Tuesday, March 27, 2012

GOAL OF THE WEEK

ZLATAN IBRAHIMOVIC - AC MILAN Vs ROMA

NITAREJEA-Diamond ft Hawa

HAOOOO-Mwasiti ft Chid Beeeeeenz

Man United yaichapa Fulham yang'ang'ania kileleni

Mshambulizi mwenye misuli Wayne Rooney alihakikisha timu yake Manchester United inapanda kileleni mwa ligi kuu ya Uingereza kwa kuichapa Fulham bao moja bila.
Rooney na Evans wakishangilia goli

Bao hilo lilifungwa katika dakika ya 29 ya kipindi cha kwanza pale Rooney alipopokea pasi safi kutoka kwa Jonny Evans.
Kwa ushindi huo sasa Mashetani wekundi wameipiku Man City kwa alama tatu.
Kufikia sasa timu zote zimecheza mechi 30 kila mmoja.
Manchester City sasa wanakibarua kigumu cha kuziba pengo la alama tatu kwani siku ya jumamosi tarehe 31 wataikaribisha Sunderland.
Vijana hao wa Roberto Mancini itawabidi waombe sana Man U wapoteze mechi yao ya siku ya Jumatatu ijayo tarehe 2 April watakapo watembelea Blackburn.
Hata hivyo mkufunzi wa Fulham Martin Jol amelalama kuwa walinyimwa mkwaju wa penalti.
Hii ni baada da ya Michael Carrick wa Manchester United kuonekana kumuangusha mshambulizi Danny Murphy katika eneo la hatari katika dakika ya 87.
Man United 1-0 Fulham

meneja huyo wa Fulham amenukulikwa akisema kuwa kila mtu aliyeshuhudia mechi hiyo alitarajia wapewe penalti.

Monday, March 26, 2012

JE WAJUA? (DID YOU KNOW?)

MAAMUZI YA TFF KUPENDELEA VILABU VIKUBWA YANAUA SOKA LETU(kusimamisha adhabu za wachezaji wa Yanga)

TFF kupitia kamati ya Usuluhishi na Nidhamu(kamati ya Tibaigana) imesimamisha adhabu walizopewa wachezaji mabondia wa Yanga, kwa madai kuwa kamati ya ligi ya TFF haina mamlaka ya kutoa maamuzi yaliyotolewa. maswali yanakuja;
1-nani alipeleka mashitaka kwenye kamati hiyo?
2-walikuwa wapi muda wote huo kusema kuwa kamati ile haina mamlaka?
3-Kamati ile ilitumia vielelezo vipi kutoa adhabu kwa wachezaji mpaka kamati ya usuluhishi na nidhamu iseme Tff hawajapeleka vielelezo?
4-Wamesimamisha adhabu zilizotolewa na kamati ya ligi na adhabu alizotoa refa zinaendelea,sasa mchezaji Mwasika aliyempa refa ngumi ya uso hakupewa hata kadi ya njano inakuwaje?
5-Kuna wachezaji kama Cannavaro wameshatumikia adhabu ya kadi aliyopewa je maamuzi mengine yatakayotolewa na kamati ya usuluhishi na nidhamu hayatamuathiri?
5-Kamati ya ligi imetoa adhabu ngapi na Hazikupingwa na kamati ya nidhamu na usuluhishi(kamati ya Tibaigana)?


Ninaamini kamati ya Ligi ya TFF ina watu makini na ni viongozi makini na hata aliyepeleka mashitaka kwenye kamati hiyo aliamini inaweza kufanya maamuzi na ndio maana kamati ikafanya kazi yake sasa hii kamati ya Tibaigana iliyotengua maamuzi hayo ninaamini walikuwa na taarifa ya maaamuzi ya kamati ya Ligi iweje wakakaa kimya mpaka sasa wakati wachezaji wameshatumikia adhabu waseme kamati haina hadhi ya kutoa maamuzi?

