Thursday, February 16, 2012

ARSENAL NYANYA YASASAMBULIWA 4-0 NA AC MILAN

Robinho alikuwa mwiba mkali kwa Arsenal

Matumaini ya Arsenal kuvuka salama robo fainali za klabu bingwa Ulaya ni kitumbua kilichotiwa mchanga, baada ya Jumatano jioni kunyoroshwa magoli 4-0 na AC Milan ya Italia katika mechi ya mkondo wa kwanza, ikiwa ni kati ya timu 16 zilizosalia katika mashindano hayo.
The Gunners hawakuwa na lao tangu Kevin-Prince Boateng alipoiwezesha Milan kupata bao la kuongoza.
AC MILAN 4-0 ARSENAL

Mchezaji wa zamani wa Manchester City, Robinho, aliongezea bao la pili kwa kichwa, na kuongezea na la tatu, kuihakikishia timu yake ilikuwa na uhakika wa kupata ushindi.
Zlatan Ibrahimovic alikamilisha kibarua kwa kuandikisha bao la nne la penalti, na wakati huohuo akiandikisha historia kwa upande wa Arsenal, ikiwa ndio matokeo mabovu zaidi ya Arsenal kufungwa kwa mabao mengi kiasi hicho katika pambano la Ulaya.
Miaka minne iliyopita, Arsenal ilikuwa ni timu ya kwanza ya Uingereza kufanikiwa kuishinda AC Milan ikiwa nyumbani, katika uwanja wa San Siro, wakati ilipopata ushindi wa magoli 2-0 katika mechi ya mkondo wa pili, na kuiondoa timu hiyo kutoka vilabu 16 vilivyokuwa vimesalia katika mashindano hayo ya klabu bingwa.

Benchi la ufundi la Arsenal likiwa limelowa kwa kipigo cha 4-0

Arsenal ya wakati huo ilikuwa tofauti kabisa na timu iliyoshiriki katika mchezo wa Jumatano jioni.
Mwaka 2008 Arsenal ilikuwa na uhodari mkuwa wa ulinzi, na ilicheza kwa ustadi na ikawa ni burudani kwa mashabiki wengi, kinyume na Arsenal ilivyopambana katika mechi hiyo ya San Siro.
Mshambulizi Robin van Persie amekuwa ni nyota msimu huu, lakini katika uwanja wa San Siro, inaelekea alikuwa zaidi ni abiria, na mkwaju wake uliokuwa na matumaini katika kipindi cha pili ukizuiwa na Christian Abbiati, na hata nguvu mpya za Thierry Henry alipoingia uwanjani baadaye hazikubadilisha lolote.
Bila shaka akiwa katika ndege kuelekea New York, Henry atawaza ni kwa nini aliamua kuichezea tena Arsenal.

Mambo magumu, wachezaji wa Arsenal Thierry Henry,nahodha Van Persie,Song (17) na Djourou(20) wakijadili jambo kabla ya kuanza mpira baada ya goli la tatu.

Meneja wa Arsenal alikuwa na matumaini kwamba Henry angelibadilisha mambo alipoingia katika kipindi cha pili, lakini hata kabla ya kuupata mpira, Milan tayari walikuwa wameandikisha bao la tatu.
Wenger atawaza pia juu ya umuhimu wa kufuzu kushirikishwa katika mechi za klabu bingwa, halafu kupigwa mabao mengi kiasi hicho.

Wednesday, February 15, 2012

PLAYBOY CALENDAR 2012



JANUARY



FEBRUARY




APRIL



MAY




JUNE



JULY


AUGUST


SEPTEMBER


OCTOBER


NOVEMBER


DECEMBER

Zambia yaingia 50 bora viwango vya FIFA, 43 Duniani ya 4 Afrika



Timu ya soka ya Zambia maarufu kama Chipolopolo wamepanda kwa nafasi 28 juu na kuingia katika 50 bora za viwango vya soka vya FIFA baada ya miaka 11 tangu ilipowahi kuwa katika 50,sasa Zambia inashika nafasi ya 4 kwa ubora wa soka barani Afrika, Zambia imepata mafanikio hayo baada ya kunyakua ubingwa wa Afrika kwa kuinyuka Ivory Coast kwa mikwaju ya penati 8 kwa 7 katika fainali kali na ya kusisimua iliyochezwa nchini Gabon katika jiji la Libraville.

Katika viwango hivyo vya soka vilivyotolewa na FIFA Ujerumani imeivuka Uholanzi na kuwa ya pili wakati huohuo Ureno(6) imepanda nafasi 1,Ivory Coast(15) imepanda nafasi 3,Mali(44) imepanda kwa nafasi 25, Ghana (23) imepanda nafasi 3 na Italy(8) imepanda nafasi 1 nazo zikipata maendeleo mazuri katika viwango vya soka Ulimwenguni.

