Tuesday, April 3, 2012

MAN UNITED YAIFYATUA BLACKBURN 2-0

Manchester United imeendelea kujichimbia kileleni mwa ligi kuu ya England baada ya kuizaba Blackburn Rovers kwa mabao 2-0. Man United wakicheza ugenini walibanwa kwa takriban dakika 80.
Baada ya kulisakama lango la Blacburn kwa dakika 80,Antonio Valencia ndiye aliandika bao la kwanza la United baada ya kuachia mkwaju mkali kutoka upande wa kulia.

Antinio Valencia akishangilia baada ya kutupia kambani goli la kuongoza la Man U


Ashley Young akiachia 'fataki' na kuandika goli la pili

Dakika tano baadaye, Ashley Young aliyeingia badala ya Paul Scholes alifunga bao maridadi na kuhakikishia United pointi tatu muhimu katika mbio za kutetea ubingwa wao.
Blackburn imerejea katika nafasi ya kumi na nane.



DIVA AMCHANA WEMA, AFAGILIA DIAMOND KUWA NA JOKATE


LOVENESS LOVE "DIVA"

Mtangazaji wa kipindi cha ala za roho kupitia kituo cha redio cha Clouds FM 88.4 Loveness Love 'Diva' amefunguka na kumchana 'live' Msanii maarufu wa filamu za bongo Wema Sepetu kwa kile kilichoonekana kukerwa na tabia 'chafu' za msanii huyo.
Kupitia kipindi cha ala za roho ambacho huendeshwa mida ya usiku kupitia kituo cha Clouds FM Diva alikitumia kipindi hicho ipasavyo kumchana Wema baada ya kupatwa na mkasa wa kuachwa solemba katika show baada ya kuwekeana makubaliano kuwa Wema afanyiwe mahojiano 'interview' lakini hakutokea.

Loveness Love "DIVA" na mpenzi wake Mo Racka

Diva alifunguka huku akimshutumu Wema kwa kutojali kazi za wenzake"Yeye ni kazi yake na wenzake tupo kazini lazima abadilike aheshimu kazi za wenzake"Alisema Diva.
Diva alielezea kuwa baada ya Wema kutotimiza makubaliano alijaribu kumtafuta katika simu ya mkononi lakini Wema alikuwa hapokei ndipo alipompigia Meneja wa Wema ajulikanae kama Martin.
Diva anasema kuwa alichojibu Meneja huyo ni kuwa Wema ni mtu anaependa 'Drama na atention' akiwa na maana Wema ni mtu wa kupenda michezo ya kuigiza na kuwafanya watu wawe makini na nini kilichotokea ni kama aina ya mtu anaependa skendo hivi ili watu waweze kumfuatilia mara kwa mara.


Wema Sepetu

Diva alikasirishwa na tabia hiyo na kusema kuwa kama Wema ni mtu wa kupenda drama ndio maana Diamond amemmwaga,'kama ni kweli Diamond anatoka na Jokate namuunga mkono kwasababu hakuna mwanaume anaependa 'drama na attention' " alisema Diva.'
'Kama unapenda penda mtu kama Jokate' aliongeza Diva kwa kile kilichoonekana kumfagilia Jokate kuwa na Diamond na kumkejeli Wema kwa kupigwa chini.
Katika kuweka msisitizo Loveness Love Diva akaweka wimbo wa Dioamond "Nimpende nani?" na akaendelea kupiga vijembe akisema mpende Jokate. Hapa alinikumbusha show ya Diamonds are forever iliyofanyika pale Mlimani City ambapo baada ya kupigwa wimbo wa Diamond Nimpende nani,ukumbi ulilipika kwa shangwe na kila mtu akimtupia jicho Wema nahisi ndio kitu kinachoitwa drama na attention anachokipenda Wema,mwisho katika Wimbo wa nimpende nani mwisho kuna kibwagizo kinachosema "nani amenuuuna?" basi Diamond alipofika katika kibwagizo hicho watu ukumbini walikuwa wakiitikia "Wemaaaaa","nani amenuuna?"..."Wemaaaaaaa".


