Thursday, November 22, 2012

BENITEZ AVAA VIATU VYA DE MATTEO





Rafael Benitez kocha mpya wa Chelsea akitokea Liverpool na sasa amerithi mikoba ya De Matteo kuinoa Chelsea.


Roberto De Matteo kocha aliepigwa chini

ARSENAL YAUA MTU LIGI YA MABINGWA ULAYA



 






Jack Wilshere akimtoka mlinda mlango wa Montpellier na kutia kambani goli la kwanza kwa Arsenal katika dakika ya 49.


Podolski akitupia bao la pili na la ushindi la Arsenal dhidi ya Montpellier katika dakika ya 63

Katika mtanange huo uliohudhuriwa na watazamaji 59,760 Vikosi vilikuwa kama ifuatavyo

Arsenal

  • 01 Szczesny
  • 03 Sagna
  • 04 Mertesacker
  • 05 Vermaelen
  • 06 Koscielny Booked
  • 08 Arteta
  • 10 Wilshere
  • 15 Oxlade-Chamberlain (Ramsey - 69' )
  • 19 Cazorla Booked (Coquelin - 84' )
  • 09 Podolski
  • 12 Giroud Booked (Gervinho - 84' )

Substitutes

  • 24 Mannone
  • 25 Jenkinson
  • 28 Gibbs
  • 16 Ramsey
  • 22 Coquelin
  • 23 Arshavin
  • 27 Gervinho

Montpellier

  • 16 Geoffrey Jourdren
  • 03 Mapou Yanga M'Biwa
  • 05 Bedimo Booked
  • 12 Congre
  • 21 El Kaoutari
  • 25 Deplagne Booked
  • 10 Belhanda
  • 13 Estrada (Joris Marveaux - 79' )
  • 20 Remy Cabella (Emanuel Herrera - 68' )
  • 08 Mounier
  • 09 Charbonnier (Martin - 68' )

Substitutes

  • 01 Laurent Pionnier
  • 04 Hilton
  • 27 Jeunechamp
  • 06 Joris Marveaux
  • 14 Pitau
  • 28 Martin
  • 11 Emanuel Herrera

MAN CITY YATOLEWA KIUME YATOA SARE NA REAL MADRID


Mfungaji wa goli la Real Madrid Karem Benzema akishangilia kwa staili ya aina yake.


Kun Aguero mfungaji wa bao la kusawazisha la Man City kwa njia ya penalti


Benzema akitupia kambani bao la kuongoza dhidi ya Man City



DI MATTEO APIGWA CHINI CHELSEA

Roberto De Matteo
 
Roberto Di Matteo amefutwa kazi na klabu ya Chelsea, baada ya kuwa meneja kwa kipindi cha miezi minane.

Di Matteo aliiwezesha Chelsea kuwa mshindi wa klabu bingwa barani Ulaya, na vile vile kupata Kombe la FA msimu uliopita, na mwezi Juni, alitia saini mkataba wa miaka miwli.

Lakini kufuatia Chelsea kuzabwa magoli 3-0 na Juventus usiku wa Jumanne, inaelekea timu hiyo itakuwa na kibarua kigumu sana cha kufanikiwa kuendelea katika michuano ya klabu bingwa, na kwa hiyo wasimamizi wa klabu wameonelea ni vyema kumtimua kutoka Stamford Bridge.

Kulingana na taarifa katika mtandao wa Chelsea, "klabu kitatoa taarifa kamili hivi karibuni kuhusiana na meneja wa timu".

Roman Abramovich, tajiri anayemiliki klabu ya Chelsea, sasa atakuwa anamtafuta meneja wa tisa, tangu kumiliki klabu mwaka 2003, na kwa muda mrefu, inaaminika amekuwa akizitamani sana huduma za aliyekuwa meneja wa Barcelona ya Uhispania, Pep Guardiola.

Lakini vile vile amewasiliana na aliyekuwa kocha wa Liverpool ya Uingereza, Rafael Benitez, na kuna uwezekano huenda akashikilia hatamu kwa muda mfupi.

Abramovich, raia wa Urusi, tayari alikuwa amewasiliana na Benitez hata kabla ya Chelsea kushindwa nchini Italia.

Wednesday, November 21, 2012

MAN UNITED CHALII YACHAPWA NA GALLATASARAY


Mfungaji wa bao pekee la Gallatasaray dhidi ya Man United Yilmaz Burak akishangilia


Hapa kazi tu










Hakika ilikuwa mechi ya undava undava na undundu undundu iliyoisha kwa bao moja kwa nunge Man United wakilala hoi

Tuesday, November 20, 2012

WENGER: THEO WALCOTT HANG'OKI ARSENAL

Theo Walcott
 
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger , amekariri kuwa klabu hiyo haina nia yoyote ya kumuuza mchezaji wake Theo Walcott, msimu wa usajili Januari mwakani.

Kufuatia uamuzi huo, Arsenal, sasa huenda ikampoteza Walcott, mwenye umri wa miaka 23, ila kupokea chochote, kwa kuwa kandarasi ya mchezaji huyo inakamilika mwisho wa msimu huu.

Ikiwa Walcott na wasimamizi wa klabu hiyo hawataafikiana lolote, kabla ya wakati huo, Walcott atakuwa huru kuanzisha mazungumzo na klabu yoyote na kama vipi akasepa Emirates.

Mazungumzo kuhusu kandarasi mpya yamekwama, na alipoulizwa ikiwa klabu hiyo itamuuza mchezaji huyo ikiwa mazungumzo hayo yataendelea hadi mwaka ujao, Wenger, alikariri kuwa hana nia yoyote ya kumpoteza mmoja wa wachezaji wake wa kutegemewa.

Mwezi Agosti mwaka huu, Walcott alikataa kusaini mkataba mpya ambao angelipwa £75,000 kwa wiki na kusisitiza kuwa, hatma yake katika klabu hiyo itategemea ikiwa atapewa nafasi ya kucheza kama mmoja wa washambulizi.

Monday, September 24, 2012

MAN U YAITULIZA LIVERPOOL ARSENAL MAN CITY HAKUNA MBABE


Manchester United imeicharaza Liverpool kwa bakora 2-1 katika dimba la Anfield katika mpambano ulioshuhudiwa na mashabiki wapatao 44,263. Liverpool ndio walikuwa wa kwanza kuzifumania nyavu za Man Unietd kupitia kwa Steven Gerrald katika dakika ya 45. Mpaka mapumziko bao lilikuwa 1-0 wenyeji akienda kupumzika kifua mbele.

Kipindi cha pili nibeebe nibeebe nibebeee ilianza na katika dakika ya 50 R Da Silva aliipatia Man U bao la kusawazisha kabla ya Robin Van Persie kutupia kambani goli la pili na la ushindi katika dakika ya 80 kwa nduki kali ya mkwaju wa penati.