Monday, April 28, 2014

CHELSEA YAIVURUGA LIVERPOOL


Demba BA akifunga goli la kwanza.

Chelsea vijana wa darajani Stanford, jijini London, wamewanyamazisha vinara wa ligi kuu ya England, Liverpool baada ya kuwachakaza mabao 2-0 katika uwanja wao wa Anfield.

Liverpool ikiwa imeuanza mchezo huo kwa kasi na kwa dhamira ya kupata ushindi ilishuhudia jahazi lake likitota katika dakika ya 45 ya kipindi cha kwanza.


Ba akisujudu kuashiria kumtukuza muumba wake aliemuwezesha kutupia goli la kwanza



Jose Mourinho akishangilia ushindi

Alikuwa ni Demba Ba aliyeanza kupeleka kilio kwa majogoo wa Liverpool pale alipounasa mpira kufuatia nahodha wa Liverpool Steven Gerrard kuteleza na Ba kupata mwanya wa kumfunga kirahisi Mignolet.

Liverpool hawakukubali kusalimu amri kwa wageni,kwani waliendelea kupeleka mashumbulizi ya hatari langoni mwa wapinzani wao wakiishia kwa kosa kosa. Liverpool wanapigania ubingwa wa ligi kuu ya England kwa mara ya kwanza katika miaka 24 iliyopita.



Steven Gerrald haamini kilichotokea

Joe Allen na Luis Suarez walizidisha mashambulizi katika lango la Chelsea, kabla ya Willian aliyeingia kipindi cha pili kufunga bao la pili kwa timu yake ya Chelsea baada ya Fernando Torres bila uchoyo akiwa katika nafasi ya kufunga alimpasia Willian na kuwaachia kilio wenyeji wao Liverpool.

Chelsea katika mchezo huo ilikuwa ikipewa nafasi finyu ya kuibuka washindi. Lakini ni Jose Mourinho aliyeibuka na kicheko, huku Brendan Rodgers akiugulia kipigo cha kwanza kwa timu yake tangu kuanza kwa mwaka huu.

Kwa ushindi huo sasa, Chelsea inaachwa pointi mbili nyuma ya Liverpool ambayo inaoongoza ikiwa na pointi 80, baada ya michezo 36. Msimamo wa timu hizo ni Liverpool pointi 80, Chelsea 78, Manchester City 74, itakuwa na pointi 77 iwapo itaifunga Crystal Palace katika mchezo wao, huku Arsenal ikichukua nafasi ya nne ikiwa na pointi 70. Manchester City na Arsenal zimecheza mechi 35 kila moja huku Liverpool na Chelsea zikiwa zimecheza mchezo mmoja zaidi.


Luis Suarez chini ya ulinzi mkali


Heka heka langoni mwa Chelsea





Mashabiki chipukizi wa Liverpool hawaamini wanachokiona uwanjani


Wanaume kazini........Willian na Allen

 

 
LIVERPOOL 0-2 CHELSEA


Thursday, April 17, 2014

MELI YA WATU 400 ILIYOZAMA KOREA YA KUSINI MAWIMBI YAKWAMISHA UOKOZI

Mawimbi makali na hali mbaya ya hewa baharini imetatiza juhudi za utafutaji na uokoaji wa takriban watu mia tatu baada ya feri ya abiria kuzama katika pwani ya Korea Kusini.
Watu tisa wamethibitishwa kuaga dunia katika mkasa huo.
 
Wengi wa abiria kwenye meli hiyo walikuwa ni wanafunzi wa shule ya upili. Takriban watu mia moja sabini wameokolewa. Kapteni wa jeshi la wanamaji la Marekani Heidi C. Agle anashiriki katika operesheni ya uokoaji.
Ameiambia BBC kuwa maandalizi yanafanywa kupeleka mtambo wa kuinua chombo hicho.
Wakati huohuo Rais Park Geun-hye, amewataka waokozi kuharakisha juhudi zao za kuwatafuta manusura wa ajali hiyo.
Rais Park -- ambaye amejionea meli hiyo mwenyewe, amesema kuwa kila dakika ni muhimu katika kuhakikisha kuwa manusura wanapatikana.
Wapiga mbizi wamekuwa wakikabiliana na mawimbi makali kujaribu kukifikia chombo hicho kilichozama hapo jana.
 
