Monday, January 16, 2012

Swansea yaiadhiri Arsenal,Man U mbele kwa mbele

Robin Van Persie aliifungia Arsenal bao la kwanza
Van Persie mfungaji wa bao la kwanza la Arsenal

Matumaini ya Arsenal kusogelea nafasi nne bora za juu za Ligi ya kandanda ya England yalivurugwa na Swansea waliosakata kandanda murua na kuweza kupata pointi tatu muhimu kwa kuilaza Arsenal mabao 3-2 katika mchezo uliokuwa wa kusisimua.
Arsenal walikuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya nne kwa bao la Robin van Persie, lakini wageni hao walionekana kuzidiwa katika kila idara na vijana wa Swansea.
Swansea ilipoiadhiri Arsenal
Scott Sinclair aliisawazishia Swansea kwa mkwaju wa penalti baada ya Aaron Ramsey kumkwatua Nathan Dyer ndani ya eneo la hatari.
Nathan Dyrea aliipatia Swanse bao la pili katika kipindi cha pili kwa makosa ya walinzi wa kati wa Arsenal
Theo Walcott aliisawazishia Arsenal kwa bao la pili na dakika moja baadae Danny Graham akaipatia Swansea bao la tatu la ushindi."Ni wazi kuwa Swansea walistahili ushindi kwani walicheza kwa kujituma na kwa kasi ileile mwanzo mwisho tofauti na Arsenal walioonekana kuwa wachovu"
Na bao maridadi lililofungwa na Leon Best katika kipindi cha kwanza liliinua Newcastle hadi nafasi ya sita ya msimamo wa Ligi Kuu ya England na kumvurugia meneja mpya wa QPR Mark Hughes mechi yake ya kwanza.
QPR mara mbili mikwaju yao iligonga mwamba katika kipindi cha kwanza kwa michomo ya Shaun Wright-Phillips na Jay Bothroyd.
Lakini Newcastle walizinduka kutoka usingizini mwanzoni mwa kipindi cha kwanza na Best alifunga bao maridadi baada ya kuwazunguka walinzi wa QPR.
Bothroyd alipoteza nafasi mbili nzuri kuipatia QPR mabao katika kipindi cha pili lakini walinzi wa Newcastle walionekana kukaa imara.

MAN UNITED YAILAZA BOLTON
Paul Scholes amefunga bao lake la kwanza baada ya kurejea tena kuichezea Manchester United ambayo imesogea na kuwa na pointi sawa na Manchester City baada ya kuilaza Bolton mabao 3-0.
Mkongwe Paul Scholes aifungia Man United bao la kwanza
Paul Scholes

United ilipoteza nafasi nyingi za kufunga kipindi cha kwanza lakini kazi nzuri aliyoifanya mlinda mlango wa Bolton Adam Bogdan iliisaidia Bolton kuepuka kipigo kikali zaidi. Alifanikiwa kuokoa mkwaju wa penalti uliopigwa na Wayne Rooney katika kipindi cha kwanza.
Lakini Scholes, ambaye sasa amefika umri wa miaka 37, alifanikiwa kupachika bao sekunde chache kabla mapumziko baada ya kuunganisha pasi ya pembeni ya Rooney.
Matukio na magoli kati ya Man na BOLTON

