Tuesday, January 24, 2012

Wenger atetea upuuzi wake wa kumpumzisha Chamberlain ilipochapwa na Man U

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger, ametetea uamuzi wake wa kumpumzisha Alex Oxlade-Chamberlain na nafasi yake kuchukuliwa na Andrey Arshavin wakati walipolazwa mabao 2-1 na Manchester United.

Wenger akitetea uamuzi wake wa kumtoa Chamberlain na kumuingiza Arshavin

Baadhi ya mashabiki wa Arsenal walisikika wakizomea wakati Oxlade-Chamberlain, aliyekuwa chachu ya kupatikana bao la kusawazisha la Arsenal, alipompatia pasi nzuri mfungaji Robin van Persie alipopumzishwa.
"Nimekuwa meneja kwa miaka 30 na nimeshabadilisha wachezaji mara 50,000. Siwajibiki kueleza sababu za kumpumzisha mchezaji kwa mtu yeyote," alisema.
Arsenal iko nyuma ya Chelsea wanaoshilikia nafasi ya nne kwa pointi tano katika mbio za kuwania kufuzu kwa ajili ya kuwania Ubingwa wa Ulaya msimu ujao.
Oxlade-Chamberlain alikuwa mmoja wa wachezaji waliong'ara kwa Arsenal katika mtanange huo uliochezwa katika uwanja wa Emirates.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 18, ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuanza kucheza mechi yake ya Ligi Kuu ya England, alikuwa akimlisha sana mipira Van Persie wakati wa kipindi cha pili ambapo Arsenal walionekana kucharuka.
"Naelewa mashabiki wamechukizwa kutokana na kumbadilisha Oxlade-Chamberlain, hasa baada ya mabadiliko hayo yaliposhindwa kuzaa matunda, lakini alianza kuchoka," Wenger alifahamisha kutokana na uamuzi wake wa kumpumzisha winga huyo wa zamani wa Southampton.
"Wiki hii alikuwa akiumwa. Arshavin ni nahodha wa timu ya taifa ya Urusi. Una kijana mwenye umri wa miaka 18 akiwa ndio anaanza kwa mara ya kwanza mechi ya Ligi Kuu na mchezaji ambaye ni nahodha wa timu ya taifa ya nchi yake na watu wanahoji kwa nini nimefanya mabadiliko hayo?"
Alipoulizwa namna kufungwa huko kulivyoiathiri timu yake, Wenger alisema ilikuwa ni mechi ya Arsenal "ambayo isingepaswa kupoteza" kabla ya kuongeza: "Imetuweka katika nafasi ngumu sana."
Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson alisema kikosi chake kilistahili kushinda hali iliyowaweka pointi tatu nyuma ya Manchester City wanaoongoza ligi kwa sasa.
"Hatimaye nilihisi kikosi chetu kilikuwa imara," alisema. "Hongera kwa wachezaji nafasi ya ulinzi, ambao walifanya kazi kubwa.
Alipoulizwa juu ya kuikamata Manchester City, alisema: "Itakuwa ni kibarua kigumu kwetu sote."

Drogba aing'arisha Ivory Coast kombe la mataifa ya Afrika


Ivory Coast imeanza kampeni ya kunyakua Kombe la Mataifa ya Afrika kwa ushindi dhidi ya Sudan walionekana kusumbua.
Nahodha Didier Drogba alifunga bao kwa kichwa kutokana na krosi iliyochongwa na Salomon Kalou, lakini haukuwa ushindi wa kujivunia sana kwa timu inayopewa nafasi kubwa ya kunyakua kombe hilo.
Sudan itakuwa imefurahi kutokana na kandanda iliyoonesha wakati walipowasumbua Ivory Coast ambayo inajengwa na wachezaji wengi nyota wanaocheza kandanda ya kulipwa Ulaya.
Ivory Coast inamatumaini itafanya vizuri katika mchezo ujao dhidi ya Burkina Faso.
Na mshambuliaji wa Angola Manucho aliipatia ushindi Angola dhidi ya Burkina Faso katika mechi yao ya ufunguzi ya kundi B michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika.
Baada ya kosakosa za kipindi cha kwanza, Angola ilifanikiwa kupachika bao la kwanza lililofungwa na Mateus aliyetumia makosa ya walinzi wa Burkina Faso kuokoa mpira.
Alain Traore baadae akaisawazishia Burkina Faso kwa mkwaju wa free-kick umbali wa yadi 25.
Lakini mshambuliaji wa zamani wa Manchester United Manucho aliifungia bao la pili Agola baada ya kuipangua ngome ya Burkina Faso.
Bao hilo la Manucho limeifanya Angola maarufu kwa jina la Palancas Negras, kuongoza kundi B baada ya mapema Ivory Coast kupata ushindi mwembaba wa bao 1-0 dhidi ya Sudan.
Burkina Faso walitibitishwa kushiriki michuano hiyo tarehe 10 mwezi wa Januari baada ya madai ya Namibia kutupwa pale waliposema Burika faso walimchezesha mchezaji asiyestahiki katika michezo ya kufuzu.

