IVORY COAST 2-0 TANZANIA
Monday, June 4, 2012
RATIBA MICHUANO YA ULAYA (EUROPEAN CHAMPIONSHIPS FIXTURES 2012)
European Championships | FIXTURES
All times CAT (SA, GMT+2)East Africa(Tanzania) + saa moja. mfano 18:00=19:00
| Friday 08 June 2012 |
| Poland | v | Greece | Warsaw National Stadium | 18:00 | |
| Russia | v | Czech Republic | Wroclaw Municipal Stadium | 20:45 |
| Saturday 09 June 2012 |
| Netherlands | v | Denmark | Metalist Stadium | 18:00 | |
| Germany | v | Portugal | Arena Lviv | 20:45 |
| Sunday 10 June 2012 |
| Spain | v | Italy | Arena Gdansk | 18:00 | |
| Ireland | v | Croatia | Poznan Municipal Stadium | 20:45 |
| Monday 11 June 2012 |
| France | v | England | Donbass Arena | 18:00 | |
| Ukraine | v | Sweden | Olympic Stadium | 20:45 |
| Tuesday 12 June 2012 |
| Greece | v | Czech Republic | Wroclaw Municipal Stadium | 18:00 | |
| Poland | v | Russia | Warsaw National Stadium | 20:45 |
| Wednesday 13 June 2012 |
| Denmark | v | Portugal | Arena Lviv | 18:00 | |
| Netherlands | v | Germany | Metalist Stadium | 20:45 |
| Thursday 14 June 2012 |
| Italy | v | Croatia | Poznan Municipal Stadium | 18:00 | |
| Spain | v | Ireland | Arena Gdansk | 20:45 |
| Friday 15 June 2012 |
| Ukraine | v | France | Donbass Arena | 18:00 | |
| Sweden | v | England | Olympic Stadium | 20:45 |
| Saturday 16 June 2012 |
| Czech Republic | v | Poland | Wroclaw Municipal Stadium | 20:45 | |
| Greece | v | Russia | Warsaw National Stadium | 20:45 |
| Sunday 17 June 2012 |
| Denmark | v | Germany | Arena Lviv | 20:45 | |
| Portugal | v | Netherlands | Metalist Stadium | 20:45 |
| Monday 18 June 2012 |
| Croatia | v | Spain | Arena Gdansk | 20:45 | |
| Italy | v | Ireland | Poznan Municipal Stadium | 20:45 |
| Tuesday 19 June 2012 |
| England | v | Ukraine | Donbass Arena | 20:45 | |
| Sweden | v | France | Olympic Stadium | 20:45 |
MAKUNDI MICHUANO YA ULAYA 2012
European Championships | LOGS
Group A
| Pos | Team | P | W | D | L | GF | GA | GD | Pts |
| 1 | Czech Republic | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
| 2 | Greece | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
| 3 | Poland | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
| 4 | Russia | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
Group B
| Pos | Team | P | W | D | L | GF | GA | GD | Pts |
| 1 | Denmark | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
| 2 | Germany | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
| 3 | Netherlands | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
| 4 | Portugal | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
Group C
| Pos | Team | P | W | D | L | GF | GA | GD | Pts |
| 1 | Croatia | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
| 2 | Italy | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
| 3 | Ireland | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
| 4 | Spain | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
Group D
| Pos | Team | P | W | D | L | GF | GA | GD | Pts |
| 1 | England | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
| 2 | France | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
| 3 | Sweden | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
| 4 | Ukraine | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
DIRK KUYT ATIMKIA UTURUKI
Dirk Kuyt
Mchezaji wa safu ya mbele ya Uhalonza Dirk Kuyt ameitosa klabu ya Liverpool na kujiunga na Fenerbahce ya Uturuki kwa mkataba wa miaka mitatu. Mshambuliaji huyo anasepa Liverpool baada ya kukipiga kwa kipindi cha miaka sita.
Kuyt mwenye umri wa miaka 31 alihamia uwanja wa Anfield mnamo mwaka 2006 na
kushiriki mara 250 akifunga jumla ya mabao 71.
Mechi yake ya kwanza kushiriki ilikua dhidi ya West Ham United mwezi Agosti mwaka 2006, alipoingia kuchukua mahala pa Peter Crouch ambapo upande wake uliondoka na ushindi wa 2-1.


Kuyt akifanya vitu vyake alipokuwa Liverpool
Bao lake la kwanza lilipatikana mwezi mmoja baadaye alipofunga bao la kwanza katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Newcastle.