Diamond "rais wa wasafi"

Jokate Mwegelo

Diva hakuishia hapo ndipo alipoanza kuuchambua wimbo wa Barnaba "Magubegube". ikumbukwe Barnaba pia alikuwepo katika show ya Diamonds are forever,show ambayo Diva aliifagilia ile mbaya akisema hakika ni next level,"Elfu hamsini(50,000) na tiketi zimeisha watu wamejaa show baab kubwa" alisema Diva.

Diamond akimlisha Wema keki enzi za mapenzi yao

Diva alipoweka wimbo wa magubegube akasema" Usiombe ukutane na magubegube,Diamond amekutana nayo na sasa yanamsumbua lakini amesimama imara na wanaume wengi wamekutana nayo" Hii ni dhahiri kuwa ni vijembe kwa Wema na kumfananisha na Gubegube.
Jamani show ya Diamonds are forever ilikuwa ni baab kubwa elfu hamsini na tiketi zimeisha watu kibao show ya nguvu ni maneno ambayo Diva aliyarudia mara kwa mara akimfagilia Diamond na kusema kuwa amefungua milango kwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya hapa bongo.

CCM YAANGUKIA PUA ARUMERU 'WHITE HAIR' CHALI


Mshindi wa kiti cha ubunge (CHADEMA) jimbo la Arumeru Joshua Nassari

NI Chadema. Tambo za muda mrefu za nani angeibuka mshindi katika kinyang'anyiro cha uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki zilifikia kikomo jana, baada ya Chadema, kunyakua jimbo hilo.  Mgombea wa chama hicho, Joshua Nassari aliibuka kidedea baada ya kupata kura 32,972 sawa na asilimia 54.91 ya kura halali 60,038 zilizopigwa katika vituo 327 vya kupigia kura jimboni humo.

Nassari alimbwaga aliyekuwa mshindani wake wa karibu, Sioi Sumari wa CCM, ambaye alipata kura 26,757 ambazo ni sawa na asilimia 44.56. Uchaguzi huo mdogo ulifanyika kufutia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Jeremia Sumari mwanzoni mwa mwaka huu.

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo jana alfajiri, Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo, Trasias Kagenzi alisema watu waliojiandikisha kupiga kura walikuwa 127,455 na waliojitokeza kupiga kura ni 60,699 sawa na asilimia 48.38 ambapo kura 661 zilikataliwa hivyo kufanya kura halali ziwe 60,038.

Kwa mujibu wa sura 343 ya sheria za uchaguzi nchini na kwa mamlaka niliyopewa namtangaza ndugu Nassari Joshua, kuwa mbunge wa jimbo hili la Arumeru Mashariki,alisema Kagenzi, kauli ambayo iliibua shangwe kwa wafuasi wa Chadema waliokuwa wakisubiri matokeo hayo usiku kucha kwenye kituo cha kujumlishia kura kilichopo katika mji mdogo wa Usa River.

Kagenzi aliwataja wagombea wengine ambao kwa ujumla wao walipata asilimia 0.53 ya kura zilizopigwa kuwa ni Abdalah Mazengo wa AFP aliyepata kura 139, Mohamad Abdalah Mohamed wa DP kura 77, mgombea wa SAUÂ Shabani Kirita aliyepata kura 22, Hamis Kieni wa NRA kura 35, wa TLP Abraham Chipaka kura 18 na mgombea wa UPDP, Charles Msuya alipata kura 18.

Idadi ya wapigakura waliojitokeza kushiriki uchaguzi huo mwaka huu waliongezeka kwa asilimia 8.2 ikilinganishwa na wapigakura 55,698 waliojitokeza Oktoba 31, 2010 kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge na madiwani.Kadhalika kura zilizokataliwa zimepungua kutoka za mwaka juzi kura 1,297 hadi kufikia kura 661 katika uchaguzi wa juzi, sawa na asilimia 49.03.

Sioi, wenzake wakacha kusaini

Mgombea wa CCM, Sioi na wagombea wengine wawili wa vyama vya NRA na UPDP jana hawakujitokeza kusaini fomu za matokeo ya uchaguzi huo licha ya kuitwa mara kadhaa na msimamizi wa uchaguzi.

Awali Sioi, alifika katika chumba cha majumuisho ya kura saa 6:15 usiku akiwa ameandamana na Makamu mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Beno Malisa na makada kadhaa wa CCM na mara baada ya kufika katika chumba hicho, walifanya mazungumzo kidogo na msimamizi wa uchaguzi.

