Friday, January 20, 2012
Vifahamu viwanja na timu Kombe la mataifa ya Afrika Equatorial Guinea na Ratiba kamili
Ramani ikionesha viwanja vitakavyotumika kombe la mataifa ya Afrika
Uwanja wa Bata,Estadio de Bata
Uwanja wa Malabo,Malabo stadium
Group A
GUINEA EQ.
LIBYA
SENEGAL
ZAMBIA
Group B
COTE D’IVOIRE
SUDAN
BURKINA FASO
ANGOLA
Group C
GABON
NIGER
MOROCCO
TUNISIA
Group D
GHANA
BOTSWANA
MALI
GUINEA
RATIBA KAMILI KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA
Group matches/Matches de groupe | |||||
No. | Match | Group(e) | Date | Time/Heure | Venue/Lieu |
01. | GUINEA EQ. vs. LIBYA | A | 21/01/2012 | 19H:30 | Bata |
02. | SENEGAL vs. ZAMBIA | A | 21/01/2012 | 22H:00 | Bata |
03. | COTE D’IVOIRE vs. SUDAN | B | 22/01/2012 | 17H:00 | Malabo |
04. | BURKINA FASO vs. ANGOLA | B | 22/01/2012 | 20H:00 | Malabo |
05. | GABON vs. NIGER | C | 23/01/2012 | 17H:00 | Libreville |
06. | MOROCCO vs. TUNISIA | C | 23/01/2012 | 20H:00 | Libreville |
07. | GHANA vs. BOTSWANA | D | 24/01/2012 | 17H:00 | Franceville |
08. | MALI vs. GUINEA | D | 24/01/2012 | 20H:00 | Franceville |
09. | LIBYA vs. ZAMBIA | A | 25/01/2012 | 17H:00 | Bata |
10. | GUINEA EQ. vs. SENEGAL | A | 25/01/2012 | 20H:00 | Bata |
11. | SUDAN vs. ANGOLA | B | 26/01/2012 | 17H:00 | Malabo |
12. | COTE D’IVOIRE vs. BURKINA FASO | B | 26/01/2012 | 20H:00 | Malabo |
13. | NIGER vs. TUNISIA | C | 27/01/2012 | 17H:00 | Libreville |
14. | GABON vs. MOROCCO | C | 27/01/2012 | 20H:00 | Libreville |
15. | BOTSWANA vs. GUINEA | D | 28/01/2012 | 17H:00 | Franceville |
16. | GHANA vs. MALI | D | 28/01/2012 | 20H:00 | Franceville |
17. | GUINEA EQ. vs. ZAMBIA | A | 29/01/2012 | 19H:00 | Malabo |
18. | LIBYA vs. SENEGAL | A | 29/01/2012 | 19H:00 | Bata |
19. | SUDAN vs. BURKINA FASO | B | 30/01/2012 | 19H:00 | Bata |
20. | COTE D’IVOIRE vs. ANGOLA | B | 30/01/2012 | 19H:00 | Malabo |
21. | GABON vs. TUNISIA | C | 31/01/2012 | 19H:00 | Franceville |
22. | NIGER vs. MOROCCO | C | 31/01/2012 | 19H:00 | Libreville |
23. | BOTSWANA vs. MALI | D | 01/02/2012 | 19H:00 | Libreville |
24. | GHANA vs. GUINEA | D | 01/02/2012 | 19H:00 | Franceville |
Quarter Finals – ¼ de finale | |||||
25. | 1st A vs. 2nd B | 04/02/2012 | 17H:00 | Bata | |
26. | 1st B vs. 2nd A | 04/02/2012 | 20H:00 | Malabo | |
27. | 1st C vs. 2nd D | 05/02/2012 | 17H:00 | Libreville | |
28. | 1st D vs. 2nd C | 05/02/2012 | 20H:00 | Franceville | |
Semi-Finals - ½ Finale | |||||
29. | Win. 25 vs. Win. 28 | 08/02/2012 | 17H:00 | Bata | |
30. | Win. 27 vs. Win. 26 | 08/02/2012 | 20H:00 | Libreville | |
3rd Place match – Match de classement | |||||
31. | Loser 29 vs. loser 30 | 11/02/2012 | 20H:00 | Malabo | |
Final/Finale | |||||
32. | Win. 29 v Win. 30 | 12/02/2012 | 20H:00 | Libreville | |
Pazia la Kombe la Mataifa ya Afrika kufunguliwa Kesho 21 jan 2012
Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika yanaanza wikendi hii, mechi ya ufunguzi ikichezewa Bata kati ya waandalizi Equatorial Guinea (wakishirikiana na Gabon) dhidi ya Libya.
