Tuesday, April 17, 2012

HUWEZI KUAMINI KIPAJI CHA SAUTI YA HUYU MTOTO

WIGAN YAITANDIKA ARSENAL EMIRATES


Di Santos akiipatia Wigan bao la kuongoza


Wigan ilithibitisha kuwa walipoifunga Manchester United haikuwa ajali na hawakubahatisha, walithibitisha hilo siku ya Jumatatu usiku Arsenal walipoichabanga Arsenal nyumbani 2-1. Wigan ilifanya unyama huo katika kampeni zake za kubakia ligi kuu ya Premier.
Kwa ushindi huo sasa Wigana inashikilia nafasi ya 16 katika msimamo wa ligi kuu ya Uingereza.
Arsenal ilikuwa inatafuta ushindi utakayoihakikishia kuongoza kwa pointi nane mbele ya Spurs bila mafanikio.

Thomas Vermaelen akiipatia Arsenal goli la kufutia machozi

Pamoja na kipigo hiko Arsenal bado wako katika nafasi ya tatu , nyuma ya vinara Manchester United na Manchester City.
Bao la kwanza la Wigan lilitupiwa kambani na Franco di Santo katika dakika ya saba na dakika moja baadaye Jordi Gomez akapigilia msumari wa pili
Thomas Vermaelen aliipatia timu ya nyumbani ya Arsenal bao lao moja la kufutia machozi.mpaka kipyenga cha mwisho Arsenal 1-2 Wigan Athletic.
ARSENAL 1-2 WIGAN

Monday, April 16, 2012

MAZISHI YA MUTHARIKA KUIGHARIMU MALAWI MILIONI 600 KUAGWA SIKU 10


Aliyekuwa Rais wa Malawi marehemu Bingu wa Mutharika

Serikali ya Malawi imetenga siku kumi kwa ajili ya wananchi wa Taifa hilo kutoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Bingu wa Mutharika.

Mwili wa kiongozi huyo unatarajiwa kuwasili leo jijini Lilongwe ukitokea katika hosipitali ya jeshi mjini Pretoria, Afrika Kusini na baadaye utapelekwa Ikulu ambako waombolezaji watapata fursa ya kuanza kutoa heshima za mwisho.

Mwenyekiti wa Kamati ya Mazishi ya Mutharika, Henry Mussa alisema kesho Jumapili mwili wa kiongozi huyo utaendelea kuwapo Ikulu na milango itakuwa wazi kwa wanafamilia na marafiki wa karibu kutoa heshima zao za mwisho na Jumatatu utawekwa katika jengo jipya la Bunge mjini Lilongwe ambako wananchi watapata fursa ya kutoa heshima hizo kwa siku mbili.

Mussa ambaye pia ni Waziri wa Serikali za Mitaa, alisema Jumatano mwili wa Mutharika utapelekwa katika mji wa Mzuzu ambako wananchi wa Kanda ya Kaskazini mwa Malawi pia watamuaga kiongozi wao, na Alhamisi mwili huo utasafirishwa kwenda Blantyre ambako utahifadhiwa Ikulu ya ndogo ya Sanjika.


Marehemu Mutharika kulia akiteta jambo na Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe enzi za uhai wake

Katika Ikulu hiyo wananchi watatoa heshima zao za mwisho kwa siku tatu hadi Jumamosi, April 21 kisha mwili huo kupelekwa katika eneo la maziko, shamba la Ndata, ambako wakazi wa eneo hilo pia watatoa heshima zao za mwisho, Jumapili Aprili 22.

Mussa alisema siku ya mazishi ambayo ni Jumatatu Aprili 23, 2012 watakaoruhusiwa kutoa heshima zao za mwisho ni wakuu wa nchi, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa na wale wa Jumuiya za Kikanda kabla ya Ibada itakayoongozwa na Kanisa Katoliki ambalo Mutharika alikuwa muumini wake.

Juzi, Ikulu ya Lilongwe ilithibitisha kwamba Rais Jakaya Kikwete ni miongoni mwa wakuu wa nchi na Serikali ambao wamealikwa kushiriki mazishi ya kiongozi huyo ambaye alifariki Aprili 5, mwaka huu kutokana na ugonjwa wa moyo.

