Monday, February 13, 2012

THE LATE WHITNEY HOUSTON PHOTOS







\

Whitney Houston’s Tumultuous Final Days



Anyone who'd followed reports of Whitney Houston's bizarre behavior in the days leading up to the Grammys had to have been "shocked, but not surprised" at reports of her demise, as the saying goes. Thursday in particular had been an obviously rough day in public for the troubled singer, whose appearance and behavior raised eyebrows among reporters, photographers, and regular folks who witnessed her erratic rounds.

First she first visited Brandy, Monica, and Clive Davis at rehearsals for the mogul's pre-Grammys party, where a Los Angeles Times reporter described her as reeking of alcohol, "visibly bloated," and "disheveled in mismatched clothes and hair that was dripping wet with either sweat or water." According to the Times, when Houston wasn't mugging and gesticulating wildly for Brandy and Monica — who were doing a media junket, as well as preparing a duet — she was alternately skipping around the lobby or "wandering aimlessly" around the Beverly Hills Hotel grounds. Reportedly, guests had even called security to report the singer doing handstands by the hotel pool.
Houston's Thursday was about to get worse… way worse. That evening, she attended a party headlined by Kelly Price at the Tru nightclub in Hollywood. As she exited, seeming intoxicated, photographers took close-ups of her legs, which appeared to be spotted with blood streaks, along with scratches on her wrists.
Wherever the blood and scratches came from, it wasn't from any publicly visible scuffle — although that had reportedly narrowly been avoided. According to the Hollywood Reporter, Houston got into a loud argument at the party with "X Factor" finalist Stacy Francis in the club's VIP section, shortly after they appeared on stage together. A source told THR that Houston got "belligerent" and that Houston's boyfriend, Ray J, actually stepped in to defend Francis' intentions. "Hands were raised" in anger, it was claimed.
Whitney Houston's moving national anthem at Super Bowl XXV inspired America
Houston's final public performance happened at the club that night. It lasted just under a minute, as she sang "Jesus Loves Me" with Price in an impromptu, ramshackle duet captured by any number of videographers in the crowd. Perhaps needless to say, she wasn't in her very best voice for what turned out to be her swansong appearance.
Houston had a much quieter Friday and early Saturday, at least publicly, even as photos of a not-so-hot mess circulated around the web. Whether the singer knew she was the butt of jokes and dire speculation or was oblivious to it in her final hours is unknown.
Just two months ago, "Saturday Night Live" had spoofed the star as out-of-touch and out-of-it in a sketch where alumnus Maya Rudolph reprised her famous Houston impression. In the skit, a hyperactive Rudolph/Houston was brought in to give Miley Cyrus some drug counseling, bragging, "I've been clean and sober since 2013."
Coming to be regarded as a lush or addict in her last months had to be a harsh rebuke for someone who'd claimed to have cleaned up while attempting a comeback a few years earlier. But the events of the past year made it clear that, in contrast to celebrated redemption stories like Robert Downey Jr.'s, rehab hadn't really taken for Houston.
Her sobriety had been a matter of public concern since the late '90s. A common public misassumption had been that if she ever got out from under the sway of husband Bobby Brown, she would be all right. "He was my drug," she told Oprah in 2009, two years after their divorce, after apparently cleaning up. "I didn't do anything without him. I wasn't getting high by myself."
Whitney Houston remembered at Clive Davis's pre-Grammy gala
But more recently, it'd started to look like her ex-husband was no longer the sole driving force of her substance abuse, if ever he had been. Last May, a Houston rep acknowledged that the singer was involve in outpatient rehab for ongoing drug and alcohol problems.
That was right around the time Houston and her daughter, Bobbi Kristina Brown, made the news for getting a little too boisterous in the front row at a series of Prince concerts in L.A. Although Prince's reps later denied there was any dispute, it was reported at the time that Prince was so fed up with Houston's behavior and requests to get up on stage that he supposedly banned her from coming to the rest of his run.
All that was just a couple of months after the March 2011 edition of the National Enquirer that featured a double-page photo spread of Bobbi Kristina allegedly snorting lines of cocaine at a party (albeit with her mom nowhere in sight).
The tabloids also reported last year that Houston's fortune had run out. With no new albums on the horizon, her best hope for career renewal was the movie Sparkle, in which she played a supporting role as Jordin Sparks' mom. The film — her first since The Preacher's Wife in 1996 — was shot late last year and will come out in August, accompanied by a soundtrack that includes two new Houston tunes.
Otherwise, Houston didn't have much of a career going at the time of her death. Her should've-been comeback album, 2009's I Look to You, sold about a million copies in the U.S. — far from a shameful number, but also far from the 13 million copies for which her 1985 debut had been certified. The most embarrassing factor was that none of the singles from the album rose above No. 70 on the Hot 100. (Houston's only top 10 single of the 2000s was a re-release of "The Star-Spangled Banner" in the patriotic days following 9/11.)
Whitney's life in photos
Houston's only major tours in the last decade were overseas, far away from the critical eyes of the American media. In September 2009, she did a short comeback concert for "Good Morning America" in Central Park. The blurring of the line between entertainment and news on morning shows became apparent as hosts Diane Sawyer and Robin Roberts lauded Houston's performance on their show, even as every other media outlet was reporting on how the voice of a generation could no longer handle the demands of even an abridged show, clean or not.
The reports of ongoing trouble for Houston never served her image the way they might have, say, Amy Winehouse's. America never wanted to think of her as a bad girl, just a perhaps more grown-up version of the Girl Next Door who'd seemed so wholesome wanting to dance with somebody who loved her. But with the chops as well as the image failing her, there wasn't much left to make a thriving recording or certainly touring career out of.
In recent days, one solution for returning Houston to the limelight without subjecting her singing voice to harsh scrutiny had seemingly been arrived at. Rumors had been floated — and published by the Hollywood Reporter — that she was up for contention as a judge on "The X Factor." Simon Cowell told Piers Morgan that Houston had not actually been approached, but that in response to the news reports (which he implied might have been instigated by Houston's camp), his team had planned to have a meeting about considering her on Monday.
Bobby Brown breaks down
But getting in that public scuffle Thursday night with Stacy Francis, an admirer who was one of the Season 1 "X Factor" finalists, might not have done Houston any favors, had she lived to come up for contention with Cowell and his producers this week.
Even in as high-profile a period as Grammy week, Houston couldn't seem to shy away from small acts of self-sabotage. Her fans can only hope it's the years when pride predominated that ultimately define her legacy.

