Friday, December 14, 2012

KOCHA WA PSG YA UFARANSA KUMRITHI MILOVAN SIMBA S.C

Mabingwa wa Soka Tanzania,Bara Simba S.C  imemtangaza Patrick Liewig ambaye ni raia wa Ufaransa kuwa kocha mpya baada ya kusitisha mkataba na kocha wa sasa Mserbia Milovan Cirkovic. Liewig ameshazifundisha PSG ya Ufaransa, Club African ya Tunisia pamoja moja klabu kubwa barani Afrika ya ASEC Mimosas ya Ivory Coast. Anatarajiwa kutua nchini baada ya wiki 2 kuanza kukinoa kikosi cha wekundu hao wa Msimbazi.

Wasifu wa Lewig
Date of birth:04.10.1950
Age:62
Nationality:-France
ΓΈ-Incumbency as manager:1,97 Years
success-ratio as manager:30,77 % Wins
38,46 % Draw
30,77 % Loss
Preferred formation:4-2-3-1
 



Patrick Liewig

WIMBO WA LEO-Hatuna Habari nao (Abdu Kiba)


KASEJA APATA MRITHI KUTOKA UGANDA

Mabingwa wa Soka Bara, Simba wamekamilisha usajili wa mrithi wa kipa Juma Kaseja, Mganda Abbel Dhaira.

Dhaira amesaini mkataba wa miaka miwili wenye thamani ya dola 40,000 (Sh43 milioni) na mshahara wa mwezi Sh2 milioni mbele ya Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hanspope.

Kusajiliwa kwa kipa huyo kunakuja baada ya muda mrefu mashabiki wa Simba kuhoji kiwango cha Kipa Juma Kaseja.
Kaseja alikuwa gumzo kwa mashabiki wa Simba katika mechi za mwisho za duru la kwanza Ligi Kuu akituhumiwa kufungwa mabao ya kizembe.
Akizungumza jana baada ya kukamilika kwa usajili wa Dhaira, Hanspope alisema wanajivunia kupata kipa mwenye umbo kubwa kama Mohamed Mwameja aliyewahi kuidakia klabu hiyo.

Hanspope alisema kusajiliwa kwa kipa huyo Mganda kulitokana na mapendekezo kutoka kwa kipa wao wa kwanza hivi sasa, Kaseja.
“Kaseja ndiye aliyependekeza kwa uongozi kumsajili kipa huyu. Tunaamini mawazo yake yataisaidia Simba kufanya vizuri kwenye michuano mbalimbali ndani na nje ya nchi.
Kwa upande wake, Dhaira alisema amefurahi kusajili Simba akiamini ni moja ya timu kubwa Afrika.
“Nimekuwa nikiisikia Smba kwa muda mrefu, nafahamu ni moja ya timu nzuri Ukanda wa Afrika Mashariki na Afrika kwa jumla,” alisema kipa huyo.



Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba S.C Zakaria Hanspope akimkaribisha Abbel Dhaira


Golikipa kutoka Uganda Abbel Dhaira akiangusha saini na Dole gumba kuichezea Simba S.C kwa nyundo mbili



Abbel Dhaira akifanya vitu vyake uwanjani

Wednesday, December 12, 2012

TYSON SASA NI MWANAMKE ASEMA TOKEA ZAMANI ALITAMANI KUWA MWANAMKE

BINGWA maarufu wa zamani katika masumbwi wa uzito wa juu duniani, Mike "IRON" Tyson, anasemekana yuko katika hali nzuri baada ya kujibadili na kuwa mwanamke katika operesheni aliyofanyiwa huko Beverly Hills, Marekani, hivi karibuni ambapo amebadili jina na anajiita Michelle.
Kuna wakati Tyson alikuwa anajulikana kama “Mtu mwenye sura mbaya zaidi duniani”!sasa ni Dem inakuwaje?


MIKE TYSON sasa anaitwa MICHELLE

“Watu wanaona ni ajabu mie kuwa mwanamke hivi sasa,” alisema Tyson ambaye aliwahi kufungwa kwa kubaka, na ambaye amefanyiwa mabadilko kadhaa ya uso, pua na viungo vingine kwa masaa 16. Aliongeza kwamba: “Hata nilipokuwa bondia nilikuwa natamani sana kuwa na matiti na nyeti za mwanamke.”
Iron Mike au Iron Maiden kama anavyojulikana sasa aliyasema hayo akiwa ametulia huku amevaa wigi la kike, suruali ya ‘jeans’ ya bluu na T-shirt yenye picha ya Vanessa Bruno ambapo alidokeza kwamba mara sehemu zote nyeti za kike zitakapojitokeza atawadhihirishia Wamarekani kwamba yeye si “mvulana mbaya” tena.
Amesema ameutunza uume wake ulioondolewa katika chupa ili kuwakumbusha wabaya wake waliokuwa wakimfanyia vitendo vya kuchukiza yeye na “wavulana wazuri” wengine huko gerezani.
Japokuwa wachambuzi wa masuala ya ndondi mwanzoni walishangazwa na maneno hayo ya Tyson, wengi wamekiri kwamba alama za yeye kupenda hivyo zilikuwepo.

