kutoka klabu ya Utrecht yuko pamoja na wenzake wa Timu ya Taifa ya Uholanzi wakijinoa kwa ajili ya michuano ya Ulaya 2012 ambapo Wadachi watachuana na Denmark katika mechi yao ya ufunguzi jumamosi ijayo.