Tuesday, February 5, 2013

BARUA YA ARSENE WENGER KWA MASHABIKI WA ARSENAL 4 FEB 2013


Wenger: 'Our defence was very solid'
Dear Arsenal supporter,

Stoke City made it difficult for us on Saturday, as they always do. They were well organised and denied us space, and when we did get chances their goalkeeper did very well.

But overall I feel we deserved to win the game and we got what we wanted, even if there was some fortune when Lukas Podolski's free-kick took a deflection.

It took some time for the goal to be given because the linesman put his flag up, but although Walcott was in an offside position he was not interfering with play. So it was the right decision to let the goal stand.

Speaking of Theo, I was impressed with the way he handled himself in what is traditionally a physical game for us. He received some strong tackles but he showed full commitment and a desire to impose himself. He is a different player now.

We knew we would have to grind out the result and that's what we did. It was crucial not to concede and I must say our defence was very solid. Nacho Monreal had a good debut, he got stronger and stronger as the game went on. There is no better introduction to English football than a game against Stoke!

We are a bit more mature now and we dealt well with Stoke's game plan. Peter Crouch is a handful because he is not only physical, he is technically very good. He uses space well and in his link play he is international class.

We are older and a bit more experienced these days and you could see that in our defence. Sagna, Nacho, Koscielny and Mertesacker - they have experience and stature.

In England you have to deal with all types of football without losing sight of how you want to play. It is not always easy because if you have a team of 10 Santi Cazorla's technically you would be very good but against a team like Stoke you would struggle.

We are in a close race with a number of teams for a Champions League place and some results went our way at the weekend with Chelsea losing and Everton drawing. We dropped points against Liverpool but we couldn't afford to do that again on Saturday.

The quality of our performance is there, the spirit is there and our belief and confidence is high. Now we must focus on another big game at Sunderland next weekend.

Thanks for your support,

Arsene Wenger's signature
Arsène Wenger

Monday, February 4, 2013

RATIBA KAMILI NUSU FAINALI,FAINALI NA MSHINDI WA TATU KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA 2013

KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA | RATIBA


SAA CAT (TZ, GMT+3)

Jumatano 06 Februari 2013
1 Mali v    Nigeria Moses Mabhida Stadium 18:00
2 Burkina Faso v    Ghana Mbombela Stadium 21:30

Jumamosi 09 Februari 2013
2 Loser SF1 v    Loser SF2 Nelson Mandela Bay Stadium 21:00

Jumapili 10 Februari 2013
1 Winner SF1 v    Winner SF2 National Stadium 21:00

NIGERIA YAIFUNGASHIA VIRAGO IVORY COAST,BURKINA FASO YAIONDOA TOGO

Timu za soka za Taifa za Nigeria na Burkina Faso zimefanikiwa kutinga katika hatua ya nusu fainali ya kombe la mataifa ya Afrika.
Nigeria"Super Eagles" wametinga hatua ya nusu fainali baada ya kuitungua timu ngumu ya Ivory Coast"Simba wa Teranga" katika mchezo uliopigwa katika dimba la Royal Bafokeng na kuhudhuriwa na mashabiki wapatao 25,000. Magoli ya nigeria yalifungwa na Emenike dk 42 na la pili lilifungwa na Mba dk ya 77, Huku lile la kufutia machozi la Ivory Coast likitupiwa kambani na Tiote dk 49 ya mchezo.

Burkina Faso wametinga hatua ya nusu fainali kwa kuiondosha timu ngumu ya Togo iliyokuwa ikiongozwa na Adebayor kwa goli moja kwa ubuyu, Goli likitupiwa kambani na Pitroipa dk 104 ikiwa ni muda wa nyongeza baada ya timu hizo kutoshana nguvu katika dakika 90. Katika mtanange huo uliomalizika kwa Togo kuondolewa katika michuano hiyo mikubwa barani Afrika mashabiki wapatao 27,000 katika dimba la Mbombela walishuhudia Togo wakifungasha virago na kurejea nyumbani.

Pisha weweeeeeeee

Hapa kazi tuuu


Mba muuaji wa goli pekee la Burkina Faso


Kweli tumetoka!!!!!!!!!!!???????????



