Thursday, June 28, 2012
USIENDESHE GARI KARIBU NA MAGARI YALIYOPAKIA MAKONTENA (ANGALIZO)
Gari kubwa lililobeba kontena likiwa limeliangukia gari dogo!!
Mashuhuda na waokoaji wakiwajibika kujaribu wawezalo kuokoa maisha ya watu..mhhh itakuwa ngumu hapa mtu kuchomoka.
Sehemu ya mbele ya gari dogo lililoangukiwa na kontena linavyoonekana. Ina maana jamaa alichoambulia kizima ni 'plate number' tu.
Mmoja kati ya timu ya waokoaji akiwa hajui aanzie wapi na aishie wapi jinsi vigari vilivyosagwa na kontena.
Watu wa huduma ya kwanza wakijaribu kuokoa maisha kwa kumuwekea maji majeruhi wa ajali hiyo huko Indonesia.
Hakuna mwenye uhakika kuwa atapona au la!!!
URENO YATOLEWA KAMASI NA SPAIN, SPAIN YATINGA FAINALI EURO 2012
Andre Iniesta akijaribu kumtoka beki wa Ureno.
Mhhh sikio la kufa halisikii dawa.....C.Ronaldo akiwa ameduwaa baada ya kipigo
Mabingwa watetezi Uhispania wametinga fainali ya EURO 2012 baada ya kuifumua Ureno 4-2 katika changamoto za mikwaju ya penalti, baada ya dakika 90 na dakika 30 za ziaida kumalizika kwa timu hizo mbili kushindwa kufungana.
Bao la penati la mwisho lilitupiwa kambani kwa umaridadi mkubwa na Cesc Fabregas, na kuwapa wenzake matumaini ya kutetea ubingwa wa EURO 2012 na sasa wanasubiri mshindi katika nusu fainali nyingine leo kati ya Ujerumani na Italia katika fainali ya Jumapili.
Fabregas, ambaye ni kiungo wa kati wa timu ya Barcelona, alipiga mkwaju
ambao baada ya kugonga mwamba upande wa kushoto, ulitambaa wavuni, na ikawa ni
tiketi ya Uhispania kufanya mipango ya kusafiri hadi Kiev, Ukraine, katika mchezo wa
fainali.
Mchezaji wa Ureno, Bruno Alves, alielekea kuwa na wasiwasi, na kushindwa kufunga mkwaju wake, baada ya mpira kugonga mwamba, na Ronaldo, akiwa amepangwa na timu yake katika nafasi ya tano kwa wapigaji penalti, hakupata hata nafasi ya kutimiza wajibu huo.
Wengine waliokosa kufunga kupitia mikwaju ya penalti ni mchezaji wa Ureno, Joao Moutinho, wakati kipa wa Uhispania, Casillas, alipoweza kuokoa kwa kuruka upande wa kkulia.
Awali mchezaji wa Uhsipania Xabi Alonso naye alikosa kutupia kambani mkwaju wa penalti, licha ya kwamba ulikuwa ni mkwaju wa kasi na uliopigwa kwa nguvu, lakini kipa Rui Patricio akaunyaka.
C.Ronaldo akijiangusha katikati ya mabeki Pique na Silva
Luis Nani wa Ureno akijaribu kukukuruka katika mechi hiyo
Beki wa Ureno Contrao akitunishiana misuli na D.Silva wa Uhispania
Beki wa Spain Gerald Pique akimmudu ipasavyo Christiano Ronaldo wa Ureno
URENO Vs UHISPANIA
Wednesday, June 27, 2012
ZITTO ALIA NA SERIKALI UNYAMA ALIOFANYIWA Dkt ULIMBOKA

Dkt. Ulimboka akiwa ktk hali mbaya mara baada yakuokotwa akiwa hajitambui,Habari zilizomwagika hivi punde zinadai kuwa Dkt Ulimboka alitekwa jana usiku mishale ya saa 6 za usiku na Watu ambao hawakuweza kufahamika mara moja,habari za wataalamu wa mambo zinasema Dkt alipigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kwa jina moja la Abeid..na wakati akiwa katika juhudi za kuonana na huyo mtu watu wawili"vipande" waliokuwa na silaha walimvamia na kumteka kabla hajaangushiwa kisago cha kufa mtu ambacho kilimuacha akiwa hoi bin taaban katika msitu wa Magwepande..kufuatia kitendo hicho wataalamu wa mambo wamefunguka kuwa wafanyakazi wa chumba cha maiti muhimbili nao wamegoma na kuna tetesi za mgomo kuwa mkubwa zaidi!
