Monday, July 9, 2012

RATIBA KOMBE LA KAGAME 2012


KAGAME CUP 2012 FIXTURE
1-Sat. 14th July 1 APR vs WAU SALAAM Uwanja wa Taifa 2pm

2-YANGA vs ATLETICO Uwanja wa Taifa 4pm

3-Sun. 15th July 3 AZAM vs MAFUNZO Chamazi 4pm

4-Mon. 16th July 4 VITA CLUB vs PORTS Uwanja wa Taifa 2pm

5-SIMBA vs URA Uwanja wa Taifa 4pm

6-Tue. 17th July 6 ATLETICO vs APR Uwanja wa Taifa 2pm

7-WAU SALAAM vs YANGA Uwanja wa Taifa 4pm

8-Wed. 18th July 8 VITA CLUB vs URA Uwanja wa Taifa 2pm

9-PORTS vs SIMBA Uwanja wa Taifa 4pm

10-Thu. 19th July 10 ATLETICO vs WAU SALAAM Uwanja wa Taifa 2pm

11-MAFUNZO vs TUSKER Uwanja wa Taifa 4pm

12-Fri. 20th July 12 PORTS vs URA Uwanja wa Taifa 2pm

13-YANGA vs APR Uwanja wa Taifa 4pm

14-Sat. 21st July 14 AZAM vs TUSKER Uwanja wa Taifa 2pm

15-SIMBA vs VITA CLUB Uwanja wa Taifa 4pm

16-Sun. 22nd July REST DAY


QUARTER FINALS

Mon. 23rd July 16 B2 vs C2
17 A1 vs C3

Tue. 24th July 18 C1 vs A2
19 B1 vs A3

Wed. 25th July REST DAY
SEMI FINALS

Thu. 26th July 20 Winner 16 vs Winner 17

Thu. 26th July 21 Winner 18 vs Winner 19

Fri. 27th July REST DAY

FINALS AND 3rd PLACE PLAY OFFS
Sat. 28th July 22 Loser 20 vs Loser 21
23 Winner 20 vs Winner 21

DIVA AFUNGUKA ANAETAKA KUMUOA AWE NA MILIONI 500 TASLIMU


Loveness Love "Diva"

Mtangazaji maarufu wa radio moja ya jijini Diva Loveness Love,Clouds Fm amefunguka na kusema kuwa anaetaka kumtoa katika geti la Mzee Malinzi ambaye ni baba yake pale msasani basi kidume huyo atahitajika kuwa na Milioni 500 Taslimu.
Mtangazaji huyo wa kipindi cha ala za roho cha Clouds FM kinachoanza saa nne za usiku alikuwa akifanya mazungumzo na mtangazaji mwenzake Adam Mchomvu katika kipindi cha XXL mida ya saa 9:30 mchana Diva alifunguka kwa kujiamini kuwa mwanaume anaetaka kumuoa ni lazima awe na milioni 500 taslimu,ndipo atamng'oa kwa Mzee Malinzi, katika mazungumzo hayo Diva alisisitiza na alipoulizwa kama hatotokea akaema basi...tungoje mimi na wewe hatujui yetu macho na masikio. Dunia hii.

Diva katika possssssssssssss

LIL WAYNE AHUDHURIA NDOA YA MAMA YAKE MZAZI

Lil-Wayne-and-Birdman-at-Ms-Citas-wedding
Lil Wayne na Birdman wakiwa kanisani wakati mama yake Lil wayne akifunga ndoa

LIl-Wayne-and-son-at-ms-Cita-and-Avery-wedding
Lil Wayne a.k.a Lil Wiz akiwa na kidume chake Sarah kanisani

Lil-Waynes-Daughter-Reginae
Binti yake Lil Wiz aitwae Reginae akiwa na mtoto wa kiume wa Birdman katika shughuli hiyo ya kukata na mundu

10
Padri akimfungisha ndoa mama yake Lil Wayne na baba yake mpya.

Birdman-at-Jacita-and-Averys-wedding
Birdman akimuongoza mama yake Lil Wayne Ms Jacinta

Lil-Wayne-gushing-over-his-mother
9 (1)
Lil Wayne akiwa na mama yake aitwae Jacinta katika ndoa ya Ms Jacinta na Avery

5 (1)
Binti yake Lil Wayne Reginae akiwaongoza wenzake kwenda kusimamia harusi ya bibi yake

Lil-Waynes-sons-by-Sarah-and-Nivea
Vijidume vya Lil Wayne,Sarah na Nivea vikitinga kanisani kusimamia harusi ya bibi yao

12
Burudani kabambe iliporomoshwa kanisani utaaaaaaaaaaaaaamu

Thursday, July 5, 2012

HASHEEM THABEET AULA OKC KUVUNA DOLA 880,000


Hasheem akifanya majamboooozz!!!