Bolton ilionekana kuimarika kipindi cha pili na Manchester United walionekana kusinzia kidogo, lakini alikuwa Danny Welbeck aliyeizindua tena Man United kwa kupachika bao la pili kabla ya Michael Carrick kufumua mkwaju wa umbali wa yadi 20 na kuandika bao la tatu.
Matokeo hayo yameonekana kuipa faraja Man United baada ya kupoteza michezo miwili ya Ligi Kuu ya England, pia kuzidi kuipa changamoto mahasimu wao Man City ambao siku ya Jumatatu watasafiri hadi Wigan kuikabili timu hiyo.
Bao pekee alilofunga Frank Lampard mapema katika kipindi cha kwanza, limeiwezesha Chelsea kuipunguzia kasi Sunderland iliyoanza kucharuka baada ya kumpata meneja mpya Martin O'Neill.
Lampard alitumia uamuzi wa haraka kuuwahi mpira na kupachika bao kwa mkwaju wa karibu baada ya fataki aliyoachia Fernando Torres kugonga mwamba na kurejea uwanjani.
Torres, Lampard na Juan Mata wote walikosa nafasi nzuri za kufunga kipindi cha kwanza.
Lakini Sunderland walipata nafasi nyingi kipindi cha kwanza na walikosa nafasi muhimu ya kupachika bao dakika za mwisho ambapo Craig Gardner na Nicklas Bendtner walishindwa kufunga.
Blackburn waliweza kuhimili vishindo licha ya mfungaji wao mashuhuri Yakubu kutolewa nje kwa kadi nyekundu dakika za mwanzo na kutoka eneo la hatari la kushuka daraja kwa mara ya kwanza tangu mwezi wa Septemba kwa ushindi mnono wa mabao 3-1 dhidi ya Fulham.
Mshambuliaji Yakubu alioneshwa kadi nyekundu kipindi cha kwanza baada ya kumfanyia rafu mbaya Danny Murphy.
Lakini wakicheza nyumbani Blacburn walifanikiwa kupata bao la kwanza lililofungwa na Morten Gamst Pedersen kwa mkwaju wa adhabu ya moja kwa moja kabla ya David Dunn kupachika bao la pili.
Damien Duff aliipatia Fulham bao la kufutia machozi, kabla ya Mauro Formica kuikamilishia kazi Blackburn kwa kuandika bao maridadi la tatu.
Victor Anichebe akiingia mchezaji wa akiba alifanikiwa kuipatia Everton pointi moja baada ya Aston Villa kuonesha kandanda ya ovyo wakicheza uwanja wa nyumbani.
Darren Bent aliipatia Aston Villa bao la kwanza baada ya kupokea pasi ya Stephen Ireland katika dakika ya 56.
Meneja wa Everton David Moyes aliona hakuna cha kuikomboa timu hiyo bila ya kumuingiza Anichebe ambaye alifanikiwa kuisawazishia Everton baada ya Landon Donovan kumchezesha kwa pasi murua.
Robbie Keane aliingia kipindi cha pili kwa Villa ikiwa ni mchezo wake wa kwanza tangu ajiunge na timu hiyo kwa mkataba wa muda mfupi, lakini hakuweza kuisaidia timu yake kuibuka na ushindi.
Bao la kichwa la dakika za mwisho lililofungwa na Steve Morison liliisaidia Norwich kushinda kwa kuilaza West Brom mabao 2-1.
Mkwaju wa juu wa Andrew Surman uliiwezesha Norwich kuandika bao la kwanza muda mfupi kabla ya mapumziko wakati West Brom wakionekana kukosa nafasi nyingi za wazi kupachika mabao.
Shane Long alizinduka haraka na kuipatia bao West Brom kwa kwaju wa penalti baada ya Jerome Thomas kuchezewa rafu.
Lakini Morison aliangushia kipigo cha nne mfululizo West Brom kwa kuandika bao la pili.
Liverpool imekosa nafasi ya kuingia katika timu tano bora za juu baada ya kubanwa na Stoke na kuandika sare ya saba kwa michezo iliyocheza uwanja wa nyumbani wa Anfield.
Dirk Kuyt alipoteza nafasi nzuri ya kuipatia bao Liverpool wakati mpira wake wa kichwa ulipotoka nje.
Martin Skrtel alidonyoa mpira wa kichwa dakika za mwisho lakini Liverpool walikuwa wamejipanga zaidi kwa kuachia mikwaju ya mbali ambayo haikuzaa matunda.
Mkwaju alioupiga Matthew Etherington kwa kumlenga mlinda mlango wa Liverpool Jose Reina ulikuwa ni moja ya majaribio machache ambayo Stoke iliyafanya. Hadi mwisho timu hizo hazikufungana.
Tottenham nayo ilikosa nafasi nyeupe ya kufikisha pointi sawa na vinara wa ligi baada ya kubanwa na kutoka sare ya bao moja kwa moja dhidi ya Wolves.
Steven Fletcher alikuwa wa kwanza kuipatia Wolves bao kwa mkwaju wa karibu baada ya mlinda mlango Brad Friedel kupangua mpira wa kichwa uliopigwa na Roger Johnson.
Luka Modric aliisawazishia Spurs kwa mkwaju wa yadi 20 baada ya kazi kubwa iliyofanywa na Gareth Bale ambaye alikosa kuuweka mpira wavuni na ukamkuta mfungaji ambaye hakufanya ajizi.
Wolves walijihami vizuri huku mlinda mlango Wayne Hennessey akiokoa michomo ya Aaron Lennon na Jermain Defoe.
Matumaini makubwa ya Tottenham yaliyoanza kuchomoza hivi karibuni ya kushinda ligi baada ya miaka 50 yalivurugika ambapo kama wangeshinda wangekuwa pointi sawa na Manchester zote mbili huko kileleni wakitenganishwa na wingi wa mabao.

