Tuesday, November 20, 2012

WENGER: THEO WALCOTT HANG'OKI ARSENAL

Theo Walcott
 
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger , amekariri kuwa klabu hiyo haina nia yoyote ya kumuuza mchezaji wake Theo Walcott, msimu wa usajili Januari mwakani.

Kufuatia uamuzi huo, Arsenal, sasa huenda ikampoteza Walcott, mwenye umri wa miaka 23, ila kupokea chochote, kwa kuwa kandarasi ya mchezaji huyo inakamilika mwisho wa msimu huu.

Ikiwa Walcott na wasimamizi wa klabu hiyo hawataafikiana lolote, kabla ya wakati huo, Walcott atakuwa huru kuanzisha mazungumzo na klabu yoyote na kama vipi akasepa Emirates.

Mazungumzo kuhusu kandarasi mpya yamekwama, na alipoulizwa ikiwa klabu hiyo itamuuza mchezaji huyo ikiwa mazungumzo hayo yataendelea hadi mwaka ujao, Wenger, alikariri kuwa hana nia yoyote ya kumpoteza mmoja wa wachezaji wake wa kutegemewa.

Mwezi Agosti mwaka huu, Walcott alikataa kusaini mkataba mpya ambao angelipwa £75,000 kwa wiki na kusisitiza kuwa, hatma yake katika klabu hiyo itategemea ikiwa atapewa nafasi ya kucheza kama mmoja wa washambulizi.

Monday, September 24, 2012

MAN U YAITULIZA LIVERPOOL ARSENAL MAN CITY HAKUNA MBABE


Manchester United imeicharaza Liverpool kwa bakora 2-1 katika dimba la Anfield katika mpambano ulioshuhudiwa na mashabiki wapatao 44,263. Liverpool ndio walikuwa wa kwanza kuzifumania nyavu za Man Unietd kupitia kwa Steven Gerrald katika dakika ya 45. Mpaka mapumziko bao lilikuwa 1-0 wenyeji akienda kupumzika kifua mbele.

Kipindi cha pili nibeebe nibeebe nibebeee ilianza na katika dakika ya 50 R Da Silva aliipatia Man U bao la kusawazisha kabla ya Robin Van Persie kutupia kambani goli la pili na la ushindi katika dakika ya 80 kwa nduki kali ya mkwaju wa penati.

Friday, September 21, 2012

ABABMBWA AKIJARIBU KUIBA GITAA


Njemba amekuwa mdogo kama "piriton" baada ya kudwakwa akijaribu kuiba kifaa cha muziki ambapo mbinu yake ilikuwa kali sana lakini anashangaa watu wamemshtukiaje?

TBL YAZIKABIDHI SIMBA NA YANGA NDINGA ZAO


Basi walilokabidhiwa mabingwa wa ligi kuu ya Tanzania bara Simba Sports Club.


Basi walilokabidhiwa Dar Young Africans (YANGA)

Thursday, September 20, 2012

CHELSEA YAGAWANA POINTI NA JUVENTUS, MAN U YAIBURUZA GALATASARAY

Oscar akishangilia goli pamoja na wenzake Ramires na David Luiz
 
Mabingwa watetezi wa klabu bingwa barani Ulaya, Chelsea ya Uingereza, wakiwa katika dimba la nyumbani la Stamford Bridge, walishindwa kuifunga Juventus ya Italia katika pambano la Jumatano usiku.

Nyota wa Chelsea alikuwa ni mchezaji Oscar kutoka Brazil, ambaye alifanikiwa kutumbukiza magoli mawili kambani katika kipindi cha kwanza; dakika ya 31 na 33.
Bao la pili liliingia kupitia mkwaju wa mbali, na ambalo lilimuacha kipa wa Juventus, Gianluigi Buffon akiwa amezubaa.
Oscar alisajiliwa na Chelsea hivi majuzi.


Hata hivyo Juventus, mabingwa wa Italia, na ambao hawakushindwa katika mechi 42 za Serie A huko nyumbani, walijikakamua na hatimaye kusawazisha na kujinyakulia pointi moja.

Arturo Vidal aliwafungia bao kabla ya kipindi cha kwanza kumalizika, na baadaye mchezaji wa zamu, Fabio Quagliarella, zikiwa zimesalia dakika tisa mechi kumalizika, alithibitisha Juventus ilikuwa na nia ya kuondoka na angalau pointi moja.


Oscar akifunga goli katika mechi dhidi ya Juventus


Oscar akimdhibiti mkongwe Andre Pirlo


Oscar akitupia Kamba ya pili


Wachezaji wa Juventus wakishangilia goli la kusawazisha


Torres akiwa chini ya ulinzi mkali


Kazi kweli kweli ..Lampard amekamwata

Kati ya mechi nane za Jumatano, Manchester United pia ilikuwa uwanjani kupambana na Galatasaray, na vijana wa Sir Alex Ferguson wakichezea nyumbani, mechi ya kundi G, walipata ushindi wa bao 1-0.
Michael Carrick aliandikisha bao hilo mapema, dakika ya 7.

Klabu hiyo ya Uturuki itadhaniwa na wengi kwamba ilinyimwa nafasi ya kusawazisha, kwa mwamuzi kuwapa penalti, baada ya Nemanja Vidic kumchezea vibaya Umut Bulup.



Picha zikionesha jinsi Carrick alivyomtesa mlinda mlango wa Galatasaray na kutia mpira kambani.

Wachezaji wa Man U wakimpongeza Carrick

Wednesday, September 19, 2012

NGORONGORO CRATER "AFRICA'S GARDEN OF EDEN"

QUICK FACTS ABOUT NGORONGORO CRATER
  • Largest unbroken caldera in the world
  • Also referred to as "Africa's Garden of Eden"
  • Crater is 12 miles (19 km) across and covers 102 square miles (264 sq km)
  • Rises over 2,000 feet above the caldera floor
  • Home to over 30,000 animals including the rare black rhino


  • Ngorongoro Crater is the world's largest unbroken caldera. Often referred to as "Africa's Garden of Eden," the crater is home to over 30,000 animals including elephants, lions, cheetahs, wildebeests, buffaloes, and the rare black rhinos. View Wildlife of Ngorongoro Crater to learn more about the wildlife and View Birds of Ngorongoro Crater to discover some of the many species that are found in the area.
    Ngorongoro Crater was created from a volcano that exploded creating the caldera wilderness haven. The crater is 12 miles (19 km) across and consumes 102 square miles (264 sq km) of wilderness. The rim of the crater rises just over 2,000 feet (610 m) above the caldera floor reaching an elevation of 7,500 feet (2,286 m).






    OMMY DIMPLES- Baadae