ZAMBIA BINGWA AFRIKA, DROGBA,TOURE,GERVINHO WAIKOSESHA UBINGWA IVORY COAST

Nahodha wa Zambia Chris Katongo na wenzake wakishangilia ubingwa
Golikipa wa Zambia Mweene akishangilia baada ya Drogba kukosa penati katika kipindi cha kwanza.

Mabingwa wapya wa Afrika Zambia "Chipolopolo"

Zambia imechukua ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika 2012 baada ya kuwafunga Ivory Coast kwa mikwaju ya penati 7-8.
Mchezo huo ulimaliza dakika 90 za kawaida, kabla ya kwenda muda wa ziada, na hadi katika mikwaju ya penati.

Chipolopolo


Mshambuliaji wa Ivory Coast Max Gradel akijaribu kumtoka mlinzi wa Zambia Nkausu


Zambia wakishangilia Baada ya Sunzu kutupia penati ya mwisho na ya ushindi.

Awali nahodha wa Ivory Coast, Didier Drogba alikosa penati ambayo ingeipa ushindi kabla ya kumalizika kwa dakika 90 za kawaida.
Ivory Coast wamekosa penati 2 kati ya walizopiga ambapo Kolo Toure na Gervinho walikosa mikwaju hiyo.
Ivory Coast wataendelea kusubiri kunyakua kombe hilo, licha ya kuwa na wachezaji kadhaa wanaocheza Ulaya hasa katika Ligi Kuu ya England.
Tembo wa Ivory Coast walipoteza katika mchezo wa fainali mwaka 2006 dhidi ya Misri kwa mikwaju ya penati.
Lakini kwa Chipolopolo, ambao wamewahi kushika nafasi ya pili mara mbili, wamemaliza kwa ushindi kwa kuhanikizwa na vifo vya wachezaji wenzao mwaka 1993, baada ya ndege yao kuanguka karibu na uwanja ilipochezewa fainali mjini Libreville.
Mara ya mwisho kwa timu hiyo kutoka Kusini mwa Afrika kufika fainali ilikuwa mwaka 1994, mwaka mmoja tu baada ya wachezaji 18 wa nchi hiyo kupata ajali ya ndege karibu na mji mkuu wa Gabon.
Wakielekea katika mchezo wa fainali, wachezaji hao wa sasa walisema wanahisi nguvu kutokana na kukumbuka janga lililowapata wenzao.
Kwa kushinda mchezo wa fainali, wameonesha dhamira ya kuwashinda wapinzani wao ambao walikuwa wakipewa nafasi kubwa ya kupata ushindi.
Penati zote za mchezo Zambia na Ivory Coast

Friday, February 10, 2012

BIG UP TIMBULO WANAOSEMA NA WASEME


Timbulo

BIG UP TIMBULO,..Wale wote wanaosema Timbulo kakopi ule wimbo wa Domo langu kutoka kundi la Xmalea wa Ivory Coast nawapinga vikali, Timbulo amekiri aliipata hiyo ngoma kabla na akachukua idea tu na sio kukopi kama inavyosemwa mitaani.
Kwa kifupi nampongeza sana Timbulo hata kama idea ni ya mtu lakini ametumia ujuzi mwingi katika kutunga na kuimba mpaka song likatoka poa..wanaomsema na nyinyi jaribuni kukopi halafu mtoe song likubalike kama mnaona ni rahisi.