Akizungumza baada ya kupata habari hizo ifuatayo ni Taarifa ya Mh Zitto.
Ujumbe amenitumia Daktari yupo pale MOI ‘Kaka Zitto,hali ya Dr.Ulimboka yuko unconscious,multiple ribs fracture na kwenye mikono pia amevunjika pamoja na taya,yuko icu wanamstabilise kwanza kwasababu hapumui vizuri,the situation here is really bad,I agree with you this is outright outrageous’Nimechukizwa sana na habari za kutekwa, kupigwa na kuumizwa vibaya kwa Dr Ulimboka, Kiongozi wa Madaktari Nchini. Mambo kama haya tumezoea kuyasikia kwenye nchi za kidikteta na kuongozwa kiimla ambapo watawala badala ya kutumia njia ya kidemokrasia na kisheria kushughulikia wanaoamini ni maadui zao katika utawala, hutumia wahuni katika Taasisi za usalama kuteka raia, kuwatesa, kuwafunga na hata kuwaua.
Sitaki kuamini kwamba Tanzania imefikia huko. Nimezungumza na baadhi ya madaktari walio karibu na Dokta Ulimboka na kujulishwa kwamba majeruhi huyu wa vitendo vya hovyo kabisa kutokea hapa nchini alikamatwa jana usiku mnamo saa sita na watu wasiojulikana na kupelekwa katika msitu wa MagwePande na kujeruhiwa vibaya. Habari hizi bado hazijathibitishwa na vyanzo huru lakini ndio zilizopo hadi hivi sasa.
Serikali kama mlinzi wa usalama kwa raia inaWAJIBU kueleza tena kwa haraka ni nini kimetokea kwa kijana huyu msomi na kiongozi wa wataalamu wenzake. Serikali INAWAJIBIKA kueleza katika nyakati kama hizi ambapo kuna mgogoro kati yake na madaktari imekuwa wapi kuhakikisha usalama wa viongozi wa madaktari ili kuepusha watu wanaoitwa ‘agente provocateure‘ kuweza kuhatarisha hali ya amani ya nchi na hata kupelekea kuweka hali ya vitisho kwa madaktari wetu.
Serikali INAWAJIBIKA kueleza kama sasa imeamua kutumia njia za kihuni kumaliza matatizo na wananchi wake.
Nimemuomba Waziri kivuli wa Afya wa CHADEMA kufuatilia suala hili kwa kwa karibu sana ili kuhakikisha kwamba ukweli wote na ukweli mtupu unafahamika. Kamwe hatuwezi kuacha Mtanzania yeyote aonewe, anyanyaswe au akandamizwe eti kwa sababu ya kudai haki yake na za wenzake. ‘An injury to one, injuries to all’
Naomba madaktari wamwangalie kwa karibu daktari mwenzao ili aweze kupata nafuu. Ulinzi uimarishwe ili kuhakikisha usalama wake.
EURO 2012 NUSU FAINALI YA MAFUNDI WANAOJUANA SPAIN Vs URENO
Christiano Ronaldo wa Ureno(Real Madrid)
Xavi Alonso wa Uhispania (Real Madrid)
Miamba ya soka barani Ulaya Ureno na Uhispania leo zitapepetana katika nusu fainali ya kwanza ya michuano ya Ulaya katika dimba la Donbass,Donetsk.
Timu hizo mbili zinakutana zikiwa zimesheheni nyota wanaocheza soka la hali ya juu huko barani Ulaya na kwa idadi kubwa ya wachezaji wanakipiga La Liga Uhispania katika timu za Real Madrid na Barcelona hakika leo hatumwi mtoto dukani.
Ureno itamtegemea zaidi Christiano Ronaldo na Beki matata Pepe, Varela,Moutinho,Meireles,Luis Nani na wengineo wengi. huku wapinzani wao Uhispania ikimtegemea zaidi A.Iniesta kama mchezeshaji na wakali wengine kama Xavi,Torres,Sergio Bosquets,Sergio Ramos,Gerald Pique,David Silva,Pedro,Fbregas na mlinda mlango mashuhuri Iker Casillas.
