Monday, April 2, 2012
PAPISS DEMBA CISSE APELEKA KILIO LIVERPOOL,CAROLL AZOMEWA MWANZO MWISHO
Demba Cisse akipiga kichwa kilichoelekea kambani kuandika goli la kwanza la Newcastle
Mabao mawili yaliyofungwa na Papiss Cisse yamezidi kuiongezea Newcastle hamu ya kucheza mashindano ya Ulaya msimu ujao baada ya kuongeza machungu kwa Liverpool iliyocheza na wachezaji 10 tu katika pambano la Ligi Kuu ya Kandanda ya England.
Cisse alitumbukiza mpira kwa kichwa baada ya kulishwa mpira wa juu na Hatem Ben Arfa katika kipindi cha kwanza kabla ya kufunga bao la pili alipopokea pasi ya Demba Ba katika nusu ya pili ya mchezo.
Demba Ba na Demba Cisse wakishangilia goli
Kiwango cha chini ya kandanda kilichooneshwa na Liverpool, ambapo mshambuliaji wao wa kati Andy Carroll alioneshwa kadi ya manjano baada ya kujiangusha kwa makusudi katika eneo la Newcastle, pia ilishuhudia mlinda mlango wao Pepe Reina kutolewa nje kwa kuoneshwa kadi ya nyekundu.
Demba Cisse(9) akijiandaa kufunga goli la pili baada ya kumpiga chenga golikipa wa Liverpool Reina.
Na kwa sasa Liverpool wamekwishapoteza michezo sita kati ya saba ya ligi.
Reina alioneshwa kadi nyekundu baada ya kuchezewa rafu na James Perch alipokuwa akijiandaa kufunga mpira uliopigwa na Mike Williamson.
Lakini baada ya kugongana na mlinzi huyo wa Newcastle, Reina alimtwanga kichwa Perch na mwamuzi Martin Atkinson hakuwa na njia nyingine ya kufanya ila kumtoa nje kwa kadi nyekundu.
Golikipa wa Liverpool Reina akimpiga kichwa Perch kitendo kilichomsababishia kuzawadiwa kadi nyekundu.
Kilikuwa kipindi kingine cha kushuhudia vijana wa Kenny Dalglish wakinyanyaswa, ambao katika msimamo wa ligi wanashikilia nafasi ya nane, pointi 11 nyuma ya Chelsea wanaoshikilia nafasi ya tano.
Na kwa wenyeji Newcastle, matokeo hayo yamewainua na kufikisha pointi sawa na Chelsea wakiwa wanatafuta nafasi muhimu ya kumaliza msimu kwa kucheza Ligi ya Ulaya.
ARSENAL YALAMBWA,CHELSEA YAUA,MAN CITY YAKABWA KOO
Manchester City walimaliza mchezo kwa mtindo wa aina yake baada ya kuwa nyuma kwa mabao 3-1 kipindi kirefu cha mchezo na kufanikiwa kusawazisha na kuwa mabao 3-3 dhidi ya Sunderland katika uwanja wa Etihad.
Sebastian Larsson alikuwa wa kwanza kuipatia bao Sunderland kabla Mario Balotelli hajasawazisha kwa mkwaju wa penalti kutokana na rafu aliyofanyiwa Dzeko.
Sunderland walijiimarisha kwa kupata bao la pili lililofungwa kwa kichwa na Nicklas Bendtner kabla ya mapumziko na walionekana dhahiri wangeibuka washindi baada ya bao la tatu la Larson.
Lakini Balotelli na Aleksandar Kolarov walibadili hali ya mchezo kwa kusawazsiha, ingawa Manchester City walikuwa wamepoteza rekodi yao ya kushinda uwanja wa nyumbani katika msimu huu.
Licha ya kucheza vizuri na kusawazisha, Man City wanafahamu fika iwapo Manchester United watailaza Blackburn siku ya Jumatatu, mabingwa hao mara 19 watasogea pointi tano nyuma ya City na kuendelea kushikilia usukani.
Lilikuwa pambano la kusisimua hasa dakika za mwisho ambapo Sunderland walionesha kandanda murua na kuweza kuwasumbua kwa muda mrefu wenyeji wao.
Lakini mara tu baada ya kutolewa mlinzi wa kati aliyecheza vizuri sana Matt Kilgallon na nafasi yake kuchukuliwa na Sotirios Krygiakos zikiwa zimesalia dakika 10 mpira kumalizika, wageni walionekana kuparaganyika.