Duru zinasema kuwa meli hiyo ilipoteza mwelekeo huku baadhi ya familia za waathriwa zikihoji mwenendo wa nahodha wa meli.
Hata hivyo nahodha huyo Lee Joon-seok aliomba msamaha na kusema ana majuto tele na kuwa hata hajui la kusema.
Dauru zinseama kuwa miongoni mwa wliofariki ni wanafunzi wanne wenye umri wa miaka 17 na mwaliamu wao mwenye umri wa miaka 25 pamoja na mfnyakazi mmoja wa meli hiyo.
Wengine wlaiofariki bado hawajatajwa.
Takwimu za hivi karibuni zinasema kuwa wtu 475 walikuwa kwenye meli hiyo huku 287 wakiwa bado hawajapatikana.
 












 


REAL MADRID YATWAA KOMBE LA MFALME..BARCELONA YELEEEEWIII

Timu ya Real Madrid Wamefanikiwa kutwaa kombe la Copa del Rey 2014/2015 .

Madrid waliwacharaza wapinzani wao wa jadi katika ligi ya nyumbani La liga Barcelona mabao 2 kwa 1 katika fainali iliyochezwa jana mbele ya mfalme wa Uhispania .
Kocha wa Madrid Carlo Ancelotti alikuwa anajikuna kichwa kwani mshambulizi wake nyota Cristiano Ronaldo hakuwa uwanjani kutokana na jeraha la mguu na hivyo ikambidi kumchezesha mshambulizi aliyegharimu kitita kikubwa
zaidi msimu huu Gareth Bale .
Na alidhibitisha udedea wake alipofuma bao la ushindi zikiwa zimesalia dakika tano tu mechi hiyo kukamilika na hivyo kuisadia kutwaa taji lake la 19 la Kombe hilo la mfalme la Copa del rey.
Real Madrid ilidhibitisha niya yao mapema kwa bao la dakika ya 11 Angel Di Maria .

 
 
Bale akishangilia goli la pili lililoipa ubingwa Madrid
 

Modric akioneshana kazi na Iniesta

Lakini ikasawazishwa na bao la Bartra katikadakika ya 68 ya kipindi cha pili.
Bao la ushindi lilifungwa na Gareth Bale dakika tano tu kabla ya mechi hiyo kukamilika .
Bale alitimuka mbio na kumpiku mlinzi wa Barca Marc Bartra katikati ya kiwanja na akafululiza hadi akampiga chenga kipa machachari Jose Manuel Pinto na kuihakikishia Madrid ushindi.
Real Madrid bado iko mbioni kuwania kombe la ligi ya Uhispania, ambapo inashikilia nafasi ya pili na alama 79 alama tatu nyuma ya wakinzani wao Athletico Madrid.
Barcelona ambayo imekuwa ikishuhudia msururu wa matokeo yasiyo ya kuridhisha katika siku za hivi punde inafunga orodha ya tatu bora ikiwa na alama 78.
Madrid sasa inamuda wa kutoka kujiandaa kwa mechi ya nusu fainali ya kombe la mabingwa barani Ulaya dhidi ya mabingwa watetezi Bayern Munich ya Ujerumani.
Mechi nyingine ya nusu fainali ya kombe la mabingwa barani Ulaya itakuwa kati ya Chelsea ya Uingereza dhidi ya Atletico Madrid.
Nusu fainali hizo zitachezwa juma lijalo.
 