Mtu Mmoja amesema kwamba: “Huko nyuma, alikuwa anapenda sana kuvaa sana glovu za kike, viatu virefu vya ngozi vya kike na magauni ya hariri, na pia alikuwa ni mtu mwenye kupenda sana heleni.” 


TYSON(MICHELLE) ENZI ZAKE ULINGONI

TYSON (KUSHOTO) AKIKABILIANA NA BRUNO (KUSHOTO)

SIKU TYSON ALIPOMNG'ATA SIKIO EVANDER

Tuesday, December 11, 2012

TAIFA QUEENS BINGWA WA MABARA WAICHAKAZA MALAYSIA KATIKA FAINALI

wachezaji wa timu ya taifa ya Netiboli, wakiwasili kwenye uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere, wakitokea Singapore walikokuwa wakishiriki mashindano ya mabara na kuibuka mabingwa. Hakika wanastahili pongezi
Taifa Queens ilipowasili nchini

Timu ya netiboli ya Tanzania (TAIFA QUEENS) imeibuka kidedea na kushinda mchezo wa fainali dhidi ya Malaysia kwa kuibanjua mabao 45-38. Kwa matokeo hayo Taifa Queens imetawazwa kuwa bingwa wa mabara kwa mwaka huu wa 2012 (IFNA Inter-Continental netball title). 
Mashindano hayo yaliyofanyika Nchini Singapore  ambayo bingwa mtetezi alikuwa Australia yameshuhudia Taifa Queens ikimaliza mashindano bila kupoteza mchezo hata mmoja. Mwenyekiti wa Chaneta Anna Bayi amesema mpaka timu zinaenda mapumziko tayari Taifa Queens walikuwa mbele kwa mabao 25-16, Waliporudi kipindi cha pili ilikuwa kumalizia kazi nzuri waliyoianza.

Timu hiyo imewasili nchini jana na kombe la mabara na medali za dhahabu na kuleta heshima mpya kwa Tanzania katika anga ya michezo, Ikumbukwe Taifa Queens ilitembeza bakuli balaa mpaka kufikia kuelekea Singapore huku wadau wenye kuweza kudhamini michezo wameng'ng'ania kupanda mbegu zisizoota kwenye mpira wa miguu, Wakati umefika wadau kuigeukia michezo mingine na huenda mungu akatujaalia kama jinsi nyota inavyoanza kuonekana katika sekta ya michezo nchini.

Hongereni sana Taifa Queens kwani mmetutoa kimasomaso na sasa Tanzania itaanza kutamkwa bila kung'atang'ata maneno katika anga za michezo duniani.

Taifa Queens wakifanya vitu vyao..wacha weeee..kalieni soka tu halafu tuone tutafika wapi!!

Weyee, Chezea Taifa Queens weweeee!!!

Sisi ndio sisi bhanaaaaa mtausaka kwa tochi hamuupati ngodo!

HAKUNA KAMA LEONEL MESSI

LIONEL Messi amevunja rekodi ya miaka 40, iliyowekwa na gwiji wa Ujerumani, Gerd Mueller baada ya kufunga mabao 86 ndani ya mwaka mmoja kwa klabu na timu ya taifa.
Mshambuliaji huyo wa Argentina alifunga mabao mawili na kuiongoza Barcelona kushinda 2-1 dhidi ya Real Betis Jumapili kwenye mchezo wa Ligi ya Hispania.






Bao lake la kwanza ni juhudi binafsi, alilifunga katika dakika 16 na kumfikia Mueller aliyeweka rekodi ya kufunga mabao 85 mwaka 1972, zikiwa zimebaki dakika tisa, Messi alifunga bao lake 86 mwaka huu.


"Kama ninavyosema wakati wote, ni vizuri kuweka rekodi hii, lakini jambo muhimu zaidi ni kuisaidia timu kushinda," alisema Messi. "Kila wakati nasema kazi yangu ni kuona timu inatwaa ubingwa wa Ligi Kuu, Ligi ya Mabingwa na Kombe la Copa del Rey."


