Wednesday, January 30, 2013

LULU SASA TUPO NAE MTAANI


Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’ (kulia) akiwa na mama yake, Luklesia Kalugila nje ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam baada ya kuachiwa huru kwa dhamana jana.

SHABIKI AKOJOLEA NDINGA YA BALOTELLI


Shabiki anayesadikiwa kuwa Man United akikojolea ndinga ya Balotelli


Baada ya kuikojolea mwingine akashusha suruali na akapanda nyuma ya "Boneti"

Gari aina ya Bentley yenye thamani ya paundi za Uingereza 160,000 inayomilikiwa na mshambuliaji mtukutu wa Manchester City ambae kwasasa amesajiliwa na AC Milan Mario Bawuah Balotelli, ilikojolewa na mtu anayeasadikiwa kuwa ni shabiki wa Manchester United ilipokuwa imepaki katika mgahawa ujulikanao kama Indian Restaurant Zouk uliopo katikati ya jiji la Manchester siku ya Jumapili jioni.

Shabiki mwingine alionekana akiungana na mwenzake kulifanyia uhalifu gari la Balotelli kwa kushusha suruali yake na kupanda nyuma ya Boneti huku akipiga kelele.
Shuhuda wa tukio hilo Michael Armorgie aliliambia gazeti la The Sun kuwa "Nilikuwa ninapita ndipo nikawaona vijana wawili wakifanya vituko kwenye gari la Balotelli,Sikuamini..mmoja alikuwa analikojolea na mwingine amepanda juu anaimba nyimbo za Manchester United".

Hii ndio ndiga ya Balotelli iliyokojolewa

DROGBA AMFUATA SNEIJDER GALATASARAY BALOTELLI ATUA AC MILAN

Galatasaray imemsajili aliyekuwa mshambulizi wa Chelsea Didier Drogba kutoka kwa klabu ya Shanghai Shenhua inayoshiriki katika ligi kuu ya Premier nchini Uchina.

Galatasaray inayocheza ligi kuu nchini Uturuki, imethibitisha kuwa Drogba amesaini mkataba wa miezoi kumi na minane na klabu hiyo.

Mchezaji hiyo mwenye umri wa miaka 34, kwa sasa yuko nchini Afrika Kusini kuiongoza kikosi cha Ivory Coast katika mashindano ya kuwania kombe la mataifa ya Afrika.

Kwa mujibu wa ujumbe uliotumwa na kampuni ya uhusiano bora inayomuakilisha mchezaji huyo Sports PR Company na kuchapishwa kwa mtandano wa kijamii wa Twitter, Drogba alisema anajiandaa kurejea tena katika michuano ya kuwania kombe la klabu binga barani ulaya kwa mara nyingine.

Galatasaray imefuzu kwa raundi ya muondoana ya kuwania kombe hilo na imepangiwa kucheza na FC Schalke 04 kutoka uUjerumani.

''Hii ni fursa nzuri ya kuichezea timu kubwa na ni nafasi ambayo siwezi kupuuza'' Alisema Drogba.
Agenti wam mchezaji huyo amesema, Drogba atajiunga la klabu hiyo ya Galatasaray baada ya kukamilika kwa michuano ya kuwania kombe la mataifa ya Afrika.

Drogba ni mchezaji wa pili wa hadhi ya juu kusajiliwa na Galatasaray baada ya Wesley Sneijder aliyejiunga na klabu hiyo kutoka klabu ya Inter Milan.

Drogba alijiunga na Shanghai Shenhua mwezi juna mwaka uliopita na ameifunga jumla ya magoli manane baada ya kucheza mechi kumi na moja.

Awali Drogba alitaka kurejea Ulaya kwa mkopo na klabu yake ya zamani ilikuwa imeanzisha mazungumzo ya kumsajili.

Lakini shirikisho la mchezo wa soka duniani FIFA lilipinga uhamisho huo, likisema kuwa linakiuka sheria za kimataifa kuhusu uhamisho na usajili wa wachezaji.

Mchezaji mwingine wa zamani wa Cheslea Nicolas Anelka huenda pia anajiandaa kukihama klabu hiyo ya Shenhua, baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu katika klabu ya Juventus.



