Wednesday, August 29, 2012

FULHAM YAMRUHUSU DEMBELE KUKIPIGA TOTTENHAM

Moussa Dembele
 
Klabu ya Tottenham Hotspurs imepata idhini ya kuendelea mbele na mchakato wa kumnasa kiungo wa kati wa klabu ya Fulham, Moussa Dembele, kufuatia vilabu hivyo kuafikiana juu ya malipo ya kumnunua mchezaji huyo.

Mchezaji huyo wa Ubelgiji yuko katika mwaka wake wa mwisho katika mkataba wa kukipiga Fulham inayochezea uwanja wa Craven Cottage, na hakushiriki katika mechi ya kombe la Capital One dhidi ya Sheffield Wednesday, wakati timu yake ilipochapwa.

Meneja wa Fulham, Martin Jol, amesema Dembele, mwenye umri wa miaka 25, yumo katika vipimo vya afya yake ndani ya klabu ya Tottenham.

Dembele alijiunga na Fulham kutoka klabu ya Uholanzi ya AZ Alkmaar, kwa gharama ya pauni milioni 5, mwaka 2010.

Hayo yakiendelea, Fulham imekuwa katika hali ya kushauriana na Kieran Richardson, baada ya kuelewana na Sunderland kuhusu kitita kinachohitajika kumpata mlinzi huyo.

Meneja wa Sunderland, Martin O'Neill alithibitisha kwamba tayari wamekubaliana juu ya kiwango cha pesa ambazo Fulham watatoa kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27.

Monday, August 27, 2012

WANAMUZIKI 10 MATAJIRI ZAIDI AFRIKA


1-Youssou Ndour

Youssou Ndou ndiye mwanamuziki tajiri zaidi barani Africa. Mshikaji anamiliki kituo kikubwa zaidi binafsi cha luninga nchini Senegal, kampuni ya magazeti na kituo cha radio.

Anamiliki pia Klabu ya Usiku(night club) na record label. Anamiliki kampuni ya nyumba na makazi. Mwaka 2004 jarida la Rolling Stone lilimwelezea kama mwanamuziki maarufu zaidi nchini Senegal na pengine barani Afrika aliye hai.
Tangu April 2012, ni waziri wa utalii na utamaduni nchini Senegal.

2-P Square
 
Hakuna msanii wa kizazi cha leo anaeweza kugusa matawi ya mapacha hawa, Peter na Paul Okoye. Wana hela chafu!
Wanachaji dola 250,000 kwa kila show ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 390 za Tanzania! Kuongezea msumari zaidi hapo ni kwamba hawa Washkaji wana show kila weekend! Mpaka sasa hivi wameshafanyiwa booking ya kufanya show sehemu mbalimbali duniani hadi March mwakani!
Nyumba yao waliyoipa jina la Squareville huko Ikeja Nigeria ina thamani ya dola milioni 3 ambazo ni zaidi ya shilingi bilioni 4.
Waliweka historia kwa kuwa wasanii wa kwanza kununua kiwanja kwenye eneo la Banana Island nchini Nigeria ambacho kina thamani ya zaidi ya dola milioni 3 pia!
Wana mkataba wa miaka mitatu na kampuni ya pili kwa ukubwa ya simu nchini Nigeria ya Globacom wakiwa kama mabalozi wake ambapo hulipwa dola milioni 1 kwa mwaka, wanamiliki pia mijengo kibao ya kupangisha.Ucpime jipangeee!
 
 
3-D Banj
Mnigeria huyu aliye chini ya label ya Kanye West, G.O.O.D Music, alitengeneza takriban dola milioni 5 kwenye kampeni ya rais wa Nigeria Goodluck Jonathan.
Anamiliki jina la ‘Koko’ linalojumuisha klabu bora za Nigeria za KokoLounge, maji ya kunywa Koko Water na Koko Mobile.
Aliwahi kufanya reality show ya TV iitwayo Koko Mansion na kulipwa dola milioni 1.Anamiliki nyumba yenye thamani ya dola milioni 1.5 jijini Atlanta. Ni mwenyekiti mtendaji wa Dbanj Records na pia ana kampuni ya ulinzi iliyofanikiwa sana.
Yeye hucharge dola 100,000 kwa show.



