Friday, November 25, 2011
SIMBA Vs AZAM HAPATOSHI FAINALI YA VIJANA LEO KARUME
TIMU za Simba na Azam FC zote za jijini Dar es Salaam, leo zinakutana katika mechi ya fainali inayotarajia kubeba taswira kubwa ya ushindani ya michuno ya Kombe la Vijana chini ya umri wa miaka 20 kwenye Uwanja wa Karume.
Upinzani wa mechi hiyo uko wazi kutokana na ubora ulioonyeshwa na vikosi hivyo mpaka kufikia hatua ya kucheza fainali.Michuano hiyo maalum kwa ajili ya kukuza vipaji, ilianza wiki mbili zilizopita na kupigwa kwenye viwanja vya Karume na Chamazi kilichopo nje kidogo ya jiji.
Simba ilikata tiketi ya kucheza fainali hizo baada ya kuifunga Toto African kwa mabao 4-1 katika mechi ya nusu fainali. Ushindi huo wa Simba ulikuwa kama kulipa kisasi kwani katika mechi ya kwanza baina ya timu hizo Toto waliifunga Simba bao 1-0.
Kwa upande wa Azam walitinga hatua ya fainali baada ya kuifundisha soka timu ya taifa ya vijana (U-17), Serengeti Boys kwa kuiangushia kipigo cha mabao 3-0.
Timu za Toto African na Serengeti Boys, zitatangulia kushuka dimbani kucheza mechi ya kusaka mshindi wa tatu, ambapo mshindi ataondoka na shilingi 500,000 na medali za Fedha.
Bingwa wa mashindano hayo ya kila mwaka, atajinyakulia shilingi 1.5milioni, Kombe na medali za Dhahabu, huku mshindi wa pili akipata medali za Shaba na kitita cha shilingi 1milioni.
Mbali na hizo pia, kutakuwa na zawadi za Mchezaji Bora atajipatia shilingi 400,000. Mfungaji Bora shilingi300,000, Kipa Bora shilingi 300,000, na timu yenye nidhamu itapata shilingi 300,000.
Makocha wa pande zote mbili Simba na Azam wametamba kila mmoja kwa upande wake kutwaa kombe hilo kulingana na kikosi chake kilivyojiandaa.
Vijana wangu wako kwenye hali nzuri ya pambano hilo na wamenihakikishia kucheza kufa na kupona kutwaa kombe hilo," alisema Seleman Matola kocha wa Simba kama ilivyo kocha wa Azam Iddy Cheche.
Msimu uliopita Ruvu Shooting ndiyo iliyotwaa kombe baada ya kuwafunga 'ndugu' zao JKT Ruvu kwa mabao 2-1 katika mechi ya fainali. Msimu huu mabingwa hao hawakuweza kufua dafu.
Upinzani wa mechi hiyo uko wazi kutokana na ubora ulioonyeshwa na vikosi hivyo mpaka kufikia hatua ya kucheza fainali.Michuano hiyo maalum kwa ajili ya kukuza vipaji, ilianza wiki mbili zilizopita na kupigwa kwenye viwanja vya Karume na Chamazi kilichopo nje kidogo ya jiji.
Simba ilikata tiketi ya kucheza fainali hizo baada ya kuifunga Toto African kwa mabao 4-1 katika mechi ya nusu fainali. Ushindi huo wa Simba ulikuwa kama kulipa kisasi kwani katika mechi ya kwanza baina ya timu hizo Toto waliifunga Simba bao 1-0.
Kwa upande wa Azam walitinga hatua ya fainali baada ya kuifundisha soka timu ya taifa ya vijana (U-17), Serengeti Boys kwa kuiangushia kipigo cha mabao 3-0.
Timu za Toto African na Serengeti Boys, zitatangulia kushuka dimbani kucheza mechi ya kusaka mshindi wa tatu, ambapo mshindi ataondoka na shilingi 500,000 na medali za Fedha.
Bingwa wa mashindano hayo ya kila mwaka, atajinyakulia shilingi 1.5milioni, Kombe na medali za Dhahabu, huku mshindi wa pili akipata medali za Shaba na kitita cha shilingi 1milioni.
Mbali na hizo pia, kutakuwa na zawadi za Mchezaji Bora atajipatia shilingi 400,000. Mfungaji Bora shilingi300,000, Kipa Bora shilingi 300,000, na timu yenye nidhamu itapata shilingi 300,000.
Makocha wa pande zote mbili Simba na Azam wametamba kila mmoja kwa upande wake kutwaa kombe hilo kulingana na kikosi chake kilivyojiandaa.
Vijana wangu wako kwenye hali nzuri ya pambano hilo na wamenihakikishia kucheza kufa na kupona kutwaa kombe hilo," alisema Seleman Matola kocha wa Simba kama ilivyo kocha wa Azam Iddy Cheche.
Msimu uliopita Ruvu Shooting ndiyo iliyotwaa kombe baada ya kuwafunga 'ndugu' zao JKT Ruvu kwa mabao 2-1 katika mechi ya fainali. Msimu huu mabingwa hao hawakuweza kufua dafu.
Thursday, November 24, 2011
Picha bora za mwaka 2011
Shamba la mahindi huko Sao Paulo,Brazil
Dente del Gigante,Italy
Kasa wa kijani picha hii ilipigwa huko Hawaii.
Ndege mtini huko Pantanal,Brazil
Msikiti wa Hazrat uliopo Afghanistan
Hema sokoni nchini Uturuki
Mwamba maeneo ya Sedona,Arizona
Jamaa aki-surf huko Hawaii
Shamba la mpunga,picha ilipigwa huko China
Sherehe ya harusi ya kabila la Samburu,picha ilipigwa nchini Kenya
Sherehe za Diwali huko India
Msikiti wa Istiklal uliopo Indonesia
Cityscape Hongkong,China
Mafuriko Thailand, Viwanda vya magari Honda na Toyota vyajaa maji
Magari yakiwa yamezama ndani ya maji kutokana na mafuriko yaliyovamia kiwanda hicho katika kitongoji cha Ayutthaya,Thailand
Magari yakiwa yameegeshwa kwenye daraja katika kiwanda cha Honda huko Ayutthaya,Thailand.
Dogo akijaribu kukatiza mitaani kwa kutumia karai kama mtumbwi wa kukatiza katika maji ya mafuriko
Waathirika wa mafuriko wakipita karibu na tawi la kiwanda cha magari cha Toyota kilichopo Don Mueang wilaya ya Bangkok huko Thailand.
Show room ya Toyota katika dimbwi la maji.
Kiwanda cha magari ya Honda kikiwa kimefurika maji katika eneo la viwanda la Rojana. Thailand.
Subscribe to:
Posts (Atom)