Wednesday, December 10, 2014

KLABU BINGWA ULAYA ARSENAL YATINGA 16 BORA KWA KISHINDO

Club ya Arsenal imefanikiwa kumaliza katika nafasi ya pili ya kundi D ,Ligi ya Mabingwa Ulaya na kutinga hatua ya kumi na sita bora ya michuano hiyo ,kufuatia ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya wenyeji Galatasaray wa nchini Uturuki.
Lukas Podolski aliifungia the Gunners bao la kwanza katika dakika ya tatu ,kabla ya Aaron Ramsey kufunga bao la pili katika dakika ya 11 na la tatu katika dakika ya 29.
Kiungo mkongwe wa Uholanzi Wesley Sneider aliifungia Galatasaray bao la kufutia machozi kwa shuti la mpira wa adhabu katika dakika ya 87 ,kabla ya Podolski kufunga goli la nne kwa Arsenal katika dakika ya 90 .
Mechi nyingine ya kundi hilo ni Borussia Dotmund imetoka sare ya bao moja kwa moja na timu ya Anderlecht ya Ubelgiji .
Ramsey akitupia kambani bao la pili
 
 Lucas Podolski muuaji wa jana 



 

Wednesday, November 26, 2014

HAYA NDIO MAJINA YA MAFISADI WALIOKULA FEDHA ZA ESCROW


Mh Zitto Kabwe akisoma ripoti ya ESCROW Bungeni jioni ya leo

HAYA NDIO MAJINA YA WALIOKULA FEDHA ZA AKAUNTI YA ESCROW KATIKA RIPOTI YA PAC INAYOSOMWA SASA BUNGENI.
Zitto: Upande wa viongozi wa kisiasa ambao waliingiziwa fedha katika akaunti zao binafsi ni; Mhe.
Andrew Chenge (Mb)
Zitto: Andrew Chenge aliingiziwa shilingi bilioni 1.6.
Zitto: Mhe. Anna Tibaijuka (Mb) na Waziri wa 62
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi shilingi bilioni 1.6.
Zitto: Mhe.William Ngeleja (Mb) na ambaye alikuwa Waziri wa Nishati na Madini alipewa shilingi milioni 40.4
Zitto: Ndg. Daniel N. Yona ambaye alikuwa pia Waziri wa Nishati na Madini alipewa shilingi milioni 40.4.
Zitto: Ndg. Paul Kimiti ambaye ni Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Sumbawanga
alipewa shilingi milioni 40.4
Zitto: Dr. Enos S. Bukuku ambaye alikuwa Mjumbe wa Bodi ya TANESCO aliingiziwa shilingi milioni 161.7.
Zitto: Upande wa Majaji Prof. Eudes Ruhangisa, aliingiziwa milioni 404.25 na J.A.K Mujulizi aliingiziwa shilingi milioni 40.4
Zitto: kwa upande wa Watumishi wa umma,Ndg. Philip Saliboko ambaye alikuwa mtumishi wa RITA aliingiziwa
shilingi milioni 40.4
Zitto: Ndg. Emmanuel Daniel Ole Naiko ambaye
alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa (TIC) aliingiziwa shilingi milioni 40.4
Zitto: Ndg. Lucy L. Appollo ambaye ni Mtumishi wa TRA aliingiziwa shilingi milioni 80.8.
Zitto: Viongozi wa Madhehebu ya
Dini walioingiziwa fedha na Benki ya Mkombozi ni Askofu 63
Methodius Kilaini shilingi 80.9
Zitto: Askofu Eusebius Nzigirwa shilingi milioni 40.4 na Mchungaji Alphonce Twimann Ye Simon shilingi milioni 40.4.
Zitto: Watu walienda kugawana fedha kwenye Benki tajwa wakiwa na mifuko ya rambo, sandarusi,
mabox, magunia na lumbesa TegetaEscrow
Zitto: Bilioni 73.5
zilitolewa na kugawanywa kwa watu mbalimbali kinyume cha
Sheria ya Benki Kuu na Taasisi za Fedha ya 2006
Zitto: Taarifa
ya benki (bank statements) yenye majina na akaunti zote
zilizoingiziwa fedha zimeambatishwa.

KLABU BINGWA ULAYA CHELSEA YATOA DOZI NZITO, MAN CITY PAPACHUPAPACHU

 
 Wachezaji wa Chelsea wakishangilia goli

Usiku wa kuamkia leo kindumbwe ndumbwe cha michuano ya Klabu Bigwa barani Ulaya kiliendelea na kushuhudia Chelsea ikitoa kipigo cha mbwa mwizi mbele ya mashabiki wa Schalke 04 ya Ujuremani pale ilipoishindilia magoli 5 bila majibu.
Manchester City ya England nao wakawabamiza wababe wengine wa Ujerumani Bayern Munich kwa kwa kuwafunga magoli 3 - 2 na kufufua matumaini ya kusonga mbele katika michuano hiyo huku magoli yote matatu ya Man City yakitiwa kimiani Sergio Aguero.
Katika mechi nyingine Paris St. Germain ya Ufaransa waliwashikisha adabu Ajax ya Uholanzi kwa kuifunga magoli 3 - 1 huku Becelona kwa upande mwingine wakiisasambua Apoel Nicosia ya Syprus kwa kuishushia kichapo cha magoli 4 kwa yai.
CSKA Moscow ya Urusi na AC Roma zikatoka suluhu ya goli moja 1 - 1
Burudani hiyo itaendelea leo ambapo Liverpool ya England baada ya kufanya vibaya katika mechi zilizotangulia leo wanajaribu bahati yao wakiwa ugenini dhidi Ludogorets ya Bulgaria.
Arsenal nao watawakaribisha Borusia Dortmud ya Ujerumani huku vita vingine vikiwa ni kati ya FC Basel ya Uswis watakaopopepetana na Real Madrid. Malmo FF ya Sweden watakuwa wenyeji wa Juventus ya Italia
 