Robin Van Persie akitupia goli mechi dhidi ya QPR
QPR imefanikiwa kupata ushindi muhimu katika jitahada zao za kuepuka kushuka daraja baada ya Samba Diakite kufunga bao lake la kwanza tangu ahamie klabu hiyo na ndio lililoizamisha Arsenal na kupunguza kasi yake ya kushinda.
Adel Taarabt alikuwa wa kwanza kupata bao kwa upande wa QPR baada ya kumpita Thomas Vermaelen na kuachia mkwaju uliojaa wavuni.
Theo Walcott aliisawazishia Arsenal akiwa ndani ya sanduku la QPR na kuachia mkwaju baada ya jitahada zake za awali kugonga mwamba.
Mlinda mlango wa QPR Paddy Kenny alimnyima nafasi ya kufunga Robin van Persie wakati walipobakia wao wawili kabla ya Diakite kupachika bao la ushindi baada ya pasi kutoka kwa Jamie Mackie.
Aston Villa ikiwa nyumbani katika uwanja wao wa Villa Park ilishindwa kuhimili vishindo vya Chelsea baada ya nahodha wao Stiliyan Petrov kugundulika amekumbwa na maradhi ya saratani ya damu.

Sturridge akipigilia msumari wa kwanza dhidi ya Aston Villa
Mabao yaliyofungwa na Daniel Sturridge na Branislav Ivanovic yaliwasaidia wageni kupata ushindi wa mapema na kumiliki mpira kwa muda mrefu.
Dakika chache baadae zikawa za kuvuti baada ya James Collins kuipatia bao la kwanza Aston Villa, kabla ya Eric Lichaj kusawazisha na kufanya ubao usomeke 2-2.
Lakini sekunde 60 baadae, Ivanovic akafumua mkwaju wa karibu na kupata bao la tatu kabla Fernando Torres kumalizia kazi kwa kufunga bao la nne na la mwisho katika muda wa nyongeza.
Timu ya Everton ikiwa imeimarika ilifanikiwa kuichambua West Brom kwa mabao 2-0, kila bao likipatikana kila kipindi na hivyo kuweza kujinyanyua juu ya mahasuimu wao wakubwa Liverpool katika msimamo wa Ligi Kuu ya England.
Leon Osman alikuwa wa kwanza kuifungia Everton kwa mkwaju wa yadi 20, baada ya kogongeana na Nikica Jelavic, na mpira ukamgonga Gareth McAuley wa West Bromich na kumzubaisha mlinda mlango Ben Foster.
Ni mkwaju wa chinichini wa Victor Anichebe ulizidisha furaha kwa Everton ambao wiki iliyopita waliweza kupata nafasi ya kucheza nusu fainali ya ya Kombe la FA Cup ambao kwa sasa wamejinyanyua hadi nafasi ya saba.
Nafasi nzuri waliyoipata West Brom Albion ilikuwa pale mkwaju wa chini uliopigwa na Paul Scharner ulipopanguliwa na mlinda mlango Tim Howard.
Fulham ilimaliza nuksi ya kupoteza michezo mitatu mfululizo ya ligi baada ya kujipatia ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Norwich City.
Alikuwa Clint Dempsey aliyeunasa mpira vizuri na kuutumukiza wavuni kabla mlinda mlango wa Norwich John Ruddy kushindwa kuzuia mkwaju wa Bryan Ruiz.
Hadi robo ya kwanza ya mchezo Fulham walikuwa tayari wameshaweka kibindoni mabao mawili.
Fulham mara mbili mikwaju yao iligonga mwamba kutokana na mashuti ya Dempsey na baadae Alex Kacaniklic - lakini mkwaju wa Aaron Wilbraham uliomgonga mchezaji wa Fulham kujaa wavuni na kuipatia Norwich bao la kufutia machozi.

Duff na Dempsey wakishangilia goli
Wigan imeendelea kuwa nafasi ya hatari ya kushuka daraja lakini imefanikiwa kusogea pointi tatu mbele na kuwa sawa na Blackburn nafasi ya 17 baada ya kuilaza Stoke City kwa mabao 2-0 kwenye uwanja wao wa DW Stadium.