Mutharika atazikwa katika shamba la Ndata katika Wilaya ya Thyolo iliyoko umbali wa Kilometa 45 Kusini mwa Blantyre, uamuzi ambao Mussa alisema ulitokana na maelekezo yake aliyoyatoa kabla hajafariki dunia.

“Kwa wale ambao tumewahi kufika Ndata alipozikwa mke wake Ether, aliweka sehemu ambayo pia angependa azikwe yeye, kwahiyo sisi ni akina nani hadi tupinge uamuzi wake?” alisema Mussa.

Mazishi kugharimu Sh600 milioni
Katika hatua nyingine Mussa alisema Serikali ya Malawi imechukua hatua za kuhakikisha kwamba hakutakuwa na uhaba wa mafuta wakati wote wa taratibu za mazishi ya Mutharika, ambayo yataigharimu nchi hiyo Kwacha150 milioni (zaidi ya Sh600 milioni).

Waziri wa Fedha wa Malawi juzi aliwasilisha bajeti ya Kwacha400 milioni (zaidi ya Sh1.6 bilioni) mbele ya kikao cha Baraza la Mawaziri lakini kikao hicho kilichokutana na chini ya Uenyekiti wa Rais Joyce Banda kikaipunguza hadi kufikia kwacha150 milioni.

Mussa alisema mbali na msaada wa lita milioni tano za mafuta ambazo Malawi imepokea kutoka Serikali ya Zambia, kiasi kingine cha lita milioni 20 kinatarajiwa kuingia mapema iwezekanavyo kwa ajili ya kuhakikisha kwamba shughuli za Serikali hazikwami.


Mwenyekiti wa kamati ya mazishi Henry Mussa ambaye pia ni Waziri wa serikali za mitaa

“Shehena ya mafuta inaingia sasa kupitia sehemu mbalimbali, katika Bandari ya Dar es Salaam (Tanzania) na Beira, pia kule Nakala na tunataraji kwamba mafuta haya yatatumika kuhakikisha shughuli za mazishi ya Rais wetu hazikwami,” alisema Mussa.

Jana Malawi ilipokea rasmi mafuta ya msaada yaliyotolewa na Zambia kupitia kwa Rais wa nchi hiyo Michael Satan yalikabidhiwa na Waziri mwenye dhamana ya Nishati nchi hiyo, Christopher Yalima kwa Rais Banda.

Uhaba wa mafuta nchini Malawi ulianza kujitokeza miaka mitatu iliyopita lakini hali inaelezwa kuwa mbaya zaidi yapata miezi miwili iliyopita, kiasi cha kusababisha bei za bidhaa kupanda hivyo kuongeza ugumu wa maisha kwa Wamalawi.
Maombolezo Ikulu
Wananchi wa Malawi wameendelea kuingia Ikulu ya Malawi kwa ajili ya maombolezo ya Mutharika pia kuwafariji wafiwa katika msiba huo.

Habari kutoka Blantyre pia zinasema maombolezo kama hayo yanaendelea katika shamba la Mutharika la Ndata ambalo pia lilifunguliwa kwa ajili ya kuwaruhusu wananchi kuhani msiba wa kiongozi wao.

Katika hatua nyingine, Makamu wa Rais wa Malawi, Khumbo Kachali aliapishwa jana na Jaji Mkuu wa nchi hiyo, Lovemore Munlo katika hafla iliyohudhuriwa na Rais Banda na mamia ya wafuasi wa chama kipya cha Peoples Party (PP).

ZUMA KUOA MKE WA SITA WIKI HII


Rais wa Afrika ya Kusini Jacob Zuma

Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ametangaza kwamba atafunga ndoa ya sita wiki hii.
Rais huyo mwenye umri wa miaka 70, atamuoa mchumba ake kwenye harusi ya kijadi huko Kwa Zulu Natal.
Gloria Bongekile Ngema, mfanya biashara kutoka Durban, ameshaonekana mara nyingi akifuatana na rais lakini kutoka juma lijalo, wawili hao watakuwa wameowana rasmi kijadi.
Harusi inatarajiwa kuwa ya fahari lakini ya faragha katika kijiji cha Nkandla, katika jimbo la Kwa Zulu Natal, nyumbani kwao Rais Zuma.