Baadaye Sioi aliondoka na makada hao majira ya saa 7 usiku na kutokomea huku Malisa akieleza kuwa mgombea huyo wa CCM jana hakuwa tayari kutoa maoni kuhusu uchaguzi huo.Tunaomba mtuache kwanza, ila katika siasa kuna kushinda na kushindwa na mwanasiasa lazima atambue haya mawili, alisema Malisa.

Mkesha wa kusubiri matokeo
Wafuasi wa Chadema na waandishi wa habari walilazimika kusubiri kwa saa zaidi ya 12 kwenye kituo hicho cha kuhesabia kura hadi saa 12.50 alfajiri ya jana wakati Kagenzi alipotangaza matokeo hayo.

Usiku huo ulikuwa ni wa taabu kutokana na mvua kubwa iliyonyesha kati ya saa 8.00 usiku na saa 12.00 alfajiri huku kukiwa na katizo la umeme kwa zaidi ya mara mbili hivyo kukatiza mara kadhaa mchakato wa kujumlisha kura.Mvua hiyo ni kubwa ya kwanza kunyesha katika Wilaya ya Meru tangu kuanza kwa kampeni za uchaguzi huo mdogo Machi 9, mwaka huu hadi juzi wakati kura zilipoanza kujumlisha.


Maandalizi ya jenereta ya dharura yaliyokuwa yamefanywa na ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi, yaliwezesha kazi hiyo kuendelea hadi mchakato mzima ulipokamilika, hivyo kuwezesha mshindi kutangazwa saa 12.54 jana alfajiri.

Masanduku ya kura na fomu za matokeo kutoka vituo vya kupigia kura vilianza kuwasilishwa kwa msimamizi wa uchaguzi saa 1.20 usiku wa juzi na ilipotimu saa 7.00 usiku jana, tayari kata zote zilikuwa zimewasilisha taarifa zake. Hata hivyo kasoro iliyojitokeza ni pale polisi walipolazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa Chadema waliokuwa wakiandamana wakishangilia ushindi kabla ya kutangazwa kwa matokeo hayo.

Kati ya saa 2.00 na saa 4.30 usiku, mabomu hayo ya machozi na ya vishindo yalirindima mfululizo katika eneo la Usa River na kusababisha maduka, migahawa na baa kufungwa mapema.

Baadhi ya wafuasi wa Chadema walikamatwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe alisema walikuwa na mpango wa kwenda kuwawekea dhamana katika Kituo Kikuu cha Arusha mjini ambako waliwekwa mahabusu.

Habari zinasema katika tafrani hiyo, gari la Mkuu wa Operesheni ya Polisi katika Uchaguzi wa Igunga, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP), Issaya Mngulu lilivunjwa kioo chake baada ya kupigwa na jiwe kutoka kwa waandamanaji.

Hicho ni chanzo cha hasira za polisi ambao walirusha mabomu ya machozi kudhibiti hali hiyo maana tusingefanya hivyo hali ingekuwa mbaya zaidi,”alisema mmoja wa viongozi wa vikosi vya polisi ambaye hata hivyo hakutaka kutajwa gazetini.

Monday, April 2, 2012

Professor Jay ft Marco Chali-KAMILI GADO

PAPISS DEMBA CISSE APELEKA KILIO LIVERPOOL,CAROLL AZOMEWA MWANZO MWISHO


Demba Cisse akipiga kichwa kilichoelekea kambani kuandika goli la kwanza la Newcastle

Mabao mawili yaliyofungwa na Papiss Cisse yamezidi kuiongezea Newcastle hamu ya kucheza mashindano ya Ulaya msimu ujao baada ya kuongeza machungu kwa Liverpool iliyocheza na wachezaji 10 tu katika pambano la Ligi Kuu ya Kandanda ya England.
Cisse alitumbukiza mpira kwa kichwa baada ya kulishwa mpira wa juu na Hatem Ben Arfa katika kipindi cha kwanza kabla ya kufunga bao la pili alipopokea pasi ya Demba Ba katika nusu ya pili ya mchezo.

Demba Ba na Demba Cisse wakishangilia goli

Kiwango cha chini ya kandanda kilichooneshwa na Liverpool, ambapo mshambuliaji wao wa kati Andy Carroll alioneshwa kadi ya manjano baada ya kujiangusha kwa makusudi katika eneo la Newcastle, pia ilishuhudia mlinda mlango wao Pepe Reina kutolewa nje kwa kuoneshwa kadi ya nyekundu.