Bao la kichwa kipindi cha pili la Antolin Alcaraz liliwapatia Wigan nafasi ya kuongoza.
Ryan Shawcross alipata nafasi nzuri ya kuifungia Stoke kwa kichwa lakini mlinda mlango wa Wigan Ali Al Habsi aliokoa.
Jean Beausejour aliipotezea nafasi nzuri Wigan, kabla Victor Moses kuifungia Wigan bao la pili dakika za mwisho za mchezo.
Matokeo hayo maana yake Wigan imekusanya pointi 28, sawa na QPR pamoja na Blackburn wakiwa juu yao.
Wolves imezidi kudhoofishwa baada ya kuongoza kwa bao moja ikajikuta ikipokea kichapo kutoka kwa Bolton na kujiongezea dhiki mkiani mwa ligi.
Michael Kightly aliipatia bao la kwanza Wolves wakiwa nyuma kwa pointi sita mkiani huku michezo iliyosalia ni sita kabla msimu haujamalizika.
Lakini Martin Petrov akaisawazishia Bolton kwa mkwaju wa penalti baada ya Roger Johnson kumchezea rafu Mark Davies na baadae Marcos Alonso akaipatia Bolton bao la pili na ubao kusomeka mabao 2-1 kwa Bolton.
Kevin Davies aliifungia Bolton bao la tatu kabla Wolves kupata bao la kufutia machozi dakika za mwisho kupitia kwa Matt Jarvis.
Muda unazidi kwenda kwa kikosi cha meneja wa Wolves Terry Connor ambacho hakijashinda katika mechi zake 10 zilizopita.
Connor, bado anahitaji ushindi wake wa kwanza tangu alipochukua hatamu za umeneja. Wolves waliongoza kipindi cha kwanza lakini iliwawia shida kutumbukiza mpira wavuni.
Balotelli atupia mbili kambani
Sebastian Larsson alikuwa wa kwanza kuipatia bao Sunderland kabla Mario Balotelli hajasawazisha kwa mkwaju wa penalti kutokana na rafu aliyofanyiwa Dzeko.
Sunderland walijiimarisha kwa kupata bao la pili lililofungwa kwa kichwa na Nicklas Bendtner kabla ya mapumziko na walionekana dhahiri wangeibuka washindi baada ya bao la tatu la Larson.
Lakini Balotelli na Aleksandar Kolarov walibadili hali ya mchezo kwa kusawazsiha, ingawa Manchester City walikuwa wamepoteza rekodi yao ya kushinda uwanja wa nyumbani katika msimu huu.
Licha ya kucheza vizuri na kusawazisha, Man City wanafahamu fika iwapo Manchester United watailaza Blackburn siku ya Jumatatu, mabingwa hao mara 19 watasogea pointi tano nyuma ya City na kuendelea kushikilia usukani.
Lilikuwa pambano la kusisimua hasa dakika za mwisho ambapo Sunderland walionesha kandanda murua na kuweza kuwasumbua kwa muda mrefu wenyeji wao.
Lakini mara tu baada ya kutolewa mlinzi wa kati aliyecheza vizuri sana Matt Kilgallon na nafasi yake kuchukuliwa na Sotirios Krygiakos zikiwa zimesalia dakika 10 mpira kumalizika, wageni walionekana kuparaganyika.
Robin Van Persie akitupia goli mechi dhidi ya QPR
QPR imefanikiwa kupata ushindi muhimu katika jitahada zao za kuepuka kushuka daraja baada ya Samba Diakite kufunga bao lake la kwanza tangu ahamie klabu hiyo na ndio lililoizamisha Arsenal na kupunguza kasi yake ya kushinda.
Adel Taarabt alikuwa wa kwanza kupata bao kwa upande wa QPR baada ya kumpita Thomas Vermaelen na kuachia mkwaju uliojaa wavuni.
Theo Walcott aliisawazishia Arsenal akiwa ndani ya sanduku la QPR na kuachia mkwaju baada ya jitahada zake za awali kugonga mwamba.
Mlinda mlango wa QPR Paddy Kenny alimnyima nafasi ya kufunga Robin van Persie wakati walipobakia wao wawili kabla ya Diakite kupachika bao la ushindi baada ya pasi kutoka kwa Jamie Mackie.
Aston Villa ikiwa nyumbani katika uwanja wao wa Villa Park ilishindwa kuhimili vishindo vya Chelsea baada ya nahodha wao Stiliyan Petrov kugundulika amekumbwa na maradhi ya saratani ya damu.