Nyota wa kikapu Mtanzania Hasheem Thabeet ameula baada ya kupata dili murua la kuhamia timu ya mpira wa Kikapu ya Oklahoma City Thunder (OKC) akitokea Portland Trail blazers ambapo kabla ya Portland alitokea Memphis Zote za nchini Marekani.
Habari zinasema Hasheem amesaini mkataba wa 'nyundo' mbili na anatarajiwa kuvuna umatemate wa kiasi cha dola za kimarekani 880,000 kwa mwaka a.k.a Nyundo.
Haya sasa vijana waliopo katika mchezo wa kikapu fuateni nyayo hizo.





Basketball sio lelemama lazima uwe umeshiba








Hasheem akiwa na rais wa Tanzania Mh Jakaya Mrisho Kikwete alipotembelea Ikulu jijini Dar es salaam

Menu time!!!!

YANGA YATIMULIWA ZANZIBAR KOCHA MPYA ATINGA DAR


Kocha mpya wa Yanga Tom Saintfiet alipowasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl J.K Nyerere,Dar es salaam.

KOCHA mpya wa Yanga, Tom Saintfiet (39) ametua nchini jana mchana, akitanguliza kauli kwamba, atatumia uzoefu wake kimataifa katika taaluma ya ukocha kuleta mageuzi makubwa ndani klabu hiyo ya Jangwani.Saintfiet, raia wa Ubelgiji alitua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kulakiwa na mamia ya mashabiki wa Yanga wakiongozwa na Katibu Mkuu, Celestine Mwesingwa.

Akizungumzia ujio wake, Saintfiet atakayerithi mikoba ya Kostadin Papic, alisema anaifahamu Yanga muda mrefu baada ya kuifuatilia katika mitandao pamoja na mashindano ya Kagame.

"Mimi siyo mgeni na Soka la Afrika, nalifahamu vizuri nimefanya kazi Nigeria, Zimbabwe, Namibia na Ethiopia. Kwa sababu hiyo, sioni kikwazo cha kushindwa kufikia malengo yangu.

"Isitoshe habari za Yanga na soka la Afrika Mashariki nazifahamu kupitia kusoma kwenye tovuti mbalimbali.

"Mwaka jana nilifuatilia kupitia kituo cha Super Sport kilichokuwa kinarusha mashindano ya Kagame," alisema Saintfiet.

"Zaidi natarajia kupata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa uongozi na mashabiki ili kazi yangu iwe rahisi kuitekeleza."

Baada ya kuzungumza na wanahabari, Saintfiet alipanda katika gari aina ya Land Cruiser mpaka makao makuu ya klabu akisindikizwa na msafara wa mabasi madogo matatu.

Makao makuu, Mtaa wa Jangwani, Saintfiet alifanya mazungumzo mafupi na Mwesigwa kisha akaelekea kwenye ukumbi na kuwasalimu mamia ya mashabiki waliokuwapo kumlaki.

"Nashukuru kwa mapokezi mazuri mliyonipa, kilichobaki ni kufanya kazi iliyonileta ili Yanga iweze kufikia mafanikio," alisema Saint Fiet.

Kwa mujibu wa msemaji wa Yanga Louis Sendeu, leo asubuhi Saintfiet atakutana na uongozi wa Yanga kwa mazungumzo kabla ya kusaini mkataba.

Wakati huohuo, habari zilizolifikia Mwananchi jana jioni zilidai kuwa Yanga imeondolewa katika michuano
ya Kombe la Urafiki inayoendelea mjini Zanzibar baada ya kukiuka masharti ya waandaaji.

"Tumeiondoa Yanga katika mashindano yetu ya Urafiki kutokana na kwenda kinyume na maelekezo ya barua ya mwaliko.

Tuliwataka kuleta timu itakayocheza michuano ya Kombe la Kagame, lakini wamefanya kinyume chake kwa kuleta timu B.

