Thursday, September 29, 2011

Yanga yafanya maangamizi yaisambaratisha Coastal Union 5-0














Davis Mwape akichanja mbuga

Kenneth Asamoah alitia kambani mabao mawili na kuiongoza Yanga kuwasambaratisha wagosi wa kaya ambao ni vibonde wa ligi Coastal Union kwa mabao 5-0 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mabingwa hao waliopoteza mvuto kwa mashabiki wao kutokana na kuanza ligi kwa kusuasua jana walionekana tofauti kabisa kwani katika dakika ya nne mshambuliaji wao wa kimataifa wa Ghana, Asamoah alifunga bao la kwanza kabla ya Shamte Ally, Davies Mwape, Nurdin Bakari na Mghana huyo kufunga kalamu hiyo ya kishindo.

Kiungo Idrisa Rajabu alitoa mchango mkubwa kwenye mauaji hayo kwa kutengeneza mabao matatu kati ya matano ikiwa ni mechi yake ya tatu kuanza kuitumikia Yanga.

Umakini huo wa safu ya ushambuliaji ya Yanga unamfanya kocha Sam Timbe kutomfikiria kabisa mshambuliaji wake Jerryson Tegete aliyefunguliwa na uongozi wake hivi karibuni.

Timbe aliwapumzisha Mwape, Shamte na Asamoah na kuwaingiza Rashid Gumbo, Julius Mrope na Hamis Kiiza.

Mabingwa hao sasa wamefikisha pointi 12, huku Coastal wakibaki mkiani na pointi zao nne katika ligi hiyo inayoongozwa na Simba yenye pointi 18.

Mshambuliaji Davies Mwape alijaribu kufunga bao la mapema katika dakika ya 2, lakini mpira wake wa kichwa ulidakwa na kipa wa Coastal Union, Omar Hamis na dakika mbili baadaye Asamoah alifungia Yanga bao la kuongoza akimalizia kwa kichwa krosi nzuri ya Idrisa Rajabu.

Mshambuliaji wa kimataifa wa zamani wa Kenya, Ben Mwalala alikaribia kuipatia timu yake bao katika dakika 11 baada ya kuunganisha vizuri krosi kutoka upande wa kulia iliyopigwa na Daniel Lianga, lakini kipa wa Yanga, Yaw Berko aliupangua mpira huo.

Winga Shamte Ally aliipatia Yanga bao la pili katika dakika ya 21 akiunganisha kwa umakini krosi ya Asamoah kutoka upande wa kushoto, wakati Wagosi hao wakishaanga uwanja wa Taifa, Mwape aliendeleza kalamu ya mabao kwa kufunga bao la tatu kwa Yanga katika dakika ya 30 kwa kuunganisha kwa shuti kali pasi ya Rashid kutoka winga ya kushoto.

Mshambuliaji Mwalala alijaribu kuwaongoza vijana wake bila ya mafanikio kwa sababu katika dakika ya 35 alipiga shuti kali lililopanguliwa na Berko na kuwa kona ambayo haikuzaa matunda.

Nurdin Bakari aliipatia Yanga bao la nne katika dakika ya 41, akimalizia pasi nzuri ya Asamoah.

Yanga ambayo safu yake ya ushambuliaji ilikuwa ikilaumiwa kwa ubutu ilionekana kuwa bora mbele ya mabeki dhaifu wa Coastal Union ambao wameruhusu timu hiyo kufungwa mechi sita kati ya nane ilizocheza msimu huu.

Coastal mabingwa wa mwaka 1988 wanaofundishwa na Hafidh Bardu walishindwa kucheza kabisa na kumtegemea Mwalala wakati wapinzani wao Yanga wakitawala asilimia 80 ya ya mchezo huo katika nafasi ya kiungo na ushambuliaji.

Asamoah alipachika bao la tano katika dakika ya 46 akipokea krosi ya Rajabu na kuifanya Yanga kushinda kwa mabao 5-0. Asamoah amefunga mabao manne tangu msimu huu wa Ligi Kuu uanze.

Kocha wa Coastal Union, Badru alimpumzisha kipa wake Hamis aliyeruhusu mabao manne na kumwingiza Godson Mmasa, pia Coastal ilimtoa Mwinyi Abdulrahman na kumuingiza Said Swed

Arsenal,Barcelona zafanya kweli ligi ya mabingwa ulaya

Arsenal 2-1 Olympiakos


Bate borisov 0-5 Barcelona


Valencia 1-1 Chelsea


AC Milan 2-0 Victoria Pulzen

Wednesday, September 28, 2011

MATOKEO MECHI ZA LIGI YA MABINGWA ULAYA

CSKA MOSCOW 2-3 INTER MILAN

REAL MADRID 3-0 AJAX

   BAYERN MUNICH 2-0 MAN CITY


               TRABZONSPOR 1-1 LILLE

 MAN UNITED 3-3 BASEL

Arsenal,Chelsea kibaruani leo ligi ya mabingwa ulaya

WINGA wa Chelsea, Juan Mata atakutana na rafiki zake wakati atakaporudi kucheza mechi Ligi ya Mabingwa dhidi ya Valencia leo ikiwa ni miezi mwezi moja tangu alipoondoka.