Bila shaka Libya itajaribu kuonyesha picha mpya, kufuatia mabadiliko ya kisiasa.
Uwanja wa Bata ambapo mechi ya ufunguzi kati ya Equatorial Guinea na Libya itachezwa.
Libya iliwashangaza wengi ilipofuzu kuingia katika mashindano hayo, baada ya kutofungana mabao (0-0) ilipocheza na Zambia.
Hii nafasi kwa timu ya Libya kuanza upya, na baada ya kuitupa bendera yake iliyokuwa na msitari wa kijani kibichi, na kuanza kutumia iliyo na rengi nyekundu na nyeupe, na kuipatia timu jina jipya la Mediterranean Knights.
Hakuna anayeweza kusema kwamba maandalizi ya michuano hii ni kazi rahisi.
Ingawa Equatorial Guinea na Gabon ni mataifa jirani, kiutamaduni na kisiasa yana tofauti kubwa.
Equatorial Guinea ni taifa ambalo limeongozwa na Teodoro Obiang, ambaye ni kati ya marais wa Afrika ambao wamekuwa madarakani kwa muda mrefu sana barani Afrika.
Kifedha, ni taifa ambalo linanawiri kutokana na utajiri wake mkubwa kwa kutoa mafuta.
Hata hivyo, nchi hiyo inalaumiwa na wengi kwa kukosa uhuru wa kujielezea, na kwa kutozingatia haki mbalimbali za binadamu.
Nchini Gabon, rais Ali Bongo ndio tu ameweza kuwa imara zaidi, baada ya kupata kuungwa mkono na wengi katika bunge la nchi hiyo, kufuatia uchaguzi wa mwezi Desemba, ambao baadhi ya viongozi wa upinzani walitaka ususiwe.
Lugha ya taifa nchini Gabon ni kifaransa, lakini kihispania kunazungumzwa Equatorial Guinea.
Miji itakayochezewa mechi iko mbalimbali, na baya zaidi, mji mkuu wa Equatorial Guinea, Malaba, upo katika kisiwa cha Bioko, karibu na Cameroon.
Mashirika mapya ya vyombo vya habari yamechukizwa na ukiritimba na ugumu katika kupata vibali vya kuingia nchini humo na kutangaza moja kwa moja mechi zitakazochezwa katika mataifa hayo.
Vile vile kuna wasiwasi hali ya usalama itakuwa vipi, katika kuwapokea mamia ya waandishi wa habari, na vikundi mbalimbali vya wafanyikazi wa mashirika ya redio na televisheni.
Mashabiki wa soka barani Afrika wanauhusudu sana kandanda.
Lakini ni wangapi watasafiri, kwa mfano, kutoka Zambia hadi Bata?
Hata hivyo, licha ya matatizo ya usafiri, kuna matumaini kwamba michuano itakuwa ya kuvutia, na mataifa kama Niger na Botswana, yaliyofuzu kushiriki kwa mara ya kwanza, yataonyesha mchezo wa kusisimua.
Wengi wataitazama Niger, hasa kwa kuwa majirani Nigeria walishindwa kufuzu; lakini watapambana na ushindani mkali kutoka kwa Gabon, Tunisia na vile vile Morocco.
Muhimu pia katika mashindano haya ni suala la ni nani hayupo.