Sturridge akipigilia msumari wa kwanza dhidi ya Aston Villa
Mabao yaliyofungwa na Daniel Sturridge na Branislav Ivanovic yaliwasaidia wageni kupata ushindi wa mapema na kumiliki mpira kwa muda mrefu.
Dakika chache baadae zikawa za kuvuti baada ya James Collins kuipatia bao la kwanza Aston Villa, kabla ya Eric Lichaj kusawazisha na kufanya ubao usomeke 2-2.
Lakini sekunde 60 baadae, Ivanovic akafumua mkwaju wa karibu na kupata bao la tatu kabla Fernando Torres kumalizia kazi kwa kufunga bao la nne na la mwisho katika muda wa nyongeza.
Timu ya Everton ikiwa imeimarika ilifanikiwa kuichambua West Brom kwa mabao 2-0, kila bao likipatikana kila kipindi na hivyo kuweza kujinyanyua juu ya mahasuimu wao wakubwa Liverpool katika msimamo wa Ligi Kuu ya England.
Leon Osman alikuwa wa kwanza kuifungia Everton kwa mkwaju wa yadi 20, baada ya kogongeana na Nikica Jelavic, na mpira ukamgonga Gareth McAuley wa West Bromich na kumzubaisha mlinda mlango Ben Foster.
Ni mkwaju wa chinichini wa Victor Anichebe ulizidisha furaha kwa Everton ambao wiki iliyopita waliweza kupata nafasi ya kucheza nusu fainali ya ya Kombe la FA Cup ambao kwa sasa wamejinyanyua hadi nafasi ya saba.
Nafasi nzuri waliyoipata West Brom Albion ilikuwa pale mkwaju wa chini uliopigwa na Paul Scharner ulipopanguliwa na mlinda mlango Tim Howard.
Fulham ilimaliza nuksi ya kupoteza michezo mitatu mfululizo ya ligi baada ya kujipatia ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Norwich City.
Alikuwa Clint Dempsey aliyeunasa mpira vizuri na kuutumukiza wavuni kabla mlinda mlango wa Norwich John Ruddy kushindwa kuzuia mkwaju wa Bryan Ruiz.
Hadi robo ya kwanza ya mchezo Fulham walikuwa tayari wameshaweka kibindoni mabao mawili.
Fulham mara mbili mikwaju yao iligonga mwamba kutokana na mashuti ya Dempsey na baadae Alex Kacaniklic - lakini mkwaju wa Aaron Wilbraham uliomgonga mchezaji wa Fulham kujaa wavuni na kuipatia Norwich bao la kufutia machozi.
Duff na Dempsey wakishangilia goli
Wigan imeendelea kuwa nafasi ya hatari ya kushuka daraja lakini imefanikiwa kusogea pointi tatu mbele na kuwa sawa na Blackburn nafasi ya 17 baada ya kuilaza Stoke City kwa mabao 2-0 kwenye uwanja wao wa DW Stadium.
Bao la kichwa kipindi cha pili la Antolin Alcaraz liliwapatia Wigan nafasi ya kuongoza.
Ryan Shawcross alipata nafasi nzuri ya kuifungia Stoke kwa kichwa lakini mlinda mlango wa Wigan Ali Al Habsi aliokoa.
Jean Beausejour aliipotezea nafasi nzuri Wigan, kabla Victor Moses kuifungia Wigan bao la pili dakika za mwisho za mchezo.
Matokeo hayo maana yake Wigan imekusanya pointi 28, sawa na QPR pamoja na Blackburn wakiwa juu yao.
Wolves imezidi kudhoofishwa baada ya kuongoza kwa bao moja ikajikuta ikipokea kichapo kutoka kwa Bolton na kujiongezea dhiki mkiani mwa ligi.
Michael Kightly aliipatia bao la kwanza Wolves wakiwa nyuma kwa pointi sita mkiani huku michezo iliyosalia ni sita kabla msimu haujamalizika.
Lakini Martin Petrov akaisawazishia Bolton kwa mkwaju wa penalti baada ya Roger Johnson kumchezea rafu Mark Davies na baadae Marcos Alonso akaipatia Bolton bao la pili na ubao kusomeka mabao 2-1 kwa Bolton.
