Monday, September 24, 2012

MAN U YAITULIZA LIVERPOOL ARSENAL MAN CITY HAKUNA MBABE


Manchester United imeicharaza Liverpool kwa bakora 2-1 katika dimba la Anfield katika mpambano ulioshuhudiwa na mashabiki wapatao 44,263. Liverpool ndio walikuwa wa kwanza kuzifumania nyavu za Man Unietd kupitia kwa Steven Gerrald katika dakika ya 45. Mpaka mapumziko bao lilikuwa 1-0 wenyeji akienda kupumzika kifua mbele.

Kipindi cha pili nibeebe nibeebe nibebeee ilianza na katika dakika ya 50 R Da Silva aliipatia Man U bao la kusawazisha kabla ya Robin Van Persie kutupia kambani goli la pili na la ushindi katika dakika ya 80 kwa nduki kali ya mkwaju wa penati.

Friday, September 21, 2012

ABABMBWA AKIJARIBU KUIBA GITAA


Njemba amekuwa mdogo kama "piriton" baada ya kudwakwa akijaribu kuiba kifaa cha muziki ambapo mbinu yake ilikuwa kali sana lakini anashangaa watu wamemshtukiaje?

TBL YAZIKABIDHI SIMBA NA YANGA NDINGA ZAO


Basi walilokabidhiwa mabingwa wa ligi kuu ya Tanzania bara Simba Sports Club.


Basi walilokabidhiwa Dar Young Africans (YANGA)

Thursday, September 20, 2012

CHELSEA YAGAWANA POINTI NA JUVENTUS, MAN U YAIBURUZA GALATASARAY

Oscar akishangilia goli pamoja na wenzake Ramires na David Luiz
 
Mabingwa watetezi wa klabu bingwa barani Ulaya, Chelsea ya Uingereza, wakiwa katika dimba la nyumbani la Stamford Bridge, walishindwa kuifunga Juventus ya Italia katika pambano la Jumatano usiku.

Nyota wa Chelsea alikuwa ni mchezaji Oscar kutoka Brazil, ambaye alifanikiwa kutumbukiza magoli mawili kambani katika kipindi cha kwanza; dakika ya 31 na 33.
Bao la pili liliingia kupitia mkwaju wa mbali, na ambalo lilimuacha kipa wa Juventus, Gianluigi Buffon akiwa amezubaa.
Oscar alisajiliwa na Chelsea hivi majuzi.


Hata hivyo Juventus, mabingwa wa Italia, na ambao hawakushindwa katika mechi 42 za Serie A huko nyumbani, walijikakamua na hatimaye kusawazisha na kujinyakulia pointi moja.

Arturo Vidal aliwafungia bao kabla ya kipindi cha kwanza kumalizika, na baadaye mchezaji wa zamu, Fabio Quagliarella, zikiwa zimesalia dakika tisa mechi kumalizika, alithibitisha Juventus ilikuwa na nia ya kuondoka na angalau pointi moja.


Oscar akifunga goli katika mechi dhidi ya Juventus


Oscar akimdhibiti mkongwe Andre Pirlo


Oscar akitupia Kamba ya pili


Wachezaji wa Juventus wakishangilia goli la kusawazisha


Torres akiwa chini ya ulinzi mkali


Kazi kweli kweli ..Lampard amekamwata

Kati ya mechi nane za Jumatano, Manchester United pia ilikuwa uwanjani kupambana na Galatasaray, na vijana wa Sir Alex Ferguson wakichezea nyumbani, mechi ya kundi G, walipata ushindi wa bao 1-0.
Michael Carrick aliandikisha bao hilo mapema, dakika ya 7.

Klabu hiyo ya Uturuki itadhaniwa na wengi kwamba ilinyimwa nafasi ya kusawazisha, kwa mwamuzi kuwapa penalti, baada ya Nemanja Vidic kumchezea vibaya Umut Bulup.



Picha zikionesha jinsi Carrick alivyomtesa mlinda mlango wa Galatasaray na kutia mpira kambani.

Wachezaji wa Man U wakimpongeza Carrick

Wednesday, September 19, 2012

NGORONGORO CRATER "AFRICA'S GARDEN OF EDEN"

QUICK FACTS ABOUT NGORONGORO CRATER
  • Largest unbroken caldera in the world
  • Also referred to as "Africa's Garden of Eden"
  • Crater is 12 miles (19 km) across and covers 102 square miles (264 sq km)
  • Rises over 2,000 feet above the caldera floor
  • Home to over 30,000 animals including the rare black rhino


  • Ngorongoro Crater is the world's largest unbroken caldera. Often referred to as "Africa's Garden of Eden," the crater is home to over 30,000 animals including elephants, lions, cheetahs, wildebeests, buffaloes, and the rare black rhinos. View Wildlife of Ngorongoro Crater to learn more about the wildlife and View Birds of Ngorongoro Crater to discover some of the many species that are found in the area.
    Ngorongoro Crater was created from a volcano that exploded creating the caldera wilderness haven. The crater is 12 miles (19 km) across and consumes 102 square miles (264 sq km) of wilderness. The rim of the crater rises just over 2,000 feet (610 m) above the caldera floor reaching an elevation of 7,500 feet (2,286 m).






    OMMY DIMPLES- Baadae


    ARSENAL YAIADHIBU MONTPELLIER

    Arsenal imeanza vyema michuano ya ligi ya mabingwa hatua ya makundi baada ya kuichabanga Montpellier kwa magoli 2-1 nyumbani kwao katika dimba la La Mosson.

    Wenyeji ndio walikuwa wa kwanza kuzifumania nyavu za wageni kwa bao maridadi la mkwaju wa penati iliyopigwa na Belhanda katika dakika ya 8 ya mchezo.
    Watoto wa London,Arsenal "The Gunners" waliibuka kama mbogo aliejeruhiwa na kusawazisha goli katika dakika ya 15 likitupiwa kambani na Lucas Podolski.

    Mtanange uliendelea huku kila timu ikisaka bao la ushindi na kuthibitisha hilo karata zilichezeka vizuri upande wa Arsenal na katika dakika ya 17 Gervinho aliwainua vitini mashabiki wa Arsenal kwa kutupia kambani goli la pili.

    Mpaka mapumziko ngoma ilinoga kwa Arsenal kuwa mbele kwa kamba 2 kwa 1 ya Montpellier.Kipindi cha pili hakikuwa na mabadiliko ya matokeo ya mchezo huo uliohudhuriwa na mashabiki wapatao 30,000 katika dimba hilo la Montpellier, na mpaka kipyenga cha mwamuzi kinaenda hewani matokeo yalikuwa Montpellier 1-2 Arsenal.

    Podolski akitupia kambani goli la kusawazisha



    Podolski akishangilia goli la kwanza

    Hapa huendi kokote we mirasta!!!

    Gibbs akijaribu kupiga majaro langoni mwa Montpellier


    Gervinho akitupia kambani goli la pili

    Gervinho - Montpellier Herault SC v Arsenal FC - UEFA Champions League
    Gervinho akishangilia goli

    Montpellier 1-2 Arsenal