Baadaye alipendwa na mashabiki wa Liverpool, kivutio kikiwa mchangon wake katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Everton kwenye uwanja wa Goodison Park mwaka 2007 kisha alipofunga 3- peke yake dhidi ya Manchester United, mahasimu wakuu wa klabu kutoka Anfield.
Kuyt ambaye ameshiriki mara 80 kwa Timu yake ya Taifa ya Uholanzi, pia alifunga dhidi ya AC Milan katika mchuano wa Ligi ya mabingwa mwezi Mayi mwaka 2007.
Msimu uliopita mshambuliaji huyo alipata shida kupata nafasi katika kikosi kikuu, akishiriki mara 22 pekee na kuletwa kama mchezaji wa ziada mara tano katika mechi tisa za mwisho wa msimu.
Kwa wakati huu mchezaji huyo aliyesajiliwa kutoka klabu ya Utrecht yuko pamoja na wenzake wa Timu ya Taifa ya Uholanzi wakijinoa kwa ajili ya michuano ya Ulaya 2012 ambapo Wadachi watachuana na Denmark katika mechi yao ya ufunguzi jumamosi ijayo.
Habari kutoka Liverpool iliyotolewa kufuatia hatua hio imesema kua Kila mmoja
anamtakia Dirk kila la heri na kumshukuru kwa mchango wake.
Aliposajiliwa, Kuyt alisema wakati huo, Kwangu mimi, Liverpool ni ndoto
iliyokamilika. Hapana cha kuilinganisha nayo klabu hii, yenye sifa na historia
ya kujivunia, alisema.Mechi yake ya kwanza kushiriki ilikua dhidi ya West Ham United mwezi Agosti mwaka 2006, alipoingia kuchukua mahala pa Peter Crouch ambapo upande wake uliondoka na ushindi wa 2-1.

Kuyt akifanya vitu vyake alipokuwa Liverpool
Bao lake la kwanza lilipatikana mwezi mmoja baadaye alipofunga bao la kwanza katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Newcastle.
Baadaye alipendwa na mashabiki wa Liverpool, kivutio kikiwa mchangon wake katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Everton kwenye uwanja wa Goodison Park mwaka 2007 kisha alipofunga 3- peke yake dhidi ya Manchester United, mahasimu wakuu wa klabu kutoka Anfield.
Kuyt ambaye ameshiriki mara 80 kwa Timu yake ya Taifa ya Uholanzi, pia alifunga dhidi ya AC Milan katika mchuano wa Ligi ya mabingwa mwezi Mayi mwaka 2007.
Msimu uliopita mshambuliaji huyo alipata shida kupata nafasi katika kikosi kikuu, akishiriki mara 22 pekee na kuletwa kama mchezaji wa ziada mara tano katika mechi tisa za mwisho wa msimu.
Kwa wakati huu mchezaji huyo aliyesajiliwa kutoka klabu ya Utrecht yuko pamoja na wenzake wa Timu ya Taifa ya Uholanzi wakijinoa kwa ajili ya michuano ya Ulaya 2012 ambapo Wadachi watachuana na Denmark katika mechi yao ya ufunguzi jumamosi ijayo.
Friday, June 1, 2012
MREMBO WA LEO-BRIA MYLES
CCM VULULUVULULU, MAIGE AFUNGUKA KUWA NAPE NI GAMBA HATARI
Katibu mkuu wa CCM Wilson Mukama
Habari kwa hisani ya gazeti la Mwanachi,Amini Yasini, Rufiji na Ahmed Makongo, Kahama
HALI ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), si shwari na Katibu Mkuu wake, Wilson Mukama amekiri kwamba hivi sasa kina mpasuko mkubwa unaotokana na makundi yanayofanana na yale ya Umoja wa Kujihami wa Nchi za Magharibi (Nato) na Umoja wa Mataifa yenye nguvu kubwa kiuchumi duniani (G8).
Wakati mtendaji mkuu huyo wa chama tawala akitoa kauli hiyo, aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige ameibuka na kumshambulia waziwazi, Katibu wa Taifa wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye akimtuhumu kukiharibu kwa utendaji mbovu, hivyo kutaka ang’olewe haraka akidai kuwa ni gamba.
Nchi zinazounda G8 ni Marekani, Canada, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Japan, Russia na Uingereza ambazo pia baadhi yao, ndizo zinazounda Nato, umoja wenye wanachama 28.
Mukama alitoa kauli hiyo juzi wilayani Rufiji wakati akizungumza na umati wa wananchi na wanachama wa chama hicho waliofurika katika Viwanja vya Corecu, Kata ya Kibiti.
