Thursday, June 14, 2012

10 Things Your Interviewer Won't Tell You


Wondering what's running through your interviewer's mind? Here are 10 things your interviewer might be thinking--but probably won't tell you:

1. You showed up too early. Many interviewers are annoyed when candidates show up more than five or 10 minutes early, since they may feel obligated to interrupt what they're doing and go out to greet the person. Some feel guilty leaving someone sitting in their reception area that long. Aim to walk in five minutes early, but no more than that.

2. We're judging how you're dressed and groomed. In most industries, a professional appearance still matters. You don't need to wear expensive clothes, but showing up in a casual outfit or clothes that don't fit properly, having unkempt hair, or inappropriately flashy makeup can harm your chances.

3. We don't want you to try to sell us. It's a turn-off when a candidate seems overly focused on closing the deal, rather than on figuring out if the job is the right fit. No hiring manager wants to think she's being aggressively sold; we want the best person for the job, not the pushiest spiel.

4. Little things count. Candidates often act as if only "official" contacts, like interviews and formal writing samples, count, but hiring managers are watching everything, including things like how quickly you respond to requests for writing samples and references, whether your email confirming the time of the interview is sloppily written, and how you treat the receptionist.

5. We might act like we don't mind you bad mouthing a former employer, but we do. We'll let you talk on once you start, but internally we're noting that you're willing to trash-talk people who have employed you in the past and are wondering if you'll do that to us too. What's more, we're wondering about the other side of the story--whether you're hard to get along with, or a troublemaker, or impossible to please.

6. You might be talking too much. Your answers to your interviewer's questions should be direct and to-the-point. Rambling and unnecessary tangents raise doubts about your ability to organize your thoughts and convey needed information quickly. If you're tempted to go on longer than two minutes, instead ask, "Does that give you what you're looking for, or would you like me to go more in depth about this?" If the interviewer wants more, she'll say so.

7. Fit really, really matters, so we think a lot about your personality. You might have all the qualifications an employer is looking for, but still not get hired because your working style would clash with the people with whom you'd be working. Remember, it's not just a question of whether you have the skills to do the job; it's also a question of fit for this particular position, with this particular boss, in this particular culture, and in this particular company.

8. We want you to talk about salary first for the exact reason you fear. Salary conversations are nerve-wracking for job seekers because they know that they risk low-balling themselves by naming a number first. And that's exactly why interviewers push candidates to throw out a number first. In an ideal world, employers would simply let candidates know the range they intend to pay, but in reality, plenty take advantage of the power disparity by making candidates talk about money first.

9. We're going to ask other people what they think of you. We're going to ask anyone who came in contact with you for their impressions--from the receptionist to the guy who you met for two minutes in the hallway.

10. We like thank-you notes, but not for the reason you think. Post-interview thank-you notes aren't just about thanking the interviewer for her time; the ones that are done well build on the conversation and reiterate your enthusiasm for the job.

EURO 2012 GOMEZ APELEKA KILIO UHOLANZI IKILALA DORO MBELE YA UJERUMANI


Pepe akishangilia baada ya kuipatia Ureno kamba ya kwanza


Ureno imeiadhibu Denmark 3-2 katika mtanange wa kundi B katika michuano ya Euro 2012.
Ushindi wa Ureno wa 3-2 dhidi ya Denmark katika michuano wa Euro 2012 unaweka matumaini ya nchi hiyo kuendelea hadi robo fainali.
Bao lililonusuru matumaini hayo lilitiwa kimyani na Silvestre Varela aliyeletwa kipindi cha pili aliyefunga bao na kufuta bao la Nicklas Bendtner la kusawazisha mapema katika kipindi cha pili.


Varela alieingia kipindi cha pili akishangilia goli la tatu na la ushindi la Ureno baada ya kutupia kambani.

Ureno iliongoza kupitia kipindi cha kwanza kupitia wachezaji wasiotarajiwa ambapo beki Pepe na Helder Postiga waliipatia Ureno mabao ya kuwapa matumaini ya kupiga hatua.

Lakini kukosa fursa kadhaa kwa nyota wao Cristiano Ronaldo kulitishia kuiangusha Ureno na kurejea nyumbani mapema.


Christia Ronaldo akijaribu kumhadaa mlinzi wa Denmark lakini alikosa mabao lukuki katika mechi hiyo

Ushindi huu unaiweka Ureno sambamba na Denmark kwa pointi kutokana na ushindi wa Denmark dhidi ya Uholanzi katika mechi ya ufunguzi kwa pande hizo mbili.

Katika mchezo wa pili siku ya Jumatano, Mario Gomez wa Ujerumani aliwafunza wachezaji wa Uholanzi namna ya kufunga mabao, walipoondoka na ushindi wa magoli 2-1.