Monday, January 23, 2012

Bob Junior apiga show nyumbani kwa "jimama" alipwa milioni 7

Msanii wa bongo fleva ambaye ni muimbaji na mtayarishaji wa muziki (Producer) na anajulikana kama Rais wa wasafi,rais wa masharobaro,shombeshombe hivi karibuni alipiga show nyumbani kwa mama mmoja mwenye mahela ya kufa mtu na kulipwa pesa taslimu shilingi za kitanzania milioni 7 bila punguzo,hapa namzungumzia Raheem Rummy Nanji a.k.a Bob Junior.


Raheem Nanji a.k.a Bob Junior katika moja ya show zake

Katika mahojiano ya Bob Junior na radio moja jijini Dar es salaam alifunguka na kuelezea jinsi ilivyokuwa. "Aaah mimi nilipewa issue kuwa kuna mama anahitaji ukapige show maeneo ya Masaki nikakubali kwa malipo ya milioni 5" Alisema Bob Junior.
Huku akitegemea labda akifika atakuta nyomi la watu wakimsubiri atoe show, Bob Junior alishangaa kuingia kwenye nyumba ya jimama lililoshiba pesa huku mama huyo akiwa peke yake,"Nilipofika nyumbani kwake nilishangaa yupo peke yake,nikamuuliza nitafanyaje show? mama akajibu we fanya show usijali".alisema Bob Junior.

Kutokana na mshtuko jimama lilimtolea uvivu Bob Junior na kumuuliza unataka kiasi gani? tofauti na mapatano ya awali safari hii Bob Junior akataka alipwe shilingi milioni 7, bila ajizi mama akakubali kutoa dau la milioni 7 ili apate show huku akiwa peke yake hapo katika "bangalow" lake.

Baada ya mama kukubali kutoa milioni 7 Bob Junior alianza kutoa show."Kweli nilipiga show huku mama akiwa peke yake, kwanza nilipiga sebene la dakika kadhaa yaani mama alicheka sanaaaa" alisema Bob Junior.
Mtangazaji wa radio hiyo alipotaka kujua kama baada ya show mama hakumpa usumbufu mwingine? Bob Junior alifunguka kama ifuatavyo,"Hamna kitu mimi baada ya kupiga show nikatambaa,mimi pale nilienda kikazi nilipopata changu nikatambaa,au nimefanya vibaya?" Bob Junior alimuuliza mtangazaji.

Man City kiboko, Man United yairarua Arsenal

Manchester United imezidi kuipa shinikizo Manchester City iliyo kwenye kilele cha Ligi kuu ya England kufuatia mkwaju wa Danny Welbeck dakika chache kabla ya mechi kumalizika.
Mwanzoni mwa mechi hii United ilikua nyuma kwa pointi sita baada ya Manchester City kuirarua Tottenham hotspurs 3-2 kwenye uwanja wa Ettihad mapema siku ya jumapili.
Man City ipoiadhibu Tottenham.

Manchester United iliongoza kwa bao la Antonio Valencia dakika moja kabla ya kipenga cha mapumziko kuipa klabu yake bao 1-0. Bao hilo lilifutwa na la nahodha wa Arsenal katika kipindi cha pili na kuonekana kama liliowaamsha wachezaji wa Arsenal.
Mabadiliko yaliyofanywa na pande hizi mbili hayakuonekana kubadili mchezo ingawa wadadisi wengi wanajiuliza sababu iliyomfanya Arsene Wenge kumuondoa mchezaji wake aliyeonyesha mchezo mzuri Alex Oxlade-Chamberlain.
Arsenal ilipolambwa na Man United
Licha ya juhudi na kuonyesha matumaini ya kuongezea mabao kwa Arsenal Manchester United ikitumia uzowefu wake na kuzingatia mpango wake waliokuja nao waliendelea kuizuia Arsenal isifurukute na kama ilivyo tabia yao ya kukamilisha tamaa yao dakika za mwisho,zikisalia dakika tisa kabla ya kumalizika kwa mechi Danny Welbeck akatikisa nyavu za Arsenal na kuipatia ushindi na pointi tatu. Arsenal 1 Manchester United 2.

