Wednesday, June 27, 2012

ZITTO ALIA NA SERIKALI UNYAMA ALIOFANYIWA Dkt ULIMBOKA


Dkt. Ulimboka akiwa ktk hali mbaya mara baada yakuokotwa akiwa hajitambui,Habari zilizomwagika hivi punde zinadai kuwa Dkt Ulimboka alitekwa jana usiku mishale ya saa 6 za usiku na Watu ambao hawakuweza kufahamika mara moja,habari za wataalamu wa mambo zinasema Dkt alipigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kwa jina moja la Abeid..na wakati akiwa katika juhudi za kuonana na huyo mtu watu wawili"vipande" waliokuwa na silaha walimvamia na kumteka kabla hajaangushiwa kisago cha kufa mtu ambacho kilimuacha akiwa hoi bin taaban katika msitu wa Magwepande..kufuatia kitendo hicho wataalamu wa mambo wamefunguka kuwa wafanyakazi wa chumba cha maiti muhimbili nao wamegoma na kuna tetesi za mgomo kuwa mkubwa zaidi!

Akizungumza baada ya kupata habari hizo ifuatayo ni Taarifa ya Mh Zitto.
Ujumbe amenitumia Daktari yupo pale MOI ‘Kaka Zitto,hali ya Dr.Ulimboka yuko unconscious,multiple ribs fracture na kwenye mikono pia amevunjika pamoja na taya,yuko icu wanamstabilise kwanza kwasababu hapumui vizuri,the situation here is really bad,I agree with you this is outright outrageous’
Nimechukizwa sana na habari za kutekwa, kupigwa na kuumizwa vibaya kwa Dr Ulimboka, Kiongozi wa Madaktari Nchini. Mambo kama haya tumezoea kuyasikia kwenye nchi za kidikteta na kuongozwa kiimla ambapo watawala badala ya kutumia njia ya kidemokrasia na kisheria kushughulikia wanaoamini ni maadui zao katika utawala, hutumia wahuni katika Taasisi za usalama kuteka raia, kuwatesa, kuwafunga na hata kuwaua.
Sitaki kuamini kwamba Tanzania imefikia huko. Nimezungumza na baadhi ya madaktari walio karibu na Dokta Ulimboka na kujulishwa kwamba majeruhi huyu wa vitendo vya hovyo kabisa kutokea hapa nchini alikamatwa jana usiku mnamo saa sita na watu wasiojulikana na kupelekwa katika msitu wa MagwePande na kujeruhiwa vibaya. Habari hizi bado hazijathibitishwa na vyanzo huru lakini ndio zilizopo hadi hivi sasa.
Serikali kama mlinzi wa usalama kwa raia inaWAJIBU kueleza tena kwa haraka ni nini kimetokea kwa kijana huyu msomi na kiongozi wa wataalamu wenzake. Serikali INAWAJIBIKA kueleza katika nyakati kama hizi ambapo kuna mgogoro kati yake na madaktari imekuwa wapi kuhakikisha usalama wa viongozi wa madaktari ili kuepusha watu wanaoitwa ‘agente provocateure‘ kuweza kuhatarisha hali ya amani ya nchi na hata kupelekea kuweka hali ya vitisho kwa madaktari wetu.
Serikali INAWAJIBIKA kueleza kama sasa imeamua kutumia njia za kihuni kumaliza matatizo na wananchi wake.
Nimemuomba Waziri kivuli wa Afya wa CHADEMA kufuatilia suala hili kwa kwa karibu sana ili kuhakikisha kwamba ukweli wote na ukweli mtupu unafahamika. Kamwe hatuwezi kuacha Mtanzania yeyote aonewe, anyanyaswe au akandamizwe eti kwa sababu ya kudai haki yake na za wenzake. ‘An injury to one, injuries to all’
Naomba madaktari wamwangalie kwa karibu daktari mwenzao ili aweze kupata nafuu. Ulinzi uimarishwe ili kuhakikisha usalama wake.