HAKUNAGA-By Suma Lee

DUSHELELE-by Alikiba

Barcelona yaichakachua Bayer Leverkusen 3-1


Alexis Sanchez akipigilia msumari wa pili

Katika mechi hiyo magoli ya Barcelona dhidi ya Bayer Leverkusen wafungaji wa magoli ya Barca ni Alexis Sanchez (2)dk 41,54 ,Messi(1)dk 88 na la kufutia machozi la Bayer Leverkusen lilifungwa na Kadlec dk 50

Beki wa Bayer Leverkusen akiokoa mpira mbele ya Messi aliekuwa akisubiri kuutupia wavuni.


Leonel Messi akichanja mbuga katikati ya beki za Bayer leverkusen

Bayer Leverkusen 1-3 Barcelona

Arsenal AC Milan kivumbi ligi ya mabingwa ulaya


Kocha wa Arsenal Arsene Wenger

AC Milan watakuwa na lengo moja la kuifunga timu ya England kwa mara ya kwanza tangu walipofanya hivyo dhidi ya Liverpool kwenye fainali ya Ligi ya Mabingwa mwaka 2007, wakati watakapowakaribisha Arsenal katika mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 bora ya mashindano hayo.
Milan iliyotwaa taji hilo mara saba kwa kuifunga Liverpool 2-1 jijini Athens miaka mitano iliyopita, baada ya hapo wamekuwa wakitolewa kwenye mashindano hayo na Arsenal, Manchester United na Tottenham Hotspur na alifanikiwa kupata sare dhidi ya Portsmouth kwenye hatua ya makundi ya Europa Ligi mwaka 2009.
Sasa wanakutana na Arsene Wenger kwa mara nyingine baada ya timu hiyo ya London kuwatoa Milan kwenye hatua ya 16 bora mwaka 2008.
Vinara hao wa Serie A, Milan watamtumia mshambuliaji wake Zlatan Ibrahimovic aliyefungiwa kucheza ligi kwa kumpiga kibao mchezaji baada ya kumaliza kifungo Jumamosi waliposhinda 2-1 dhidi ya wapinzani wao mbio za ubingwa wa Italia, Udinese huku chipukizi Stephan El Shaarawy na Maxi Lopez wakionyesha uwezo mkubwa wa kufunga.
Chipukizi El Shaarawy huenda akawekwa benchi ili kumpisha Ibrahimovic pamoja na kuwa kwenye kiwango cha juu kwa sasa na inavyoonekana kama mshambuliaji wa Sweden wataanza pamoja na Robinho.
Kocha Massimiliano Allegri ana wachezaji wengi majeruhi, lakini kumeonekana na mabadiliko kidogo na kutoa nafasi ya kurejea kwa kipa Christian Abbiati na beki wa kati Alessandro Nesta kuivaa Arsenal, ambayo imeshinda mechi zake zote za Ligi ya Mabingwa ilizocheza San Siro dhidi ya Milan.
Gennaro Gattuso na Alberto Aquilani bado ni majeruhi, lakini kuna nafasi ya Alexandre Pato na Kevin-Prince Boateng kuwepo kikosi leo.
Mabingwa watetezi Milan wanaongoza Serie A kwa tofauti ya pointi mbili, lakini Juventus inayoshika nafasi ya pili ina mchezo moja mkono.
“Ushindi wetu dhidi ya Udinese una maana kubwa, tumetoka kufungwa mechi tatu kati ya tano,” alisema kocha Allegri.
Milan, iliyofuzu kwa hatua hiyo pamoja na mabingwa watetezi Barcelona, hadi sasa wameshindwa kurudia mafanikio yao ya mwaka 2007.

MBINU za WENGER

Mafanikio katika mchezo huo ni mbinu atakayotumia Wenger kama atacheze kwa kujilinda zaidi na kutaka sare au kujaribu kushambulia ili kupata ushindi wake wa tatu dhidi ya Milan.

Wenger anatakiwa kujihadhari pia na mashambulizi ya Milan kwa kucheza kwa uangalifu zaidi, lakini kiungo wake Aaron Ramsey anaamini bao la ugenini linaweza kuwa jibu la mafanikio yao.Aliimbia Arsenal TV Online: “Kama tutacheza na kufanikiwa kupata bao na kurudi Emirates hayo yatakuwa matokeo ya kujivunia zaidi kwetu.
“Ni matumaini yangu, tutaweza kupata mabao mengi ya kuweza kuwaondoa kwenye mashindano.”
Vikosi:

AC Milan: 32-Christian Abbiati; 20-Ignazio Abate, 33-Thiago Silva, 5-Philippe Mexes, 15-Djamel Mesbah; 23-Massimo Ambrosini, 4-Mark Van Bommel, 10-Clarence Seedorf; 27-Kevin-Prince Boateng; 11-Zlatan Ibrahimovic, 70-Robinho
Arsenal: 13-Wojciech Szczesny; 3-Bacary Sagna, 5-Thomas Vermaelen, 6-Lauren Koscielny 17-Alex Song; 8-Mikel Arteta, 7-Tomas Rosicky, 16-Aaron Ramsey, 15-Alex Oxlade-Chamberlain; 10-Robin van Persie, 14-Theo Walcott

Mwamuzi: Viktor Kassai (Hungary).