Song la Timbulo Domo langu

Nimesikiliza kipindi mtoto Adam Mchomvu anamponda Timbulo kwa kusema eti kakopi na kupesti, nadhani elimu Adam hana ya nini maana ya kukopi na kupesti. Kukopi na kupesti inamaana haubadilishi kitu unachukua kitu kama kilivyo toka sehemu moja na kukiweka sehemu nyingine bila kupunguza ama kuongeza kitu.
Katika song waliloimba hao wa Ivory Coast wameimba lugha tofauti na melody tofauti, Hapo utaona kazi kubwa ameifanya Timbulo ya kupata idea halafu akatafuta mashairi yake binafsi yakaendana na ile idea halafu akaimba kwa ustadi mpaka ikakubalika sio kazi ndogo kama unabisha jaribu wewe uone kama utapata kitu.
Ni kazi sana kuchukua idea ya mtu halafu ukatoa kitu kikakubalika kuliko kile kilichokupatia idea kuliko kutoa kitu chako binafsi, mara nyingi hata wasanii wa nje huwa wanajitahidi kutoa track kali na inapofikia kutoa remix wanahakikisha iwe kali kuliko track halisi, haina maana ukitoa track kali ikapendwa halafu ukatoa remix ikawa utumbo inakuwa haina maana.
Mwisho kabisa Adam na wenzako naomba niwape maana ya sanaa na msanii inawezekana hamjui ndio maana mnaropoka tu.

Sanaa ni upangaji wa dhana kulingana na hisia na mawazo ya msanii, na msanii ni mtu anaepanga dhana kulingana na hisia na mawazo yake.
Timbulo songa mbele wanaopiga kelele ni mashabiki wa muziki na sio wapenzi wa muziki kwani kuna tofauti kubwa kati ya mshabiki na mpenzi.
Big up Timbulo kama kukopi ni rahisi hakuna asietaka track yake iwe juu waambie na wao wakopi tuone.

PINDA anastahili kuwajibishwa


Waziri mkuu Mizengo Pinda

Madaktari wamerudi makazini baada ya kuafikiana na serikali kutoka katika mgomo uliodumu kwa takribani wiki mbili.
Sasa basi kama serikali ina uwezo wa kuwasikiliza madaktari na wakaafikiana warudi makazini kama alivyofanya waziri mkuu Mh Mizengo Kayanza Pinda, kwanini hawakuwasikiliza mapema na wakaafikiana kabla ya watanzania wasio na hatia kupoteza maisha yao kutokana na mgomo huo?
Ina maanisha serikali imefanya uzembe kwa kitu ambacho wana uwezo nacho,na uzembe huo umesababisha usumbufu,maumivu,gharama,hasara na VIFO vya watanzania walipa kodi walioiweka serikali hii madarakani, je ni nani anawajibika katika hili? nani atafidia gharama,muda,maumivu na VIFO vya watanzania wasio na hatia kutokana na mgomo huo wa madaktari uliodumu kwa takribani wiki mbili?
Kwa ukweli huu je? nitakuwa nina makosa kama nikisema Viongozi wote wenye dhamana katika serikali hii wawajibike kwa hili, nina maanisha kuanzia Rais wa nchi na "mnyororo" wote unaofuatia baada ya yeye.

Watanzania wenzangu nina uchungu mkubwa kutokana na vifo vya watu wasio na hatia kupoteza maisha kwa uzembe wa watu wachache tena ambao wapo kwa ridhaa ya wananchi walioteseka na waliopoteza maisha kutokana na uzembe wa serikali wa kutokuwasikiliza wananchi wanahitaji nini kwa wakati gani. Ni nani serikalini alikuwa hajui kuwa madaktari wanaandaa mgomo? bila shaka madaktari ni watu wasomi na makini sidhani kama walikurupuka tu asubuhi na kusema leo tunagoma bila sababu na bila taarifa, kama matatizo na sababu zao kugoma zilijulikana kwanini wakapuuzwa na wao kufikia hatua ya kugoma na kusababisha hasara,maumivu na VIFO vya watanzania walipa kodi wasio na hatia? wapo wanapaswa kuwajibika kuanzia kiongozi aliepokea taarifa hizo kama alitakiwa kuzifikisha kwa anaefuatia baada ya yeye na anaefuatia mpaka mwenye maamuzi ya mwisho wote hawa wanapaswa kuwajibika.

