Tuesday, July 3, 2012

ANDRE INIESTA MCHEZAJI BORA EURO 2012 TORRES MFUNGAJI BORA


Andre Iniesta Mchezaji bora EURO 2012

Kiungo wa Uhispania, Andres Iniesta amenyakua tuzo ya uchezaji bora wa Euro 2012, huku mwenzake Fernando Torres akinyakua tuzo ya ufungaji bora iliyotolewa na Shirikisho la Soka la Ulaya ( UEFA).
Kiungo huyo wa Hispania mwenye miaka 28, aliyechangia ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Italia usiku wa Jumapili iliyopita, alitajwa kuwa mchezaji bora wa mechi hiyo ya fainali na Kamati ya Ufundi iliyoundwa na watu 11.
Nyota huyo wa Barcelona alishindwa kufunga bao na kutegeneza moja katika fainali hiyo, lakini amepata tuzo hiyo kutokana na mchango wake wa jumla ulivyowawezesha Hispania kutetea taji lao.
Iniesta alitegeneza bao muhimu lililofungwa na Jesus Navas likiwa ni bao pekee dhidi ya Croatia kwenye mchezo wa mwisho wa makundi, huku pasi yake nyingine kwa Cesc Fabregas katika mchezo wa fainali ikimsaidia Fabregas kupiga krosi iliyomkuta David Silva aliyefunga bao la kwanza.
Katika tuzo hiyo Iniesta alifanikiwa kuwapiku Andrea Pirlo wa Italia na nyota mwezake wa Barcelona, Xavi aliyetwaa tuzo hiyo mwaka 2008.
Iniesta amekuwa miongoni mwa wachezaji 10 wa Hispania wanaounda kikosi cha wachezaji 23 wa mashindano hayo.
Naye mshambuliaji wa Hispania, Fernando Torres amefanikiwa kutwaa Kiatu cha Dhahabu kufuatia kuibuka mfungaji bora na kumpiku mwenzake wa Ujerumani,Mario Gomez.
Mshambuliaji huyo mwenye miaka 28, alifunga bao moja katika ushindi wao wa mabao 4-0 dhidi ya Italia na kumfanya kuwa mchezaji pekee aliyefunga mabao katika mechi mbili tofauti za fainali.
Bao hilo lilimfanya kuwa sawa na Gomez aliyefunga mabao matatu na kutegeneza bao moja kwenye michuano hiyo iliyofikia tamati jana.
Hata hivyo, Uefa iliamua kumpa Torres zawadi hiyo kutokana na kutumia muda mchache uwanjani na kufunga mabao.
Nyota huyo wa Hispania alitumia dakika 189 kucheza mashindano hayo kulinganisha na Gomez aliyetumia dakika 280.
Wachezaji wengine wanne waliofunga mabao matatu ni Mario Balotelli (Italia), Cristiano Ronaldo (Ureno), chipukizi wa Russia, Alan Dzagoev na nyota wa Croatia, Mario Mandzukic.
Tuzo hiyo inamfanya Torres kumaliza vizuri zaidi msimu wa 2011/12 baada ya kutwaa Kombe la FA na Ligi ya Mabingwa akiwa na klabu yake ya Chelsea, lakini ameshindwa kuingia kwenye kikosi cha wachezaji 23 wa michuano ya Euro 2012 kilichotajwa jana na Uefa.
Hispania imekuwa timu ya kwanza ya taifa kutwaa mataji matatu mfululizo tangu, Euro 2008, Kombe la Dunia 2010 na Euro tena mwaka huu.
Andres Iniesta Andres Iniesta of Spain in action during the UEFA EURO 2012 group C match between Spain and Ireland at The Municipal Stadium on June 14, 2012 in Gdansk, Poland.
Andres Iniesta of Spain with the ball during the UEFA EURO 2012 final match between Spain and Italy at the Olympic Stadium on July 1, 2012 in Kiev, Ukraine.
A.Iniesta akitiririka




Huwa anakusanya Vijiji kama hivi


Fernando Torres mfungaji bora EURO 2012


Torres akitupia kambani mechi ya fainali dhidi ya Italia



Baba na wana

Famili inahusika katika ushindi bhanaa

Torres akiwa amebeba "ndoo" ya EURO 2012

Monday, July 2, 2012

SPAIN BINGWA EURO 2012 YAITUNGUA ITALIA 4-0


Uhispania waliandikisha historia kwa maarifa ambayo sio rahisi kuiga, kwa kuitungua Italia magoli 4-0 katika fainali ya Euro 2012 usiku wa Jumapili, mjini Kiev, Ukraine.

Licha ya mchezo mzuri wa Italia, vijana wa meneja wa Uhispania, Vicente del Bosque walithibitisha kwamba kimataifa wanaweza kujigamba wao ndio wenye mchezo bora zaidi duniani, kwa kuzingatia namna walivyoichezea timu ya Italia, na kuwalazimisha kusalimu amri.