EURO 2012 NUSU FAINALI YA MAFUNDI WANAOJUANA SPAIN Vs URENO


Christiano Ronaldo wa Ureno(Real Madrid)

Xavi Alonso wa Uhispania (Real Madrid)

Miamba ya soka barani Ulaya Ureno na Uhispania leo zitapepetana katika nusu fainali ya kwanza ya michuano ya Ulaya katika dimba la Donbass,Donetsk.
Timu hizo mbili zinakutana zikiwa zimesheheni nyota wanaocheza soka la hali ya juu huko barani Ulaya na kwa idadi kubwa ya wachezaji wanakipiga La Liga Uhispania katika timu za Real Madrid na Barcelona hakika leo hatumwi mtoto dukani.

Ureno itamtegemea zaidi Christiano Ronaldo na Beki matata Pepe, Varela,Moutinho,Meireles,Luis Nani na wengineo wengi. huku wapinzani wao Uhispania ikimtegemea zaidi A.Iniesta kama mchezeshaji na wakali wengine kama Xavi,Torres,Sergio Bosquets,Sergio Ramos,Gerald Pique,David Silva,Pedro,Fbregas na mlinda mlango mashuhuri Iker Casillas. 

Ureno wamefika hatua ya nusu fainali baada ya Kujikusanyia pointi 6 na kukamata nafasi ya pili katika kundi B. na hivyo kuingia katika hatua ya robo fainali ambapo walikutana na Ugiriki na kufanikiwa kuwasambaratisha wagiriki kwa bao moja kwa nunge likitiwa kambani na Christiano Ronaldo katika dakika ya 78.

Uhispania ilifanikiwa kutinga katika hatua ya robo fainali za michuano ya EURO 2012 pale ilipojikusanyia pointi 7 na kuibuka kidedea katika kundi C, katika hatua ya robo fainali hizo ilikutana na vigogo wengine wa Ulaya Ufaransa na bila aibu kuwafurumusha nje ya michuano hiyo kwa mabao 2 kwa buyu huku mabao yote yatupiwa kambani na Xavi Alonso katika dakika ya 18 na 90.

Katika mtanange wa Nusu fainali ya leo kati ya Ureno na Uhispania ni vigumu mno kutabiri nani ataibuka meno nje kwa jinsi vikosi vyote vilivyosheheni nyota wanaojuana mno kwa ukweli kuwa wanatoka katika vilabu ambavyo hukutana mara kwa mara katika ligi za Ulaya sana sana La Liga ya Uhispania na Premier league ya Uingereza.

Andre Iniesta wa Uhispania (Barcelona)

Gerard Pique Gerard Pique of Spain in action during the International Friendly between Spain and England at the Ramon Sanchez Pizjuan Stadium on February 11, 2009 in Seville, Spain.  (Photo by Alex Livesey/Getty Images) *** Local Caption *** Gerard Pique
Gerald Pique wa Uhispania (Barcelona)


Torres wa Uhispania (Chelsea)

Cesc Fabregas - Spain v Italy - Group C: UEFA EURO 2012
Fabregas wa Uhispania (Barcelona)


Xavi Hernandez (Barcelona)

Moutinho wa Ureno (Sporting Lisbon)


Pepe wa Ureno (Real Madrid)


Silvester Valera wa Ureno (FC Porto)


Luis Nani wa Ureno (Manchester United)

Tuesday, June 26, 2012

STAR WA BONGO MOVIE FLORA MVUNGI KATIKA KASHFA YA UTAPELI WA 200,000/=


Flora Mvungi

Star maarufu katika tasnia ya filamu za kibongo "Bongo Movies" Flora Mvungi ameshutumiwa kupokea mlungula wa kiasi kadhaa unaofikia shilingi za kibongo laki mbili (200,000) kutoka kwa mtayarishaji wa filamu chipukizi aliejulikana kwa jina moja la Othman.

