Katika kupambana na tatizo la usafiri na pia kukabiliana na foleni zisizokwisha maeneo ya mijini hatimae kumeibuka usafiri wa aina yake ambao unajulikana kama "Burger" Aina hii ya usafiri haitofautiani sana na ile ya Mshikaki lakini hii inabeba watu wengi zaidi kwa kutumia chombo kilekile cha usafiri....haya sasa wakazi wa pale Dar es salaam usafiri huu utawafaa sanaa!!
Thursday, July 19, 2012
WATANZANIA WAENDELEA KUPOTEZA MAISHA KWA AJALI ZA MELI, HII TENA
WATU 60 wanahofiwa kufa maji na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya boti iliyokuwa imebeba abiria wanaokadiriwa kufikia 250 ikitokea Dar es Salaam kwenda Unguja, Zanzibar kuzama baharini.Hii ni ajali ya pili mbaya kutokea katika kipindi cha miezi 10 tangu ilipotokea nyingine ya Meli ya Mv Spice Islander ambayo inakadiriwa kuwa watu wapatao 200 walifariki dunia.Boti hiyo iliyoondoka jana Dar es Salaam majira ya saa 6:00 mchana na kutarajiwa kufika Bandari ya Malindi, Zanzibar saa 9:30 jioni, ilizama eneo la Pungume karibu kilomita 48 kutoka Bandari ya Zanzibar.
Inaelezwa kuwa, ilianza kuzama saa 7:30 mchana kutokana na kupigwa na mawimbi mazito ya bahari.
Hata hivyo, Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu wa Zanzibar, Hamad Masoud Hamad alithibitisha vifo vya watu 12 hadi vilivyoripotiwa ilipotimu saa 12:30 jioni jana wakati kazi ya uokoaji ikiwa inaendelea.
Baadaye saa 1:00 Ofisa Habari na Mawasiliano wa Wizara hiyo, Nafisa Madai aliwaambia waandishi wa habari kuwa idadi hiyo ilikuwa imeongezeka hadi kufikia 24 na majeruhi walikuwa 145.Madai alisema wakati boti hiyo inaondoka Dar es Salaam, ilikuwa na abiria 250 wakiwamo watoto 31 na wafanyakazi tisa.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Said Shaaban akizungumzia ajali ya boti hiyo ya Mv Skad, inayomilikiwa na Kampuni ya Meli Seagull alisema: “Vikosi vya uokoaji tayari vinaelekea katika eneo hilo ili kusaidia majeruhi na kufuatilia yaliyotokea.”
Maofisa kadhaa wa Serikali wakiongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi walifika Bandari ya Malindi na Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu Zanzibar, Hamad Masoud Hamad aliongoza msafara wa viongozi wengine kwenda katika eneo la tukio.
Awali, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi alisema kuwa, hadi alipopata taarifa, watu waliokuwa wamefariki dunia ni saba na 124 ndiyo waliokuwa wameokolewa. Alisema meli hiyo ina uwezo wa kubeba abiria 300 na waliosafiri siku ya tukio hawazidi 250.
Awali, taarifa zilieleza kuwa watu 10 waliokolewa na maiti zaidi ya 60 zimenasa katika boti hiyo na kuvifanya vikosi vya uokoaji vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Polisi na KMKM kupata wakati mgumu kwenye zoezi la uokoaji.Kazi ya kuokoa maisha ya watu waliozama kwenye boti hiyo na kuopoa maiti ilifanywa kwa kutumia boti nne zikiwamo za Serikali na zile zinazomilikiwa na Kampuni ya Azam Marine.
Hata hivyo, ilielezwa kwamba boti za polisi zilichelewa kwenda katika eneo la tukio kutokana na kukosekana kwa mafuta.
Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kufika bandarini, Balozi Seif aliwataka wananchi kutulia na kusubiri wakiwa nyumbani wakati Serikali ikifanya juhudi za uokoaji.
Shughuli nyingi za usafiri zilivurugika kutokana na tukio hilo na Meli ya Mv Sea Bus ililazimika kufuta safari zake kupisha kazi hiyo ya uokoaji.
Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), imesema inafuatilia tukio hilo kwa karibu ili kubaini chanzo.
Ofisa Uhusiano wa Sumatra, David Mziray alisema jana muda mfupi baada ya ajali hiyo kuwa, wanawasiliana na Kituo cha Utafutaji na Uokoaji Majini (MRCC), ili kupata taarifa kamili kabla ya kuujulisha umma.
Baadhi ya abiria wakisubiri uokozi
Waokoaji wakiwa katika boti ya Kilimanjaro wakiopoa maiti ya mzungu
Muokoaji akiwa na maiti
Meli ya MV Skagit ikiwa imezama katika bahari ya Chumbe
Abiria akichomolewa baharini na kikosi cha uokoaji
Jopo la madaktari likitoa huduma ya kwanza kwa majeruhi wa ajali ya meli katika bahari ya Chumbi
Umati wa wananchi wakiwa katika bandari ya Malindi wakifuatilia tukio la ajali ya meli ya Mv Seagull(Skagit)
"Najuuuuta kuifahamu Tanzania".....Inaelekea ndivyo mzungu huyu anavyofikiria
Boti ya KMKM ikiwa katika uokozi
Maiti ikitolewa baharini
Majeruhi akiwa amebebwa tayari kwa kupatiwa huduma ya kwanza
Wednesday, July 18, 2012
SHOW YA LEKA DUTIGITE UWANJA WA LAKE TANGANYIKA KIGOMA POTEZA MBAYAA

