Friday, July 20, 2012

DENNIS RODMAN AKUTANA NA BABA YAKE PHILANDER RODMAN BAADA YA NYUNDO 42


Dennis Rodman

Mchezaji wa zamani na maarufu wa muda wote wa mchezo wa Mpira wa Kikapu(Basketball) Dennis Rodman hatimae amekutana na baba yake mzazi aitwae Philander Rodman baada ya baba huyo kumuacha mama yake Dennis miaka 48 iliyopita.

Dennis Rodman aliewahi kuzichezea timu za Pistons,Spurs,Bulls,Lakers na Mavericks hakuonana na baba yake kwa miaka 42 na hivi karibuni kukubali kukutana na baba yake huko Manila nchini Phillipines wakati wa mechi za Basketball.

Philander Rodman Jr ni baba wa watoto 29 kwa mama 16 alisema alipatwa na mshangao na furaha pale mwanae alipokubali kukutana nae huko Manila jumatano ya tarehe 19 july 2012, baada ya jaribio lake kushindikana mwaka 2006 siku ya michezo kama hiyo huko Manila,Phillipines.

Dennis Rodman akielezea kwa hisia na uchungu kuwa alikuwa na wakati mgumu katika maisha yake kwa kulelewa na mama tu na kukosa mfano wa kufuata kutoka kwa mzazi wa kiume(baba) ndani ya nyumba, 

Philander Rodman Jr (Baba mzazi wa Dennis Rodman)

Yafuatayo ni maneno ya Rodman akielezea hisia zake;
 "I never really knew my father, Philander Rodman. He was in the Air Force in New Jersey, where I was born, and when I was three we packed up and came back to Dallas where my mother is from. We did this when my father stopped coming home.
My father isn't part of my life. I haven't seen him in more than thirty years, so what is there to miss? I just look at it like this: Some man brought me into this world. That doesn't mean I have a father; I don't. I could say, 'This is my father. This is my dad,' but that doesn't sound right to me. I grew up with my mother and two younger sisters, Debra and Kim. There wasn't a male role model in my life until I got to college and started getting my [act] together."

Baba nae alikuwa na haya ya kusema;
''I've been trying to meet him for years. And then last night, boom, I met him. I was really, really happy and very surprised,'' he told The Associated Press.
''I really, really felt good,'' he said. ''It's the beginning of something new.''


Baba na Mwana walipokutana baada ya miaka a.k.a Nyundo 42

Mzee ulinitosa au?.........

Rodman akisaini vitabu vya kumbukumbu kwa mashabiki wake huko Manila nchini Phillipines ambako ndiko alipokutana na baba yake 19 july.


Rodman enzi zake akikipiga na Pistons


Rodman enzi zake akikipiga na Chicago Bulls



Hapa akikipiga na Spurs


Hapa akikipiga L.A Lakers



Enzi akikipiga na Dallas Mavericks


Rodman katika swaga na mbabe wa mieleka maarufu Hulk Hogan..na alama za Freemasons


Haya ..Hii alama inasemekana ni ya Freemasons!

Thursday, July 19, 2012

USAFIRI MPYA KUKABILI FOLENI MIJINI

Katika kupambana na tatizo la usafiri na pia kukabiliana na foleni zisizokwisha maeneo ya mijini hatimae kumeibuka usafiri wa aina yake ambao unajulikana kama "Burger" Aina hii ya usafiri haitofautiani sana na ile ya Mshikaki lakini hii inabeba watu wengi zaidi kwa kutumia chombo kilekile cha usafiri....haya sasa wakazi wa pale Dar es salaam usafiri huu utawafaa sanaa!!

WATANZANIA WAENDELEA KUPOTEZA MAISHA KWA AJALI ZA MELI, HII TENA


WATU 60 wanahofiwa kufa maji na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya boti iliyokuwa imebeba abiria wanaokadiriwa kufikia 250 ikitokea Dar es Salaam kwenda Unguja, Zanzibar kuzama baharini.Hii ni ajali ya pili mbaya kutokea katika kipindi cha miezi 10 tangu ilipotokea nyingine ya Meli ya Mv Spice Islander ambayo inakadiriwa kuwa watu wapatao 200 walifariki dunia.Boti hiyo iliyoondoka jana Dar es Salaam majira ya saa 6:00 mchana na kutarajiwa kufika Bandari ya Malindi, Zanzibar saa 9:30 jioni, ilizama eneo la Pungume karibu kilomita 48 kutoka Bandari ya Zanzibar.
Inaelezwa kuwa, ilianza kuzama saa 7:30 mchana kutokana na kupigwa na mawimbi mazito ya bahari.