Kevin Davies aliifungia Bolton bao la tatu kabla Wolves kupata bao la kufutia machozi dakika za mwisho kupitia kwa Matt Jarvis.
Muda unazidi kwenda kwa kikosi cha meneja wa Wolves Terry Connor ambacho hakijashinda katika mechi zake 10 zilizopita.
Connor, bado anahitaji ushindi wake wa kwanza tangu alipochukua hatamu za umeneja. Wolves waliongoza kipindi cha kwanza lakini iliwawia shida kutumbukiza mpira wavuni.
Saturday, March 31, 2012
WEMA AMWAGA CHOZI KWA KUTOLEWA NISHAI NA DIAMOND UKUMBINI KATIKA SHOW KALI MLIMANI CITY
Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya, Diamond Platinum akiwarusha mashabiki waliohudhuria katika tamasha lake la Diamond Are Forever lililofanyika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar e
Diamond akitema cheche katika tamasha hilo
Diamond akitia mbwembwe mbele ya mashabiki wake
Dancers wakimpa support Diamond kufanya makamuzi
Sehemu ya umati wa mashabiki waliohudhuria show hiyo
Diamond akiendeleza makamuzi mbele ya mashabiki
Diamond anazidi kuwapagawisha mashabiki
Songombingo lilianzia pale Dimond aliposhuka stejini na kwenda kwenye meza waliyokaa wakina Steve Nyerere na Mboni Masimba na ndipo walipompa t-shirt ambayo kwa mujibu wa udadisi na uchunguzi wa udadavuzi wa mambo wa Kajuna Blog, ilisemekana kuwa t-shirt hiyo ilikuwa inapicha ya mwanadada ambaye alikuwa akitoa na Diamond kwa sasa. Na ilikuwa ni maalum kwa ajili ya kumrusha roho Wema Sepetu.
Kazi ikaanza Mboni Masimba anamvalisha T'shirt yenye picha ya mpenzi mpya wa Diamond Steve Nyerere anatunza
Mhh........shabiki huyu akimtunza Diamond Dola za kimarekani watu vinywa wazi kulikoni?
Baada ya kutunza dolare za kutosha akaachia tabasamu nene
Wema nae akanyanyuka kwenda kutunza na pesa zikakataliwa
Wema kaganda akilazimisha Diamond apokee zile pesa bila mafanikio..ndio kwanzaaa kidume kiko bizeeeee!!!!!
Baada ya Diamond kugoma kutunzwa na Wema,Wema aliondoka stejini kwa hasira mithili ya Simba aliejeruhiwa
'Michuzi' aliyoikataa Diamond ikiwa stejini haijui iende wapi....
Hapo sasa 'Nimpende nani' uwanjani
Mlimbwende Jokate Mwegelo akijiachia na mashostito zake.
Diamond akimwaga mauno katika meza aliyokaa Jokate
Mwanadadafada Mboni Masimba akiwa ametinga T'shirt yenye picha ya kifaa kipya cha Diamond
Baadhi ya wadau walimuita mshereheshaji wa show hiyo Taji Liundi akambembeleze Diamond aende kumuomba msamaha Wema lakini Diamond akasema 'nope'
Diamond akijiachia na warembo
Mashosti wakijaribu kumbembeleza Wema aache kulia kwani hayo yote ni ya dunia
Duuuh..Wema akizidi kumwaga chozi!
"sitakiiiiiiiiiiiii aaaaaaaaaaaaaaaaah aaaaaaaaaaaaaaaaaaaahhhh wakunifanyia hivi mimi jamani aaaaaaaaaaaaaaaaah aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaah diamond diamond aaaaahhh aaaaaahhhhhh!!
Ommy Dimpoz akitoa ushuhuda walipotokea na Diamond
Ushuhuda ulimgusa Diamond na kumwaga chozi "mhmhhmmmmmm"
Amini na Barnaba wakimpa shavu Diamond katika show hiyo.
Hatimae Wema atuliza machungu kwa kumtunza Barnaba! "chukuaaa si anajifanya mjanja ataona akinitaka tena simtaki"
JOHN BOKO"ADEBAYOR" ACHOKA KUZOMEWA ASEMA 'STARS SASA BAAAAAAAASSSS'

JOHN BOKO 'ADEBAYOR'
Kinara wa mabao katika historia ya klabu ya Azam FC na kinara wa mabao katika ligi kuu ya Vodacom inayoendelea, John Raphael Boko 'Adebayor' ameliandikia barua shirikisho la soka nchini TFF ya kustaafu kuichezea timu ya Taifa 'Taifa Stars'. Huku akimuacha njia panda kocha wa kikosi hicho Jan Poulsen.