David Silva aliifungia Uhispania bao la kwanza, na kabla nusu ya kwanza ya mchezo kumalizika, mchezaji mpya wa Barcelona, Jordi Alba aliandikisha bao la pili, baada ya kukimbia kwa kasi na kumalizia kwa ustadi kabisa.

Ingawa Italia walikuwa na upungufu wa mchezaji mmoja, baada ya kumpoteza mchezaji wa zamu wa tatu Thiago Motta baada ya kujeruhiwa, walicheza kwa bidii, lakini wataalamu wa kandanda kwa upande wa kupokezana mpira, Uhispania, waliwadunisha kabisa.

Fernando Torres aliingia kama mchezaji wa zamu, na akafanikiwa kuubadilisha mchezo, na akiandikisha bao la tatu la Uhispania, kabla ya mwenzake katika klabu ya Chelsea, Juan Mata, kuandikisha bao la nne na la mwisho la Italia, na ambalo bila shaka liliwavunja moyo kabisa mashabiki wote wa Italia.

Mchezo huo bila shaka umeyazima matamshi ya baadhi ya watu ambao awali walimlazimu kocha wa Uhispania Del Bosque na wachezaji wake kujitetea katika mkutano na waandishi wa habari, kabla mechi ya fainali kuanza, kwamba mchezo wao katika mashindano ya Euro 2012 umekosa msisimko.

Lakini usiku wa Jumapili mambo yalikuwa tofauti.

Maarifa yote yaliyowawezesha kuwa mabingwa wa Euro 2008 na vile vile Kombe la Dunia la mwaka 2010 nchini Afrika Kusini yalijitokeza.

Ilikuwa ni fainali ambayo ilimvunja moyo kabisa kocha wa Italia, Cesare Prandelli, lakini bila shaka haikuwa fedheha kushindwa na timu yenye maarifa ya hali ya juu kiasi hicho.

Italia itaweza kujivunia namna ilifika katika fainali, licha ya kushindwa kwa magoli mengi na timu ambayo ilikuwa ni wazi imo katika kiwango cha pekee.

Tulia ngedere weeee!! Kazi kati ya Pique na Balotelli


Kambaa..David Silva akianza kuwatia njaa Italia





Friday, June 29, 2012

RIDHIWANI KIKWETE AFANYIWA KITU MBAYA


Ridhiwani Kikwete akiwa na mwendeshaji The Mboni Show, Mboni Masimba

Katika dunia ya leo maendeleo ya sayansi na teknolojia yamekuwa yakileta tija kila kukicha na kukuza ustawi wa jamii mbalimbali. Kwa kuizungumzia teknolojia ya mawasiliano ambayo imekuwa kwa kasi na kuifanya jamii yetu kuishi maisha ya kisasa ambayo kila kazi imerahisishwa, Maendeleo hayo yamewezesha jamii mbali mbali kubadilishana ujuzi na kuvumbua vitu vipya kila kukicha na kutokana na ukweli juu ya utendaji wa teknolojia hizo sasa dunia imekuwa ni ndogo mno yaani kama kijiji kimoja ambapo watu wanaweza kufanya shughuli mbalimbali bila kujali umbali waliopo baina yao na haya yote ni matunda ya Maendeleo ya teknolojia ya mawasiliano.

Maendeleo hayo na faida zote pia kuna madhara ya matumizi ya teknolojia hizo hususani za mawasiliano ambapo katika dunia ya sasa kuna mitandao ya kijamii ambayo huwaweka watu karibu zaidi, Na miongoni mwa wahanga wa madhara ya teknolojia hizi ni Ridhiwani Kikwete ambaye ni mtoto wa Rais wa Tanzania Mh Dk Jakaya Mrisho Kikwete.

Akizungumzia yaliyomsibu kutokana na teknolojia ya mawasiliano wakati akihojiwa katika kipindi Cha The Mboni Show kinachoendeshwa na Mboni Masimba na kurushwa na kituo bora kabisa kwa vijana wa kisasa cha East Africa (EATV), Ridhiwani alisema maendeleo ya teknolojia yamemuathiri pale account yake ya mtandao wa Kijamii wa FACEBOOK (ambao umejizolea umaarufu mkubwa ulimwenguni kwa hivi sasa) ilipovamiwa ama kupokwa na wahalifu wanaojulikana kama kitaalamu kama "HACKERS". Walitumia utaalamu wao na kujimilikisha account hiyo na kupost status ambayo ilizua utata mkubwa kwa Ridhiwani na familia yake.