4-Koffi Charles Antony Olomide
Mfalme wa Lingala Koffi  anacharge tabriban Euro 100,000 kwa show. Jamaa hupiga show nchini Ufaransa zinazojaza karibu watu 80,000 ambapo tiketi moja ni Euro 30 sawa na shilingi elfu 60.Amekwishatoa albam zaidi ya saba ambazo zimemuingizia mamilioni ya dola.
 
5-Salif Keita
Salif Keita ukipenda unaweza kumuita  ‘Sauti ya dhahabu ya Africa’, ni miongoni mwa watu wanyenyekevu lakini matajiri sana barani Afrika.Msanii huyo albino anamiliki kisiwa chake binafsi nchini Mali.Anamiliki majumba na mali zingine nchini Ufaransa na Mali.

6-Fally Ipupa
Msanii huyu anajulikana kama ‘Mfalme mpya wa Lingala’ wa DRC. Kutoka kuwa mcheza show wa zamani wa Koffi Olomide, anasifika kwa kuleta usasa zaidi kwenye muziki wa Lingala. Ameshakuwa balozi wa brand nyingi za nguo nchini Ufaransa, concerts zenye gharama na kuuza kopi kibao za albam zake.
 
7-2 face idibia
Msanii huyu wa Nigeria anamiliki nyumba za kupangisha zenye gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 7.Hulipwa kuanzia dola 50,000 - 80,000 kwa show.namiliki pia klabu ya usiku ya nguvu na biashara zingine zinazomuingizia hela nyingi.
8-Hugh Masekela
Huyu ni miongoni mwa wanamuziki wa Jazz wanaoheshimika zaidi barani Africa. Anamiliki mobile studio yenye mafanikio makubwa nchini Botswana. Hushiriki kwenye matamasha makubwa duniani na huingiza mamilioni ya dola kutokana na mauzo ya albam zake.
9-Banky W
Ukiweza muite Mr. Capable pia. Banky W hufanya show mara tatu ama nne kwa wiki zinazomuingiza mshiko mrefu mno. Aliwahi kuwa balozi wa kampuni ya simu ya Estisalat ya Nigeria ambapo alitumika kwenye matangazo yake.

Kwa sasa ni balozi wa Samsung Mobile. Amewahi kufanya kampeni ya Coca Cola-Nigeria na Microsoft’s Anti-cyber Crime Initiative.
Kutokana na kuingiza hela nyingi amenzisha mradi kuwasaidia wasiojiweza kwa kuwalipia ada watoto wenye uwezo darasani chini ya Mr. Capable Foundation.

10-Chameleone
Mzee wa Valuvalu anafunga list kwa kuwa msanii mwenye hela zaidi kuliko wote Afrika Mashariki.Anamiliki gari Cadillac Escalade yenye thamani kubwa, Mercedes Benz ML 320, Super Custom, convertible na Premio.

Anaishi kwenye nyumba yenye gharama kwenye maeneo ya wazito huko Seguku Hill kwenye viunga vya Kampala, simu zake mwenyewe na mali zingine nyingi.

Matumizi ya nyimbo zake yanamuingiza mamia kwa maelfu ya Euro!

DIAMOND AMSHIRIKISHA J MARTINS KWENYE SONG JIPYA


Naseeb Abdul "DIAMOND"

J Martins

Baada ya kufanya makamuzi ya nguvu kwenye shoo ya Big Brother Africa nchini Afrika ya Kusini, Diamond alianza kupata mialiko mbalimbali kutoka kwa wasanii wakubwa barani Afrika, na hivi sasa anatarajia kukamilisha kolabo yake anayoifanya na mwanamuziki kutoka Nigeria J Martin.

Kwa mujibu wa Diamond hivi sasa amesharekodi sehemu zake kwenye wimbo huo katika studio za MJ Records chini ya Prodyuza Marko Chali.