Kocha wa Nigeria Steven Kesh akishangilia kutinga nusu fainali

Huendi kokote weweeeeeeeeee

Adebayor akimwaga "udambwidambwi"

Burkina Faso wakishangilia baada ya kutinga nusu fainali

Ivory Coast 1-2 Nigeria
Burkina Faso 1-0 Togo

MAN CITY "YANASANA" NA LIVERPOOL

Mabingwa watetezi wa ligi kuu England Manchester City jana walishindwa kuendeleza mbio za kuifukuzia Man U kileleni pale walipolazimishwa sare ya mabao 2-2 na Liverpool katika dimba lao la nyumbani la Ettihad katika mpambano uliohudhuriwa na mashabiki wapatao 47,301.

Alikuwa ni Edwin Dzeko alieanza kuzifumania nyavu za Liverpool katika dakika ya 22 kabla ya Daniel Sturridge kuwanyamazisha mashabiki wa Liverpool katika dakika ya 28 ya mchezo. Mpaka mapumziko matokeo yalikuwa 1-1.

Katika kipindi cha pili alikuwa ni Mchezaji mkongwe Steven Gerrard alietupia mpira kambani na kuandika bao la 2 kwa Liverpool katika dakika ya 72 na kuamsha nderemo na vifijo katika dimba la Ettihad huku wenyeji wakiwa wanaona haya, Ilikuwa ni dakika ya 77 pale Aguero alipowapatia hafueni wenyeji kwa kutupia kambani bao la kusawazisha.
Mpaka mwisho wa mchezo matokeo yalikuwa Man C 2-2 Liverpool.

Sturridge akifumua shuti lililoelekea moja kwa moja kambani

Nimeuaaaaa...Sturridge akishangilia goli

Imoooooo...Steven Gerrard akiachia nduki kuandika bao la pili


Nimeuaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!

Aguero akishangilia goli baada ya kumzidi maarifa Mlinda mlango wa Liverpool Reina
 
Man C 2-2 Liverpool
 

Wednesday, January 30, 2013

LULU SASA TUPO NAE MTAANI


Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’ (kulia) akiwa na mama yake, Luklesia Kalugila nje ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam baada ya kuachiwa huru kwa dhamana jana.

SHABIKI AKOJOLEA NDINGA YA BALOTELLI


Shabiki anayesadikiwa kuwa Man United akikojolea ndinga ya Balotelli


Baada ya kuikojolea mwingine akashusha suruali na akapanda nyuma ya "Boneti"

Gari aina ya Bentley yenye thamani ya paundi za Uingereza 160,000 inayomilikiwa na mshambuliaji mtukutu wa Manchester City ambae kwasasa amesajiliwa na AC Milan Mario Bawuah Balotelli, ilikojolewa na mtu anayeasadikiwa kuwa ni shabiki wa Manchester United ilipokuwa imepaki katika mgahawa ujulikanao kama Indian Restaurant Zouk uliopo katikati ya jiji la Manchester siku ya Jumapili jioni.

Shabiki mwingine alionekana akiungana na mwenzake kulifanyia uhalifu gari la Balotelli kwa kushusha suruali yake na kupanda nyuma ya Boneti huku akipiga kelele.
Shuhuda wa tukio hilo Michael Armorgie aliliambia gazeti la The Sun kuwa "Nilikuwa ninapita ndipo nikawaona vijana wawili wakifanya vituko kwenye gari la Balotelli,Sikuamini..mmoja alikuwa analikojolea na mwingine amepanda juu anaimba nyimbo za Manchester United".

Hii ndio ndiga ya Balotelli iliyokojolewa

DROGBA AMFUATA SNEIJDER GALATASARAY BALOTELLI ATUA AC MILAN

Galatasaray imemsajili aliyekuwa mshambulizi wa Chelsea Didier Drogba kutoka kwa klabu ya Shanghai Shenhua inayoshiriki katika ligi kuu ya Premier nchini Uchina.

Galatasaray inayocheza ligi kuu nchini Uturuki, imethibitisha kuwa Drogba amesaini mkataba wa miezoi kumi na minane na klabu hiyo.

Mchezaji hiyo mwenye umri wa miaka 34, kwa sasa yuko nchini Afrika Kusini kuiongoza kikosi cha Ivory Coast katika mashindano ya kuwania kombe la mataifa ya Afrika.