Saturday, January 14, 2012

Three die after huge Italian cruise ship runs aground



ROME (Reuters) - At least three people were killed and rescuers were looking for other victims Saturday after a large Italian cruise ship carrying more than 4,000 people ran aground overnight, took on water and tipped over

A dramatic nighttime rescue operation involving lifeboats, ships and helicopters was continuing hours after the 114,500 gross tonnes Costa Concordia hit a sandbar near the island of Giglio as passengers were eating dinner.
"We were sitting down do dinner and we heard this big bang. I think it hit some rocks. There was a lot of panic, the tables overturned, glasses were flying all over the place and we ran for the decks where we put on our life vests," passenger Maria Parmegiano Alfonsi told Sky Italia television.
The 290-metre-long ship took on water and started listing.
Pictures taken by rescued passengers after daybreak and broadcast on television showed the shiny, multi-story luxury vessel on its side and about half submerged on the sandbar just a few hundred metres (yards) from Giglio.
The luxury cruise ship Costa Concordia leans after it ran aground off the coast of the Isola del Giglio island, Italy, gashing open the hull and forcing some 4,200 people aboard to evacuate aboard lif
Coast guard Captain Luciano Nicastro and police official Giuseppe Lunardi said three people were confirmed dead, fewer than the six reported earlier by Italian media.
But, speaking on live television, Nicastro said rescue workers were still searching the ship, which had just started a winter Mediterranean cruise, and the waters around it.
Lunardi said some people had jumped off the ship while it was listing.
"The rescue operation is still going on," Fire brigades official Luca Cari said on television about 10 hours after the accident.
He said rescue workers were still checking decks that remained above water and that scuba divers would then check the decks that have been submerged.
Rescuers surround the luxury cruise ship Costa Concordia after it ran aground off the coast of Isola del Giglio island, Italy, gashing open the hull and forcing some 4,200 people aboard to evacuate ab
"This is difficult because the ship is enormous," Cari said, adding that the ship was now listing at about 90 degrees but would likely remain in that position and not sink because of the sand below.
Most of the 3,200 passengers and 1,023 crew on board the ship had been evacuated to the island of Giglio and from there were being taken to the mainland.
The luxury cruise ship Costa Concordia leans after it ran aground off the coast of Isola del Giglio island, Italy, gashing open the hull and forcing some 4,200 people aboard to evacuate aboard lifeboa

Alfonsi said she and other passengers were first put up in churches on the island and later, with only some blankets to protect them from the cold, were later taken to the mainland.
Another unnamed coast guard official on television said the ship was believed to have suffered a large gash on its side.Rescue workers help a woman at Porto Santo Stefano, after a cruise ship ran aground on a sandbar off the west coast of Italy overnight at Giglio island
Most of the passengers on board were believed to be Italian but the cruises are popular with foreigners too.
The cruise ship company said the cause of the incident was being investigated.
(Reporting By Philip Pullella; Editing by Matthew Jones)
Passengers of the luxury ship that ran aground off the coast of Tuscany arrive on a ferry in Porto Santo Stefano, Italy, Saturday, Jan. 14, 2012. A luxury cruise ship ran aground off the coast of Tusc