Kocha Andre Villas-Boas alitumia karibu dola 40.4 milioni kumsajili nyota huyo mwenye miaka 23 na tayari ameonyesha uwezo wake kwa kufunga kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi E walioshinda 2-0 dhidi ya Bayer Leverkusen.“Nipo tayari kucheza dhidi yake na wote tunamsubili,” alisema winga Valencia, Pablo Hernandez aliyekuwa wakilala chumba kimoja na Mata.

“Itakuwa ni siku yake nzuri kurudi nyumbani, lakini hatutakuwa na urafiki uwanjani. Tutafanya kila kitu kuhakikisha tunawafunga pamoja na Juan, baada ya hapo tutamtakia mfanikio mema.”

Chelsea wapo ipo kwenye kiwango cha juu baada ya kushinda 4-1 dhidi ya Swansea City pale Jumamosi na kuwafanya wapande hadi nafasi ya tatu katika Ligi Kuu, nyuma kwa pointi tatu kwa vinara Manchester United na Manchester City.Mshambuliaji wa Hispania, Fernando Torres alitolewa nje kwa kadi nyekundu dakika 39 pale Jumamosi, lakini anaonekana kurudi kwenye kiwango chake akiwa ameshafunga mabao mawili katika mechi mbili mfululizo.

Safu ya ushambuliaji wa Chelsea imeimarika na kurejea kwa nyota wa Ivory Coast, Didier Drogba aliyeingia kuingia akitokea benchi na kufunga baada ya wiki nne za kuwa nje kwa sababu ya kuumia.

LONDON, Robin van Persie ameanza kuthibisha kwamba anaweza kuiongoza Arsenal anategemewa kuibeba klabu hiyo leo kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Olympiakos.Van Persie alichukua unahodha huo baada ya Cesc Fabregas kutimikia Barcelona, Robin alifunga mabao mawili waliposhinda 3-0 dhidi ya Bolton Wanderers Jumamosi.

Olympiakos wenyewe wamepoteza mechi tisa walizocheza dhidi ya timu za England kwenye mashindano ya Ulaya, wakiwa wamefungwa mabao 29 na wao kufunga moja tu.

Van Persie, 28, ameshafunga mabao matano msimu huu na Wenger anaamini Mdachi huyo aliyeripotiwa na vyombo vya habari vya England, Jumatatu hataki kuharakisha kuongeza mkataba wake wake unamalizika 2013, kuwa kwa sasa amekuwa na anaweza kuongoza kwenye ufungaji na kuwatia moyo wenzake.

“Robin amekuwa kutoka mvulana anayesumbuliwa na presha za jamii wakati anakuja hapa na leo ni mtu mzima,” Wenger aliimbia tovuti ya Arsenal.Hilo alitakuwa vumbi pekee kutimka wiki hii Ulaya mashariki wakati BATE Borisov watakapowakaribisha mabingwa wa Ulaya, Barcelona katika mchezo wa Kundi H hapo leo.

BATE walitoka sare1-1 na Belshina Bobruisk pale Ijumaa, Barca walituma salamu kwa kuisambaratisha Atletico Madrid 5-0 Jumamosi huku mchezaji bora wa Dunia, Lionel Messi alifunga mabao matatu peke yake.

KIKOSI KITAKACHOKABILIANA NA MORROCCO HIKI HAPA


Tanzania imetangaza kikosi kitakachopambana na Morrocco katika michuano ya kufuzu kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwakani.
Taarifa iliyotolewa na chama cha soka cha Tanzania TFF imesema Taifa Stars ambayo inafundishwa na kocha Jan Poulsen itaondoka Oktoba 6 kwenda Morrocco, na kujitupa uwanjani Oktoba 9 mjini Marrakech kupambana na timu ya taifa ya Morrocco.