Boko amefikia uwamuzi huo kutokana na kuchoshwa na tabia za mashabiki wanao hudhuria mechi za Timu ya Taifa kumzomea kila anapopagwa.
Kwa mujibu wa Taarifa iliyowekwa kwenye ukurasa wa Azam FC ndani ya Facebook unasema kuwa Boko amewaomba TFF walikemee suala la wachezaji kuzomewa wakiwa na jezi ya Taifa.
"John Boko astaafu kuchezea timu ya taifa na sasa anaelekeza nguvu zake kwa timu yake ya Azam FC, kwa mujibu wa barua yake kwa TFF Boko amewaomba viongozi wa soka nchini kukemea tabia ya zomea zomea Kama walivyokemea uharibifu wa Mali za uwanja," ili eleza taarifa hiyo.
Katika blog ya Shaffih Sports imemnukuu Boko akisema; "Nimefikia maamuzi haya baada ya kufikiria sana, nimekuwa nikijitoa kwa hali na mali kulitumikia taifa langu lakini mashabiki wa timu yetu wanaona sifai, hivyo ni bora nijitoe au nistaafu kuichezea timu hiyo ili kuepekana na dhahama zao. Naitakia kila kheri timu yangu ya taifa naipenda na nitaendelea kuipenda siku zote."
Boko ni miongoni mwa washambuliaji bora nchini kwa kizazi hiki, na amekuwa chaguo la Poulsein toka aachane na washambuliaji wa TP Mazembe, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu kwa madai ya kwamba hawajitumi wakiwa na timu ya Taifa.
Kama Poulsein akiendelea na uwamuzi wake wakutowajumuisha washambuliaji hao wa TP Mazembe, ni wazi kuwa atakuwa na wakati mgumu katika kusaka washambuliaji watakao ziba mwanya huo.
LIGI KUU TANZANIA BARA NYASI KUTOA 'JASHO' LEO SIMBA Vs LYON, YANGA Vs COASTAL UNION
Kocha wa Simba S.C Milovan Cirkovic.
Mbilingembilenge za ligi kuu Tanzania bara zinaendelea leo ambapo kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, mabingwa watetezi Yanga watakakuwa wageni wa Coastal Union, huku vinara wa ligi Simba wakiwa na kazi mbele ya African Lyon kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo.
Mabingwa hao wa kihistoria wa Tanzania, timu za Simba na Yanga watashuka dimbani wakiwa na malengo tofauti kila mmoja, Yanga wenyewe wanajua kupoteza mchezo huo ni kupoteza ndoto yao ya kutetea ubingwa wao huku Simba wakitaka ushindi wajiimarishe kileleni kabla ya kuelekea Algeria kuivaa ES Setif.
Kocha wa Yanga Kostadin Papic.
Yanga hivi sasa inashikilia nafasi ya tatu ikiwa na pointi 43, hivyo ushindi dhidi ya Coastal utasaidia kupunguza pengo kati yake na kinara Simba inayoongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 47, pia kuiondoa Azam FC katika nafasi ya pili ambayo ina pointi 44 kabla ya mechi yake ya kesho dhidi ya Ruvu JKT.
Ukweli ni kwamba uzito wa mechi kati ya Yanga na Coastal Union unazidishwa na taswira tofauti za timu zote mbili hivi sasa pamoja na uwepo wa kocha Jamhuri Kihwelo 'Julio'.
Mabingwa hao wa mwaka 1988, Coastal Union waliojikusanyia pointi 29 baada ya kuzinduka na kushinda mechi sita mfululizo za raundi ya pili wenyewe wanatarajiwa kuendeleza rekodi hiyo kwa kusaka pointi tatu zitakazoipandisha juu kutoka katika nafasi ya sita iliyojiweka mpaka sasa.
Kocha wa Coastal, Kihwelo 'Julio' ameapa kuwadharirisha wapinzani wake kwenye mchezo huo akitarajiwa kuwatumia nyota kama Benard Mwalala, Edwin Mukenya kufikia malengo yake ingawa pia yupo Aziz Gilla anayecheza hapo kwa mkopo akitokea Simba.