Zuma na mkewe wake mtarajiwa, Bi Gloria Bongekile Ngema

Rais Zuma ni mtu anayefuata mila za kabila lake la Zulu.
Mwenyewe amezaliwa na baba aliyekuwa na wake kadha.
Na ndoa yake kwa Bi Ngema ni ya sita, ingawa kutoka juma lijalo atakuwa na wake wane tu.
Mmoja, ambaye ni waziri wa serikali, alimuacha.
Na mwengine alijiiuwa.
Nyumba ya Rais Zuma imetengenezwa sana ili kuweza kuweka familia yake.
Inafikiriwa ana watoto 20.
Lakini hivi karibuni alisema ndoa ya juma lijalo ndio itakuwa ya mwisho.

MAN U YAIFUMUA ASTON VILLA 4-0, CHELSEA YAIZABUA SPURS 5-1

Chelsea thrash Spurs to reach FA Cup final
Drogba na wachezaji wenzake wakishangilia goli

Chelsea iliwachapa Tottenham mabao 5-1 nakuingia katika fainali za kombe la FA ambapo watakutana na Liverpool.
Hata hivyo ushindi huyo haukukosa manung'uniko baada ya refa kuipa Chelsea goli ambalo ilidaiwa kuwa mpira ulikuwa haujavuja mstari wa goli.
Utata huo sasa umeibua mjada kwamba kuna haja ya kuanzishwa mara moja kwa utaalam wa kuangalia kama mpira umevuka mstari wa goli au la.

Goooooooooooooooal!!!

Ushindi huo mnono umempa raha mkufunzi wa Chelsea Roberto di Matteo kwani umeiweka katika hali nzuri ya kupambana na Barcelona watakapowatembelea siku ya Jumatano.
Wakati Chelsea wakifurahia ushindi wao Spurs walikua na malalamiko chungu nzima kwani walidai kuwa walikuwa wanaonewa pale mpuliza kipenga ,Martin Atkinson alipowapa Chelsea bao la utata.

MAN UNITED YAUA

Manchester United imeongeza wigo wa pointi hadi tano dhidi ya Manchester City kileleni mwa Ligi Kuu ya Kandanda ya England lakin i ushindi wao dhidi ya Aston Villa uligubikwa kwa mara nyingine na penalti iliyoonekana ni ya utata.

Wayne Rooney - Manchester United v Aston Villa - Premier League
Rooney akitupia kambani kwa mkwaju wa penati

Ashley Young, ambaye alifanikiwa kupata penalti wakati Manchester United walipocheza na QPR, kwa mara nyingine alifanikiwa kupata penalti baada ya kutegewa na Ciaran Clark.
Kuguswa huko kwa Young kulikuwa kudogo sana lakini Wayne Rooney alifanikiwa kufunga mkwaju huo wa penalti kabla Danny Welbeck kuipatia Manchester United bao la pili.
Villa iliimarika kidogo baada ya kipindi cha pili lakini walikuwa Rooney na Nani walioandika mabao mengine mawili yaliyohitimisha karamu ya mabao 4-0.
Wayne Rooney - Manchester United v Aston Villa - Premier League
Rooney katikati na Young mgongoni pamoja na Carrick wakishangilia goli la Rooney

Manchester United walionekana kikosi bora zaidi katika kipindi cha kwanza na ushindi huo umepunguza pia deni la mabao ya kufunga na Manchester City na sasa kuwa manne.
Lakini bado swali litaendelea kubakia kwa wapenzi wa kandanda juu ya Young anavyojiangusha na aliposhutumiwa alipofanya hivyo dhidi ya QPR, ambapo Shaun Derry aliadhibiwa kwa kumsukuma mshambuliaji huyo wa pembeni na alioneshwa kadi nyekundu.
Rufaa iliyokatwa na Rangers ilitupiliwa mbali na Chama cha Kandanda cha England na shutuma zitaendelea kumuandama Young kutokana na alivyofanya kwa mara nyingine.
Na kubwa zaidi Young alifanya hivyo kwa timu aliyowahi kuichezea na itaongeza zaidi chumvi kwenye jeraha kwa timu ya Aston Villa.
Wayne Rooney - Manchester United v Aston Villa - Premier League
Rooney akishangilia bao