Demba Cisse(9) akijiandaa kufunga goli la pili baada ya kumpiga chenga golikipa wa Liverpool Reina.

Na kwa sasa Liverpool wamekwishapoteza michezo sita kati ya saba ya ligi.
Reina alioneshwa kadi nyekundu baada ya kuchezewa rafu na James Perch alipokuwa akijiandaa kufunga mpira uliopigwa na Mike Williamson.
Lakini baada ya kugongana na mlinzi huyo wa Newcastle, Reina alimtwanga kichwa Perch na mwamuzi Martin Atkinson hakuwa na njia nyingine ya kufanya ila kumtoa nje kwa kadi nyekundu.

Golikipa wa Liverpool Reina akimpiga kichwa Perch kitendo kilichomsababishia kuzawadiwa kadi nyekundu.

Kilikuwa kipindi kingine cha kushuhudia vijana wa Kenny Dalglish wakinyanyaswa, ambao katika msimamo wa ligi wanashikilia nafasi ya nane, pointi 11 nyuma ya Chelsea wanaoshikilia nafasi ya tano.
Na kwa wenyeji Newcastle, matokeo hayo yamewainua na kufikisha pointi sawa na Chelsea wakiwa wanatafuta nafasi muhimu ya kumaliza msimu kwa kucheza Ligi ya Ulaya.

ARSENAL YALAMBWA,CHELSEA YAUA,MAN CITY YAKABWA KOO

Manchester City walimaliza mchezo kwa mtindo wa aina yake baada ya kuwa nyuma kwa mabao 3-1 kipindi kirefu cha mchezo na kufanikiwa kusawazisha na kuwa mabao 3-3 dhidi ya Sunderland katika uwanja wa Etihad.
Mario Balotelli aliyefunga mabao mawili kwa Man City
Balotelli atupia mbili kambani

Sebastian Larsson alikuwa wa kwanza kuipatia bao Sunderland kabla Mario Balotelli hajasawazisha kwa mkwaju wa penalti kutokana na rafu aliyofanyiwa Dzeko.
Sunderland walijiimarisha kwa kupata bao la pili lililofungwa kwa kichwa na Nicklas Bendtner kabla ya mapumziko na walionekana dhahiri wangeibuka washindi baada ya bao la tatu la Larson.
Lakini Balotelli na Aleksandar Kolarov walibadili hali ya mchezo kwa kusawazsiha, ingawa Manchester City walikuwa wamepoteza rekodi yao ya kushinda uwanja wa nyumbani katika msimu huu.
Licha ya kucheza vizuri na kusawazisha, Man City wanafahamu fika iwapo Manchester United watailaza Blackburn siku ya Jumatatu, mabingwa hao mara 19 watasogea pointi tano nyuma ya City na kuendelea kushikilia usukani.
Lilikuwa pambano la kusisimua hasa dakika za mwisho ambapo Sunderland walionesha kandanda murua na kuweza kuwasumbua kwa muda mrefu wenyeji wao.
Lakini mara tu baada ya kutolewa mlinzi wa kati aliyecheza vizuri sana Matt Kilgallon na nafasi yake kuchukuliwa na Sotirios Krygiakos zikiwa zimesalia dakika 10 mpira kumalizika, wageni walionekana kuparaganyika.

Robin Van Persie akitupia goli mechi dhidi ya QPR

QPR imefanikiwa kupata ushindi muhimu katika jitahada zao za kuepuka kushuka daraja baada ya Samba Diakite kufunga bao lake la kwanza tangu ahamie klabu hiyo na ndio lililoizamisha Arsenal na kupunguza kasi yake ya kushinda.
Adel Taarabt alikuwa wa kwanza kupata bao kwa upande wa QPR baada ya kumpita Thomas Vermaelen na kuachia mkwaju uliojaa wavuni.
Theo Walcott aliisawazishia Arsenal akiwa ndani ya sanduku la QPR na kuachia mkwaju baada ya jitahada zake za awali kugonga mwamba.
Mlinda mlango wa QPR Paddy Kenny alimnyima nafasi ya kufunga Robin van Persie wakati walipobakia wao wawili kabla ya Diakite kupachika bao la ushindi baada ya pasi kutoka kwa Jamie Mackie.
Aston Villa ikiwa nyumbani katika uwanja wao wa Villa Park ilishindwa kuhimili vishindo vya Chelsea baada ya nahodha wao Stiliyan Petrov kugundulika amekumbwa na maradhi ya saratani ya damu.