Akielezea mkasa huo wa "kupigwa" Tshs 200,000/= za kibongo na staa wa filamu nchini Mtayarishaji huyo wa filamu a.k.a Producer amesema Alikubaliana na Flora ampatie kiasi hicho ili aweze kushiriki katika filamu anayoiandaa inayoenda kwa jina la MZIWANDA. Othman anasema walipokubaliana alimtumia Flora mkwanja huo kwa njia ya Tigopesa, lakini ilipofika muda wa kuwa mahala pa kutayarisha filamu (Location) Staa huyo hakutokea kwa visingizio lukuki. Lakini Producer huyo akafunguka kuwa safari hii ilikuwa mara ya nne kuzinguliwa na Flora katika maswala mazima ya kufika eneo la tukio maarufu kama Location.

Producer Othman alipokuwa akihojiwa na kituo kimoja maarufu cha redio hapa nchini alifunguka hayo na ndipo mtangazaji wa kipindi hicho alipoamua kuwaunganisha kwa njia ya simu, katika hali ya mshangao staa huyo alikana kumfahamu Producer huyo wa movie za kibongo lakini alikiri kuwa kuna filamu ambayo aliitwa akashiriki lakini kutokana na sababu fulanifulani hakufika na akaahidi aitwe mambo yatakapokuwa tayari.
Utamu ukanoga pale mtangazaji alipomvutia kamba Flora Mvungi na kisha akamuuliza maswali kadhaa halafu akamuweka hewani wapeane makavu na producer, Hali ilikuwa ya majibizano makali Flora akikana kupokea mkwanja hali iliyoonekana kumkera zaidi Producer huyo na akisisitiza kuwa staa huyo asijifanye mjanja kwani yeye ana uthibitisho wa Message alizomtumia pesa ghafla Flora akakata simu nganjaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!! Hali hii iliacha SINTOFAHAMU ikiwa imetanda katika sakata hilo.

DOGO JANJA AFANYA KUFURU MLIMANI CITY, MANUNUZI MIL 2.5


Abdul Aboubakar Chande "Dogo Janja"

Unaweza usiamini na huenda ukahisi labda ni story za town, lakini ukweli ndio huo, Siku chache baada ya kutua Bongo na Pipa (Ndege) akitokea Kilimanjaro na kujiunga na kampuni ya Mtanashati Entertainments ya jijini, nyota wa Bongo Fleva , Abdul Abubakar Chande ‘Dogo Janja’ mwishoni mwa wiki iliyopita alisomea kisomo maalumu cha kuomba Mwenyezi Mungu amnyooshee mambo yake na "umatemate" zaidi pindi atakapoanza kushusha ngoma mpya.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa kisomo hicho kichoshudiwa na Teentz.com, Mkurugenzi wa kampuni hiyo Ostaz Juma na Musoma alisema kuwa wameamua kumfanyia kisomo hicho kwa lengo la kuweka kazi zote za Dogo janja mikononi mwa Mungu kwa kuwa wanaamini wapo watu ambao hawajafurahishwa na mpango mzima wa dogo huyo kurejea Bongo

Katika shopingi hiyo Dogo janja alitumia zaidi ya shilingi Milioni 2.5 za kibongo kununua vitu mbalimbali, kama Seti 5 za viatu, Suti 4, Jeans 10, T shirt 10,miwani 5, simu aina ya BlackBerry, Laptop na vitu vingine kibao .
Huku akionekana mwenye furaha kubwa Dogo Janja aliiambia Teentz.com kuwa amefuahi kwa kiasi kikubwa kwa yale yote ambayo Ostaz Juma na kundi zima la Mtanashati kwa yote wanayomfanyia hivi sasa kwani hatakuwa na malipo mengine zaidi ya kuwafanyia kazi nzuri zenye kiwango.

“Nina furaha sana, hakika namshukuru Ostaz kwa yote anayofanya kwangu sina la kusema zaidi wasubiri ngoma za kweli zitakazokuwa kama shukurani kwao kwa sababu ndiyo kitu pekee ambacho naweza kukifanya kwao” alisema Dogo Janja.