Ureno wamefika hatua ya nusu fainali baada ya Kujikusanyia pointi 6 na kukamata nafasi ya pili katika kundi B. na hivyo kuingia katika hatua ya robo fainali ambapo walikutana na Ugiriki na kufanikiwa kuwasambaratisha wagiriki kwa bao moja kwa nunge likitiwa kambani na Christiano Ronaldo katika dakika ya 78.
Uhispania ilifanikiwa kutinga katika hatua ya robo fainali za michuano ya EURO 2012 pale ilipojikusanyia pointi 7 na kuibuka kidedea katika kundi C, katika hatua ya robo fainali hizo ilikutana na vigogo wengine wa Ulaya Ufaransa na bila aibu kuwafurumusha nje ya michuano hiyo kwa mabao 2 kwa buyu huku mabao yote yatupiwa kambani na Xavi Alonso katika dakika ya 18 na 90.
Katika mtanange wa Nusu fainali ya leo kati ya Ureno na Uhispania ni vigumu mno kutabiri nani ataibuka meno nje kwa jinsi vikosi vyote vilivyosheheni nyota wanaojuana mno kwa ukweli kuwa wanatoka katika vilabu ambavyo hukutana mara kwa mara katika ligi za Ulaya sana sana La Liga ya Uhispania na Premier league ya Uingereza.
Andre Iniesta wa Uhispania (Barcelona)
Gerald Pique wa Uhispania (Barcelona)

Torres wa Uhispania (Chelsea)
Fabregas wa Uhispania (Barcelona)
Xavi Hernandez (Barcelona)
Moutinho wa Ureno (Sporting Lisbon)
Pepe wa Ureno (Real Madrid)
Silvester Valera wa Ureno (FC Porto)
Luis Nani wa Ureno (Manchester United)
Tuesday, June 26, 2012
STAR WA BONGO MOVIE FLORA MVUNGI KATIKA KASHFA YA UTAPELI WA 200,000/=

Flora Mvungi
Star maarufu katika tasnia ya filamu za kibongo "Bongo Movies" Flora Mvungi ameshutumiwa kupokea mlungula wa kiasi kadhaa unaofikia shilingi za kibongo laki mbili (200,000) kutoka kwa mtayarishaji wa filamu chipukizi aliejulikana kwa jina moja la Othman.
Akielezea mkasa huo wa "kupigwa" Tshs 200,000/= za kibongo na staa wa filamu nchini Mtayarishaji huyo wa filamu a.k.a Producer amesema Alikubaliana na Flora ampatie kiasi hicho ili aweze kushiriki katika filamu anayoiandaa inayoenda kwa jina la MZIWANDA. Othman anasema walipokubaliana alimtumia Flora mkwanja huo kwa njia ya Tigopesa, lakini ilipofika muda wa kuwa mahala pa kutayarisha filamu (Location) Staa huyo hakutokea kwa visingizio lukuki. Lakini Producer huyo akafunguka kuwa safari hii ilikuwa mara ya nne kuzinguliwa na Flora katika maswala mazima ya kufika eneo la tukio maarufu kama Location.
Producer Othman alipokuwa akihojiwa na kituo kimoja maarufu cha redio hapa nchini alifunguka hayo na ndipo mtangazaji wa kipindi hicho alipoamua kuwaunganisha kwa njia ya simu, katika hali ya mshangao staa huyo alikana kumfahamu Producer huyo wa movie za kibongo lakini alikiri kuwa kuna filamu ambayo aliitwa akashiriki lakini kutokana na sababu fulanifulani hakufika na akaahidi aitwe mambo yatakapokuwa tayari.
Utamu ukanoga pale mtangazaji alipomvutia kamba Flora Mvungi na kisha akamuuliza maswali kadhaa halafu akamuweka hewani wapeane makavu na producer, Hali ilikuwa ya majibizano makali Flora akikana kupokea mkwanja hali iliyoonekana kumkera zaidi Producer huyo na akisisitiza kuwa staa huyo asijifanye mjanja kwani yeye ana uthibitisho wa Message alizomtumia pesa ghafla Flora akakata simu nganjaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!! Hali hii iliacha SINTOFAHAMU ikiwa imetanda katika sakata hilo.
Subscribe to:
Posts (Atom)