Sturridge akipigilia msumari wa kwanza dhidi ya Aston Villa

Mabao yaliyofungwa na Daniel Sturridge na Branislav Ivanovic yaliwasaidia wageni kupata ushindi wa mapema na kumiliki mpira kwa muda mrefu.
Dakika chache baadae zikawa za kuvuti baada ya James Collins kuipatia bao la kwanza Aston Villa, kabla ya Eric Lichaj kusawazisha na kufanya ubao usomeke 2-2.
Lakini sekunde 60 baadae, Ivanovic akafumua mkwaju wa karibu na kupata bao la tatu kabla Fernando Torres kumalizia kazi kwa kufunga bao la nne na la mwisho katika muda wa nyongeza.
Timu ya Everton ikiwa imeimarika ilifanikiwa kuichambua West Brom kwa mabao 2-0, kila bao likipatikana kila kipindi na hivyo kuweza kujinyanyua juu ya mahasuimu wao wakubwa Liverpool katika msimamo wa Ligi Kuu ya England.
Leon Osman alikuwa wa kwanza kuifungia Everton kwa mkwaju wa yadi 20, baada ya kogongeana na Nikica Jelavic, na mpira ukamgonga Gareth McAuley wa West Bromich na kumzubaisha mlinda mlango Ben Foster.
Ni mkwaju wa chinichini wa Victor Anichebe ulizidisha furaha kwa Everton ambao wiki iliyopita waliweza kupata nafasi ya kucheza nusu fainali ya ya Kombe la FA Cup ambao kwa sasa wamejinyanyua hadi nafasi ya saba.
Nafasi nzuri waliyoipata West Brom Albion ilikuwa pale mkwaju wa chini uliopigwa na Paul Scharner ulipopanguliwa na mlinda mlango Tim Howard.
Fulham ilimaliza nuksi ya kupoteza michezo mitatu mfululizo ya ligi baada ya kujipatia ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Norwich City.
Alikuwa Clint Dempsey aliyeunasa mpira vizuri na kuutumukiza wavuni kabla mlinda mlango wa Norwich John Ruddy kushindwa kuzuia mkwaju wa Bryan Ruiz.
Hadi robo ya kwanza ya mchezo Fulham walikuwa tayari wameshaweka kibindoni mabao mawili.
Fulham mara mbili mikwaju yao iligonga mwamba kutokana na mashuti ya Dempsey na baadae Alex Kacaniklic - lakini mkwaju wa Aaron Wilbraham uliomgonga mchezaji wa Fulham kujaa wavuni na kuipatia Norwich bao la kufutia machozi.

Duff na Dempsey wakishangilia goli

Wigan imeendelea kuwa nafasi ya hatari ya kushuka daraja lakini imefanikiwa kusogea pointi tatu mbele na kuwa sawa na Blackburn nafasi ya 17 baada ya kuilaza Stoke City kwa mabao 2-0 kwenye uwanja wao wa DW Stadium.
Bao la kichwa kipindi cha pili la Antolin Alcaraz liliwapatia Wigan nafasi ya kuongoza.
Ryan Shawcross alipata nafasi nzuri ya kuifungia Stoke kwa kichwa lakini mlinda mlango wa Wigan Ali Al Habsi aliokoa.
Jean Beausejour aliipotezea nafasi nzuri Wigan, kabla Victor Moses kuifungia Wigan bao la pili dakika za mwisho za mchezo.
Matokeo hayo maana yake Wigan imekusanya pointi 28, sawa na QPR pamoja na Blackburn wakiwa juu yao.
Wolves imezidi kudhoofishwa baada ya kuongoza kwa bao moja ikajikuta ikipokea kichapo kutoka kwa Bolton na kujiongezea dhiki mkiani mwa ligi.
Michael Kightly aliipatia bao la kwanza Wolves wakiwa nyuma kwa pointi sita mkiani huku michezo iliyosalia ni sita kabla msimu haujamalizika.
Lakini Martin Petrov akaisawazishia Bolton kwa mkwaju wa penalti baada ya Roger Johnson kumchezea rafu Mark Davies na baadae Marcos Alonso akaipatia Bolton bao la pili na ubao kusomeka mabao 2-1 kwa Bolton.
Kevin Davies aliifungia Bolton bao la tatu kabla Wolves kupata bao la kufutia machozi dakika za mwisho kupitia kwa Matt Jarvis.
Muda unazidi kwenda kwa kikosi cha meneja wa Wolves Terry Connor ambacho hakijashinda katika mechi zake 10 zilizopita.
Connor, bado anahitaji ushindi wake wa kwanza tangu alipochukua hatamu za umeneja. Wolves waliongoza kipindi cha kwanza lakini iliwawia shida kutumbukiza mpira wavuni.

