Wednesday, July 27, 2011

BATISTA ATIMULIWA ARGENTINA

Sergio Batista amekubali kuacha ukocha wa timu ya taifa ya Argentina baada ya nchi hiyo kutolewa hatua ya robo fainali ya kuwania kombe la Copa America.

Sergio Batista
Wenyeji Argentina walitolewa na mabingwa Uruguay kwa mikwaju ya penalti.
Batista, mwenye umri wa miaka 48, amekuwa akiifundisha Argentina kwa mwaka mmoja sasa, awali akiwa kocha wa muda, baada ya Diego Maradona kutimuliwa kufuatia kutolewa katika Kombe la Dunia mwaka 2010.
Msemaji wa Chama cha Soka cha Argentina (AFA) amesema Batista hajatimuliwa, lakini imeamuliwa "kutengua" mkataba wake.
Argentina, ambayo mara ya mwisho kunyakua kombe muhimu ilikuwa mwaka 1993 waliposhinda mashindano ya Copa America, wamefuta mechi ya kirafiki dhidhi ya Romania mjini Bucharest iliyopangwa kuchezwa tarehe 10 mwezi wa Agosti.
"Makocha wa Argentina kwa viwango vyote wanafanyiwa tathmini na tume ta makocha wa taifa," aliongeza Bialo.
"Hakuna muda maalum uliowekwa, hakuna sababu ya kuharakisha kumchagua kocha mpya, kwa hiyo kuna mchakato wa kuwasoma na kuwafikiria makocha."

BECKHAM AMTETEA BALOTELLI

David Beckham amemtetea Mario Balotelli kutokana na utata uliojitokea wakati akiwa karibu na lango alipoupiga mpira kwa kisigino badala ya kufunga, hali iliyomsabababishia atolewa nje na meneja wake wakati Manchester City ilipopambana na LA Galaxy.

Balotelli

Meneja wa Manchester City Roberto Mancini alihoji umahiri wa mchezaji huyo baada ya makusudi kukataa kufunga bao la wazi.
"Niliangalia tena, kutokana na tabia yake, naamini alidhani alikuwa ameotea," alisema Beckham, huku akimshauri Balotelli aendelee kufunga katika mechi zijazo.
"Mario amekuwa mchezaji hodari kwa miaka michache iliyopita na bado ni kijana mdogo sana."
Nahodha huyo wa zamani wa England, ambaye aliwahi kuichezea Manchester United ambao ni mahasimu wakubwa wa Manchester City, ameongeza: "Ataendelea kurjirekebisha, nina hakika.
"Lakini iwapo unadhani umeotea au la, hiyo haina maana. Kuna vijana wengi wadogo wanaziangalia hizi timu na wachezaji nyota waliokuja hapa.. Ni lazima uoneshe umahiri wako an ufunge bao."
Mancini, ambaye alizozana na Balotelli wakati akitoka uwanjani baada ya dakika 31, amesisitiza mshambuliaji huyo alipokuwa Inter Milan na yeye akiwa meneja wake alijua hakuwa ameotea.
"Katika soka kila wakati unatakiwa kuonesha umahiri, kila wakati unakuwa makini na kwa wakati ule hakuwa makini na hakuonesha umahiri wake," alisema.

Tuesday, July 26, 2011

RATIBA LEAGUE 1 (UFARANSA) AGOSTI 6-14


Saturday 6th August
20:00AC Ajaccio vs Toulouse
20:00AS Nancy vs Lille
20:00Brest vs Evian TG
20:00Caen vs Valenciennes
20:00Marseille vs Sochaux
20:00Montpellier vs Auxerre
20:00Nice vs Lyon
20:00PSG vs Lorient
Sunday 7th August
16:00Dijon vs Rennes
20:00Bordeaux vs St Etienne
Saturday 13th August
18:00Lorient vs Bordeaux
18:00Lyon vs AC Ajaccio
18:00Rennes vs PSG
18:00Sochaux vs Caen
18:00St Etienne vs AS Nancy
18:00Toulouse vs Dijon
20:00Valenciennes vs Brest
Sunday 14th August
16:00Auxerre vs Marseille
16:00Evian TG vs Nice
20:00Lille vs Montpellier