"Ingawaje nipo katika mchakato wa kusafiri kuelekea Marekani, lakini tayari nimeshaingiza voko za kazi yangu kwa Marco Chali na punde kolabo hiyo itaiva kama ilivyopikwa katika chungu safi.

"Chorus ya wimbo huo nimeimba mimi na mcheza shoo wangu Mose Iyobo"
anasema Diamond ambaye ameamua kumpa shavu dansa wake kutokana na kuonyesha uwezo mzuri katika kuimba.

J Martin ambaye kwa sasa yupo nchini Marekani akichukua kozi maalum ya miezi mitatu ya masuala ya utayarishaji, tayari anausubiri wimbo huo ili aingize sauti yake.

Katika safari hii Diamond anakwenda na madansa wake wote wanne na msemaji wake. Diamond atafanya shoo katika mkutano mkubwa unaofanyika Marekani ambao wahudhuriaji wamemtaka akawape burudani.

WAZIRI WA USALAMA LIBYA AJIUZULU


Waziri wa usalama wa Libya aliejiuzulu Fawzi Abdel A'al

Taarifa kutoka Libya zinasema kuwa waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Fawzi Abdel A'al, amejiuzulu.
Sababu ya kujiuzulu kwake haijafahamika mara moja.

Kujiuzulu kwa bwana Fawzi kumetokea siku moja baada ya polisi katika mji mkuu, Tripoli, kutuhumiwa kushindwa kuwazuwia Waislamu wenye msimamo mkali wasibomoe msikiti na kaburi la Wasufi mchana kweupee.

Friday, August 24, 2012

BARCELONA YAIBANGUA REAL MADRID 3-2 SUPERCOPA


Christian Ronaldo akishangilia goli la kwanza

Makosa ya mlinda mlango wa Barca Victor Valdes yaliipatia goli la pili Real Madrid katika muda wa lala salama kabla ya Barca kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 katika mchezo wa kwanza wa Supercopa nchini Uhispania mchezo huo ukipigwa katika dimba la Nou Camp, Mchezo wa Pili utachezwa jumatano ijayo katika dimba la Santiago Bernabeu.

Pedro, Messi kwa mkwaju wa penati na Xavi mabao yao yaliibeba Barcelona baada ya kuwa nyuma kwa goli maridadi la kichwa lililotupiwa kambani na Christian Ronaldo katika dakika ya 55 ya mchezo katika dimba la Nou Camp.

Zikiwa zimesalia dakika 5 mtanange huo uishe Angel Di Maria alimharasi Mlinda mlango Victor Valdes katika lango la Barcelona baada ya beki kumrudishia kipa wake na Di Maria kufanikiwa kumnyang'anya mpira V.Valdes na kutupia kambani goli la pili la Real Madrid.

Vilanova akishuhudia maboko ya Valdes akiwa kocha mkuu kwa mara ya kwanza katika mechi ya "Clasico" . "Ni mchezo wa timu hivyo yeyote anaweza kufanya makosa, sichukulii uzito wowote kosa lile" alisema Vilanova.
Wote tunafahamu jinsi Valdes amekuwa mtu muhimu wa kuanzisha mipira nyuma ili kuendana na mfumo wa uchezaji wa Barca.
"Kama atakuwa anapiga mipira mirefu muda wote hatutoweza kuendana na mfumo wa uchezaji wetu, hivyo tutamfariji na kumshauri aendelee na mchezo huo" Aliongeza Vilanova.

PEDRO AOTEA(Offside)
Mascherano alimpenyezea mpira wa juu Pedro na kwa umaridadi aliutuliza mbele ya Coentrao na kutupia kambani kuandika bao la kusawazisha. Luninga zilionesha shambulizi hilo na kupendekeza kuwa Pedro alianzia kwa kuotea kitu ambacho Mourinho hakusita kukizungumzia
"Sijafurahishwa na goli la kwanza la Barca,ni makosa ya kiuamuzi" Alisema Mourinho.