Umati wa watu waliohudhuria Show ya Leka Dutigike iliyofanyika katika uwanja wa Lake Tanganyika,Kigoma na kushirikisha wasanii wote ambao ni wazaliwa ama wenye asili ya Kigoma. Wakiongozwa na wabunge Vijana Mh Zitto Kabwe,Halima Mdee,Ester Bulaya na Joshua Nassari.
Wasanii wanaounda kundi hilo la wasanii wa Mkoa wa Kigoma ni Chege,Mwasiti,Banana Zorro,Peter Msechu,Diamond,Linex,Fid Q,Baba Levo,Makomando,Abdu Kiba,Ommy Dimpoz,Recho na wengineo wengi.

Wasanii wanaounda kundi la Kigoma All Stars

Mh Zitto Kabwe akizungumza na wananchi waliohudhuria uwanja wa Lake Tanganyika


Mh Halima Mdee (mbele), Ester Bulaya(katikati) na Joshua Nassari wakiserebuka


Wabunge wakiserebuka
Fid Q akifanya makamuzi

Mwasiti nae akitoa burudani
HAPPY BIRTHDAY NELSON MANDELA "MADIBA"

Nelson Rolihlahla Mandela ametimiza miaka 94. Alizaliwa 18 Julai 1918. Aliwahi kuwa Rais wa Afrika ya Kusini na alishika wadhifa huo tangu mwaka 1994 mpaka 1999. Nakutakia maisha mema mzee Madiba Afrika bado inahitaji busara zako!
Mzee wa Afrika Nelson Mandela akiwa amebeba kombe la dunia pale Afrika ya Kusini ilipokuwa mwenyeji wa kombe hilo mwaka 2010 na Uhispania kuibuka bingwa wa Dunia katika ardhi ya Afrika.
Nelson Mandela enzi za kupigania uhuru
Tuesday, July 17, 2012
MAAJABU YA MSIKITI SHEIKH ZAYED NI MSIKITI MZURI KULIKO YOTE DUNIANI

Msikiti wa Sheikh Zayed Uliopo Falme za Kiarabu (U.A.E) ni msikiti mkubwa kuliko yote katika falme za kiarabu na ni msikiti wa Nane kwa ukubwa duniani. Na inasadikika kuwa ndio msikiti mzuri kuliko yote Duniani, msikiti huu ulijengwa katika kumbukumbu za kumuenzi marehemu Sheikh Zayed Bin Sultan Al Nahyan ambaye alikuwa sheikh maarufu katika falme za kiarabu na ndie mwaanzilishi wa Falme za kiarabu
Ifuatayo ni historia fupi ya Msikiti wa Sheikh Zayed,
Only freshly fallen snow can reflect the light with more intensity. Like a mirage the building soars above the shimmering Abu Dhabi heat.
The 82 domes and 1,096 rooms are not an optical illusion, but belong to a mesmerizing mosque of superlatives on the edge of this city in the Gulf, a house of worship that seems to beckon visitors from afar.
To the faithful, this glorious building is known as the Sheikh Zayed Mosque, although its full title is Sheikh Zayed bin Sultan Al Nahyan, since it was named after the founder of the United Arab Emirates. He was the man who initiated this masterpiece in marble, the very whiteness of which is a symbol of peace to Muslims.
The blindingly white façade reminds onlookers of the Taj Mahal in India and the ethereal magnificence of the mosque is emphasized by the use of translucent stone from the finest quarries in Italy, Greece, India and China.
A total of 115,119 square metres of the stone was used for the four minarets and the outer facade alone. The Emirates' founding father ordered the same material for his burial place close by, a modest mausoleum where he was buried aged 86 on November 2, 2004, three years before the vast house of prayer was officially inaugurated.
When he laid the foundation stone in 1996, Sheikh Zayed marked the start of the construction of the largest mosque in the UAE and the third most sizeable in the Islamic world. The muezzin summons worshippers to a complex spread over 22,412 square metres. It can accommodate a total of 30,000 people, 23,000 of them within the cavernous main prayer hall which is also made of marble.
Only the best is good enough for a mosque of such enormous proportions. The building contains the world's largest hand-woven Persian carpet. A small army of 1,200 weavers toiled for 18 months to complete this floor covering, using up 38 tonnes of wool in the process. They used 2.2 billion knots in its creation and the carpet covers an area of 5,625 square metres.