RATIBA BUNDESLIGA AGOSTI 5-AGOSTI 20


Friday 5th August
19:30Borussia Dortmund vs Hamburg
Saturday 6th August
14:30Augsburg vs SC Freiburg
14:30Cologne vs Wolfsburg
14:30Hannover 96 vs TSG Hoffenheim
14:30VfB Stuttgart vs Schalke 04
14:30Werder Bremen vs FC Kaiserslautern
17:30Hertha Berlin vs Nurnberg
Sunday 7th August
14:30Mainz vs Bayer Leverkusen
16:30Bayern Munich vs Borussia M'gladbach
Saturday 13th August
14:30Hamburg vs Hertha Berlin
14:30Nurnberg vs Hannover 96
14:30SC Freiburg vs Mainz
14:30Schalke 04 vs Cologne
14:30TSG Hoffenheim vs Borussia Dortmund
14:30Wolfsburg vs Bayern Munich
17:30Borussia M'gladbach vs VfB Stuttgart
Sunday 14th August
14:30FC Kaiserslautern vs Augsburg
16:30Bayer Leverkusen vs Werder Bremen
Friday 19th August
19:30Borussia M'gladbach vs Wolfsburg
Saturday 20th August
14:30Augsburg vs TSG Hoffenheim

HOFFENHEIM KUIPIKU CELTIC KUMSAJILI MUSONA TOKA KAIZER CHIEFS

Timu ya Hoffeinheim ya Ujerumani ina matumaini makubwa ya kuizidi kete klabu ya Celtic ya Uskotchi katika mbio za kumuwania mshambuliaji mzimbabwe Musona mwenye umri wa miaka 21 anaekipiga Kaizer Chiefs ya kusini mwa afrika.
Musona
Katika ligi ya Afrika ya kusini iliyoisha Musona aliweka rekodi ya kufunga magoli 15 katika mechi 28 alizocheza katika ligi hiyo na kishawishi Celtic kutangaza ofa ya dau la paundi za Uingereza 2.2 milioni ili kumsajili mchezaji huyo. Lakini wajerumani wanaona Musona ndio chaguo sahihi katika kuziba pengo la Mghana Prince Tagoe waliemtoa kwa mkopo kwenda Partizan Belgrade baada ya kutofanya vizuri tangu alipojiunga na timu hiyo mwaka 2009 akiwa amefunga magoli mawili tu katika mechi 19 alizocheza katika ligi hiyo ya Ujerumani maarufu kama "Bundesliga" Ingawaje matumaini ya kumnasa Musona yanaweza kufifia kutokana na ukweli kuwa timu ya Hoffeinheim imetangaza dau dogo la paundi za Uingereza 1.3 milioni ukilinganisha na dau lililotolewa na Celtic la paundi za uingereza 2.2 milioni.

MAGOLI YA FAINALI COPA AMERICA URUGUAY ILIPOINYANYASA PARAGUAY

Suarez, Forlan waonesha viwango.

MANCINI ANA MATUMAINI YA KUMNASA SERGIO AGUERO

Meneja wa Man City Roberto Mancini amefunguka na kusema kuwa ana matumaini makubwa ya kumnasa Sergio Aguero kutoka Atletico Madrid mwishoni mwa wiki hii. Man C inafungua milango ya maongezi na Atletico Madrid kwa kuwa Srgio amekuwa ni mmoja kati ya wachezaji anaowahitaji katika kikosi chake.
Sergio Aguero
Pamoja na upinzani uliopo kutoka kwa Real Madrid na Juventus ambao nao wanatajwa kumuwania Sergio lakini Mancini ana matumaini ya kushinda kinyang'anyiro hicho mwishoni mwa mwezi huu."Sielewi kwa sasa lakini ninachojua Atletico walikuwa na maongezi na Sergio kabla ya mwisho wa wiki" alisema Mancini.
"Nafikiri kati ya siku nne au tano kabla ya mechi inayofuata,na inaweza kuwa wiki hii tukamaliza mazungumzo"Alioneza Mancini.
"Aguero amecheza Copa America, kama tukikubalina nataka nizungumze nae mwenyewe kwasababu nataka nijue maoni yake(kuhusu kucheza Manchester City)" Alifunguka zaidi kocha huyo wa Manchester City.