Gomez (23) akitupia kambani goli la kwanza la Ujerumani

Hapa hapatoshi!!! Robben akijaribu kufanya udambwidambwi katika mtanange huo

Mshambulizi huyo wa Bayern Munich kwa upesi aliweza kugeuka alipopokea mpira kutoka kwa Bastian Schweinsteiger na kuandikisha bao la kwanza la Ujerumani katika dakika ya 24, na baadaye kuongezea la pili katika dakika ya 38, katika kuhakikisha Uholanzi itaondoka katika michuano ya Euro 2012 mapema.


Robin Van Persie na Van Der Vaart wakishangilia goli la kufutia machozi lililotupiwa kambani na Van Persie

Robin van Persie, ambaye alishindwa kuitumia nafasi nzuri iliyojitokeza na kuiwezesha Uholanzi kuongoza kufunga, hatimaye aliwafungia bao la kujituliza, lakini timu yake ikashindwa kufunga magoli zaidi.
DENMARK  2-3  URENO


UJERUMANI  2-1  UHOLANZI

DI MATTEO NAMBA YA BAHATI YAFYATUKA SASA KOCHA MKUU CHELSEA


Kocha alielamba dume Chelsea Roberto Di Matteo

Chelsea hatimaye imemteua Roberto Di Matteo kama meneja wake wa kudumu kwa kutiliana saini mkataba wa miaka miwili na sasa Di Matteo ana uhakika na umatemate kama kocha mkuu kwa nyundo mbili.
Di Matteo aliwekwa kama kocha wa mda kufuatia kutimuliwa kwa Andre Villas-Boas mnamo mwezi Machi, na akaweza kuiongoza klabu hio akifanikiwa kuifikisha na kushinda fainali ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya na vilevile kombe la FA la England.


Di Matteo kulia akiteta jambo na kocha alietimuliwa Andre Villa Boas, ambae sasa Di Matteo ndie amerithi Mikoba yake.

Meneja huyo aliyekua kiongozi wa MK Dons na pia West Brom, Di Matteo alipoteza mechi tatu tu kati ya mechi 21 alizosimamia, na kutokana na hali hiyo wachezaji wengi wa klabu waliunga mkono ateuliwe kama meneja wa kudumu hususan baada ya kushinda kombe lililoikwepa klabu hio kwa mda mrefu la Mabingwa wa Ulaya.

Di Matteo akiwa ameshikilia ndoo ya Ubingwa wa Ulaya alipoiwezesha Chelsea kulinyakua hivi karibuni baada ya ukata wa kombe hilo kwa muda mrefu na kumhakikishia Di Matteo kuwa na uhakika wa umatemate kwa miaka miwili kama kocha mkuu





Cherekochereko asie na mwana aeleke jiwe Di Matteo juujuu baada ya kutwaa kombe la mabingwa wa Ulaya

Tuesday, June 12, 2012

EURO 2012 UINGEREZA YAKABANA KOO NA UFARANSA, UKRAINE YAISAMBARATISHA SWEDEN


Andriy Shevchenko akitupia kambani kwa kichwa goli la kwanza

Mwachemwache kati ya Ibrahimovic wa Sweden na Khacheridi wa Ukraine

Mtanange wa michuano kombe la mataifa ya Ulaya umeendelea kwa mtindo wa kipekee kwa wenyeji Ukraine kuishushia kichapo Sweden cha mabao 2-1, huku mshambuliaji matata Andriy Shevchenko 'Sheva' akifunga mabao yote mawili maridadi kabisa kukamilisha siku njema kwa waandaaji hao wenza wa michunao ya UEFA EURO 2012 katika kundi D.
Zlatan Ibrahimovic aliifungia Sweden goli la pekee dakika saba baada ya kipindi cha mapumziko. Kisha baadaye mchezaji nyota wa zamani wa timu ya Milan, Shevchenko mwenye umri wa miaka 35 aliwasazisha dakika tatu baada ya bao la Ibrahimovic na kisha kupachika bao la ushindi dakika ya 68 ya mchezo.


Schevchenko akitupia la pili


Schevchenko akishangilia msumari wa pili

Ibrahimovic akishangilia goli la kufutia machozi

Baada ya mechi hiyo Schevchenko alisema anahisi ni kama ana umri wa miaka 20 na wala sio 35. "Tuna nafasi nzuri ya kusonga mbele katika michuano hii. Najisikia vizuri. Ulikuwa mchuano wa kihistoria kwetu. Ni ushindi wa kihistoria," aliongeza kusema Schevchenko.
Kocha wa Sweden, Erik Hamren hajaridhishwa na matokeo hayo. Amesema ili kushinda mechi zao wanahitaji wachezaji 11 waonyeshe mchezo wa hali ya juu kabisa. "Leo pengine watano au sita walionyesha ujuzi ninaoutaka. Hiyo haitoshi," akaongeza kusema kocha huyo.
UKRAINE Vs SWEDEN


Ufaransa yatoka sare na England
Kwenye mechi ya kwanza ya kundi D, England ilitoka sare ya 1:1 dhidi ya Ufaransa. Mkwaju wa 'freekick' uliopigwa na Steven Gerrard baada ya mwenzake James Milner kufanyiwa madhambi na Patrice Evra wa Ufaransa, ulipachikwa wavuni na Joleon Lescott kwa kichwa dakika ya 30 ya mpambano huo. Samir Nasri aliutikisa wavu wa England na kusawazisha dakika chache baadaye.