Messi amefunga mabao 74 kwa Barcelona na 12 kwa timu yake ya taifa ya Argentina mwaka huu. Amebakiza michezo mitatu kabla ya kufunga mwaka huu na huenda akatengeneza rekodi mpya. Mueller alifunga mabao 85 akiwa na Bayern Munich na Ujerumani Magharibi.
Messi mwenye miaka 25 alivunja rekodi ya gwiji wa Brazil, Pele aliyeifungia Brazil na Santos mwaka 1958 mabao 75, lakini nyota huyo wa Argentina, Novemba 11 alivunja rekodi hiyo kwa kufunga bao la 75 na 76 na kuanza kuisaka rekodi ya Mueller.


Baada ya kuweka rekodi ya kufunga mabao 50, msimu uliopita, Messi ameiongoza Barcelona kuanza msimu huu kwa kishindo wakishinda mechi 14 na kutoka sare moja kati ya 15. Pia ameshafunga mabao 30 kwenye michuano yote aliyoichezea timu mpaka sasa.


"Hakuna mchezaji mwingine kama Messi," alisema kocha Barcelona, Tito Vilanova. "Siyo kwa sababu ya uwezo wake wa kufunga, lakini ni pamoja na ujuzi wake wa kutoa pasi, kuwatoka mabeki, na kuelewa mchezo kwa haraka."


Messi, ambaye Novemba 2 alikuwa baba wa mtoto wa kiume aitwaye Thiago, pia ametajwa kwenye wachezaji watatu wanaowania tuzo ya mwanasoka bora wa mwaka wa FIFA akiwa pamoja na Andres Iniesta na mshambuliaji wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo.
Messi ametwaa tuzo wa Ballon d'Or mara tatu mfululizo na kuisaidia Barcelona kutwaa ubingwa wa La Liga mara tatu, Ligi ya Mabingwa mara mbili na mataji mengi 10.


Pia, anategemewa kuwa mchezaji wa kwanza kuchukua tuzo ya mwanasoka bora wa dunia kwa mara ya nne. Mshindi atatangazwa Januari 7.

Monday, December 10, 2012

MAN CITY YAANGUKIA PUA MBELE YA MAN U


Rooney akishangilia goli la kwanza



Robin Van Persie
Mpambano mkali kati ya Man City waliowakaribisha Man U katika dimba la Ettihad ulimalizika kwa Man U kuwatambia Man City nyumbani kwao kwa kuwatatika bakora 3 kwa 2. Man City walifanya juhudi za makusudi kutaka kushinda lakini bahati haikuwa yao baada ya kuwa nyuma kwa magoli mawili mpaka dakika ya 59 pale Yaya Toure akiipatia Man City goli la kwanza kufuatia mawili ya Man United yaliyowekwa kimiani na Rooney katika dakika ya 15 na 28.
Alikuwa ni PJ Zabaleta alieisawzishia Man City katika dakika ya 85 kabla ya Robin Van Persie kupigilia msumari wa moto katika dakika ya 90 akipiga faulo maridadi iliyoelekea moja kwa moja kambani. Mpaka mwisho wa mtanange huo Wageni waliibuka kidedea kwa mabao 3 kwa 2 za wenyeji.

Yafuatayo ni matokeo ya mechi zilizopigwa weekend hii

Barclays Premier League | RESULTS


09 December
West Ham2 - 3  Liverpool
M Noble (pen 35)
S Gerrard (og 42)
G Johnson (10)
J Cole (75)
J Collins (og 78)
Upton Park Attendance (35005)
09 December
Everton2 - 1   Tottenham
S Pienaar (89)
N Jelavic (90)
CD Dempsey (75)
Goodison Park Attendance (36494)
09 December
Man City2 - 3Man Utd
Y Toure (59)
PJ Zabaleta (85)
W Rooney (15)
W Rooney (28)
R van Persie (90)
Etihad Stadium
08 December
Swansea3 - 4  Norwich
MPC Michu (50)
J de Guzman (58)
MPC Michu (90)
S Whittaker (15)
S Bassong (39)
G Holt (43)
R Snodgrass (76)
Liberty Stadium Attendance (20294)
08 December
Arsenal2 - 0   West Brom
M Arteta (pen 25)
M Arteta (pen 63)
Emirates Stadium Attendance (60083)
08 December
Wigan2 - 2   QPR
J McCarthy (18)
J McCarthy (73)
R Nelsen (25)
D Cisse (70)
The DW Stadium Attendance (17163)
08 December
Southampton  1 - 0  Reading
J Puncheon (60)
St. Mary's Stadium Attendance (29331)
08 December
Aston Villa0 - 0  Stoke
Villa Park Attendance (30110)
08 December
Sunderland1 - 3  Chelsea
A Johnson (65) FJS Torres (10)
FJS Torres (pen 45)
JMG Mata (48)
Stadium of Light Attendance (39273)

Man City 2-3 Man United

Arsenal 2-0 West Brom

West Ham 2-3 Liverpool

Swansea 3-4 Norwich