VENUS WILLIAM AONDOLEWA MAPEMA WIMBLEDON


Venus akirudisha mchomo kwa mpinzani wake Elena Vesnina

Bingwa mara tano katika mashindano ya tennis ya Wimbledon, Mmarekani Venus Williams, amesema hana nia ya kuachana na mchezo huo baada ya kuondolewa katika siku ya kwanza ya mashindano ya mwaka 2012 ya Wimbledon, katika raundi ya kwanza, alipopokea kipigo kitakatifu kutoka kwa mchezaji Mrusi, Elena Vesnina.
Venus, mwenye umri wa miaka 32, na anayeugua ugonjwa unaofahamika kama Sjogren's Syndrome, alishindwa 6-1 6-3 siku ya Jumatatu.
Mpinzani wake Vesnina amepangwa katika nafasi ya 79 katika orodha ya wachezaji bora zaidi wa tennis wa kike ulimwenguni.

Kiboko ya Venus Williams,Elena Vesnina akipeleka mchomo kwa Venus

"Haiwezekani nipumzike tu na kukata tamaa," alielezea Williams.

"Sina muda wa kujisikitikia. Hilo sio jambo zuri. Nitautumia muda wangu katika mawazo yanayonipa nguvu. Ninaupenda mchezo huu."

Mara ya kwanza Williams kushindwa katika raundi ya kwanza ilitokea mwaka 1997, wakati alipoingia pambano lake la kwanza la Wimbledon, na wakati huo alikuwa hata hayumo miongoni mwa wale waliopangwa katika mashindano hayo kama wachezaji bora.

Ni wanawake wawili tu ulimwenguni ambao wameshawahi kupata ubingwa wa Wimbledon mara nyingi kumshinda Williams, lakini tangu mwaka 2008, hajawahi kuibuka bingwa wa mashindano hayo.

Mara tu baada ya ushindi wake wa mwisho, iligunduliwa kwamba anaugua ugonjwa wa Sjogren's Syndrome, na ambao humfanya mgonjwa kujihisi ni mchovu mno, na katika sehemu mifupa inaungana, maumivu.

Ayaaaaaaaa nimechapwa!!!!!


Kudadekii leo Venus hutoki hapa!!

Venus Williams baada ya kupokea kichapo kitakatifu kutoka kwa Mrusi Elena Vesnina


Monday, June 25, 2012

EURO 2012 ITALIA YATINGA NUSU FAINALI WAKATI ASHLEY WAWILI WAKIIGHARIMU UINGEREZA


Barwuah Balotelli akipiga tik-tak ambayo ilipaa langoni mwa Uingereza

Gianluigi Buffon akiokoa mchomo wa Johnson ambao almanusra uzae bao kwa Uingereza

Timu ya soka ya Uingereza imetupwa nje katika mashindano ya Euro 2012, baada ya kunyukwa na Italia usiku wa Jumapili katika robo fainali, kwa changamoto ya mukwaju ya penalti 4-2 mjini Kiev, Ukraine, kufuatia muda wa kawaida na dakika 30 zaidi kumalizika kwa timu hizo mbili kutofungana.

Italia sasa itavaana na Ujerumani katika mechi ya nusu fainali.
Alessandro Diamanti alifunga bao la kuamua mshindi katika mikwaju hiyo ya penalti, baada ya Ashley Young na Ashley Cole kukosa kufunga mabao kupitia mikwaju waliyopiga.

Vijana wa meneja Roy Hodgson ilikuwa wazi walilemewa katika mchezo mzima, lakini ni hali ya imani na uvumilivu iliwafanya kuwa na matazamio ya kuishinda Italia.

Italia iliweza kugonga mwamba, na bao la Antonio Nocerino lilikataliwa baada ya mwamuzi kusema aliotea mpira.