Monday, December 12, 2011

Tottenham yaangukia pua kwa Stoke City

Adebayor mfungaji wa bao pekee la Tottenham kwa penati

Rekodi ya Tottenham kupata ushindi katika mechi 11 mfululizo ilivunjwa na timu ya Stoke City siku ya Jumapili baada ya mchezaji wa zamani wa Tottenham Matthew Etherington kuingiza magoli mawili dhidi ya moja la Spurs.
Etherington aliingiza goli la kwanza katika dakika ya 13 na baada ya dakika 30 akaongeza la pili.
Tottenham walipata goli lao moja kupitia kwa mkwaju wa penalti lililofungwa na katika dakika ya 62.
Tottenham walijitahidi ili wapate kusawazisha lakini matumaini yao yakafifia baada ya Younes Kaboul kuonyeshwa kadi nyekundu.
Spurs pia hawakufurahishwa na baadhi ya maamuzi yaliyotolewa na refarii Chris Foy.
Tottenham sasa wana alama 31 ikiwa ni alama tano nyuma ya Manchester United walio kwenye nafasi ya pili.

Sunderland 2- 1 Blackburn.

Katika matokeo mengine ya ligi kuu nchini England Sunderland walipata ushindi wa magoli mawili kwa moja dhidi ya Blackburn Rovers.
Ushindi huu umempa kocha mpya wa Sunderland Martin O'Neill mwanzo mzuri.
Hii ilikuwa mechi ya kwanza kwa O'Neille kama msimamizi wa Sunderland tangu achukue uongozi baada ya Steve Bruce kupigwa kalamu.
Ushindi huu ambao ni wao wa tatu tangu ligi ianze umeipandisha Sunderland hadi nafasi ya 16

Thursday, December 8, 2011

KILIMANJARO STARS KUTINGA FAINALI YA CECAFA LEO?












Kilimanjaro stars

LEO ni siku ya 363 tangu Uganda Cranes na Kilimanjaro Stars ya Tanzania Bara zilipokwaana katika nusu fainali mwaka jana ya Michuano ya Tusker Chalenji na leo timu hizo zinarudiana katika hatua hiyo.

Timu hizo zilimaliza dakika 120 zikiwa suluhu na katika mikwaju ya penalti, Bara ilishinda penalti 5-4.

Leo hii, timu hizo zinakutana kwenye Uwanja wa Taifa kuwania kucheza fainali. Ni wazi Uganda hawatotaka kurudia makosa ya mwaka jana wakati Bara inataka kuendeleza rekodi yake ya ushindi kama ilivyokuwa mwaka jana.

Kivutio kikubwa katika mchezo wa leo ni beki wa Kilimanjaro Stars, Juma Nyosso atakayesimama na mshambuliaji wa The Cranes, Emmanuel Okwi.

Itakumbukwa mwaka jana, wawili hao walivyokuwa wakichezeana ubabe na leo wanakutana tena. Nyosso na Okwi wanaitumikia klabu ya Simba.

Bara iliingia hatua hiyo baada ya kuilaza Malawi bao 1-0 wakati Uganda iliifungisha virago Zimbabwe kwa kuilaza idadi hiyo.

Mchezo huo unaotarajiwa kuwa na ushindani, utatanguliwa na mechi nyingine ya nusu fainali kati ya Rwanda na Sudan ambazo pia zinawania tiketi ya fainali ya michuano hiyo. Fainali imepangwa kufanyika keshokutwa.

Kocha Mkuu wa Kilimanjaro Stars, Charles Boniface Mkwasa alisema kuwa vijana wake wote wapo kamili kwa mechi hiyo dhidi ya Uganda ambayo ni mabingwa mara 11 wa mashindano hayo ya Chalenji tangu yalipoanzishwa mwaka 1973.

Alisema amefanyia kazi kasoro kadhaa kwa kushirikiana na msaidizi wake Jamhuri Kihwelu na ana matumaini makubwa wa kufanya vizuri kwenye mchezo huo.