Hata hivyo, Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu wa Zanzibar, Hamad Masoud Hamad alithibitisha vifo vya watu 12 hadi vilivyoripotiwa ilipotimu saa 12:30 jioni jana wakati kazi ya uokoaji ikiwa inaendelea.

Baadaye saa 1:00 Ofisa Habari na Mawasiliano wa Wizara hiyo, Nafisa Madai aliwaambia waandishi wa habari kuwa idadi hiyo ilikuwa imeongezeka hadi kufikia 24 na majeruhi walikuwa 145.Madai alisema wakati boti hiyo inaondoka Dar es Salaam, ilikuwa na abiria 250 wakiwamo watoto 31 na wafanyakazi tisa.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Said Shaaban akizungumzia ajali ya boti hiyo ya Mv Skad, inayomilikiwa na Kampuni ya Meli Seagull alisema: “Vikosi vya uokoaji tayari vinaelekea katika eneo hilo ili kusaidia majeruhi na kufuatilia yaliyotokea.”

Maofisa kadhaa wa Serikali wakiongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi walifika Bandari ya Malindi na Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu Zanzibar, Hamad Masoud Hamad aliongoza msafara wa viongozi wengine kwenda katika eneo la tukio.

Awali, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi alisema kuwa, hadi alipopata taarifa, watu waliokuwa wamefariki dunia ni saba na 124 ndiyo waliokuwa wameokolewa. Alisema meli hiyo ina uwezo wa kubeba abiria 300 na waliosafiri siku ya tukio hawazidi 250.

Awali, taarifa zilieleza kuwa watu 10 waliokolewa na maiti zaidi ya 60 zimenasa katika boti hiyo na kuvifanya vikosi vya uokoaji vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Polisi na KMKM kupata wakati mgumu kwenye zoezi la uokoaji.Kazi ya kuokoa maisha ya watu waliozama kwenye boti hiyo na kuopoa maiti ilifanywa kwa kutumia boti nne zikiwamo za Serikali na zile zinazomilikiwa na Kampuni ya Azam Marine.

Hata hivyo, ilielezwa kwamba boti za polisi zilichelewa kwenda katika eneo la tukio kutokana na kukosekana kwa mafuta.

Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kufika bandarini, Balozi Seif aliwataka wananchi kutulia na kusubiri wakiwa nyumbani wakati Serikali ikifanya juhudi za uokoaji.

Shughuli nyingi za usafiri zilivurugika kutokana na tukio hilo na Meli ya Mv Sea Bus ililazimika kufuta safari zake kupisha kazi hiyo ya uokoaji.
Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), imesema inafuatilia tukio hilo kwa karibu ili kubaini chanzo.
Ofisa Uhusiano wa Sumatra, David Mziray alisema jana muda mfupi baada ya ajali hiyo kuwa, wanawasiliana na Kituo cha Utafutaji na Uokoaji Majini (MRCC), ili kupata taarifa kamili kabla ya kuujulisha umma.


Baadhi ya abiria wakisubiri uokozi


Waokoaji wakiwa katika boti ya Kilimanjaro wakiopoa maiti ya mzungu


Muokoaji akiwa na maiti



Meli ya MV Skagit ikiwa imezama katika bahari ya Chumbe


Abiria akichomolewa baharini na kikosi cha uokoaji




Jopo la madaktari likitoa huduma ya kwanza kwa majeruhi wa ajali ya meli katika bahari ya Chumbi


Umati wa wananchi wakiwa katika bandari ya Malindi wakifuatilia tukio la ajali ya meli ya Mv Seagull(Skagit)







"Najuuuuta kuifahamu Tanzania".....Inaelekea ndivyo mzungu huyu anavyofikiria


Boti ya KMKM ikiwa katika uokozi


Maiti ikitolewa baharini


Majeruhi akiwa amebebwa tayari kwa kupatiwa huduma ya kwanza



Wednesday, July 18, 2012

SHOW YA LEKA DUTIGITE UWANJA WA LAKE TANGANYIKA KIGOMA POTEZA MBAYAA


Umati wa watu waliohudhuria Show ya Leka Dutigike iliyofanyika katika uwanja wa Lake Tanganyika,Kigoma na kushirikisha wasanii wote ambao ni wazaliwa ama wenye asili ya Kigoma. Wakiongozwa na wabunge Vijana Mh Zitto Kabwe,Halima Mdee,Ester Bulaya na Joshua Nassari.

