Wednesday, December 7, 2011

Nusu fainali CECAFA ni Kilimanjaro Stars vs Uganda,Sudan vs Rwanda

Uganda itamenyana na wenyeji Tanzania Bara katika nusu fainali ya Kombe la Cecafa siku ya Alhamisi, baada ya timu zote mbili kushinda katika mechi za robo fainali siku ya Jumanne mjini Dar es salaam.
Uganda Cranes waliishinda Zimbabwe 1-0 katika mechi ya kwanza, nao Kilimanjaro Stars wakawafurahisha mashabiki wa nyumbani kwa kuifunga Malawi 1-0 katika robo fainali ya mwisho.
Bao lao la Tanzania Bara la ushindi lilifungwa na Nurdin Bakari katika dakika ya 35, kwa kukamilisha pasi kutoka Mrisho Ngasa.
Tanzania Bara ndio mabingwa watetezi wa kombe hilo.
Zimbabwe waliudhibiti mchezo dhidi ya Uganda lakini wakakosa bahati ya kufunga.
Hamis Kiiza ndiye aliyefungia Uganda bao hilo moja.
Nusu fainali nyingine siku ya Alhamisi itakuwa kati ya Sudan na Rwanda.

Friday, December 2, 2011

Video za nyimbo za marehemu Mr Ebbo





REST IN PEACE MR EBBO


Mr Ebbo

Mahakama yamkataa mkuu wa mashitaka aliyeteuliwa na Zuma

Rais wa Afrika ya Kusini Jacob Zuma

Mahakama moja ya Afrika Kusini imeharamisha hatua ya Rais Jacob Zuma ya kumteua Menzi Simelane kuwa mkuu wa mashtaka.

Mahakama hiyo imesema kuwa kuna mambo fulani kumhusu Simelanea ambayo yanatilia dosari sifa yake, kwani kuna wakati alitoa ushahidi wa uongo.

Chama cha Upinzani cha Democratic Alliance (DA) kilikuwa kimewasilisha kesi ikidai kuwa Bwana Simelane ni kibaraka wa Bwana Zuma.

Chama hicho kiliambia mahakama kuwa Simelane angeliwalinda watu fulani mashuhuri kutokana na kushitakiwa

Lakini Rais Zuma amekuwa akikanusha madai hayo huku akishikilia kuwa Bwana Simelane alikuwa ana sifa na uwezo wa kishikilia wadhifa huo wa mkuu wa mashitaka wa Afrika Kusini. Zuma pia alisema kuwa ilikuwa haki yake kama rais kuamua ni nani anastahili kuwa mkuu wa mashitaka na hiyo sio kazi ya mahakama.

Jaji wa Mahakama ya juu zaidi ya Rufaa Mahomed Navsa amesema kuwa kuteuliwa kwa Simelane kuwa Mkurugenzi wa Mashitaka ilikuwa kinyume cha katiba ya nchi.

Kiongozi wa chama cha upinazi cha DA Helen Zille ametaja uamuzi wa mahakama kama ushindi kwa demokrasia.

Amesema katika siku za hivi karibuni rais Zuma amekuwa akifanya uteuzi uliojaa utata ukiwemo uteuzi wa jaji Mkuu.

She said Mr Zuma had made several controversial appointments recently - including that of chief justice wa Afrika kusini.