Utamu wa mchezo ulianza pale Sergio Ramos alipomuangusha Andre Iniesta katika eneo la hatari katika dakika ya 70, bila kung'ata filimbi wala kupepesa macho mwamuzi wa mchezo huo aliamuru lipigwe tuta, Messi alitupia kambani mkwaju maridadi wa penati na kufikisha goli la 14 katika mechi zilizozikutanisha Barcelona na Real Madrid.

Iniesta alikokota gozi na kukusanya kijiji kabla hajatoa pasi murua kwa Xavi nae bila ajizi akatupia kambani goli la tatu katika dakika ya 78, kabla ya Cassilas kuondoa mchomo wa Messi aliekaribia kutupia kambani goli la nne.

"Matokeo ya mchezo yamekuwa magumu tofauti na matarajio yetu na nafasi tulizotengeneza, Na sasa itatubidi tucheze mchezo mzuri mechi ya marudiano kama tunataka kubeba kombe" Pedro alisema katika kituo cha luninga cha Uhispania.
 
Messi kama kawaida yake amekusanya kijiji

Hapatoshi ni Ronaldo na Dani Alves

Alexis Sanchez akikabiliwa vilivyo na Coentrao
 
Messi akishangilia baada ya kutupia kambani kwa mkwaju wa penati


Wachezaji wa Barcelona wakiwaaga mashabiki baada ya kuichabanga Madrid 3-2

Jose Mourinho wa Real Madrid akipeana mkono na Tito Vilanova wa Barcelona baada ya mechi ya Supercopa kumalizika.

Thursday, August 23, 2012

LEO NDIO LEO BARCELONA Vs REAL MADRID



Kocha wa Barca Tito Vilanova

Kocha wa Real Madrid Jose Mourinho

TITO Vilanova alikuwa Barcelona kama msaidizi wa Pep Guardiola wakati alipotawala vichwa vya habari Agosti mwaka jana baada ya kuchapwa kibao cha usoni na kocha wa Real Madrid, Jose Mourinho kwenye mchezo wa Hispania Super Cup.

Leo ni mwaka umepita tangu tukio hilo limetokea na Tito amechukua jukumu la rafiki yake la kuifundisha Barca sasa anakutana tena na Mourihno katika mchezo wake wa kwanza mgumu kama kocha utakaofanyika kwenye Uwanja wa Nou Camp (saa 5:30 usiku).

Mabingwa watetezi Barca wamefuzu kucheza hatua hiyo baada ya kutwaa ubingwa wa Kombe la Mfalme na hiyo itakuwa mechi ya kwanza ya kupima ubora wa kikosi cha Vilanova dhidi ya mabingwa wa Ligi Kuu.

Uhasama baina ya wachezaji uliosabishwa na kadi tatu nyekundu kwa wachezaji wa Real mwaka 2011 pamoja na picha za televisheni kuonyesha Mourinho akimzaba kibao Vilanova umepungua kwa kiasi kikubwa.

Tukio hilo lilisababisha Mourinho kufungiwa mechi mbili za Super Cup, na Vilanova mechi moja kwa kuonyesha ishara mbaya, lakini adhabu hizo zote zimefutwa na rais wa shirikisho la soka la Hispania, Angel Maria Villar.

Mourinho, amekataa kuomba msamaha kwa yeyote, lakini mashabiki wa Madrid wamejitokeza na kukiriki kuwa kocha wao alifanya kosa.

Imeanza Ligi Vyema,
Barca imeanza vizuri kampeni zake za kusaka ubingwa wa ligi kuu kwa ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Real Sociedad Jumapili iliyopita, huku wapinzani wake Real Madrid wakilazimishwa sare 1-1 nyumbani na Valencia.

Kuanza vizuri kwa Vilanova katika ligi kumechagizwa na kurejea kwa mshambuliaji wake David Villa aliyekuwa nje kwa zaidi ya miezi nane baada ya kuvunjika mguu, lakini Jumapili alifanikiwa kufunga bao kwenye ushindi wao mnono wa mabao matano.

Mshambuliaji huyo wa Hispania bado hajawa fiti na kuna uwezekano leo akapumzishwa kama itakavyokuwa kwa kiungo mpya Alex Song.