Sio tu Nigeria, lakini miamba mingine ya soka, Afrika Kusini, Cameroon na wachezaji hodari wa Misri, wote walishindwa kufuzu.
Je, kukosekana kwao kutakuwa na athari gani katika ubora wa mechi zitakazochezwa?
Ama labda mashabiki wengi watayageuzi mashindano kisogo kwa kukosekana miamba hiyo?
Lakini pasipo majina hayo makubwa, hii ni nafasi kwa wageni pia kuondoka na kombe.
Ivory Coast wanatazamiwa na wengi kuondoka na ushindi, lakini mataifa ya Ghana na Senegal pia yana nafasi nzuri.
Kutokuwepo kwa Misri ni matumaini kwa mabingwa hapo zamani, Morocco au Tunisia, kutazamiwa na mashabiki wa Afrika ya Kaskazini kulifikisha kombe huko.
Monday, January 16, 2012
Swansea yaiadhiri Arsenal,Man U mbele kwa mbele
Van Persie mfungaji wa bao la kwanza la Arsenal
Matumaini ya Arsenal kusogelea nafasi nne bora za juu za Ligi ya kandanda ya England yalivurugwa na Swansea waliosakata kandanda murua na kuweza kupata pointi tatu muhimu kwa kuilaza Arsenal mabao 3-2 katika mchezo uliokuwa wa kusisimua.
Arsenal walikuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya nne kwa bao la Robin van Persie, lakini wageni hao walionekana kuzidiwa katika kila idara na vijana wa Swansea.
Swansea ilipoiadhiri Arsenal
Scott Sinclair aliisawazishia Swansea kwa mkwaju wa penalti baada ya Aaron Ramsey kumkwatua Nathan Dyer ndani ya eneo la hatari.Nathan Dyrea aliipatia Swanse bao la pili katika kipindi cha pili kwa makosa ya walinzi wa kati wa Arsenal
Theo Walcott aliisawazishia Arsenal kwa bao la pili na dakika moja baadae Danny Graham akaipatia Swansea bao la tatu la ushindi."Ni wazi kuwa Swansea walistahili ushindi kwani walicheza kwa kujituma na kwa kasi ileile mwanzo mwisho tofauti na Arsenal walioonekana kuwa wachovu"
Na bao maridadi lililofungwa na Leon Best katika kipindi cha kwanza liliinua Newcastle hadi nafasi ya sita ya msimamo wa Ligi Kuu ya England na kumvurugia meneja mpya wa QPR Mark Hughes mechi yake ya kwanza.
QPR mara mbili mikwaju yao iligonga mwamba katika kipindi cha kwanza kwa michomo ya Shaun Wright-Phillips na Jay Bothroyd.
Lakini Newcastle walizinduka kutoka usingizini mwanzoni mwa kipindi cha kwanza na Best alifunga bao maridadi baada ya kuwazunguka walinzi wa QPR.
Bothroyd alipoteza nafasi mbili nzuri kuipatia QPR mabao katika kipindi cha pili lakini walinzi wa Newcastle walionekana kukaa imara.
MAN UNITED YAILAZA BOLTON
Paul Scholes amefunga bao lake la kwanza baada ya kurejea tena kuichezea Manchester United ambayo imesogea na kuwa na pointi sawa na Manchester City baada ya kuilaza Bolton mabao 3-0.
Paul Scholes
United ilipoteza nafasi nyingi za kufunga kipindi cha kwanza lakini kazi nzuri aliyoifanya mlinda mlango wa Bolton Adam Bogdan iliisaidia Bolton kuepuka kipigo kikali zaidi. Alifanikiwa kuokoa mkwaju wa penalti uliopigwa na Wayne Rooney katika kipindi cha kwanza.
Lakini Scholes, ambaye sasa amefika umri wa miaka 37, alifanikiwa kupachika bao sekunde chache kabla mapumziko baada ya kuunganisha pasi ya pembeni ya Rooney.