Naomba niwe muwazi katika hili sidhani kama adhabu hizo wangekuwa wamepewa wachezaji wa Oljoro au Coastal Union kamati ya Tibaigana ingehangaika kuzisimamisha na kutumia muda kukaa vikao vingine, ikumbukwe hapo gharama zimetumika kuita waandishi wa habari pale habari maelezo watu wakaacha kazi zao wakakaa kusikiliza maamuzi ya kamati ya Ligi na watu wakalipana posho na waandishi wakatumia gharama kuandika habari ya adhabu za wachezaji hao na wananchi wakatumia pesa zao kununua magazeti kupata habari hizo halafu mwisho wa siku pamoja na usumbufu na gharama zote hizo anatokea mtu na kusema maamuzi yametolewa na kamati isiyokuwa na mamlaka,najiuliza mlikuwa wapi muda wote huo kama sio hii kamati ya Tibaigana kufanya kazi kwa maslahi ya timu fulani?

Hakika soka letu kwa utendaji wa kubabaisha kama huu litaendelea kudidimia wadau tujiandae kupinga adhabu itakayotolewa na kamati ya usuluhishi na nidhamu ambayo kwa hili hatuna imani nayo.

SIMBA YAFANZA KWELI YAWARUDISHA ES SETIF ALGERIA VICHWA CHINI


Wachezaji wakisalimiana kabla ya mpambano huo kuanza

Timu ya soka ya Simba ya jijini Dar es salaam imefanya kweli katika kombe la shirikisho kwa kuifunga timu ngumu ya ES Setif kutoka algeria katika mechi ya awali iliyopigwa katika dimba kuu la Taifa jijini Dar es salaam kwa kuibuka na ushindi mnono wa bao 2-0.
Katika mchezo huo uliokuwa na upinzani mkali Waarabu walionekana kucheza mchezo wa kujihami huku wakifanya mashambulizi ya kushtukiza lakini ngome ya Simba iliyoongozwa na Kelvin Yondan sambamba na Nyosso wakisaidiwa vyema zaidi na beki za kushoto na kulia smbso ni Shomari Kapombe na Maftah na pale katika milingoti miwili alikuwepo Tanzania one Juma K Juma.
Katika mpambano huo uliohudhuriwa na mashabiki 41,000 na zaidi Mpaka mapumziko hakukuwa na timu iliyoweza kuliona lango la mwenzake.

Kosakosa langoni mwa Setif

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi zaidi hasa kwa timu ya Simba kana kwamba kocha alishawasoma Setif mchezo wao wa kutegea na kufanya mashambulizi ya kushtukiza kwa kucheza pasi fupifupi katika nusu yao na wanapofika nusu ya pili kuelekea langoni mwa Simba walikuwa wakipiga pasi ndefu.Simba kipindi hiki walikuja na kasi na kufanya mashambulizi mengi katika lango la Setif na tabu ililetwa langoni mwa Setif kwa juhudi kubwa za viungo waliocheza kwa ushirikiano mzuri kati ya Kazimoto,Machaku na Haruna Moshi"Boban" ambapo kwa kiasi kikubwa Simba wana kila sababu kujivunia beki ya kulia na kushoto yaani Maftah na Kapombe waliofanya kazi kubwa kupandisha mashambulizi mbele na hii ilileta nafuu kwa washambuliaji Okwi,Sunzu na Boban.
Felix Sunzu alitumika vizuri kuwaweka mabeki wa Setif katika wasiwasi na kujikuta wakimkaba kwa jihadi na kutoa mianya kwa Okwi na Boban kuleta mashambulizi langoni mwao.
Baada ya dakika 75 za ukame wa magoli ndipo jitihada za wachezaji wa Simba zilipozaa matunda wakati Mshambuliaji wa Kimataifa toka Uganda Emmanuel Okwi alipotupia kambani bao la kwanza na kuamsha shamrashamra kwa wapenzi wa Simba na hata wale wasio na mapenzi na Simba waliohudhuria katika dimba kuu la Taifa.









Mashabiki wa Yanga waliokuwa wakiibeza Simba lakini mwisho wa siku walitoka uwanjani na chupi yao mkononi na aibu tele

Goli la Okwi liliamsha morari kwa wachezaji wa Simba na Setif walioonekana kama wamezinduka toka usingizini na kuanza kusaka bao la kusawazisha lakini jitihada zao ziligonga mwamba pale Mshambuliaji mwingine wa Simba toka Zambia Felix Sunzu alipotupia kambani goli la pili katika dakika ya 80 baada ya kipa wa Setif kutema kombora la Machaku.