Naipinga kauli ya Waziri mkuu Mizengo Pinda alipotangaza kuwa serikali imeamua kuwasimamisha kazi naibu katibu mkuu Wizara ya afya na ustawi wa jamii mama Blandina Nyoni na mganga mkuu wa serikali Dk Deo Mtasiwa, na kusema kuwa swala la mawaziri kuwajibika ni la kisiasa. Hapa mkuu sijakuelewa kabisa swala la huduma na haki ya jamii wewe unasema ni la kisiasa? BIG NO, wanapaswa kuwajibika haraka sana.

Watanzania wenzangu hatutaonekana wakorofi au hatufai kama tukiishinikiza serikali kuwawajibisha wote waliopo katika utekelezaji wa madai ya madaktari kwa kuwa hakuna lolote linaloweza kulipa machungu ya wafiwa na maisha ya watanzania waliopoteza maisha pasipo hatia
MUNGU IBARIKI TANZANIA     MUNGU WABARIKI WATANZANIA HASA WALALAHOI

Al-Shabaab waungana rasmi na AL-Qaeda waapa kuiangamiza Marekani

Mkuu wa Al-Shabaab Ahmed Godane

Kundi la Waislam wenye itikadi kali nchini Somalia, al-Shabaab, limetangaza kuwa linaungana na kundi la al-Qaeda.
Tamko hilo limetolewa katika picha ya video iliyotolewa na makundi hayo mawili

Yusuf Garaad wa Idhaa ya Kisomali ya BBC ambaye ameitazama video hiyo amesema kundi hilo ambalo jina lake kamili ni Harakat al Mujahiddin al Shabaab, limetangaza rasmi kuungana na al-Qaeda.
Madai ya muungano huo yametolewa na kiongozi wa al-Shabaab, Ahmed Godane, au maarufu kama Abu Zubair.
Mkuu wa al-Qaeda, Ayman al-zawahiri

Akizungumza kwa lugha ya Kiarabu,Abu Zubair amesema sasa watatii maelekezo kutoka kwa kiongozi wa al-Qaeda, Ayman al-Zawahiri.
Akizungumzia Marekani, Ahmed Godane amesema wakati wa dola pekee duniani- Marekani - sasa umefikia mwisho na kuwa utawala wa Uislam ndio utachukua mamlaka.
Kiongozi wa al-Qaaeda, Ayman al-Zawahiri, ambaye pia ameonekana katika video hiyo, ameisifia al-Shabaab na kukiri na kukubali kwa kundi hilo kuungana na al-Qaeda.
Amesema hizo ni habari njema kwa wafuasi wake.

Wapiganaji

Al-Zawahiri amesema Somalia itakuwa ngome ya Jihad katika pembe ya Afrika na kuongeza kuwa watateketeza kile alichotaja kuwa ni kiburi cha majeshi ya Kikristo kutoka Marekani, Ethiopia na Kenya dhidi ya Wasomali.
Ametoa wito kwa al-Shabaab kulinda watu wake hasa wale ambao ni dhaifu, na pia kutaka kwa wananchi wa Somalia kuunga mkono uamuzi wa vijana wao, akimaanisha al-Shabaab.
Al-Shabaab ni kundi lenye wapiganaji maelfu kadhaa, wengi wao wakiwa ni Wasomali. Hata hivyo wanao pia wapiganaji wa kigeni kutoka katika nchi zinazoizunguka Somalia na hata sehemu nyingine duniani.
Mitindo yao ya upiganaji ni pamoja na mabomu ya kujitoa mhanga na pia ya kutegwa ndani ya magari.

Mwenendo

Al-Shabaab kwa sasa inadhibiti maeneo kadhaa ya kusini na kati ya Somalia.
Katika miezi kadhaa iliyopita wamekuwa wakibanwa kutoka pande kadhaa. Mjini Mogadishu wanapambana na majeshi ya kulinda amani ya Umoja wa Afrika, Amisom, yenye wanajeshi kutoka Uganda, Burundi na Djibouti. Majeshi hayo yanadhibiti zaidi mji mkuu, Mogadishu.
Upande wa kusini, majeshi ya Kenya yameshambulia ngome za al-Shabaab ardhini, baharini na angani. Majeshi ya Ethiopia pia yanashambulia kundi hilo kwa upande wa kaskazini na tayari wameteka mji wa Beled Weyne, mji muhimu katikati mwa Somalia.
Kuungana kwa al-Shabaab na al-Qaeda huenda kukabadili mwenendo mzima wa mzozo wa Somalia.