Drogba katika uzi wa Shenhua


Wesley Sneijder

BALOTELLI ATUA AC MILAN

Mkurugenzi wa klabu ya AC Millan, Umberto Gandini amethibitisha kuwa klabu hiyo imemsajili mshambuliaji wa Manchester City Mario Balotelli kwa mkataba wa miaka minne na nusu.

Balotelli, 22, anatarajiwa kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu mjini Milan siku ya Jumatano kabla ya kusaini wake na klabu hiyo.

Inakisiwa kuwa AC Milan imemsajili mchezaji huyo kwa kitita cha pauni milioni 20.

Awali Manchester City ilianzisha mazungumzo na vilabu vya AC Milan na Juventus kuhusu uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wake Mario Balotelli, na ripoti zinasema kuwa, Balotelli atauzwa ikiwa vilabu hivyo vitaweza kulipa fedha wanazo taka.

Klabu hiyo imesema mchezji huyo mwenye umri wa miaka 22, anakisiwa kugharibu pauni milioni ishirini na moja mbali na fedha zingine za ziada.

Balotelli hana haraka ya kuuzwa na Manchester City imesema haina mipango ya kupunguza mshahara wake ili aondoke.

Kinyume na matarajio ya wengi Balotelli amesafiri na wachezaji wa Manchester City watakaocheza na QPR katika mechi ya ligi kuu ya premir leo usiku.

Milan ilianzisha mazungumzo na Man City, kuhusu mchezaji huyo kutoka Italia na kuna ripoti kuwa klabu ya Juventus vile vile imewasilisha ombi la kutka kumsajili Balotelli, ambaye alijiunga na Manchester City Agosti mwaka wa 2010 kwa kitita cha pauni milioni 24.

 Mario Baruah Balotelli


Swaga za kitaani

Mapema siku ya Jumatatu, naibu kocha mkuu wa Man City, David Platt, alisema kuwa Balotelli hatajiunga na AC Millan mwezi huu.

Siku ya Ijumaa wiki iliyopita, kocha wa Man City Roberto Mancini, alikariri hana nia ya kumuuza kuwa mchezaji huyo kutoka Italia.

Balotelli ambaye amefunga goli moja baada ya kucheza mechi kumi na nne msimu huu, amekumba na kashfa nyingi tangu aliposajiliwa.

Tukio la hivi karibuni, likiwa mzozo kati yake na Mancini katika uwanja wao wa mazoezi mwanzo wa mwezi huu.

Makamu wa rais wa AC Milan Adriano Galliani amesema ikiwa Manchester City itapunguza bei ya mchezaji huyo, basi huenda wakamsajili.

Monday, January 28, 2013

SIMBA, YANGA, AZAM ZAANZA VYEMA DURU LA PILI

MABINGWA watetezi, Simba jana walianza kwa kishindo duru la pili Ligi Kuu Bara kwa kuitungua African Lyon mabao 3-1, katika mechi ambayo kila upande ulikosa kufunga penalti katika kila kipindi.
Ushindi kama huo pia uliandikwa na Azam FC iliyotumia vizuri Uwanja wa Chamazi kuiogesha kipigo Kagera Sugar ya Kagera, kadhalika Coastal Union kule Mkwakwani Tanga dhidi ya Mgambo Shooting.

Wachezaji wa Simba wakimnyanyua Ngassa baada ya kufunga goli.

Simba imefikisha pointi 26, lakini ikiendelea kubaki nyuma ya Azam kwa tofauti ya pointi moja, na Yanga inayocheza leo haijaathiriwa na matokeo ya mechi za jana.
Katika mchezo huo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wachezaji Mrisho Ngassa wa Simba na
Shamte Ally wa Lyon walikosa penalti. Penalti ya Ngassa ingeweza kumpa ‘hat trick’ kama siyo kipa wa Lyon, Abdu Seif kuicheza dakika ya 66 kufuatia Ibrahim Issac kumkwatua Ramadhan ‘Redondo’ Chombo.

