Wednesday, August 22, 2012

ADEBAYOR ATUA TOTTENHAM

Emmanuel Adebayor
Emmanuel Adebayor

Emmanuel Adebayor amekamilisha mipango ya kuhamia Tottenham Hotspur kutoka Manchester City kwa kitita cha pauni milioni 5.
Mshambulizi huyo kutoka Togo alionyesha umahiri wake msimu uliopita, akiichezea Tottenham kwa mkopo, kwa kufunga jumla ya magoli 17 katika ligi kuu ya Premier.

Adebayor atakuwa ni kati ya wachezaji wenye mishahara mikubwa katika klabu hiyo ya uwanja wa White Hart Lane.

Adebayor, mwenye umri wa miaka 28, alikuwa akilipwa na Manchester City pauni milioni 175,000 kwa wiki.

Mshambulizi huyo, ambaye zamani alikuwa akiichezea Arsenal, alifichua habari za kujiunga na Tottenham kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter: “Tottenham niko njiani! Natamani magoli. Kaeni chonjo.”

Mkataba wa Adebayor ulikuwa uendelee kwa miaka miwili zaidi na klabu ya Man City, na kwa kipindi kirefu katika misimu miwili iliyopita alikuwa akiichezea Real Madrid ya Uhispania, na kisha Tottenham.

“Ninafurahi kujiunga kabisa na Spurs baada ya klabu kuelewana na Manchester City,” aliongezea Adebayor.

“Pengine ilichukua muda mrefu kinyume na ilivyotazamiwa, lakini nimefurahi sana kurudi Tottenham Hotspur. Nilifurahi sana nilipokuwa hapa msimu uliopita, na ni matumaini yangu tutaweza kwa pamoja kufanikiwa hata zaidi.”

Inafahamika kwamba Spurs walikataa kubadilisha mipango yao ya mishahara ili kufanikisha mipango ya kumpata Adebayor.

Lakini kutokana na Adebayor kukataa kupunguziwa mshahara, mabingwa wa ligi kuu Manchester City walikubali kuongezea zaidi tofauti ya senti atakazopokea Adebayor katika klabu ya Tottenham, na kiwango alichozoea Man City cha pauni 175,000.

Tottenham watamlipa pauni 80,000 kwa wiki, na Man City ilibidi kukubali kuongezea tofauti ya elfu 95,000 kwa wiki, ili kuyafanikisha makubaliano kati ya vilabu hivyo viwili.

Makubaliano hayo yanahitimisha ubishi ulioendelea kwa muda mrefu, kuhusu ikiwa Adebayor alistahili kulipwa bakshishi na marupurupu mengineyo iwapo angelisisitiza kuondoka Man City pasipo makubaliano kamili kati yake na klabu hiyo.
Mavituz ya Adebayor

Tuesday, August 21, 2012

EVERTON YAIDUNGA MAN UNITED KIMOKO


Fellaini akipiga kichwa kilichozama moja kwa moja kambani kuandika goli la pekee la Everton

Kimuhemuhe cha ligi kuu ya Uingereza kimendelea jana jumatatu huku mamilioni ya mashabiki wa soka duniani wakishuhudia Timu ya Everton ikichabanga Manchester united kwa bakora moja kwa yai katika dimba la Goodison Park, mchezo huo ulishuhudiwa na watazamaji wapatao 38,415.

Katika mtanange huo goli la pekee la Everton lilitupiwa kambani na Fellaini katika dakika ya 56 na kuwaacha hoi Man United.


Cleverley wa Man U akioneshana umwamba na Pienaar wa Everton

Fellaini akishangilia goli

Hapa kazi tuu..Welbeck akiwa chini ya ulinzi mkali


Van Persie akitia mchomo katika mpambano huo

Ngoma ngumu..Rooney na Kagawa wakiwa wameloa baada ya kuchapwa goli la kwanza
 


Daah hivi kweli tumechapwa?