Matukio na magoli kati ya Man na BOLTON
Bolton ilionekana kuimarika kipindi cha pili na Manchester United walionekana kusinzia kidogo, lakini alikuwa Danny Welbeck aliyeizindua tena Man United kwa kupachika bao la pili kabla ya Michael Carrick kufumua mkwaju wa umbali wa yadi 20 na kuandika bao la tatu.
Matokeo hayo yameonekana kuipa faraja Man United baada ya kupoteza michezo miwili ya Ligi Kuu ya England, pia kuzidi kuipa changamoto mahasimu wao Man City ambao siku ya Jumatatu watasafiri hadi Wigan kuikabili timu hiyo.
Bao pekee alilofunga Frank Lampard mapema katika kipindi cha kwanza, limeiwezesha Chelsea kuipunguzia kasi Sunderland iliyoanza kucharuka baada ya kumpata meneja mpya Martin O'Neill.
Lampard alitumia uamuzi wa haraka kuuwahi mpira na kupachika bao kwa mkwaju wa karibu baada ya fataki aliyoachia Fernando Torres kugonga mwamba na kurejea uwanjani.
Torres, Lampard na Juan Mata wote walikosa nafasi nzuri za kufunga kipindi cha kwanza.
Lakini Sunderland walipata nafasi nyingi kipindi cha kwanza na walikosa nafasi muhimu ya kupachika bao dakika za mwisho ambapo Craig Gardner na Nicklas Bendtner walishindwa kufunga.
Blackburn waliweza kuhimili vishindo licha ya mfungaji wao mashuhuri Yakubu kutolewa nje kwa kadi nyekundu dakika za mwanzo na kutoka eneo la hatari la kushuka daraja kwa mara ya kwanza tangu mwezi wa Septemba kwa ushindi mnono wa mabao 3-1 dhidi ya Fulham.
Mshambuliaji Yakubu alioneshwa kadi nyekundu kipindi cha kwanza baada ya kumfanyia rafu mbaya Danny Murphy.
Lakini wakicheza nyumbani Blacburn walifanikiwa kupata bao la kwanza lililofungwa na Morten Gamst Pedersen kwa mkwaju wa adhabu ya moja kwa moja kabla ya David Dunn kupachika bao la pili.
Damien Duff aliipatia Fulham bao la kufutia machozi, kabla ya Mauro Formica kuikamilishia kazi Blackburn kwa kuandika bao maridadi la tatu.
Victor Anichebe akiingia mchezaji wa akiba alifanikiwa kuipatia Everton pointi moja baada ya Aston Villa kuonesha kandanda ya ovyo wakicheza uwanja wa nyumbani.
Darren Bent aliipatia Aston Villa bao la kwanza baada ya kupokea pasi ya Stephen Ireland katika dakika ya 56.
Meneja wa Everton David Moyes aliona hakuna cha kuikomboa timu hiyo bila ya kumuingiza Anichebe ambaye alifanikiwa kuisawazishia Everton baada ya Landon Donovan kumchezesha kwa pasi murua.
Robbie Keane aliingia kipindi cha pili kwa Villa ikiwa ni mchezo wake wa kwanza tangu ajiunge na timu hiyo kwa mkataba wa muda mfupi, lakini hakuweza kuisaidia timu yake kuibuka na ushindi.
Bao la kichwa la dakika za mwisho lililofungwa na Steve Morison liliisaidia Norwich kushinda kwa kuilaza West Brom mabao 2-1.
Mkwaju wa juu wa Andrew Surman uliiwezesha Norwich kuandika bao la kwanza muda mfupi kabla ya mapumziko wakati West Brom wakionekana kukosa nafasi nyingi za wazi kupachika mabao.
Shane Long alizinduka haraka na kuipatia bao West Brom kwa kwaju wa penalti baada ya Jerome Thomas kuchezewa rafu.
Lakini Morison aliangushia kipigo cha nne mfululizo West Brom kwa kuandika bao la pili.
Liverpool imekosa nafasi ya kuingia katika timu tano bora za juu baada ya kubanwa na Stoke na kuandika sare ya saba kwa michezo iliyocheza uwanja wa nyumbani wa Anfield.