Lescott akipiga ndosi iliyokwenda moja kwa moja kambani na kuipatia England bao la kuongoza

Bao la Nasri lilikuwa na umuhimu mkubwa zaidi kuliko kusawazisha tu kwa sababu limeisaidia Ufaransa kuepuka aibu nyengine baada ya balaa la michuano ya kombe la dunia mwaka 2010 nchini Afrika Kusini na michunao ya kufuzu kwa EURO 2008 ambapo wachezaji walirejea nyumbani wakiwa na aibu baada ya kutolewa kwenye raundi ya kwanza.
Nasri mwenyewe amesema ana imani wanayo nafasi nzuri katika michuano ya mwaka huu na lengo lao ni kufika robo fainali. "Hatujapoteza kwa hiyo ni muhimu kuzingatia mpambano wetu dhidi ya Ukraine siku ya Ijumaa."


Mwajiri wetu mmoja kaka adoadoo!!! ndivyo Nasri wa Ufaransa anavyomuambia mlinda mlango wa Uingereza Joe Hart ambae wanakipiga nae Manchester City 

mwachemwache kati ya Ashley Cole na Samir Nasri

Huendi popote hapa!!! Gerradi akimpiga mkwara Ribery

Kocha wa Ufaransa, Laurent Blanc, amesema hawajafurahishwa sana na matokeo ya mechi hiyo lakini hawajavunjika moyo. "Tungepoteza mechi hii kama hatungejitahidi, lakini ukiangalia kwa ujumla tumecheza vizuri zaidi kuliko England," ameongeza kusema kocha huyo. Naye kocha wa England, Roy Hodgson kwa upande wake amesema mechi ilikuwa ngumu lakini wameridhika na matokeo.
Ufaransa sasa itachuana na Ukraine ambayo iko katika nafasi nzuri ya kufuzu kwa robo fainali huko Donetsk Ijumaa ijayo. England kwa upande wao wataumana na Sweden.
FRANCE Vs ENGLAND

Monday, June 11, 2012

KAMA UNA MOYO MWEPESI DON WATCH DIS!!!!

HII NI KWELI TUPU (18+)

STARS YAWALIZA GAMBIA,SAMATTA KAMA KAWA


Mshambuliaji wa Star Mbwana Samatta"Samagoal" akipiga kichwa langoni mwa Gambia

Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars jana iliwatoa kimasomaso watanzania baada ya kuibugiza Gambia kwa mabao 2-1 katika mchezo mkali uliopigwa katika dimba kuu la taifa jijini Dar es salaam.Gambia ndio walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa mshambuliaji Mustafa Jarju akitupia kambani kwa kichwa.
Wakati Gambia wakiamini wataiadhiri Stars nyumbani hamad...Shomari Kapombe akazifuta ndoto za wagambia kwa kusawazisha goli maridadi akitupia kambani kwa kichwa na kufanya matokeo kuwa 1-1 dakika ya 65 ya mtanange huo.

Mbwana Samatta"Samagoal" kama wanavyomuita mashabiki wa TP Mazembe ya kule jamhuri ya kidemokrasia ya kongo anakokipiga alikuwa mwiba mkali katika mechi hiyo kwa udambwidambwi wake kama kawa akaipepeta ngome ya Gambia kwa kumuadhiri beki wa kushoto kwa vyenga vya maudhi na kumuacha chini,Samatta alimimina krosi maridadi langoni katika mwachemwache ndipo beki wa Gambia akaunawa mpira katika eneo la hatari na mwamuzi bila ajizi akatenga maguu kumi na mbili ya mtu mzima..kama analia Erasto Nyoni akatupia kamba ya pili kwa Stars na ndipo hekaheka ,nderemo,mwachemwache zilipoibuka katika dimba kuu la Taifa..mpaka mwisho wa Mchezo Stars 2-1 Gambia. na Stars imejiweka pazuri katika kampeni za kuwania kushiriki kombe la dunia nchini Brazil 2014.

Kikosi cha Stars

Kikosi cha Gambia


Mbwana Samatta akiwa amewekwa chini baada ya kutaka kuleta madhara langini mwa Gambia


Nyinyi watoto wadogo tuu!!! 


Mwachemwache kati ya Samatta na mabeki wa Gambia


Kambaaaaaaa!! Erasto Nyoni akishangilia pamoja na Samatta baada ya Nyoni kutupia kamba ya pili na ya ushindi ya Stars


Ndio ukubwa kakaa..Ndivyo anavyosema kocha wa Stars Kim Poulsen akimwambia kocha wa Gambia Luciano Mancini baada ya mtanange kumalizika kwa Star kuibuka washindi