"Wametusababishia hasara kubwa, mashabiki wamekasirishwa, hawana tena hamu ya kuja uwanjani," alisema msemaji wa Chama cha Soka Zanzibar (ZFA), Munir Zakaria.

Walipoulizwa viongozi wa Yanga hawakuwa tayari kusema lolote kwa madai kuwa walikuwa na jukumu kubwa la mapokezi ya kocha wao mpya.

Katika hatua nyingie, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) jana ilitoa kiasi cha Sh20 milioni kwa ajili ya kufanikisha maandalizi ya Uchaguzi Mdogo kuziba nafasi zilizoacha wazi kufuatia uongozi wa awali kujiuzulu.

Uchaguzi huo umepangwa kufanyika jijini Dar es Salaam Julai 14 kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee.
Akikabidhi hundi jana, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro George Kavishe alisema pesa hizo ni sehemu ya udhamini wa TBL kwa Yanga.
WASIFU WA KOCHA MPYA YANGAKuzaliwa:
29-3-1973
Timu za Taifa:
Namibia,
Ethiopia,
Zimbabwe
Qatal
Klabu:
Al Gharafa (Qatal)
Rops(Finland),
B71 (Visiwa vya Island)
BV Cloppenburg ya Ujerumani.



Umati wa mashabiki wa Yanga waliofika Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl JK Nyerere kumlaki kocha wao mpya Tom Saintfiet






Kocha mpya wa Yanga kutoka Ubelgiji Tom Saintfiet akizungumza na mapaparazzi katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl JK Nyerere jijini Dar es salaam.

Tuesday, July 3, 2012

ANDRE INIESTA MCHEZAJI BORA EURO 2012 TORRES MFUNGAJI BORA


Andre Iniesta Mchezaji bora EURO 2012

Kiungo wa Uhispania, Andres Iniesta amenyakua tuzo ya uchezaji bora wa Euro 2012, huku mwenzake Fernando Torres akinyakua tuzo ya ufungaji bora iliyotolewa na Shirikisho la Soka la Ulaya ( UEFA).
Kiungo huyo wa Hispania mwenye miaka 28, aliyechangia ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Italia usiku wa Jumapili iliyopita, alitajwa kuwa mchezaji bora wa mechi hiyo ya fainali na Kamati ya Ufundi iliyoundwa na watu 11.
Nyota huyo wa Barcelona alishindwa kufunga bao na kutegeneza moja katika fainali hiyo, lakini amepata tuzo hiyo kutokana na mchango wake wa jumla ulivyowawezesha Hispania kutetea taji lao.
Iniesta alitegeneza bao muhimu lililofungwa na Jesus Navas likiwa ni bao pekee dhidi ya Croatia kwenye mchezo wa mwisho wa makundi, huku pasi yake nyingine kwa Cesc Fabregas katika mchezo wa fainali ikimsaidia Fabregas kupiga krosi iliyomkuta David Silva aliyefunga bao la kwanza.
Katika tuzo hiyo Iniesta alifanikiwa kuwapiku Andrea Pirlo wa Italia na nyota mwezake wa Barcelona, Xavi aliyetwaa tuzo hiyo mwaka 2008.
Iniesta amekuwa miongoni mwa wachezaji 10 wa Hispania wanaounda kikosi cha wachezaji 23 wa mashindano hayo.
Naye mshambuliaji wa Hispania, Fernando Torres amefanikiwa kutwaa Kiatu cha Dhahabu kufuatia kuibuka mfungaji bora na kumpiku mwenzake wa Ujerumani,Mario Gomez.
Mshambuliaji huyo mwenye miaka 28, alifunga bao moja katika ushindi wao wa mabao 4-0 dhidi ya Italia na kumfanya kuwa mchezaji pekee aliyefunga mabao katika mechi mbili tofauti za fainali.
Bao hilo lilimfanya kuwa sawa na Gomez aliyefunga mabao matatu na kutegeneza bao moja kwenye michuano hiyo iliyofikia tamati jana.
Hata hivyo, Uefa iliamua kumpa Torres zawadi hiyo kutokana na kutumia muda mchache uwanjani na kufunga mabao.
Nyota huyo wa Hispania alitumia dakika 189 kucheza mashindano hayo kulinganisha na Gomez aliyetumia dakika 280.
Wachezaji wengine wanne waliofunga mabao matatu ni Mario Balotelli (Italia), Cristiano Ronaldo (Ureno), chipukizi wa Russia, Alan Dzagoev na nyota wa Croatia, Mario Mandzukic.
Tuzo hiyo inamfanya Torres kumaliza vizuri zaidi msimu wa 2011/12 baada ya kutwaa Kombe la FA na Ligi ya Mabingwa akiwa na klabu yake ya Chelsea, lakini ameshindwa kuingia kwenye kikosi cha wachezaji 23 wa michuano ya Euro 2012 kilichotajwa jana na Uefa.
Hispania imekuwa timu ya kwanza ya taifa kutwaa mataji matatu mfululizo tangu, Euro 2008, Kombe la Dunia 2010 na Euro tena mwaka huu.
Andres Iniesta Andres Iniesta of Spain in action during the UEFA EURO 2012 group C match between Spain and Ireland at The Municipal Stadium on June 14, 2012 in Gdansk, Poland.
Andres Iniesta of Spain with the ball during the UEFA EURO 2012 final match between Spain and Italy at the Olympic Stadium on July 1, 2012 in Kiev, Ukraine.
A.Iniesta akitiririka




