Reese Witherspoon akitimbwirika maeneo ya Hawaii
Sunday, August 28, 2011
Friday, August 26, 2011
Mwanadada Eva Carneiro daktari mpya wa Chelsea
Eva Carneiro akiwa katika benchi la Chelsea
Drogba akikatiza katika Benchi la Chelsea kushoto anaonekana Daktari wa timu mwanadada Eva, sasa sijui Drogba ndio anauza sura kwa kujipitisha ili aopoe?
Benchi la wachezaji wa akiba la Chelsea kushoto kocha Ferreira na kushoto mwisho mwanadada daktari Eva Carneiro
Tetesi za usajili Majuu zilizotoka hivi punde
Juventus yamuwania Malouda
Mkurugenzi wa Juventus Giussepe Marota ameeleza waziwazi juu ya kumhitaji Malouda katika kikosi chake, kama wakikubaliana watamchukua Malouda mwenye miaka 31 kwa kitita cha paundi za uingereza milioni 5.
Alvaro Perreira kutua Chelsea
Wakati wanatarajia kumuuza Malouda Chelsea wametangaza kuongeza dau kumnasa mchezaji wa Porto ambaye ni raia wa Uruguay Alvaro Perreira, baada ya Porto hapo awali kukataa kitita cha paundi za uingereza milioni 16.6 na sasa wapo tayari kuongeza dau kumnasa Perreira.
Emanuele Giacherini atua Juventus
Juventus imefanikiwa kumnyaka Emanuelle 26, kutoka klabu ya Cesena na hivi sasa yupo Turin akifanyiwa vipimo vya afya.
Mkurugenzi wa Juventus Giussepe Marota ameeleza waziwazi juu ya kumhitaji Malouda katika kikosi chake, kama wakikubaliana watamchukua Malouda mwenye miaka 31 kwa kitita cha paundi za uingereza milioni 5.
Alvaro Perreira kutua Chelsea
Wakati wanatarajia kumuuza Malouda Chelsea wametangaza kuongeza dau kumnasa mchezaji wa Porto ambaye ni raia wa Uruguay Alvaro Perreira, baada ya Porto hapo awali kukataa kitita cha paundi za uingereza milioni 16.6 na sasa wapo tayari kuongeza dau kumnasa Perreira.
Emanuele Giacherini atua Juventus
Juventus imefanikiwa kumnyaka Emanuelle 26, kutoka klabu ya Cesena na hivi sasa yupo Turin akifanyiwa vipimo vya afya.
LEONEL MESSI MCHEZAJI BORA ULAYA 2011-2012 Xavi namba 2, Ronaldo aambulia kura 2
MESSI
Leonel Messi mshambuliaji wa kutisha na kuogopwa wa F.C Barcelona ya Spain ameibuka kidedea na kuwa mchezaji bora zaidi wa soka barani ulaya 2011-2012.
Messi alitangazwa mshindi baada ya droo iliyofanyika Monaco kupanga makundi ya klabu bingwa ulaya 2011-2012, katika kinyang'anyiro hiko Messi aliwapiku Xavi kwa kura 11 na kuwa wa pili huku akimzidi Christian Ronaldo wa Real Madrid aliyekuwa wa tatu kwa kura nyingi ambapo Ronaldo aliambulia kura tatu tu.
Matokeo yalikuwa kama ifuatavyo;
1 Lionel Messi (ARG) – FC Barcelona (39 votes)
2 Xavi Hernández (ESP) – FC Barcelona (11 votes)
3 Cristiano Ronaldo (POR) – Real Madrid CF (3 votes)
4 Andrés Iniesta (ESP) – FC Barcelona
5 Falcao (COL) – ex FC Porto (Club Atlético de Madrid)
6 Wayne Rooney (ENG) – Manchester United FC
7 Nemanja Vidić (SRB) – Manchester United FC
8 Zlatan Ibrahimović (SWE) – AC Milan
Gerard Piqué (ESP) – FC Barcelona
10 Manuel Neuer (GER) – ex FC Schalke 04 (FC Bayern München)
Fainali UEFA Super Cup ni BARCELONA vs F.C PORTO leo
Leonel Messi mchezaji bora wa ulaya 2011-2012
Fainali ya UEFA super Cup Leo inawakutanisha wababe wawili yaani Barcelona ya Spain na F.C Porto. Mchezo huo utakaopigwa leo 26 agosti 2011 majira ya saa 18:45-20:45 GMT katika dimba la Stade Louis II jijini Monaco.
Barcelona bingwa mtetezi wa kombe hilo anakutana na bingwa wa ligi ya ulaya F.C Porto, Barcelona imeshachukua kombe hilo mara 3 wakati F.C Porto wamelinyaka mara 1 tu, Barcelona ni ya 2 kwa ubora ulaya 2011-2012 na F.C Porto ni ya 7 kwa takwimu za Shirikisho la soka la ulaya(UEFA).
Katika mechi hiyo timu zinatarajiwa kupangwa kama ifuatavyo;
FC Barcelona :
David Villa, Lionel Messi, Victor Valdes, Adriano Correia, Daniel Alves; Sergio Busquets, Xavi Hernandez, Andres Iniesta, Eric Abidal, Javier Mascherano, Pedro Rodriguez.
FC Porto :
Helton,Fucile, Souza, Joao Mourinho, Freddy Guarin, Alvaro Pereira, Rolando, Otamendi, Varela/James Rodriguez, Kleber, Hulk.
MAKUNDI KLABU BINGWA ULAYA MAN CITY KUNDI LA KIFO, ARSENAL USO KWA USO NA MARSEILLE, MAN UNITED NA BENFICA, CHELSEA NA VALENCIA
Katika droo iliyochezeshwa jana kupanga timu katika hatua ya makundi Timu ya Man City ndio inatajwa kuwa katika kundi la kifo ikikutana na Bayern Munich ya Ujeruman,Villareal ya Spain na Napoli ya Italia. Makundi yako kama ifuatavyo;
Group A:
Bayern Munich, Villarreal, Manchester City, Napoli.
Group B:
Inter Milan, CSKA Moscow, Lille, Trabzonspor.
Group C:
Manchester United, Benfica, Basle, Otelul Galati.
Group D:
Real Madrid, Lyon, Ajax, Dinamo Zagreb.
Group E:
Chelsea, Valencia, Bayer Leverkusen, Genk.
Group F:
Arsenal, Marseille, Olympiakos, Borussia Dortmund.
Group G:
FC Porto, Shakhtar Donetsk, Zenit St Petersburg, Apoel.
Group H:
Barcelona, Ac Milan, Bate Borisov, Viktoria Plzen
Subscribe to:
Posts (Atom)