Kadri mechi ilivyoendelea, ndivyo wachezaji wa England nao walionekana wachovu, na ikielekea walitazamia bahati zaidi kuliko kujitahidi kuimarisha kiwango cha mchezo wao, na penalti kwao bila shaka ikawa sio za kutegemewa tena.

Baada ya mechi, nahodha Steven Gerrard alisema: "Wachezaji walicheza kadri ya uwezo wao wote. Nilidhani tungelipata bahati katika mikwaju ya penalti, lakini mambo hayakuwa hivyo. Ukiongoza katika penalti, unashikilia matumaini kwamba mambo yatasalia hivyo, lakini Italia ndio waliokuwa na bahati. Vijana waliokuwa walinzi walifanya kazi nzuri mno, na kuiletea nchi fahari, lakini tunarudi nyumbani na mioyo ya huzuni, na hili ni jambo gumu kulikubali."

England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
Balotelli akijaribu kombora langozi mwa Uingereza bila matumaini
England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
Ngoma inogile Lescott na Balotelli
England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final

England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final

England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
Imooooo..Joe Hart akichumpa kuokoa penati bila mafanikio
England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
Wachezaji wa Uingereza waliokosa penati A.Cole na A.Young na wenzao wakiwa hawaamini kilichojiri katika dimba la Olympic mjini Kiev

England v Italy - UEFA EURO 2012 Quarter Final
John Terry akimtuliza Ashley Cole na Jermain Defoe akimtuliza Ashley Young baada ya Ashley wawili kukosa mikwaju ya penati katika mtanange dhidi ya Italia

Mikwaju ya penati Uingereza na Italia

Friday, June 22, 2012

CHRISTIANO RONALDO AIPELEKA URENO NUSU FAINALI EURO 2012


Gooooooooo!! Christiano Ronaldo akitupia kambani kwa kichwa maridadi

Woyoooooo nimemaliza kaziiiiiii!!! Ronaldo akishangilia goli lililoipeleka Ureno nusu fainali

Mshambuliaji hodari Christiano Ronaldo aliwaridhisha mashabiki wa Ureno kwa kucheza vizuri sana usiku wa Alhamisi, na juhudi zake zimeiwezesha Ureno kuifumua Jamhuri ya Czech bao 1-0 na kufanikiwa kutinga katika hatua ya nusu fainali.

Ronaldo, ambaye alifunga magoli mawili wakati Ureno ilipocheza na Uholanzi, aliweza kuichachafya ngome ya Czeck na mashuti mawili kugonga mlingoti wa goli.

Hatimaye aliweza kutupia kambani kwa kichwa, huku zikiwa zimesalia dakika 12 kabla ya mechi kumalizika, na kipa Petr Cech akiweza kuufikia mpira, lakini hakuweza kuuzuia kutokana na nguvu nyingi zilizotumiwa na Ronaldo.


Peter Cech akikabiliana na Christiano Ronaldo

Ilikuwa dhahiri kwamba wachezaji wa Czech waliingia uwanjani wakiwa na nia ya kuimarisha ngome yao, na wala sio kushambulia, na kamwe hawakumtisha kabisa kipa wa Ureno.

Ureno sasa itakutana aidha na Uhispania au Ufaransa katika juhudi za kufuzu kwa fainali.

Bila shaka timu ambayo itakutana na Ureno itakuwa na wasiwasi ni vipi itaweza kumzuia Ronaldo, ambaye baadhi ya wadau wa soka wanasema kwa sasa ndiye mchezaji bora zaidi barani Ulaya.

Kiungo Miguel Veloso akimrukia Ronaldo kwa furaha

Portuguese Football Fans AFP/Getty Images
Mashabiki wa Soka wa Ureno wakiwa katika viwanja vya Campo Pequeno Square jijini Lisbon,Ureno wakiangalia mechi ya nusu fainali kati ya chama lao na Jamhuri ya Czech mechi iliyokuwa ikipigwa katika dimba la Warsaw nchini Poland. 

PORTUGAL  1-0  CZECH REPUBLIC