Naye kocha wa Yanga, Kostadin Papic bila shaka ataingiza timu uwanjani akiwa katika hali ya kujiamini baada ya nyota wake waliokuwa kifungoni kufunguliwa kwa muda hivyo itakuwa ni hiyari yake kuwatumia au la.
Silaha za Papic zinazoweza kuonekana leo baada ya kunasuliwa kwa muda kutoka katika kifungo cha Kamati ya Ligi kutokana na utovu wa nidhamu ni mabeki, Nadir Haroub na mwenzake Stephano Mwasika, pamoja na viungo Omega Seme, Nurdin Bakari na mshambuliaji Jerryson Tegete.
Mechi hiyo itachezeshwa na mwamuzi Rashid Msangi wa Dodoma ambaye atasaidiwa na Rashid Lwena (Ruvuma) na Issa Malimali (Ruvuma).
Vita nyingine itakuwa jijini Dar es Salaam, wakati vinara wa ligi Simba wakiwa kwenye kiwango bora zaidi watakapowakabili ndugu zao African Lyon.
Kocha Milovan Cirkovic amewasisitizia wachezaji wake kutofanya uzembe utakaotoa nafasi kwa wapinzani wao ili kujiweka vizuri kabla ya kuivaa ES Setif wiki ijayo.
Simba itashuka dimbani bila ya kiungo wake Patrick Mafisango aliyesimamishwa na uongozi kutokana na utovu wa nidhamu.
Hata hivyo, Cirkovic licha ya kuwa na akiba ya kutosha ya wachezaji mahiri pia atakuwa na furaha baada ya kurejea kwa beki aliyekuwa majeruhi Juma Jabu.
Kesho matajiri wa Chamazi, Azam watakuwa wenyeji wa Ruvu JKT timu iliyopoteza makali yake katika siku za hivi karibuni.
Friday, March 30, 2012
WABUNGE KWENDA KUISHANGILIA SIMBA S.C ALGERIA
Mh Zitto Kabwe ataongoza kikosi cha wabunge kwenda Algeria kuipa Support Simba S.C
WABUNGE watano wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamethibitisha kuambatana na Simba katika safari ya kuelekea Algeria tayari kwa kuivaa ES Setif katika pambano la marudiano lililopangwa kupigwa Aprili 6, nchini humo.
Pambano dhidi ya Waaarabu hao kutoka katika jiji la Setif nchini humo ni la marudiano baada ya pambano la awali lililofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuishuhudia Simba ikiondoka na ushindi wa 2-0.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Simba, Ismail Rage aliwataja wabunge hao kuwa ni pamoja na Zito Kabwe (Kigoma Kusini), Musa Hassani Zungu(Ilala), Asnein Murij, Murtaza Mangungu(Kilwa Kaskazini)na Khalifa Suleiman Khalifa(Gando).
Alisema kuwa wakati safari ya wabunge Mangungu, Murij na Khalifa itaanzia Dar es Salaam, Kambwe ataanzia safari yake ya kuelekea Algeria akitokea nchini Nigeria huku Zungu akitarajiwa kuungana nao akitokea nchini Morocco alikodai yupo kwa sasa.
Aliongeza kuwa mbali ya wabunge hao, mashabiki 18 wa klabu pia wamethibitisha kuwa watasafiri na kikosi cha timu yao kwa ajili ya kuwaunga mkono ikiwa ni baada ya kununua tiketi za ndege.
"Kimsingi maandalizi ya safari ya Algeria yanaendelea vizuri na hapa tunapoongea tayari wabunge watano akiwemo mheshimiwa Zitto, Zungu, Murij, Mangungu na Klalifa wamethibitisha kuungana nasi kule Algeria."
Kuhusu mapokezi pindi watakapotua nchini Algeria, Rage alisema mpaka wakati huu uongozi wake umekuwa ukiwasiliana mara kwa mara na wanafunzi wanaosoma nchini humo kwa ajili ya kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa.
"Hatuna ofisi ya ubalozi Algeria, lakini tunashukuru Wizara ya Mambo ya Nje inatupa msaada mkubwa, pia tuna mawasiliano na wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma kule ambapo tayari wamejipanga kutupokea na kutupa msaada utakaohitajikika,"alisema Rage
Subscribe to:
Posts (Atom)