Ubabe na undava kama kawa kama dawa




Mwaka wa shetani..duuu hatuambilii chochote
 
BARCELONA 1-2 MADRID

Thursday, April 10, 2014

BARCELONA, MAN U ZATUPWA NJE UEFA

Matumaini ya timu ya Manchester United kufanya maajabu katika ligi ya mabingwa barani Ulaya, UEFA yaliyeyuka jana usiku wa Jumatano baada ya kupokea kipigo kutoka kwa mabingwa watetezi wa michuano hiyo, Bayern Munich ya Ujerumani cha magoli 3-1.
Hayo yalikuwa ni matokeo ya mchezo wa marudiano baada ya mechi ya kwanza iliyochezwa katika uwanja wa Old Trafford, timu hizo kutoka sare ya magoli 1-1.
 
Patrice Evra akishangilia bao alilotupia
 
Mandzukic akishangilia baada ya kusawazisha goli
 
 Kikosi cha kocha David Moyes, kilionekana kingebadili matokeo hayo na kupenya hatua ya nusu fainali baada ya beki wa kushoto wa Manchester United Patrice Evra kuukwamisha mpira kimiani kufuatia kombora kali alilolimimina katika lango la Bayern na kuifanya timu yake iongoze katika dakika ya 57 ya mchezo.
Hata hivyo furaha ya Manchester Ilizimwa kabla hawajakaa vitini  dakika ya 59 mshambuliaji wa Bayern, Mario Mandzukic aliisawazishia timu yake kwa mpira wa kichwa.
Vijana wa Bayern walizidisha mashambulio katika lango la Manchester United na juhudi zao zilizaa goli katika dakika ya 68 lililofungwa na Tomas Muller.
 
Pisha njiaaa.. Robben akijaribu kumpita Evra

Arjen Robben alihitimisha safari ya Manchester United baada ya kukwamisha goli la tatu katika dakika ya 76 na kuifanya Bayern Munich kusonga mbele kwa jumla ya mabao 4-2.
UEFA inatarajia kupanga makundi mawili ya timu nne zilizofuzu kucheza hatua ya nusu fainali.
Timu hizo ni Bayern Munich mabingwa watetezi ya Ujerumani walioitoa Manchester United, Atletico Madrid ya Hispania ikiwaondoa Barcelona pia ya Hispania, Real Madrid nayo ikiindoa katika michuano hiyo Borrusia Dortmund ya Ujerumani na Chelsea ya Uingereza ikiisambaratisha PSG ya Ufaransa.



Mfungaji wa goli pekee na la ushindi la Atletico lililoiondoa Barcelona UEFA


Tulia wewe mtoto wa mama...Neymar chini ya ulinzi mkali


David Villa akishangilia kuiondosha Barcelona katika michuano ya UEFA

 


Yeleewiii tumetolewa hivihivi

 
ATLETICO MADRID 1-0 BARCELONA


 
BAYERN MUNICH 3-1 MAN UTD



Thursday, April 3, 2014

UEFA PSG YAICHARAZA CHELSEA, REAL MADRID YAITANDIKA DORTMUND

Kocha wa Chelsea Jose Mourinho ametangaza wazi kuudhika sana na safu yake butu ya mashambulizi.
Mourinho aliyasema hayo punde baada ya kushuhudia PSG ya Ufaransa ikiititima 'the blues' mabao matatu kwa moja katika mkondo wa kwanzawa mechi ya robo fainali ya kombe la mabingwa Barani Ulaya.
 
