Tuesday, November 27, 2012

R.I.P HUSSEIN RAMADHAN MKIETE "SHARO MILIONEA"

Msanii wa vichekesho na muziki wa kizazi kipya Hussein Ramadhan Mkiete a.k.a Sharo Milionea amefariki katika ajali ya gari iliyotokea kijiji cha Lusanga,Muheza mkoani Tanga Siku ya jumatatu ya tarehe 26/11/2012 majira ya saa mbili usiku.
Habari zilizothibitishwa na kamanda wa polisi wa mkoa wa Tanga Constatine Massawe. kifo cha Sharo Milionea kimesababishwa na ajali aliyoipata wakati gari yake aina ya Toyota Harrier ilipopasuka tairi na kugonga mti eneo la Maguzoni.
Mwili wa marehemu Sharo umehifadhiwa katika hospitali Teule Tanga kwa kusubiria taratibu za mazishi zitakazofanywa na ndugu wa marehemu, Mungu ailaze roho ya marehemu Hussein Ramadhan Mkiete a.k.a SHARO MILIONEA Mahala pema peponi,AMIN!


Marehemu Hussein Ramadhan Mkiete "SHARO MILIONEA" enzi za uhai wake.


Sharo Milionea akifanya shopping mwezi huu kabla ya kupata ajali iliyoondoa uhai wake.



VIDEO ZA NYIMBO ZA SHARO MILIONEA

Monday, November 26, 2012

MAN CITY, CHELSEA HAKUNA MBABE

Timu za soka za Chelsea na Man City ziliumana katika mwendelezo wa mbio za kuwania ubingwa wa ligi kuu ya Uingereza katika uwanja wa Stamford Bridge.
Katika mpambano huo wa wababe hao kutoka suluhu na ikiwa mechi ya kwanza kwa kocha mpya wa Chelsea Rafael Benitez akichukua nafasi ya kocha kipenzi cha mashabiki wa Chelsea Roberto De Matteo.
Mashabiki wa Chelsea hawakufurahishwa na kitendo cha De Matteo kutimuliwa na wameonesha kwa kiasi kikubwa hawamkubali kabisa Rafael Benitez ambaye ameshindwa kuipa matumaini mema Liverpool alipokuwa kocha mkuu na sasa yupo Chelsea itakuwaje? ngoja tusubirie lakini mashabiki na mimi mwenyewe hatumkubali Benitez kama tunavyomkubali De Matteo.




Mashabiki wa Chelsea na ujumbe wa kumdhihaki Benitez na kumtukuza De Matteo


Benitez akiwa kibaruani lakini mashabiki hawamkubali hata kidogo

Roberto Mancini kocha wa Man City akitoa maelekezo katika mpambano huo


Huu Haaa!! Kazi Vicent Company na Torres


Tulia wewe bwana mdogo tuu!!! Torres akiwa chini ya ulinzi mkali


Ukijipendekeza nakupasua!!! Ramires akimtuliza Aguero


Aaaah mi nimeshachoka msiniseme sana bhanaa wanakaba kama nini!!

MPIGIE KURA MCHEZAJI UNAYETAKA ACHUKUE TUZO YA MCHEZAJI BORA AFRIKA 2012 YA BBC

Majina ya wachezaji watano wanaowania tuzo la BBC la mchezaji bora zaidi barani Afrika mwaka 2012 yamewekwa hadharani.

Bofya Yahya Toure.
Mcheza kiungo kutoka Ivory Coast, anayeichezea Manchester City ya Uingereza. Toure aliiongoza Manchestert City kushinda kombe la ligi kuu ya Premier ya England kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya miaka 44 iliyopita.


Bofya Demba Ba
kwa sasa ni mmoja wa wachezaji nyota wa klabu ya Newcastle na kufikia sasa tayari amefunga jumla ya magoli 6 katika ligi kuu ya premier la England na anatarajiwa kujumuishwa kwenye kikosi cha Senegal kitakachocheza katika fainali ya kombe la mataifa bingwa barani Afrika.


Bofya Didier Drogba
Ni noadha wa timu ya taifa ya Ivory Coast, amewahi kuongoza Chelsea kushinda kombe la ligi kuu ya Premier ya England pamoja na kombe la klabu bingwa barani ulaya.


Bofya Christopher Katongo
Ni mchezaji wa timu ya taifa ya Zambia maarufu kama Chipolopolo na aliiongoza timu hiyo kushinda fainali ya kombe la mataifa bingwa barani Afrika


Bofya Younes Belhanda
Ni mchezaji mwenye umri wa miaka 22, na mmoja wa wachezaji waliotia fora na kuisaidia klabu ya Montepellier, kushinda kombe la ligi kuu kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya karne moja tangu klabu hiyo ilipobuniwa.