Dirk Kuyt alipoteza nafasi nzuri ya kuipatia bao Liverpool wakati mpira wake wa kichwa ulipotoka nje.
Martin Skrtel alidonyoa mpira wa kichwa dakika za mwisho lakini Liverpool walikuwa wamejipanga zaidi kwa kuachia mikwaju ya mbali ambayo haikuzaa matunda.
Mkwaju alioupiga Matthew Etherington kwa kumlenga mlinda mlango wa Liverpool Jose Reina ulikuwa ni moja ya majaribio machache ambayo Stoke iliyafanya. Hadi mwisho timu hizo hazikufungana.
Tottenham nayo ilikosa nafasi nyeupe ya kufikisha pointi sawa na vinara wa ligi baada ya kubanwa na kutoka sare ya bao moja kwa moja dhidi ya Wolves.
Steven Fletcher alikuwa wa kwanza kuipatia Wolves bao kwa mkwaju wa karibu baada ya mlinda mlango Brad Friedel kupangua mpira wa kichwa uliopigwa na Roger Johnson.
Luka Modric aliisawazishia Spurs kwa mkwaju wa yadi 20 baada ya kazi kubwa iliyofanywa na Gareth Bale ambaye alikosa kuuweka mpira wavuni na ukamkuta mfungaji ambaye hakufanya ajizi.
Wolves walijihami vizuri huku mlinda mlango Wayne Hennessey akiokoa michomo ya Aaron Lennon na Jermain Defoe.
Matumaini makubwa ya Tottenham yaliyoanza kuchomoza hivi karibuni ya kushinda ligi baada ya miaka 50 yalivurugika ambapo kama wangeshinda wangekuwa pointi sawa na Manchester zote mbili huko kileleni wakitenganishwa na wingi wa mabao.
Saturday, January 14, 2012
Three die after huge Italian cruise ship runs aground
ROME (Reuters) - At least three people were killed and rescuers were looking for other victims Saturday after a large Italian cruise ship carrying more than 4,000 people ran aground overnight, took on water and tipped over
A dramatic nighttime rescue operation involving lifeboats, ships and helicopters was continuing hours after the 114,500 gross tonnes Costa Concordia hit a sandbar near the island of Giglio as passengers were eating dinner.
"We were sitting down do dinner and we heard this big bang. I think it hit some rocks. There was a lot of panic, the tables overturned, glasses were flying all over the place and we ran for the decks where we put on our life vests," passenger Maria Parmegiano Alfonsi told Sky Italia television.
The 290-metre-long ship took on water and started listing. Pictures taken by rescued passengers after daybreak and broadcast on television showed the shiny, multi-story luxury vessel on its side and about half submerged on the sandbar just a few hundred metres (yards) from Giglio.
Coast guard Captain Luciano Nicastro and police official Giuseppe Lunardi said three people were confirmed dead, fewer than the six reported earlier by Italian media.
But, speaking on live television, Nicastro said rescue workers were still searching the ship, which had just started a winter Mediterranean cruise, and the waters around it.
Lunardi said some people had jumped off the ship while it was listing.
"The rescue operation is still going on," Fire brigades official Luca Cari said on television about 10 hours after the accident.
He said rescue workers were still checking decks that remained above water and that scuba divers would then check the decks that have been submerged.
"This is difficult because the ship is enormous," Cari said, adding that the ship was now listing at about 90 degrees but would likely remain in that position and not sink because of the sand below.
Most of the 3,200 passengers and 1,023 crew on board the ship had been evacuated to the island of Giglio and from there were being taken to the mainland.
Alfonsi said she and other passengers were first put up in churches on the island and later, with only some blankets to protect them from the cold, were later taken to the mainland.
Another unnamed coast guard official on television said the ship was believed to have suffered a large gash on its side.
Most of the passengers on board were believed to be Italian but the cruises are popular with foreigners too.
The cruise ship company said the cause of the incident was being investigated.(Reporting By Philip Pullella; Editing by Matthew Jones)
Subscribe to:
Posts (Atom)