UNAONA UTAAAAAAAMU MAMBO YA BAIKOKO

WAZIRI MKUU ETHIOPIA AAGA DUNIA

Aliekuwa waziri mkuu wa Ethiopia marehemu Meles Zenawi

Waziri mkuu wa Ethiopia Meles Zenawi amefariki dunia akiwa na umri wa miaka hamsini na saba na ni mmoja wa viongozi wenye ushawishi mkubwa na ambaye utawala wake ulikumbwa na utata barani afrika.
Hali yake ya afya imekuwa ikiangaziwa kwa majuma kadhaa sasa ingawaje hakukuwa na thibitisho kuhusu alichokuwa akiugua hasa.
Taarifa ya baraza la mawaziri imesema kuwa Zenawi alikuwa akipokea matibabu ng'ambo na afya yake ilikuwa ikiimarika lakini akazidiwa siku ya Jumapili alipolazimika kurejeshwa hospitali, ''Ingawaje madaktari wake walifanya kila wawezalo, alifariki jana mwendo wa 23:40,'' taarifa hiyo imesema.
Bwana Zenawi alikuwa kiongozi wa Ethiopia wakati taifa hilo lilipoingia vitani na nchi jirani ya Eritrea mwaka 1998.
Meles Zenawi aliingia mamlakani mwaka 1991 baada ya mapinduzi lakini akapokea sifa kutoka kwa mataifa ya magharibi.
Waziri mkuu wa Kenya raila Odinga ameiambia BBC kuwa ana hofu kuhusu hali nchini Ethiopia kufuatia kifo cha Meles Zenawi.
Alisema kuwa hali nchini humo sio nzuri huku vita vya kikabila vikiendelea kuwa tishio.
Bwana Odinga alimtaja Zenawi kama kiongozi mashuhuri na mwenye elimu bora, aliyejitolea kuunganisha bara la afrika.
Naibu waziri mkuu Hailemariam Desalegn anatarajiwa kuchukua wadhifa huo.

Friday, August 17, 2012

RATIBA KAMILI LIGI KUU UINGEREZA (BARCLAYS PREMIER LEAGUE)

RATIBA YA Barclays Premier League

Mechi zote kwa saa za TANZANIA(EAST AFRICAN TIME)
Saturday 18 August 2012                                                                             
Arsenal v Sunderland Emirates Stadium 17:00
Fulham v Norwich Craven Cottage 17:00
QPR v Swansea Loftus Road Stadium 17:00
Reading v Stoke Madejski Stadium 17:00
West Brom v Liverpool The Hawthorns 17:00
West Ham v Aston Villa Upton Park 17:00
Newcastle v Tottenham Sports Direct Arena 19:30
Sunday 19 August 2012
Wigan v Chelsea The DW Stadium 15:30
Man City v Southampton Etihad Stadium 18:00
Monday 20 August 2012
Everton v Man Utd Goodison Park 22:00
Wednesday 22 August 2012
Chelsea v Reading Stamford Bridge 21:45
Saturday 25 August 2012
Swansea v West Ham Liberty Stadium 14:45
Southampton v Wigan St. Mary's Stadium 17:00
Sunderland v Reading Stadium of Light 17:00
Tottenham v West Brom White Hart Lane 17:00
Norwich v QPR Carrow Road 17:00
Aston Villa v Everton Villa Park 17:00
Man Utd v Fulham Old Trafford 17:00
Chelsea v Newcastle Stamford Bridge 20:30
Sunday 26 August 2012
Stoke v Arsenal Britannia Stadium 15:30
Liverpool v Man City Anfield 18:00

HAYA NDIO "MAJEMBE" YALIYOWAHI KUUZWA NA WENGER


Baada ya Arsenal Wenger kumuuza Mshambuliaji wetu hatari Robin Van Persie kwa mahasimu wetu Manchester United mimi ninajifariji na maneno haya ya Kocha wetu wa kuheshimika zaidi kwetu Arsenal Wenger...lakini roho inaumaaaaa!!

Nafarijika zaidi na maneno ya Arsene Wenger ninapowakumbuka wachezaji mashuhuri na wakaliii aliowahi kuwauza na kamwe yeye hajawahi kununua Nyota katika soka..wapige chapo hapo chini.....

Thienry Henry









Patrick Vieira


Ashley Cole



Samir Nasri

Cesc Fabregas - Arsenal v Stoke City - Premier League
Cesc Fabregas

Thursday, August 16, 2012

KOFFI OLOMIDE AMPA KISAGO PRODUCER, AFIKISHWA KWA "PILATO"

Koffi Olomide performing in 2005
Koffi Olomide akipiga show kabla ya kudakwa na wama usalama
 
Mwanamuziki mashuhuri wa jamuhuri ya kidemokrasia ya kongo(DRC) Koffi Charles Antony Olomide amewekwa chini ya ulinzi kwa kosa la kumshambulia mtayarishaji wake wa muziki(Producer).
 
Koffi alitiwa mikononi mwa polisi siku ya jumatano baada ya "Fracas" katika Hotel moja ilioyopo katika mji mkuu wa DRC Kinshansa, Umati wa watu ulifurika katika chumba mahakama kumuona mwanamuziki huyo akipandishwa kizimbani kujibu tuhuma za kumshambulia Producer wake. Katika kesi hiyo Koffi Olomide anatetewa na mawakili 10.
 
Habari zaidi zinasema Koffi Olomide anamdai Producer huyo kiasi cha Euro 3,000 sawa na dola za kimarekani  3,680 na ni sawa na Paundi za Uingereza 2,345 na ni zaidi ya Shilingi za Kitanzania 5,800,000.
 
Mwanamuziki huyo anaepiga muziki wa dansi kwa staili ya SOUKOUSS neno linalotokana na neno la kifaransa "Secouer" Likimaanisha "Tingisha", Kesi yake iliahirishwa na kama akipatikana na hatia anaweza kuhukumiwa kifungo cha miezi sita jela