Thursday, May 3, 2012

BURUDANI TIME (18+)

PAPISS DEMBA CISSE ATUPIA KAMBANI GOLI LA MSIMU WAKATI NEWCASTLE IKIIADHIBU CHELSEA

Goli la msimu la Demba Cisse dhidi ya CHELSEA

Timu ya soka ya Newcastle United jana waliwaadhiri wababe walioingia fainali ya ligi ya mabingwa barani ulaya timu ya Chelsea katika mtanange wa ligi kuu ya Uingereza kwa kuigaragaza kwa magoli 2-0 katika dimba lao la nyumbani hapa naizungumzia Stamford bridge.

 Papiss Cisse Chelsea
Papiss Demba Cisse akiachia mkwaju ulioelekea moja kwa moja kwenye nyavu za Chelsea zikimuacha golikipa Peter Cech akiwa ananing'inia bila mafanikio

Katika mechi hiyo Demba Cisse alitupia kambani mara mbili ambapo dakika ya 19 alimtesa vilivyo Peter Cech wa Chelsea na dakika za nyongeza akatupia la pili na kukamilisha shughuli iliyokuwa na pilipili nyingi kwa upande wa Chelsea wakati Newcastle wakiifurahia kwa ndimu iliyokolea.

Wednesday, May 2, 2012

FULHAM YAVUNJA MWIKO KWA LIVERPOOL YAICHAPA 1-0


Beki wa Liverpool Skrtel akiutazama mpira uliomgonga ukielekea wavuni

Bao la kujifunga la Martin Skrtel lilileta masikitiko mengi usiku wa Jumanne wakati walipoikaribisha Fulham katika uwanja wa Anfield, na kuwasaidia wageni kuandikisha historia, ikiwa ni mara yao ya kwanza kupata ushindi katika uwanja huo.

Lakini inaelekea meneja wa Liverpool, Kenny Dalglish, hakuwa na wasiwasi mno, kwani tangu mwanzo aliichezesha timu dhaifu, wachezaji wake mahiri akiwapumzisha na anakusudia kuwatumia kikamilifu katika pambano la fainali la Kombe la FA mwishoni mwa wiki.

Liverpool walipata nafasi za kusawazisha, lakini Mark Schwarzer hakuwa mbunifu katika kumalizia na kuelekeza mikwaju vyema.


Mshikemshike katika mechi hiyo

Fulham pia walishindwa kujiongezea mabao, kwani Kerim Frei aligonga mwamba, na kipa wa Liverpool Doni pia aliweza kuiokoa timu yake kutoka kwa makombora zaidi ya Pavel Pogrebnyak na Clint Demsey.

Matokeo hayo yanamaanisha Fulham sasa ina pointi 49, sawa na Liverpool.


Ngoma nzito Climp Dempsey na Martin Kelly

Liverpool imo katika nafasi ya nane, na msimu huu imeshinda mechi tano tu, kati ya 18, na sasa wameachwa nyuma kwa pointi tatu na Everton, ambao pia usiku wa Jumanne walikamilisha mechi yao kwa sare ya 1-1 dhidi ya Stoke City.


Dunny Murphy akimkwatua Albert Riera wa Liverpool

Bila shaka mechi hii itakumbukwa na mashabiki wengi wa Liverpool, na ambao watajiuliza timu yao imejiandaa vipi katika kupambana na Chelsea katika fainali ya Kombe la FA, Jumamosi, tarehe 5 Mei.

MATOKEO KIDATO CHA SITA 2012

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2012

MATOKEO KIDATO CHA SITA 2012

MATOKEO KIDATO CHA SITA 2012