Akielezea kuhusu mkasa huo anasema baada ya ile status kuonekana akiwa hajui hili wala lile alipokea simu usiku wa saa saba, na mara alipopokea hakupata hata salamu na neno la kwanza akaulizwa,"Hivi wewe zinakutosha?" alipatwa na mshangao asijue la kufanya. ndipo alipoingia kwenye internet akagundua kuwa kuna kitu kimefanyika kwenye account yake ya FACEBOOK.
Baada ya kufuatilia sana wale wote waliodhani kuwa maneno yale aliyaandika Ridhiwani waligundua kuwa kweli sio yeye bali kuna wahalifu wa mitandaoni ndio waliomfanyia kitendo kile.
Ridhiwani anasema "haiingii akilini,Rais ni baba yangu halafu niseme maneno kama yale, na itakuwa ni usaliti kwa Chama changu kwani mimi ni mwanachama wa CCM,Hata kama nawapenda wapinzani siwezi kusema kwenye internet nitakaa nalo moyoni"

Wageni wa The Mboni Show kushoto Ridhiwani Kikwete,Mboni,Barnaba na Lisa Jensen


Mboni Masimba katikati akiwa na wageni wake Ridhiwani na Lisa Jensen






Linsa Jensen na Barnaba wakisalimiana na mashabiki waliohudhuria kipindi cha The Mboni Show

BALOTELLI AWALIZA WAJERUMANI AIPELEKA ITALIA FAINALI EURO 2012


Mpira uliopigwa na Balotelli ukitinga kambani kuandika bao la kwanza

Barwuah Balotelli alitupia kambani magoli mawili ya kupendeza mno na kuiwezesha timu yake ya Italia kuishangaza na kuiacha kinywa wazi Ujerumani kwa kuitandika magoli 2-1 katika nusu fainali ya Euro 2012, na kujihakikishia nafasi ya kucheza mechi ya fainali mjini Kiev dhidi ya Uhispania.

Mabao ya mtukutu huyo wa klabu ya Manchester City ya England, alitupia goli la kwanza wavuni kwa kichwa, na la pili kwa mkwaju wa kasi mno katika uwanja wa mjini Warsaw, na Italia kuwathibitishia Wajerumani katika kipindi cha kwanza kwamba ilikuwa na nia kamili ya kufika fainali.
Wajerumani, kufuatia mshituko, walianza kucheza kwa makini zaidi, lakini bao lao la penalti, ambalo lilipatikana katika dakika ya 92, kupitia Mesut Ozil, lilichelewa mno, na halikuweza kuwaokoa.

Italia kamwe hawajawahi kushindwa na Ujerumani katika mashindano makubwa, na wamefanikiwa sasa kucheza mechi nane dhidi ya Ujerumani pasipo kushindwa.

Hii sasa itakuwa mara ya tatu kwa Italia kuingia fainali za michuano hii ya mataifa ya Ulaya, na wataingia fainali kama timu inayodhaniwa kuwa dhaifu ikilinganishwa na mabingwa watetezi Uhispania.

Timu hii ya meneja Cesare Prandelli ilistahili ushindi, kwani sio tu waliweza kupambana na Ujerumani ambayo iliwashinda wapinzani wao kwa urahisi, bali pia walifunga mabao yao mapema katika kipindi cha kwanza.

Timu hiyo ya Azzurri ilikuwa na nafasi ya kujiongezea magoli, lakini ilicheza kwa tahadhari kwa kuhofia kwamba iwapo ingeliongoza mashambulizi zaidi dhidi ya Italia, kulikuwa na uwezekano wa ngome yao kuachwa ikiwa dhaifu, na Wajerumani kuwashambulia.

Italia 2-1 Ujerumani


Mtaalamu Pirlo akiyoyoma na mpira


Balotelli akishangilia bao la pili


Gomez akipiga kichwa kilichopaa golini


I am superman...Balotelli akitunisha misuli baada ya kutupia kambani bao maridhawa


Ukiujua ni raha sana..kama nnaliaaaaaaaa!!!


Viti vya moto..wajerumani wamesepa!!!


Mesut Ozil



Wera weraaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!


Mlinga mlango wa Italia Gianluigi Buffon akishangilia ushindi dhidi ya Ujerumani



Muuaji wa Ujeruman Barwuah Balotelli akishangilia ushindi mwanana



Thursday, June 28, 2012

SUMMER SUMMA-C.KHiD


USIENDESHE GARI KARIBU NA MAGARI YALIYOPAKIA MAKONTENA (ANGALIZO)

www.dilsedesi.org
Gari kubwa lililobeba kontena likiwa limeliangukia gari dogo!!

www.dilsedesi.org
Mashuhuda na waokoaji wakiwajibika kujaribu wawezalo kuokoa maisha ya watu..mhhh itakuwa ngumu hapa mtu kuchomoka.

www.dilsedesi.org
Sehemu ya mbele ya gari dogo lililoangukiwa na kontena linavyoonekana. Ina maana jamaa alichoambulia kizima ni 'plate number' tu.

www.dilsedesi.org
Mmoja kati ya timu ya waokoaji akiwa hajui aanzie wapi na aishie wapi jinsi vigari vilivyosagwa na kontena.

www.dilsedesi.org
Watu wa huduma ya kwanza wakijaribu kuokoa maisha kwa kumuwekea maji majeruhi wa ajali hiyo huko Indonesia.

www.dilsedesi.org

www.dilsedesi.org
Hakuna mwenye uhakika kuwa atapona au la!!!

61 Easy Ways To Lose Weight

61 Easy Ways To Lose Weight