Huwa anakusanya Vijiji kama hivi


Fernando Torres mfungaji bora EURO 2012


Torres akitupia kambani mechi ya fainali dhidi ya Italia



Baba na wana

Famili inahusika katika ushindi bhanaa

Torres akiwa amebeba "ndoo" ya EURO 2012

Monday, July 2, 2012

SPAIN BINGWA EURO 2012 YAITUNGUA ITALIA 4-0


Uhispania waliandikisha historia kwa maarifa ambayo sio rahisi kuiga, kwa kuitungua Italia magoli 4-0 katika fainali ya Euro 2012 usiku wa Jumapili, mjini Kiev, Ukraine.

Licha ya mchezo mzuri wa Italia, vijana wa meneja wa Uhispania, Vicente del Bosque walithibitisha kwamba kimataifa wanaweza kujigamba wao ndio wenye mchezo bora zaidi duniani, kwa kuzingatia namna walivyoichezea timu ya Italia, na kuwalazimisha kusalimu amri.

David Silva aliifungia Uhispania bao la kwanza, na kabla nusu ya kwanza ya mchezo kumalizika, mchezaji mpya wa Barcelona, Jordi Alba aliandikisha bao la pili, baada ya kukimbia kwa kasi na kumalizia kwa ustadi kabisa.

Ingawa Italia walikuwa na upungufu wa mchezaji mmoja, baada ya kumpoteza mchezaji wa zamu wa tatu Thiago Motta baada ya kujeruhiwa, walicheza kwa bidii, lakini wataalamu wa kandanda kwa upande wa kupokezana mpira, Uhispania, waliwadunisha kabisa.

Fernando Torres aliingia kama mchezaji wa zamu, na akafanikiwa kuubadilisha mchezo, na akiandikisha bao la tatu la Uhispania, kabla ya mwenzake katika klabu ya Chelsea, Juan Mata, kuandikisha bao la nne na la mwisho la Italia, na ambalo bila shaka liliwavunja moyo kabisa mashabiki wote wa Italia.

Mchezo huo bila shaka umeyazima matamshi ya baadhi ya watu ambao awali walimlazimu kocha wa Uhispania Del Bosque na wachezaji wake kujitetea katika mkutano na waandishi wa habari, kabla mechi ya fainali kuanza, kwamba mchezo wao katika mashindano ya Euro 2012 umekosa msisimko.

Lakini usiku wa Jumapili mambo yalikuwa tofauti.

Maarifa yote yaliyowawezesha kuwa mabingwa wa Euro 2008 na vile vile Kombe la Dunia la mwaka 2010 nchini Afrika Kusini yalijitokeza.

Ilikuwa ni fainali ambayo ilimvunja moyo kabisa kocha wa Italia, Cesare Prandelli, lakini bila shaka haikuwa fedheha kushindwa na timu yenye maarifa ya hali ya juu kiasi hicho.

Italia itaweza kujivunia namna ilifika katika fainali, licha ya kushindwa kwa magoli mengi na timu ambayo ilikuwa ni wazi imo katika kiwango cha pekee.

Tulia ngedere weeee!! Kazi kati ya Pique na Balotelli


Kambaa..David Silva akianza kuwatia njaa Italia