Tuesday, July 10, 2012
MPAMBANO WA SOKA WABUNGE WA SIMBA NA YANGA KATIKA PICHA
Timu za wabunge wa Simba na Yanga wakiimba wimbo wa Taifa kabla ya mpambano
Waamuzi wa mpambano huo wakipiga picha ya pamoja na manahodha wa timu zote mbili
Wabunge wa Simba katika Dua kabla ya mtanange kuanza
Wabunge wa Yanga nao wakipiga dua kabla ya mtanange kurindima
Mashabiki wakiwahi mpambano
Mtanange umeanza
Mwamuzi wa mtanange huo Athuman Kazi akifuatilia kwa karibu kuhakikisha haki inatendeka
Mh Zitto Kabwe wa Simba akitoa pasi murua kama Iniesta vile!
Mbunge wa Simba akitiririka na kabumbu
Katibu uenezi wa CCM Nape Nnauye akifuatilia mpambano wa Wabunge wa Simba na wale wa Yanga katika dimba kuu la Taifa jijini Dar es salaam
Benchi la ufundi la Wabunge wa Simba wakifuatilia mpambano
Benchi la ufundi la Wabunge wa Yanga wakiongozwa na kocha mkuu mpya wa Yanga
Mbunge wa Yanga akiwa hoi bin taaban
Mbunge wa Yanga akijaribu kuihadaa ngome ya wabunge wa Simba
Hali tete mlinda mlango wa wabunge wa Yanga baada ya kichapo kwa njia ya matuta 3-2
Wera weraaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!! wabunge wa Simba hatimae waliwachapa wa Yanga katika matuta baada ya dakika 90 kumalizika kwa sare ya 0-0
Nani kama Simbaaaa woyooooo woyooooooooo
Hakunagaa zaidi ya Simba hakunagaa, hakunaaa hakunaaaa hakunaaaaaaaaaa!!!
Weraaaaa tupishe tupiteeee, tupisheeeee tupishe tupiteeeeeeee..Wabunge wa Simba wakiongozwa na Mh Zitto Kabwe na William Ngeleja kuserebuka baada ya kuwaangushia kisago wenzao wa Yanga kwa mikwaju ya penati 3-2
Mpambano Wabunge SIMBA Vs YANGA
Katika mtanange huo baada ya dakika 90 na kipyenga cha mwamuzi Athumani kazi kupulizwa matokeo yalikuwa ni 0-0. Mpambano huo wa kufurahisha na kusisimua uliopigwa katika dimba kuu la Taifa jijini Dar es salaam ikiwa ni katika mchezo wa hisani kukusanya pesa kuchangia ujenzi wa mabweni kwa shule za sekondari nchini!
shukrani za pekee kwa waandaaji wa tamasha hilo ambalo pia liliwakutanisha wasanii wa Bongo flava na Bongo Movie hali kadhalika mpambano wa Masumbwi kati ya wasanii maarufu nchini na wenye kutengeneza vichwa vya habari katika redio na magazeti mbalimbali hapa nchini, ni Wema Sepetu na Jaquiline Wolper ambapo katika mpambano mpambano huo uliodumu kwa raundi mbili matokeo yalikuwa ni droo hakukuwa na mshindi.
Subscribe to:
Posts (Atom)