Friday, January 20, 2012

Ucheshi wa Computer (computer humor)

SilentFun The Best Group Join It

SilentFun The Best Group Join It

SilentFun The Best Group Join It






SilentFun The Best Group Join It

Vifahamu viwanja na timu Kombe la mataifa ya Afrika Equatorial Guinea na Ratiba kamili


Ramani ikionesha viwanja vitakavyotumika kombe la mataifa ya Afrika


Uwanja wa Bata,Estadio de Bata


Uwanja wa Malabo,Malabo stadium

Group A
GUINEA EQ.
LIBYA
SENEGAL
ZAMBIA
 
Group B
COTE D’IVOIRE
SUDAN
BURKINA FASO
ANGOLA

Group C
GABON
NIGER
MOROCCO
TUNISIA

Group D
GHANA
BOTSWANA
MALI
GUINEA
                                     RATIBA KAMILI KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA
 
Group matches/Matches de groupe
No.
Match
Group(e)
Date
Time/Heure
Venue/Lieu
01.
GUINEA EQ. vs. LIBYA
A
21/01/2012
19H:30
Bata
02.
SENEGAL vs. ZAMBIA
A
21/01/2012
22H:00
Bata
03.
COTE D’IVOIRE vs. SUDAN
B
22/01/2012
17H:00
Malabo
04.
BURKINA FASO vs. ANGOLA
B
22/01/2012
20H:00
Malabo
05.
GABON vs. NIGER
C
23/01/2012
17H:00
Libreville
06.
MOROCCO vs. TUNISIA
C
23/01/2012
20H:00
Libreville
07.
GHANA vs. BOTSWANA
D
24/01/2012
17H:00
Franceville
08.
MALI vs. GUINEA
D
24/01/2012
20H:00
Franceville
09.
LIBYA vs. ZAMBIA
A
25/01/2012
17H:00
Bata
10.
GUINEA EQ. vs. SENEGAL
A
25/01/2012
20H:00
Bata
11.
SUDAN vs. ANGOLA
B
26/01/2012
17H:00
Malabo
12.
COTE D’IVOIRE vs. BURKINA FASO
B
26/01/2012
20H:00
Malabo
13.
NIGER vs. TUNISIA
C
27/01/2012
17H:00
Libreville
14.
GABON vs. MOROCCO
C
27/01/2012
20H:00
Libreville
15.
BOTSWANA vs. GUINEA
D
28/01/2012
17H:00
Franceville
16.
GHANA vs. MALI
D
28/01/2012
20H:00
Franceville
17.
GUINEA EQ. vs. ZAMBIA
A
29/01/2012
19H:00
Malabo
18.
LIBYA vs. SENEGAL
A
29/01/2012
19H:00
Bata
19.
SUDAN vs. BURKINA FASO
B
30/01/2012
19H:00
Bata
20.
COTE D’IVOIRE vs. ANGOLA
B
30/01/2012
19H:00
Malabo
21.
GABON vs. TUNISIA
C
31/01/2012
19H:00
Franceville
22.
NIGER vs. MOROCCO
C
31/01/2012
19H:00
Libreville
23.
BOTSWANA vs. MALI
D
01/02/2012
19H:00
Libreville
24.
GHANA vs. GUINEA
D
01/02/2012
19H:00
Franceville

Quarter Finals – ¼ de finale
25.
1st A vs. 2nd B
04/02/2012
17H:00
Bata
26.
1st B vs. 2nd A
04/02/2012
20H:00
Malabo
27.
1st C vs. 2nd D
05/02/2012
17H:00
Libreville
28.
1st D vs. 2nd C
05/02/2012
20H:00
Franceville
Semi-Finals - ½ Finale
29.
Win. 25 vs. Win. 28
08/02/2012
17H:00
Bata
30.
Win. 27 vs. Win. 26
08/02/2012
20H:00
Libreville

3rd Place
match – Match de classement
31.
Loser 29 vs. loser 30
11/02/2012
20H:00
Malabo

Final/Finale
32.
Win. 29 v Win. 30
12/02/2012
20H:00
Libreville

Messi na Cristian Ronaldo nani zaidi ? tazama video hii ya maujuzi yao