Ngassa akiwachachafya mabeki wa African Lyon

Shamte naye alishindwa kulenga lango baada ya penalti yake kwenda nje kufuatia madhambi ya Paul Ngalema dhidi ya Fred Lewis dakika ya 30.
Redondo alifunga bao la mapema zaidi mzunguko wa pili, baada ya kutumia dakika mbili tangu kuanza mpira kutikisa kamba za Lyon akimalizia pasi ya Mrisho Ngassa.
Lyon walijibu shambulizi dakika ya nne na ustadi wa Juma Kaseja ulimnyima bao Jacob Massawe baada ya shuti lake kuchezwa na kipa huyo namba moja Msimbazi.
Mashuti mawili ya Ngassa dakika ya 4 na 6 yangeweza kubadilisha matokeo kama siyo kukosa shabaha na kwenda moja kwa moja mikononi mwa kipa wa Lyon, Abdul Seif.
Ngassa alirekebisha makosa yake kwa kufanya matokeo kuwa 2-0 baada ya kuwazidi ujanja mabeki wa Lyon akimalizia pasi ya Jonas Mkude.
Alikuwa Ngassa tena akipachika bao la tatu, la pili kwake kwenye mchezo huo shuti akimalizia mpira wa krosi uliopigwa na Haruna Chanongo dakika ya 35. Kipindi cha pili, Kocha Patrick Liewig aliwapumzisha Paul Ngalema na Mussa Mudde na kuingia Kigi Makasi na Komalibil Keita.

Mlinda mlango wa Afrikan Lyon akiondosha hatari langoni mwake.

Lyon walipunguza makali ya tofauti ya mabao ya kufungwa baada ya Bright Ike kumtungua Kaseja dakika ya 60 likiwa bao pekee kwao kwenye mchezo huo.
Pamoja na ushindi huo, Kocha Liewig alisema mchezo ulikuwa mgumu, ingawa pia hakusita kueleza hisia akiwalaumu wachezaji wake kucheza ovyo kipindi cha pili.
Mkwakwani Tanga, Union walifikisha pointi 25 na kupanda mpaka nafasi ya nne kwenye msimamo kwa mabao ya Philipo Mutasela, Danny Lihanga na Haroun Mahundi, huku bao la Mgambo likifungwa na Peter Mwaliyanzi.




Wachezaji wa Yanga wakimpongeza Tegete baada ya kutupia goli dhidi ya Prisons ambapo Yanga ilishinda 3-1.


Mabeki wa Prisons wakiondosha hatari langoni mwao

 

LIVERPOOL TOTTENHAM ZAFUNGASHIWA VIRAGO KOMBE LA FA

Tottenham imebanduliwa nje ya mashindano ya kuwania kombe la FA baada ya kulazwa magoli mawili kwa moja na Leeds United.

Luke Varney aliifungia Leeds bao lake la kwanza kabla ya Ross McCormack, kufunga la pili. Tottenham ambayo inashiriki katika ligi kuu ya Premier nayo ikapata bao lake kupitia kwa mchezaji wake Clint Dempsey.
 



Mtukutu El-Hadji Dioff akishangilia kuibandua Tottenham

Katika mechi nyingine Chelsea, nusura iage mashindano hayo baada ya kulemewa na Bendford.

Hata hivyo Fernando Torres aliifungia Chelsea bao lake la pili na kuiepushia aibu kubwa.

Timu hizo mbili zilitoka sare ya kufungana mabgoli mawili kwa mawili.

Liverpool vile vile, imeondolewa kwenye michuano hiyo ya FA, baada ya kunyukwa magoli 3-2 na Oldham, ambayo inashiriki katika ligi daraja ya kwanza.

Timu zingine za ligi kuu ambazo zimefuzu kwa raundi ijayo ni pamoja na Manchester United, Everton, Arsenal, Wigan, reading na Manchester City.

Norwich, QPR na stoke city zinaungana na timu ambazo zimefunganya virago vyao katika michuano hiyo ya FA.

Wachezaji wa Liverpool hoi baada ya kubanduliwa nje ya kombe la FA na Oldham

Wayaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa


Wachezaji wa Oldham wakishangilia baada ya kuidungua Liverpool

Leeds 2-1 Tottenham
 
 
 
Oldham 3-2 Liverpool
Chelsea 2-2 Brandford

CLUB YA USIKU YA KISS YATEKETEA KWA MOTO WATU 233 WAFARIKI DUNIA

Raia wa Brazili wanaomboleza vifo vya watu mia mbili thelathini na watatu waliofariki dunia katika ajali ya moto iliyotokea kwenye ukumbi wa muziki katika mji wa kusini wa Santa Maria.