"Tumejipanga vizuri kuhakikisha tunaibuka na ushindi katika mchezo wa kesho (leo) dhidi ya Uganda ambayo imeonyesha uwezo mkubwa katika mashindano haya tangu yalipoanza kutimua vumbi.

"Baada ya ushindi wa jana (juzi) dhidi ya Malawi kwa hakika vijana wapo katika morali ya hali ya juu ukilinganisha na mechi nyingine zilizotangulia.

Katika hatua nyingine, Mkwasa amewataka Watanzania wote kushikamana na kuinunga mkono timu hiyo ili kuwatia nguvu za kupigana wachezaji wa Kilimnjaro Stars ili kuibuka na ushindi kwenye mchezo huo.

Naye kocha wa Uganda, Bobby Williamson alisema kuwa leo timu yake itashuka uwanjani kwa kazi moja tu ya kuhakikisha inaibuka na ushindi katika mchezo huo licha ya kudai kuwa itakabiliwa na upinza mkubwa kutoka wa Kilimanjaro Stars.

Alisema Kilimanjaro Stars ilianza mashindano hayo vibaya lakini kadri mashindano hayo yanavyo zidi kusonga mbele inabadilika na kufanya vizuri hivyo mchezo huo wa leo hautakuwa mwepesi kwake huku akidai kuwa baadhi ya wachezaji wa timu hizo wanafahamiana.

Naye Calvin Kiwia anaripoti kuwa nahodha wa Uganda, Andrew Mwesiga amesema watahakikisha wanakuwa makini na winga wa Kili Stars, Mrisho Ngassa kuhakikisha haleti madhara.

Beki huyo mkongwe aliyekuwa akishuhudia pambano la robo fainali baina ya Kili Stars na Malawi alisema anamuona Ngassa kuwa ndiye mchezaji pekee hatari wa kuchungwa.

"Ni mchezaji mzuri, ana mbio na uwezo wakupiga chenga, hatuna budi kuweka tahadhari kubwa juu yake kuhakikisha haleti madhara kwetu," alisema Mwesiga.
"Tanzania 'Kili Stars' wanamtumia sana kutengeneza mashambulizi yake, nafikiri ndiye mchezaji ambaye tunaweza tukamwekea ulinzi zaidi," alisisitiza.

Alisema anaamini wakifanikiwa kufanya hivyo na kumdhibiti watakuwa wamejitengenezea nafasi nzuri ya kushinda pambano hilo na kutua fainali.
"Nafikiri 'Ngassa' ndio roho ya timu ya Tanzania anajituma vizuri na kucheza kwa ushirikiano na wenziye," alisema.
Ngassa hajaifungia Kili Stars bao lakini ametoa mchango mkubwa kwenye kikosi hicho, akitoa pasi ya mwisho kwa Nurdin Bakari aliyeifungia Tanzania bao la ushindi dhidi ya Malawi na penalti iliyofungwa na Mwinyi Kazimoto mchezo wa makundi na Zimbabwe

Wednesday, December 7, 2011

Nusu fainali CECAFA ni Kilimanjaro Stars vs Uganda,Sudan vs Rwanda

Uganda itamenyana na wenyeji Tanzania Bara katika nusu fainali ya Kombe la Cecafa siku ya Alhamisi, baada ya timu zote mbili kushinda katika mechi za robo fainali siku ya Jumanne mjini Dar es salaam.
Uganda Cranes waliishinda Zimbabwe 1-0 katika mechi ya kwanza, nao Kilimanjaro Stars wakawafurahisha mashabiki wa nyumbani kwa kuifunga Malawi 1-0 katika robo fainali ya mwisho.
Bao lao la Tanzania Bara la ushindi lilifungwa na Nurdin Bakari katika dakika ya 35, kwa kukamilisha pasi kutoka Mrisho Ngasa.
Tanzania Bara ndio mabingwa watetezi wa kombe hilo.
Zimbabwe waliudhibiti mchezo dhidi ya Uganda lakini wakakosa bahati ya kufunga.
Hamis Kiiza ndiye aliyefungia Uganda bao hilo moja.
Nusu fainali nyingine siku ya Alhamisi itakuwa kati ya Sudan na Rwanda.