Kikosi hicho cha wachezaji 23 ni:

Makipa:


Shabani Dihile  (JKT Ruvu Stars)
Juma Kaseja  (Simba)
Shabani Kado   (Yanga)


Mabeki:


Shadrack Nsajigwa (Yanga)
Erasto Nyoni (Azam)
Idrissa Rajab (Sofapaka, Kenya)
Amir Maftah (Simba)
Aggrey Morris (Azam)
Juma Nyoso (Simba)
Victor Costa (Simba)


Viungo:


Henry Joseph (Kongsvinger IL, Norway)
Nurdin Bakari (Yanga)
Shabani Nditi (Mtibwa Sugar)
Jabir Aziz (Azam)
Nizar Khalfan (Vancouver Whitecaps, Canada)
Mrisho Ngassa (Azam)
Ramadhan Chombo (Azam)


Washambuliaji:


Abdi Kassim (DT Long An, Vietnam
Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC)
Dan Mrwanda (DT Long An, Vietnam)
Athuman Machupa (Vasalund IF, Sweden)
John Bocco (Azam)
Hussein Javu (Mtibwa Sugar)


Tanzania iko kundi D, pamoja na Algeria, Jamhuri ya Afrika ya Kati na Morrocco.

Tanzania ina pointi 5 baada ya michezo mitano na kushinda mmoja, sawa na Algeria. Morrocco na Jamhuri ya Afrika ya Kati zinaongoza kundi hilo zikiwa na pointi 8.

Tuesday, September 27, 2011

Oljoro yawachakaza walioidindia Simba yawalamba Toto 2-0

JKT Oljoro iliyopanda daraja msimu huu imetafuna mfupa uliowashinda Simba baada ya kuinyuka Toto African mabao 2-0 kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Pia jana Azam F.C ilishindwa kuendeleza kazi yake ya ushindi baada ya kulazimishwa suluhu na Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi wakati kwenye uwanja wa Chamazi, JKT Ruvu vilevile waligawana pointi na Villa Squad.

Timu za Kanda ya Ziwa zilijijengea jina wiki iliyopita baada ya kutibua rekodi ya Simba, ambapo Kagera Sugar ilitoka sare ya 1-1 na na timu hiyo halafu Toto African ikatoka nayo sare ya 3-3 na vinara hao wa ligi, lakini mambo yamekuwa tofauti baada ya timu hizo mbili zote kupokea kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa vijana wa Arusha.

Iliwachukua dakika sita Oljoro JKT kupata bao la kuongoza kupitia Sunday Mussa aliyepokea pasi nzuri kutoka kwa Paul Nonga na kupiga shuti lililojaa wavuni.

Wakati Toto wakiwa hawaamini kinachotokea Oljoro waliandika bao la pili dakika ya 18 kupitia Amir Hamadi akiunganisha kwa kichwa krosi nzuri ya Nonga iliyomshinda kipa wa Toto, Mustapha Mabrouk aliyekuwa ametoka nje kidodo ya goli lake.

Mzuka wa mechi dhidi ya Simba haukuwa kwa Toto kwani nyota wao Mnigeria Darlington Enyima alikosa bao dakika 38 baada ya kupiga shuti nje akiwa yeye na kipa wa Oljoro.

Katika dakika ya 43 Castol Mumbala alitoa pasi mbaya kwa kipa wake ambaye alishindwa kutuliza mpira huo kwa mguu na kuamua kuudaka hivyo mwamuzi kumzawadia kadi ya njano Mustapha Mabrouk kwa kitendo hicho.

Kwa ushindi waliopata Oljoro wanasogea hadi nafasi ya tatu wakiwa na pointi 13 katika michezo nane, lakini ndoto ya timu ya Azam ya kuisogelea Simba kileleni ilififia baada ya kulazimishwa suluhu na Ruvu Shooting katika mechi ya ligi.

Mshambuliaji John Boko wa Azam alikosa bao katika dakika ya 32 baada ya kushindwa kumalizia kwa umakini krosi ya Ibrahim Mwaipopo.

Shooting walijibu mapigo kupitia Abdallah Juma aliyekosa bao katika dakika ya 62 baada ya kuwatoka mabeki wa Azam na kupiga shuti lililopanguliwa na kipa Mwadini Ally na kutoka nje.

Mshambuliaji John Boko alifunga bao katika mechi hiyo, lakini mwamuzi alilikataa hivyo kocha wa Azam, Stewart Hall alilalamikia bao hilo, lakini mwamuzi alisema mfungaji ameotea na kuahidi kupeleka picha ya video ya tukio hilo TFF kama uthibitisho.

Katika mechi hiyo wahudumu wa huduma ya kwanza wa Redcross walikuwa hawajavaa sare zao za kazi walipokuwa wakiingia uwanjani kuwahudumia wachezaji katika mechi hiyo ya Azam dhidi ya Ruvu Shooting.