Alisema baadhi ya wanachama wa CCM wamekuwa ni wasaka madaraka na wanapokosa huamua kuunda makundi ya uhasama ambayo hawataki kuyavunja pindi mchakato wa kutafuta mgombea unapomalizika.
“Makundi yaliyoundwa tangu 2005 na 2010 yanaendelea kukitafuna chama, wanachama wakinyimwa uongozi wanaanza uhasama, hatufiki malizeni makundi,” alisema.
Alisema makundi hayo pia yako katika Wilaya za Mkuranga na Rufiji, ambako katika ziara yake amebaini mpasuko mkubwa unaotokana na fitina na uhasama miongoni mwa wapenzi na makada wa CCM na kusisitiza kwamba hayafai na ni hatari kwa mustakabali wa chama hicho kikongwe barani Afrika.
“Nikiwa Mkuranga nilitaarifiwa kuwa kuna makundi ya Nato na G8 na sasa nimefika Rufiji nimeyakuta makundi hayo. Jamani makundi hayo ya nini?”
Mukama ambaye aliwahi kushika nafasi mbalimbali za kiutendaji zikiwemo za Ukuu wa Wilaya ya Mafia akimrithi mtangulizi wake Hemedi Mkali, alisema aliwahi kugombea ubunge wa viti vya Taifa kupitia Juwata (iliyokuwa Jumuiya ya Wafanyakazi Tanzania), na aliposhindwa alikubali matokeo.
Alisema Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere aliwahi kusema bila CCM imara nchi yetu itayumba, akimaanisha kuwa hakuna chama mbadala cha kuongoza nchi zaidi yake.
Waziri mkuu wa kwanza na Raisi wa Kwanza wa TANZANIA hayati baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Alitoa mfano wa Chama cha Democrat cha Marekani kwamba wanachama wake hawana kadi, bali mapenzi ya chama yako mioyoni mwao na wanapojiunga hawafanyi hivyo kwa lengo la kusaka madaraka... “Hii ni tofauti kubwa na nchi zetu ambako mtu akijiunga na chama kitu kwanza kufikiria ni kusaka madaraka,” alisema.
Alisema chama hicho kina mkakati madhubuti wa kupambana na watu wachache wanaotaka kukimiliki wakitumia nguvu ya fedha.
Alisema baadhi ya wanachama wa kawaida wamejiona kuwa hawana nafasi katika chama chao wakiamini kuwa kimetekwa na wenye fedha na kuongeza kwamba mwanachama wa kawaida hawezi kuongoza bila rushwa.
“Hapana! Chama chetu hakitakubali hali hiyo. Ni hatari sana kwa mustakabali wa chama chetu na nchi yetu,” alisema na kuongeza kuwa wanachama wa kawaida wanatakiwa kugombea hata kama hawana fedha.
Alisema chama kipo katika uchaguzi wake wa ndani na kuwataka wanachama kufanya uamuzi sahihi wa kuchagua viongozi waadilifu wasiotumia rushwa, kwani kufanya hivyo kunaweza kusababisha kuingia watu katika uongozi waliotoa rushwa.
Katika mikutano yake hiyo, Mukama alitamba kuwa chama chake hakitishwi na wapita njia akimaanisha wapinzani wanaodai kuwa hakijafanya kitu.
Alisema CCM ni chama makini na sikivu katika kusikiliza kero za wananchi akitamba kwamba kimejenga Daraja la Mkapa ambalo limekuwa kiunganishi kati ya Mikoa ya Lindi, Mtwara na Dar es Salaam na umeme wa gesi unaotoka kusini ambao wananchi wa Rufiji wananufaika nao kwa sasa.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Rufiji, Mrisho Matimbwa alisema katika uchaguzi uliopita wa chama hicho kulikuwa na makundi mawili, ya Bush na Al Qaeda ambayo kwa sasa yamekufa na kubakia mpasuko katika halmashauri kuu ambako aliahidi kuutatua.
Maige na Nape
Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM Nape Nnauye
Mbunge wa Msalala(CCM) Ezekiel Maige
Akizindua matawi mawili ya wakereketwa wajasiriamali wa CCM katika Kijiji cha Isaka, Kahama, Shinyanga, Maige ambaye ni Mbunge wa Msalala alimtaka Nape kuacha tabia yake ya kutoa kauli ambazo kwa namna moja au nyingine zinaelekea kukidhoofisha chama.
Alimtaka kupima utendaji wake tangu alipoishika nafasi hiyo ya Itikadi na Uenezi na kujiuliza ni wanachama wangapi wameingia ndani ya chama hicho.