Saturday, March 31, 2012

WEMA AMWAGA CHOZI KWA KUTOLEWA NISHAI NA DIAMOND UKUMBINI KATIKA SHOW KALI MLIMANI CITY











Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya, Diamond Platinum akiwarusha mashabiki waliohudhuria katika tamasha lake la Diamond Are Forever lililofanyika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.











Diamond akitema cheche katika tamasha hilo














Diamond akitia mbwembwe mbele ya mashabiki wake














Dancers wakimpa support Diamond kufanya makamuzi










Sehemu ya umati wa mashabiki waliohudhuria show hiyo













Diamond akiendeleza makamuzi mbele ya mashabiki











Diamond anazidi kuwapagawisha mashabiki











Songombingo lilianzia pale Dimond aliposhuka stejini na kwenda kwenye meza waliyokaa wakina  Steve Nyerere na Mboni Masimba na ndipo walipompa t-shirt ambayo kwa mujibu wa udadisi na uchunguzi wa udadavuzi wa mambo wa Kajuna Blog, ilisemekana kuwa t-shirt hiyo ilikuwa inapicha ya mwanadada ambaye alikuwa akitoa na Diamond kwa sasa. Na ilikuwa ni maalum kwa ajili ya kumrusha roho Wema Sepetu.













Kazi ikaanza Mboni Masimba anamvalisha T'shirt yenye picha ya mpenzi mpya wa Diamond Steve Nyerere anatunza














Mhh........shabiki huyu akimtunza Diamond Dola za kimarekani watu vinywa wazi kulikoni?












Baada ya kutunza dolare za kutosha akaachia tabasamu nene














Wema nae akanyanyuka kwenda kutunza na pesa zikakataliwa














Wema kaganda akilazimisha Diamond apokee zile pesa bila mafanikio..ndio kwanzaaa kidume kiko bizeeeee!!!!!












Baada ya Diamond kugoma kutunzwa na Wema,Wema aliondoka stejini kwa hasira mithili ya Simba aliejeruhiwa









'Michuzi' aliyoikataa Diamond ikiwa stejini haijui iende wapi....













Hapo sasa 'Nimpende nani' uwanjani














Mlimbwende Jokate Mwegelo akijiachia na mashostito zake.














Diamond akimwaga mauno katika meza aliyokaa Jokate
















Mwanadadafada Mboni Masimba akiwa ametinga T'shirt yenye picha ya kifaa kipya cha Diamond














Baadhi ya wadau walimuita mshereheshaji wa show hiyo Taji Liundi akambembeleze Diamond aende kumuomba msamaha Wema lakini Diamond akasema 'nope'













Diamond akijiachia na warembo













Mashosti wakijaribu kumbembeleza Wema aache kulia kwani hayo yote ni ya dunia














Duuuh..Wema akizidi kumwaga chozi!
"sitakiiiiiiiiiiiii aaaaaaaaaaaaaaaaah aaaaaaaaaaaaaaaaaaaahhhh wakunifanyia hivi mimi jamani aaaaaaaaaaaaaaaaah aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaah diamond diamond aaaaahhh aaaaaahhhhhh!!















Ommy Dimpoz akitoa ushuhuda walipotokea na Diamond














Ushuhuda ulimgusa Diamond na kumwaga chozi "mhmhhmmmmmm"














Amini na Barnaba wakimpa shavu Diamond katika show hiyo.
















Hatimae Wema atuliza machungu kwa kumtunza Barnaba! "chukuaaa si anajifanya mjanja ataona akinitaka tena simtaki"