PIGA KURA HAPA
Bofya Ukitaka kupiga kura unaweza kufungua anwami hii ya mtandao na kumbuka maagiza yametolewa kwa lugha ya Kiingereza.

Thursday, November 22, 2012

BENITEZ AVAA VIATU VYA DE MATTEO





Rafael Benitez kocha mpya wa Chelsea akitokea Liverpool na sasa amerithi mikoba ya De Matteo kuinoa Chelsea.


Roberto De Matteo kocha aliepigwa chini

ARSENAL YAUA MTU LIGI YA MABINGWA ULAYA



 






Jack Wilshere akimtoka mlinda mlango wa Montpellier na kutia kambani goli la kwanza kwa Arsenal katika dakika ya 49.


Podolski akitupia bao la pili na la ushindi la Arsenal dhidi ya Montpellier katika dakika ya 63

Katika mtanange huo uliohudhuriwa na watazamaji 59,760 Vikosi vilikuwa kama ifuatavyo

Arsenal

  • 01 Szczesny
  • 03 Sagna
  • 04 Mertesacker
  • 05 Vermaelen
  • 06 Koscielny Booked
  • 08 Arteta
  • 10 Wilshere
  • 15 Oxlade-Chamberlain (Ramsey - 69' )
  • 19 Cazorla Booked (Coquelin - 84' )
  • 09 Podolski
  • 12 Giroud Booked (Gervinho - 84' )

Substitutes

  • 24 Mannone
  • 25 Jenkinson
  • 28 Gibbs
  • 16 Ramsey
  • 22 Coquelin
  • 23 Arshavin
  • 27 Gervinho

Montpellier

  • 16 Geoffrey Jourdren
  • 03 Mapou Yanga M'Biwa
  • 05 Bedimo Booked
  • 12 Congre
  • 21 El Kaoutari
  • 25 Deplagne Booked
  • 10 Belhanda
  • 13 Estrada (Joris Marveaux - 79' )
  • 20 Remy Cabella (Emanuel Herrera - 68' )
  • 08 Mounier
  • 09 Charbonnier (Martin - 68' )

Substitutes

  • 01 Laurent Pionnier
  • 04 Hilton
  • 27 Jeunechamp
  • 06 Joris Marveaux
  • 14 Pitau
  • 28 Martin
  • 11 Emanuel Herrera

MAN CITY YATOLEWA KIUME YATOA SARE NA REAL MADRID


Mfungaji wa goli la Real Madrid Karem Benzema akishangilia kwa staili ya aina yake.


Kun Aguero mfungaji wa bao la kusawazisha la Man City kwa njia ya penalti


Benzema akitupia kambani bao la kuongoza dhidi ya Man City



DI MATTEO APIGWA CHINI CHELSEA

Roberto De Matteo
 
Roberto Di Matteo amefutwa kazi na klabu ya Chelsea, baada ya kuwa meneja kwa kipindi cha miezi minane.

Di Matteo aliiwezesha Chelsea kuwa mshindi wa klabu bingwa barani Ulaya, na vile vile kupata Kombe la FA msimu uliopita, na mwezi Juni, alitia saini mkataba wa miaka miwli.

Lakini kufuatia Chelsea kuzabwa magoli 3-0 na Juventus usiku wa Jumanne, inaelekea timu hiyo itakuwa na kibarua kigumu sana cha kufanikiwa kuendelea katika michuano ya klabu bingwa, na kwa hiyo wasimamizi wa klabu wameonelea ni vyema kumtimua kutoka Stamford Bridge.

Kulingana na taarifa katika mtandao wa Chelsea, "klabu kitatoa taarifa kamili hivi karibuni kuhusiana na meneja wa timu".

Roman Abramovich, tajiri anayemiliki klabu ya Chelsea, sasa atakuwa anamtafuta meneja wa tisa, tangu kumiliki klabu mwaka 2003, na kwa muda mrefu, inaaminika amekuwa akizitamani sana huduma za aliyekuwa meneja wa Barcelona ya Uhispania, Pep Guardiola.

Lakini vile vile amewasiliana na aliyekuwa kocha wa Liverpool ya Uingereza, Rafael Benitez, na kuna uwezekano huenda akashikilia hatamu kwa muda mfupi.

Abramovich, raia wa Urusi, tayari alikuwa amewasiliana na Benitez hata kabla ya Chelsea kushindwa nchini Italia.