Alisema sasa hivi kuna wimbi kubwa la wanachama wa chama hicho kuhama na kukimbilia upinzani na kusema ni wajibu wa Nape kupima na kuona kuwa kazi ya itikadi na uenezi haiwezi na kwani hajui wajibu wake akisema ni mtu wa kumhurumia.
Maige alisema mbali ya kushindwa kuzuia wimbi la wanachama kukihama CCM pia hapaswi kuvumiliwa kutokana na kauli yake kwamba hata kama wanachama watahama wote na akabaki yeye (Nape) peke yake, haitakufa. Alisema kauli hiyo haikijengi chama, bali kuchochea makundi ambayo yanaweza kukibomoa.
Alisema akiwa mwana CCM anaona kwamba sasa hivi Nape amekuwa hafanyi kazi ya uenezi na kukirejeshea haiba na mvuto ambao umepotea kwa wananchi na kwamba, kazi anayoifanya sasa ni kukuza makundi na kusema ovyo.
Aliendelea kumshambulia Nape kwa maneno akisema amejenga jeuri, kiburi, dharau na ulevi wa madaraka huku akidai kwamba kitendo cha CCM kupoteza wanachama zaidi ya 10,000 kwa wakati mmoja mkoani Arusha na sehemu nyingine wanachama 3,000 ni ishara ya hatari lakini, Nape amekuwa akiwaita wanaohama kwamba ni mzigo.
“Huyu Nape ni lazima atupishe. amekifanya chama kama mali yake, yeye ndiye mwenye jukumu la kueneza sera za chama na kutafuta wanachama wapya, lakini ndiyo kwanza anasema waachwe waondoke, Chadema wanatamba kila siku yeye hajali, huyu nasema ni gamba ni bora atupishe,” alisema.
Baada ya mashambulizi hayo, Maige alijitetea kwamba maneno yake dhidi ya Nape yasitafsiriwe kama ni kuulilia uwaziri: “Ni uchungu nilionao kwa chama changu kuona kila siku zinavyokwenda ndivyo tunavyopoteza idadi kubwa ya wanachama, tuliyemkabidhi jukumu la uenezi anasema hajali, sasa huyu si atupishe mapema kabla mambo hayajaharibika?”
“Nikuombe Mwenyekiti wa CCM Mkoa mzee wangu, Mgeja (Hamis), nafikiri ninyi wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec ya CCM) mnapaswa kuchukua hatua haraka juu ya Nape... huyu sasa ni tatizo. Chama kitawafia hivihivi mkiona, avuliwe gamba maana tukisubiri ajivue atatuchelewesha, CCM ni wanachama si Nape.”
Wakati Maige akitoa maneno hayo, Mgeja alikuwa ameinamisha kichwa chake chini huku mikono ikiwa kichwani, lakini wana CCM na wananchi wengine walikuwa wakishangilia.
Aidha, Maige aliwalaumu viongozi wa CCM katika ngazi ya wilaya na kata ambao wamekuwa na tabia ya kutowatembelea wananchi katika maeneo yao kusikiliza kero zao wakisubiri mpaka viongozi wa kitaifa ndipo na wao wajitokeze.
“Jamani inakuwaje kiongozi mwenezi wa CCM kata ama wilaya anakaa kimya kabisa hakuna kazi yoyote anayoifanya! Viongozi wa aina hii wasipewe nafasi kabisa katika uchaguzi ujao. Tupate safu ya viongozi wenye kukifia chama chetu.”
“Maana kama watu wanakuja na Operesheni Sangara hakuna anayesimama kujibu, Operesheni Vua Gamba Vaa Gwanda hakuna aliyewajibu wala CCM haijatafuta operesheni yoyote ile kukabiliana nao, sasa wameanza Operesheni Movement For Change (M4C), sisi na Nape wetu kimya tunawaangalia tu wanazoa wanachama. Tuwe makini chagueni viongozi wenye uchungu na chama,” alisema Maige.
Alipotakiwa kuzungumzia tuhuma hizo za Maige, Nape alisema: “Nasubiri taarifa rasmi ya chama na nikiyakuta hayo nitajibu. CCM ina taratibu zake katika utendaji wake wa kazi. Katika taratibu hizo, ziara zote za viongozi wetu zinaandikiwa taarifa ambayo lazima zipite kwangu. Hayo unayosema yakinifikia, nitayajibu lakini siwezi kuzungumza bila hakika kwamba amesema.”
Thursday, May 31, 2012
Subscribe to:
Posts (Atom)