Villa walishindwa kuivunja rekodi dhidi yao wanapopambana na Manchester United, ambapo wamewahi kushinda mara moja tu katika mechi 31.
Jambo muhimu ni kwamba wapo pointi sita juu ya msatari wa kuteremka daraja na sasa wanajiandaa kwa pambano dhidi ya Sunderland, Bolton na West Brom ambapo lazima watafute pointi kujihakikishia hawateremki daraja.

Friday, April 13, 2012

Main differences between Messi and Cristiano Ronaldo



Obvious personality differences aside,
  1. Both began as right sided inside forwards/wingers. However as of current, Ronaldo plays as a Left Forward supporting a striker in the Higuain model. Messi plays right down the middle but cuts in from the right side.
  2. Ronaldo shoots with his right foot mostly, Messi uses the left.
  3. Ronaldo has a more confrontational style, while orginally a trickster, he has developed great speed and acceleration and uses his naturally strong physique to power past defenders. He still uses stepovers when facing a player but more for intimidation than actual use. Messi lacks the power however has a very low centre of gravity, allowing him to turn with the ball at a much higher speed than Ronaldo or any other player save for team mate Iniesta. His superior ball control and flawless technique means he rarely uses tricks or power, preferring to glide past any opponent. Also he is more prone to using a one-two pass (in line with the Barca philosophy) to bypass a tough opponent, something Ronaldo has seldom used in Madrid.
  4. Ronaldo puts in a lot of power in his shots, often needing a large space to properly execute a shot. he tends to shoot from the left side on his right foot towards the far post. Messi's style for long range goals is to cut inside towards the left before unleashing a left footed shot towards the far post. He is able to do so in an unbelievably small amount of space since he requires virtually no backlift (the movement of a foot backwards so as to give power to the shot).
  5. Ronaldo is more prone to hit the byline than Messi. This can be attributed to the fact that Barca has virtually no target inside the box. (Dani Alves does hit the byline very often in one-twos with Messi, but Messi himself stays in the 6yard box for a cross to feet).
  6. Ronaldo is a genuine aerial threat due to physical prowess, Messi possesses a good jump, but is no target man.

Assume what you may of who is superior, but it is an endless argument. Both have changed their playing style over the years so the answer too has changed several times in the past.

Attitude and versatility.

While I find Messi more endearing, I think Ronaldo has more assets as a footballer than Messi. It's a shame though, since all these assets are hidden behind his primma donna attitude.

Messi's strengths:

  • He's a better dribbler (Ronaldo dribbles but Messi is more efficient)
  • Does not dive nor complain when decisions don't go his way unlike Ronaldo
  • Humble. Messi will never say this[1]

Ronaldo's strengths:
  • Ambidextrous (Messi almost always relies on his left foot)
  • Superior shooting and free kick taking skills.
  • Superior aerial ability and overall speed.

Another point to note is that Messi has only played well so far for a single team(Barcelona). Anytime he shows up for Argentina, he is a no show. Ronaldo on the other hand has proven himself at Manchenster United, Portugal national team and now at Real Madrid. I think this attests to Ronaldo's versatility.

Thursday, April 12, 2012

KIFO CHA KANUMBA CHAIBUA MJADALA WIZI WA KAZI ZA WASANII


Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mh Zitto Kabwe, ambaye pia ni msemaji wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni.

Suala la wizi wa kazi za wasanii nchini, limeibua mjadala mkali bungeni huku Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto akipendekeza mtu atakayekamatwa akiuza CD na DvD feki za kazi za wasanii atozwe faini isiyopungua sh50 milioni.

Mbunge huyo ambaye pia ni Naibu Msemaji wa Kambi rasmi ya upinzani Bungeni, alipendekeza kuwa mtu yeyote atakayekutwa na kazi feki za wasanii naye aadhibiwe vikali ili kujenga Utamaduni wa Watanzania kuacha kununua kazi za wizi wasaniii.