Wasanii wanaounda kundi hilo la wasanii wa Mkoa wa Kigoma ni Chege,Mwasiti,Banana Zorro,Peter Msechu,Diamond,Linex,Fid Q,Baba Levo,Makomando,Abdu Kiba,Ommy Dimpoz,Recho na wengineo wengi.

Wasanii wanaounda kundi la Kigoma All Stars


Mh Zitto Kabwe akizungumza na wananchi waliohudhuria uwanja wa Lake Tanganyika




Mh Halima Mdee (mbele), Ester Bulaya(katikati) na Joshua Nassari wakiserebuka



Wabunge wakiserebuka


Fid Q akifanya makamuzi


Mwasiti nae akitoa burudani

HAPPY BIRTHDAY NELSON MANDELA "MADIBA"


Nelson Rolihlahla Mandela ametimiza miaka 94. Alizaliwa 18 Julai 1918. Aliwahi kuwa Rais wa Afrika ya Kusini na alishika wadhifa huo tangu mwaka 1994 mpaka 1999. Nakutakia maisha mema mzee Madiba Afrika bado inahitaji busara zako!

Mzee wa Afrika Nelson Mandela akiwa amebeba kombe la dunia pale Afrika ya Kusini ilipokuwa mwenyeji wa kombe hilo mwaka 2010 na Uhispania kuibuka bingwa wa Dunia katika ardhi ya Afrika.


Nelson Mandela enzi za kupigania uhuru

Tuesday, July 17, 2012

MAAJABU YA MSIKITI SHEIKH ZAYED NI MSIKITI MZURI KULIKO YOTE DUNIANI


Msikiti wa Sheikh Zayed Uliopo Falme za Kiarabu (U.A.E) ni msikiti mkubwa kuliko yote katika falme za kiarabu na ni msikiti wa Nane kwa ukubwa duniani. Na inasadikika kuwa ndio msikiti mzuri kuliko yote Duniani, msikiti huu ulijengwa katika kumbukumbu za kumuenzi marehemu Sheikh Zayed Bin Sultan Al Nahyan ambaye alikuwa sheikh maarufu katika falme za kiarabu na ndie mwaanzilishi wa Falme za kiarabu

Ifuatayo ni historia fupi ya Msikiti wa Sheikh Zayed,

Only freshly fallen snow can reflect the light with more intensity. Like a mirage the building soars above the shimmering Abu Dhabi heat.

The 82 domes and 1,096 rooms are not an optical illusion, but belong to a mesmerizing mosque of superlatives on the edge of this city in the Gulf, a house of worship that seems to beckon visitors from afar.

To the faithful, this glorious building is known as the Sheikh Zayed Mosque, although its full title is Sheikh Zayed bin Sultan Al Nahyan, since it was named after the founder of the United Arab Emirates. He was the man who initiated this masterpiece in marble, the very whiteness of which is a symbol of peace to Muslims.

The blindingly white façade reminds onlookers of the Taj Mahal in India and the ethereal magnificence of the mosque is emphasized by the use of translucent stone from the finest quarries in Italy, Greece, India and China.

A total of 115,119 square metres of the stone was used for the four minarets and the outer facade alone. The Emirates' founding father ordered the same material for his burial place close by, a modest mausoleum where he was buried aged 86 on November 2, 2004, three years before the vast house of prayer was officially inaugurated.

When he laid the foundation stone in 1996, Sheikh Zayed marked the start of the construction of the largest mosque in the UAE and the third most sizeable in the Islamic world. The muezzin summons worshippers to a complex spread over 22,412 square metres. It can accommodate a total of 30,000 people, 23,000 of them within the cavernous main prayer hall which is also made of marble.

Only the best is good enough for a mosque of such enormous proportions. The building contains the world's largest hand-woven Persian carpet. A small army of 1,200 weavers toiled for 18 months to complete this floor covering, using up 38 tonnes of wool in the process. They used 2.2 billion knots in its creation and the carpet covers an area of 5,625 square metres.