Mchezaji pekee mwenye uhakika wa kuanza leo ni Lionel Messi ambaye msimu uliopita alifunga mabao 73 ndiye atakayeongoza mashambulizi dhidi ya Real.

"Timu bado imebaki ile ile na falsafa na mtindo ni ule kama ilivyokuwa enzi za Guardiola," Messi aliimbia Barca TV.

"Bado wachezaji wote wanahamu ya kupata mataji. Nataka kushinda kila kitu na kocha Tito."

Kinara wa ufungaji wa Real, Cristiano Ronaldo bado hajawa fiti na katika mchezo wa kwanza wa ligi uliofanyika kwenye uwanja wa Bernabeu alishindwa kupiga hata shuti moja golini.

"Bado sijawa fiti kwa asilimia 100, lakini natumaini nitarudi kwenye kiwango changu haraka," alisema Ronaldo.

Mreno mwenzake Pepe ameondolewa kwenye kikosi kitachocheza mechi hiyo baada ya kuumizwa wakati alipogongana na kipa wake Iker Casillas kwenye mchezo wao wa Jumapili dhidi ya Valencia.

Pamoja na Barca kutawala sana mechi za 'clasicos' chini ya Guardiola, lakini Real wamepoteza mechi moja tu wakiwa na Mourinho kati ya mara nne walizokutana Catalunya

Wednesday, August 22, 2012

ADEBAYOR ATUA TOTTENHAM

Emmanuel Adebayor
Emmanuel Adebayor

Emmanuel Adebayor amekamilisha mipango ya kuhamia Tottenham Hotspur kutoka Manchester City kwa kitita cha pauni milioni 5.
Mshambulizi huyo kutoka Togo alionyesha umahiri wake msimu uliopita, akiichezea Tottenham kwa mkopo, kwa kufunga jumla ya magoli 17 katika ligi kuu ya Premier.

Adebayor atakuwa ni kati ya wachezaji wenye mishahara mikubwa katika klabu hiyo ya uwanja wa White Hart Lane.

Adebayor, mwenye umri wa miaka 28, alikuwa akilipwa na Manchester City pauni milioni 175,000 kwa wiki.

Mshambulizi huyo, ambaye zamani alikuwa akiichezea Arsenal, alifichua habari za kujiunga na Tottenham kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter: “Tottenham niko njiani! Natamani magoli. Kaeni chonjo.”

Mkataba wa Adebayor ulikuwa uendelee kwa miaka miwili zaidi na klabu ya Man City, na kwa kipindi kirefu katika misimu miwili iliyopita alikuwa akiichezea Real Madrid ya Uhispania, na kisha Tottenham.

“Ninafurahi kujiunga kabisa na Spurs baada ya klabu kuelewana na Manchester City,” aliongezea Adebayor.

“Pengine ilichukua muda mrefu kinyume na ilivyotazamiwa, lakini nimefurahi sana kurudi Tottenham Hotspur. Nilifurahi sana nilipokuwa hapa msimu uliopita, na ni matumaini yangu tutaweza kwa pamoja kufanikiwa hata zaidi.”

Inafahamika kwamba Spurs walikataa kubadilisha mipango yao ya mishahara ili kufanikisha mipango ya kumpata Adebayor.

Lakini kutokana na Adebayor kukataa kupunguziwa mshahara, mabingwa wa ligi kuu Manchester City walikubali kuongezea zaidi tofauti ya senti atakazopokea Adebayor katika klabu ya Tottenham, na kiwango alichozoea Man City cha pauni 175,000.

Tottenham watamlipa pauni 80,000 kwa wiki, na Man City ilibidi kukubali kuongezea tofauti ya elfu 95,000 kwa wiki, ili kuyafanikisha makubaliano kati ya vilabu hivyo viwili.

Makubaliano hayo yanahitimisha ubishi ulioendelea kwa muda mrefu, kuhusu ikiwa Adebayor alistahili kulipwa bakshishi na marupurupu mengineyo iwapo angelisisitiza kuondoka Man City pasipo makubaliano kamili kati yake na klabu hiyo.
Mavituz ya Adebayor