SHAKHTAR 5-0 CHELSEA

Friday, October 31, 2014

RAIS WA BURKINA FASO APIGWA CHINI

 
Rais alieenguliwa madarakani nchini Burkina Faso, Campaore

Msemaji wa jeshi amewaambia waandishi wa habari mjini Ouagadougou kuwa bwana Compaore hayuko mamlakani tena.
Rais Compaore alikuwa ametangaza kuwa atajiuzulu baada ya kipindi cha serikali ya mpwito ya mwaka mmoja .
Lakini wanasiasa wa upinzani wakakataa kata kat kuendelea kwa utawala wake na wakamtaka ajiuzulu maramoja.
Rais Compaore alikuwa ameongoza kwa zaidi ya miaka 27 tayari.
Kumeripotiwa maandamano mapya nchini Burkina Faso ya kutaka kujiuzulu mara moja kwa rais wa nchi hiyo Blaise Compaore.
Viongozi wa upinzani wanakutana kwenye mkji mkuu Ouagadougou kukubaliana kwa pamoja hatua watakazochukua.
Siku ya Alhamisi waandanamaji walikarisishwa na jitihada za rais za kuongeza kipindi chake chake miaka 27 madarakani na wakateketeza bunge na kusaka kituo cha runinga cha serikali.


Bwana Compaore alitupilia mbali jitihada za kubadilisha katiba ambayo ingemruhusu kuwania tena muhula mwingine kama rais lakini akasema kuwa atabaki madarakani kwa mwaka moja zaidi .
<span >Viongozi wa Upinzani Nchini Burkina Faso wamewaomba waandamanaji kutolegeza kamba bali kuendelea na maandamano huku wakimtaka Rais Blaise Campaore ang'atuke mamlakani mara moja.
Licha ya Rais Compaore wa Burkina Faso kuhutubia taifa siku moja baada ya vurugu kubwa na kutangaza kuvunja serikali waandamanaji hawataki kusikia kwamba apewe muda wa mwaka mmoja ndipo aondoke madarakani.
Jana jioni kiongozi wa Jeshi Jeneral Honore Traore alitangaza kuundwa kwa serikali ya mpito itakayodumu kwa kipindi cha mwaka mmoja japo hakusema itaongozwa na nani.
 
Wananchi wa Burkina Faso wakiwa katika maandamano

Monday, October 27, 2014

NAHODHA WA BAFANABAFANA AUAWA KWA RISASI


Senzo Meyiwa enzi za uhai wake

Nahodha ambaye pia ni golikipa wa timu ya soka ya taifa la Afrika kusini Senzo Meyiwa amefariki dunia baada ya kupigwa risasi. Jeshi la polisi la nchi hiyo limesema.
Tukio hilo limeripotiwa kutokea katika nyumba ya mpenzi wake iliyopo katika mji wa Vosloorus kusini mwa Johannesburg.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 aliichezea klabu ya Orlando Pirates na alicheza mechi nne zilizopita za timu yake ya taifa katika mechi za kufuzu za fainali ya mataifa ya Afrika.
Jumamosi alikuwepo katika tukio la timu yake pindi waliposonga mbele katika nusu fainali ya ligi ya Afrika kusini.
Katika maelezo yake Jeshi la polisi la afrika kusini limesema kwamba Meyiwa ameripotiwa kufariki wakati akiwasili hospitalini.
 
Senzo enzi za uhai wake akifanya vitu uwanjani







Marehemu Senzo akinyaka mpira Bafanabafana ilipoumana na Nigeria

MAN UTD YAIVIMBIA CHELSEA ZATOKA SARE

Mashabiki wa soka wakijiandaa kuingia kushuhudia mpambano

Haikuchukua muda mwingi punde tu baada ya kuanza kwa kipute hicho, mchezaji mkongwe Didier Drogba akawainua mashabiki wa Chelsea baad ya kufunga goli zuri la kichwa.
Goli hili liliweza kudumu hadi dakika za nyongeza za mchezo huo na kuwapa matumaini mashabiki wa timu hiyo kuamini kuwa wangekusanya point zote tatu kutoka kwa Man U.
Dakika ya 93 ya mchezo Mholanzi Robin van Persie akawainua mashabiki wa timu yake pamoja na kocha wake Louis van Gaal baada ya kuisawazishia timu yake kwa shuti kali la guu la kushoto na kufanya matokeo kuwa ni sare ya 1-1 mpaka kipyenga cha mwisho.
Baada ya kupata goli la dakika za lala salama Kocha Louis Van Gaal hajafurahishwa na timu yake ya Manchester United japokuwa vijana hao wa Old Trafford wameweza kuondoka na point moja muhimu katika mchezo dhidi ya Chelsea uliochezwa katika dimba la Old Trafford. '' hatujatumia faida ya kuwa nyumbani na tungeweza kushinda mchezo huu'' alisema Mholanzi huyo.
Goli la kichwa la Didier Drogba liliisaidia Chelsea kushika usukani katika mchezo huo kabla ya Robin van Persie kusawazisha na kuwasaidia vijana
 
Didier Drogba akitupia kambani kwa kichwa goli la kuongoza


Drogba akishangilia


Niacheni jamaniii hapa kazi tuuu

Di Maria akimhadaa Willian


 
Van Persie akitupia goli la kusawazisha


Wachezaji wa Man Utd wakishangilia goli ka kusawazisha dhidi ya Chelsea

Kocha wa Chelsea Jose Mourinho akisalimiana na kocha wa Man Utd Van Gaal

 
MAN UTD 1-1 CHELSEA