Wayaaaaaaaa
 
Laveziiiii wayaaaaaaaaaaaa

Wenyeji PSG waliweka wazi ari yao ya kusonga mbele baada ya dakika pekee kupitia kwa Ezequiel Lavezzi .
Vijana wa Jose Mourinho nao wakajifurukuta na kufanya mashambulizi ambayo yalizaa penalti baada ya Oscar kuchezewa visivyo katika eneo la lango.
Eden Hazard akafanya mambo kuwa 1-1 katika dakika ya 27.
Nipe nikupe iliendelea hadi kipindi cha pili PSG walipofaidika na bao la kujifunga mwenyewe la David Luiz kunako dakika ya 61.
Hawakukomea hapo ,Javier Pastore alihakikisha Chelsea itakuwa na mlima wa kupanda nyumbani kwao Stamford Bridge katika mkondo wa pili mbali na kuibua kumbukumbu za mwaka wa 2004 timu hizo
mbili ziliposajili matokeo sawia na hayo PSG ilipokuwa mbioni kucheza katika fainali ya kombe la mabingwa .
Aidha mechi ya kwanza kwa mkufunzi Jose Mourinho alipochukua hatamu Stamford bridge ilikuwa dhidi ya Paris St-Germain mwezi September 2004.
Wakati huo The Blues waliwatandika PSG 3-0 John Terry na Didier Drogba wakiandikisha majina yao katika orodha ya wafungaji.
 
Ibrahimovic akiwanjonjofya wachezaji wa Chelsea
 
Mwamuzi na wachezaji wa PSG wakimuangalia Zlatan Ibrahimovic baada ya kutengenezwa na Ramires.

Hatoki mtu hapa.....Ibrahimovic akioneshana udamwidambwi na David Luiz

ThiagoSilva na Torres hakatwi mtu hapa

We bwege tuuu......mwamuzi wa pembeni akiwahi mpambano kati ya Cavani na Luiz

''Mhhh hali tete'' Kocha wa Chelsea Jose Mourinho akiduwazwa na matokeo.

REAL MADRID Vs DORTMUND

 Vigogo wa ligi kuu ya Uhispania ambao wamekuwa wakisuasua katika mechi za la liga Real Madrid, wamedhibitisha udedea wao katika ligi ya mabingwa bara Uropa baada ya kuiadhibu vikali Borussia Dortmund ya Ujerumani katika mkono wa kwanza wa robo fainali ya mchuano huo iliyochezwa Santiago Bernabeu.
Real iliilaza Borussia Dortmund mabao matatu kwa Ubuyu .
Real ilidhihirisha nia yao mapema Gareth Bale alipofuma bao la kwanza kunako dakika ya tatu ya mechi hiyo.
 
 
Bale akitupia kambani bao la kwanza
 
CR9 akishangilia baada ya kutengeneza kamba ya pili

Isco alitikisa wavu na bao la pili katika dakika ya 27, huku bao la tatu likifungwa naye Cristiano Ronaldo dakika ya 57 kipindi cha pili.
Bao hilo la mchezaji bora msimu wa 2013 lilimsaidia Ronaldo kusawazisha rekodi ya idadi kubwa ya mabao kuwahi kufungwa kwa msimu mmoja wa dimba hilo la mabingwa barani Uropa.
Bao la Ronaldo lilikuwa la 14 katika mechi nane za ligi ya mabingwa , sawia na rekodi iliyowekwa na Lionel Messi katika mwaka wa 2011-2012.
Kwa upande wao Dortmund ambao walishindwa katika fainali mwaka uliopita na Bayern Munich watajilaumu wenyewe kwa kutotumia vyema fursa 12 walizopata kushambulia lango la Real.
Hata hivyo vijana hao wa Jurgen Klopp walidhihirisha wazi bila nyota wao Robert Lewandowski safu yao ya ushambulizi ni butu.
Wajerumani hao wanajuma moja tu kusahihisha makosa walioyafanya jana kabla ya mechi ya marudio ambayo imeratibiwa kuchezwa tarehe 8 Aprili huko ujerumani.


Namie nimooooooooooooo...Isco akishangilia goli pamoja na Bale
 
Safi sana dogo, CR9 akimpongeza Isco

Msifikiri nimefurahi naumiaaaaaaaaa...kocha wa Borussia Dortmund
 
PSG 3-1 CHELSEA
 
REAL MADRID 3-0 DORTMUND