Maafisa wanasema kuwa wengi wa waathiriwa walikuwa ni wanafunzi waliokufa baada ya kushindwa kupumua kutokana na moshi mkubwa .

Wengine zaidi ya mia moja wanapata matibabu hospitalini . Serikali ya Brazil imetangaza siku tatu za maombolezo . Taarifa zinasema kuwa moto huo ulianza wakati waimbaji wa bendi moja walipowasha fataki.


Baadhi ya ndugu ya waliopoteza maisha wakilia kwa uchungu

Maswali sasa yamekuwa yakiulizwa kuhusu usalama wa kumbui za starehe, huku kukiwa na madai kuwa cheti cha huduma za zima moto kilikuwa kimepitwa na wakati. Hili ni jana kubwa la moto kuwahi kuikumba Brazil kwa zaidi ya miongo mitano

Familia za waathiriwa wamekuwa wakiomboleza juu ya majeneza za jamaa zao katika ukumbi wa mamozezi ambao unatuimika kama jumba la kuhifadhia maiti.
Kwa sababu ya heshima kwa waliofariki, serikali iliakhirisha sherehe iliyotarajiwa kufanyika leo Jumatatu katika mji mkuu, Brasilia, kuadhimisha siku 500, kabla ya kombe la dunia kungo'a nagna nchini humo mwaka ujao.

Mazishi ya kwanza mjini Santa Maria yanatarajiwa kufanyika leo , kwa mujibu wa magazeti ya nchi humo.

Maafisa wa utawala wametoa majina ya waathiriwa hao,230 huku maiti watatu wakisalia kutotambuliwa.

Kulingana na taarifa za kituo cha televisheni cha Globo,wengi wa waathiriwa walikuwa kati ya umri wa miaka16 na 20.

Zaidi ya watu 100 wanapokea matibabu baada ya kushindwa kupumua kutokana na moshi mkubwa.

Watu wakitimua mbio wakati moto ukiendelea kuwaka ukumbini hapo






Vikosi vya zima moto vikijaribu kuzima moto katika club ya disco ya Santa Maria








































Thursday, January 24, 2013

ANAMILIKI MAGARI YA KIFAHARI 7,000 YENYE THAMANI YA DOLA BILLIONI 7

Sultani wa Brunei ni mpenzi mkubwa wa magari ya kifahari, anamiliki magari ya kifahari yapatayo 7,000 yenye thamani ya dola za kimarekani billioni 7 ambayo yamepaki katika garage kubwa katika kasri lake.  Ili aweze kuendesha magari yote bila kurudia hata siku moja itamchukua miaka 20 kuweza kumaliza kuyaendesha magari yote..mhhh mbongo wa kawaida baiskeli ni kitendawili hayaaa!!
Fun & Info @ Keralites.net
Sultani wa Brunei

Kwa mujibu wa gazeti mashuhuri la Daily Mirror la tarehe 30 juni 2010, anamiliki magari yafuatayo;
604 Rolls Royce’s, 574 Mercedes-Benzes,
452 Ferraris,

382 Bentleys,
209 BMWs,
179 Jaguars,
134 Koenigseggs,

21 Lamborghinis,
11 Aston Martins,
and 1 SSC.

Fun & Info @ Keralites.net
Gereji ya magari ya Sultani kwa juu

Fun & Info @ Keralites.net
Kwa mbele

Fun & Info @ Keralites.net
Kwa ndani

Fun & Info @ Keralites.net
SSC ultimate aero  ($740,000 )
 

Fun & Info @ Keralites.net
Leblanc Mirabeau ($765,000 )

Fun & Info @ Keralites.net
Koenigsegg CCX ($1.1 Million )

 
Fun & Info @
Keralites.net
Koenigsegg CCXR ($1.3 Million)

Fun &
Info
@ Keralites.net


Maybach Landaulet ($1.4 Million )

Fun & Info
 @ Keralites.net
Lamborghini Reventon ($1.42 Million)

Fun & Info @ Keralites.net
Lamborghini Reventon Roadster ($1.56 Million )

Fun & Info @ Keralites.net
Pagani Zonda Cinque Roadster ($1.8 Millions)

Fun & Info @
Keralites.net
Bugatti Veyron 16 4 Grand Sport 57 ($1.67 Million )

Fun & Info @
Keralites.net
 Koenigsegg Trevita  ($2.21 Million )