Wabunge hao walichachamaa Bungeni mjini Dodoma jana wakati wakichangia hotuba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Cyril Chami kuhusu muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria mbalimbali za biashara wa mwaka 2011.

Zitto alisema biashara ya sanaa nchini imekukuwa haiangaliwi kikamilifu na kwamba mazishi ya msanii nguli wa filamu nchini, Steven Kanumba yaliyofanyika juzi yamedhihirisha kuwa Watanzania ni wapenzi wa sanaa ikiwamo filamu na muziki.

Mbunge huyo alipendekeza wasanii wote wasajiliwe na kila mmoja awe na nambari ya mlipa kodi (TIN) ili zoezi la Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) la kutoa stika za ushuru liwe na mafanikio kwa kuwa kila msanii atakuwa anafahamika TRA.

Naye Mbunge wa Viti Maalumu, Martha Mlata (CCM) alipendekeza kuanzishwa kwa Wizara ya Utamaduni na Sanaa na kuhoji serikali inashikwa na kigugumizi gani kuipatia sekta ya sanaa wizara yake kamili kutokana na umuhimu wake.

Pia alibainisha kuwa suala la mikataba ya usambazaji wa kazi za sanaa za wasanii lina utata na kutoa mfano kwa CD moja ya muziki, msanii hulipwa Sh150 huku mapato makubwa yakiishia kwa wasambazaji wanaonufaika na kazi hizo.

“Wasanii wananufaika tu umaarufu lakini wanaendelea kuwa masikini kwa kuibiwa kazi zao na jasho lao….hivi kuna tatizo gani kuweka Wizara ya Utamaduni na Sanaa itakayosimamia kwa dhati haki za wasanii?”alihoji Mbunge huyo katika mchango wake huo.
Pia alipendekeza mabadiliko hayo ya sheria yatamke waziwazi wasanii wananufaika vipi na mapato wanayopata wamiliki wa vituo vya Televisheni vinavyotumia kazi za wasanii ikiwamo filamu na muziki kwa kuwa vingi havilipi mrahaba kwa wasanii.

Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi (Chadema) 'Sugu' alisema tatizo la viongozi wa serikali ni kushughulikia suala la haki miliki za kazi za wasanii kisiasa na kuwaacha wasanii wakiendelea kuibiwa kazi zao na kunufaisha watu wachache.

“Pamoja na Steven Kanumba (marehemu) kutengeneza filamu 50 lakini amekufa masikini… Rais wetu amekwenda vichochoroni alipokuwa akiiishi…Waziri Mkuu amekwenda vichochoroni kama kuna mtu angetaka kuwateka angewateka” alisema.

Mbunge huyo alipendekeza wanaokamatwa wakiiba kazi za wasanii washitakiwe kwa uhujumu uchumi huku akisisitiza Chama cha Haki Miliki na Shiriki (Cosota) imeshindwa kazi na kutaka pia studio ya wasanii iliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete irudishwe Basata.

Akiwasilisha muswada huo wa sheria, Dk. Chami alisema mswada huo unapendekeza kufanya marekebisho katika sheria mbalimbali za biashara kwa lengo la kuboresha mazingira ya kufanyia biashara ikiwamo udhibiti wa bidhaa bandia.

Chini ya mabadiliko hayo ya sheria, serikali inapendekeza kuwapo kwa sheria mpya inayowapa nafasi watu mbalimbali kuweza kuanzisha kampuni zinazomilikiwa na mtu mmoja badala ya sheria ya sasa inayolazimisha kutafuta washirika.

Akiwasilisha maoni ya kamati ya kudumu ya Bunge ya viwanda na biashara, mwenyekiti wa kamati hiyo, Mahmoud Mgimwa alisema wafanyabiashara wengi wadogo wanaingia hatiani kwa kununua biadhaa bandia kwa wafanyabiashara wakubwa wasio waaminifu.

Kamati hiyo imeshauri kuwa udhibiti wa bidhaa bandia ufanyike kwa kufuatilia mwagizaji wa mwanzo na kumchukulia hatua ikiwamo kumwadhibu na kwamba adhabu kwa mfanyabiashara mdogo anayekutwa na bidhaa bandia iondolewe