Pia mashabiki waliojitokeza kwenye uwanja wa Mabatini kushuhudia pambano hilo walilalamikia uchache wa tiketi uliowafanya washindwe kuingia uwanjani hapo ili kushuhudia mchezo huo.

Akizungumza baada ya mechi hiyo kumalizika kocha wa Shooting, Boniface Mkwasa alisema mchezo ulikuwa mgumu, lakini amewasifu wachezaji wake kwa kucheza kwa moyo na kupata matokeo hayo mazuri na sasa wanajipanga kuikabili Mtibwa Sugar.

Wakati Mkwasa akisifu kiwango cha wachezaji wake hali ilikuwa tofauti kwenye Uwanja wa Chamazi kwani kocha wa JKT Ruvu, Charles Kilinda aliwalaumu wachezaji wake kwa kushindwa kucheza kama kawaida yao na kusababisha timu hiyo kupoteza pointi kwenye mchezo huo.

"Sijawahi kuona timu yangu ikicheza mpira mbovu kama waliocheza leo tangu nilipoanza kuifundisha miaka minne iliyopita,"alisema Kilinda.

Kilinda aliongeza labda wamechoka kwa sababu wapo wachezaji wachache kwenye kikosi chake kwa sababu wengine wamekwenda kwenye kozi za kijeshi.

Hata hivyo timu ya JKT Ruvu watajilaumu wenyewe kwa kupoteza nafasi nyingi za kufunga kupitia washambuliaji wake Hussein Bunu, Rajab Chau na Emmanuel Linjechele katika dakika ya 20, 32, 38 na 40 kwa mashuti yao kutoka nje.

JKT Ruvu wanaosifika kwa kucheza soka ya pasi nyingi na kuvutia walishindwa kuonyesha mchezo wao huo mbele ya Villa Squad na kushuhudia timu hizo zikienda mapumziko zikiwa hazijafungana.

Ruvu walimtoa Alhaji Zege na kumwingiza Haruna Adolf wakati Villa walimpumzisha Mohamed Kijuso na nafasi yake kuchukuliwa na Allu Bilal.

Katika mchezo huo makipa wa timu zote mbili Mohamed Bambino wa Villa Squad na Hamis Nyangalio wa JKT Ruvu walifanya kazi kubwa kulinda magoli yao.

SIMBA, MTIBWA ZAINGIZA Sh 74 mil

Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Mtibwa Sugar iliyochezwa Septemba 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh 74,345,000.

Watazamaji waliokata tiketi kushuhudia mechi hiyo walikuwa 13,285 ambapo kiingilio kilikuwa sh 5,000 kwa viti vya bluu na kijani, sh 7,000 rangi ya chungwa, sh 15,000 kwa VIP C na B na sh 20,000 kwa VIP A.

Eneo lililoingiza watazamaji wengi ni kwenye viti vya bluu na kijani ambapo waliingia mashabiki 11,798 wakati eneo lililoingiza watazamaji wachache ni la VIP A ambapo waliingia mashabiki 58.

Baada ya kuondoa gharama za awali za mchezo ambazo ni sh 11,637,000 na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambayo ni sh 11,340,762.70 kila timu ilipata
sh 15,410,171.19.
Mgawo mwingine ulikwenda kwa gharama za mchezo (sh 5,136,723.73), uwanja (sh 5,136,723.73), TFF (sh 5,136,723.73), Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu- FDF (sh 2,568,361.86), Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam- DRFA (sh 2,054,689.49) na Baraza la Michezo la Taifa- BMT (sh 513,672.37).

Monday, September 26, 2011

WATU MAARUFU WENYE MAHUSIANO WANAWAKE WAFUPI NA WANAUME MIRABA MINNE

WILL & JADA   photo | Jada Pinkett Smith, Will Smith
Will Smith(6'2") na mkewe Jada Pinkett Smith (5') hii inaonesha suala la urefu haliathiri mapenzi ya kweli.

KIM & KRIS   photo | Kim Kardashian, Kris Humphries
Kim Kardashian (5'3") na mumewe Kris (6'9")


SACHA & ISLA   photo | Isla Fisher, Sacha Baron Cohen
Sacha(6'3'') na Isla (5'3'')


SHAQ & NICOLE   photo | Shaquille O'Neal

















Shaq(7'1'') na Nicole(5'2")


REESE & JIM   photo | Jim Toth, Reese Witherspoon
Reese na Jim


DAX & KRISTEN   photo | Dax Shepard, Kristen Bell
Kristen(5'1") na Dax(6'1")


CHRIS & ELSA   photo | Chris Hemsworth, Elsa Pataky
Chris(6'3") na mkewe Elsa (5'4")