Kwa mujibu wa ujumbe uliotumwa na kampuni ya uhusiano bora inayomuakilisha mchezaji huyo Sports PR Company na kuchapishwa kwa mtandano wa kijamii wa Twitter, Drogba alisema anajiandaa kurejea tena katika michuano ya kuwania kombe la klabu binga barani ulaya kwa mara nyingine.

Galatasaray imefuzu kwa raundi ya muondoana ya kuwania kombe hilo na imepangiwa kucheza na FC Schalke 04 kutoka uUjerumani.

''Hii ni fursa nzuri ya kuichezea timu kubwa na ni nafasi ambayo siwezi kupuuza'' Alisema Drogba.
Agenti wam mchezaji huyo amesema, Drogba atajiunga la klabu hiyo ya Galatasaray baada ya kukamilika kwa michuano ya kuwania kombe la mataifa ya Afrika.

Drogba ni mchezaji wa pili wa hadhi ya juu kusajiliwa na Galatasaray baada ya Wesley Sneijder aliyejiunga na klabu hiyo kutoka klabu ya Inter Milan.

Drogba alijiunga na Shanghai Shenhua mwezi juna mwaka uliopita na ameifunga jumla ya magoli manane baada ya kucheza mechi kumi na moja.

Awali Drogba alitaka kurejea Ulaya kwa mkopo na klabu yake ya zamani ilikuwa imeanzisha mazungumzo ya kumsajili.

Lakini shirikisho la mchezo wa soka duniani FIFA lilipinga uhamisho huo, likisema kuwa linakiuka sheria za kimataifa kuhusu uhamisho na usajili wa wachezaji.

Mchezaji mwingine wa zamani wa Cheslea Nicolas Anelka huenda pia anajiandaa kukihama klabu hiyo ya Shenhua, baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu katika klabu ya Juventus.



Drogba katika uzi wa Shenhua


Wesley Sneijder

BALOTELLI ATUA AC MILAN

Mkurugenzi wa klabu ya AC Millan, Umberto Gandini amethibitisha kuwa klabu hiyo imemsajili mshambuliaji wa Manchester City Mario Balotelli kwa mkataba wa miaka minne na nusu.

Balotelli, 22, anatarajiwa kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu mjini Milan siku ya Jumatano kabla ya kusaini wake na klabu hiyo.

Inakisiwa kuwa AC Milan imemsajili mchezaji huyo kwa kitita cha pauni milioni 20.

Awali Manchester City ilianzisha mazungumzo na vilabu vya AC Milan na Juventus kuhusu uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wake Mario Balotelli, na ripoti zinasema kuwa, Balotelli atauzwa ikiwa vilabu hivyo vitaweza kulipa fedha wanazo taka.

Klabu hiyo imesema mchezji huyo mwenye umri wa miaka 22, anakisiwa kugharibu pauni milioni ishirini na moja mbali na fedha zingine za ziada.

Balotelli hana haraka ya kuuzwa na Manchester City imesema haina mipango ya kupunguza mshahara wake ili aondoke.

Kinyume na matarajio ya wengi Balotelli amesafiri na wachezaji wa Manchester City watakaocheza na QPR katika mechi ya ligi kuu ya premir leo usiku.

Milan ilianzisha mazungumzo na Man City, kuhusu mchezaji huyo kutoka Italia na kuna ripoti kuwa klabu ya Juventus vile vile imewasilisha ombi la kutka kumsajili Balotelli, ambaye alijiunga na Manchester City Agosti mwaka wa 2010 kwa kitita cha pauni milioni 24.

 Mario Baruah Balotelli


Swaga za kitaani

Mapema siku ya Jumatatu, naibu kocha mkuu wa Man City, David Platt, alisema kuwa Balotelli hatajiunga na AC Millan mwezi huu.

Siku ya Ijumaa wiki iliyopita, kocha wa Man City Roberto Mancini, alikariri hana nia ya kumuuza kuwa mchezaji huyo kutoka Italia.

Balotelli ambaye amefunga goli moja baada ya kucheza mechi kumi na nne msimu huu, amekumba na kashfa nyingi tangu aliposajiliwa.

Tukio la hivi karibuni, likiwa mzozo kati yake na Mancini katika uwanja wao wa mazoezi mwanzo wa mwezi huu.

Makamu wa rais wa AC Milan Adriano Galliani amesema ikiwa Manchester City itapunguza bei ya mchezaji huyo, basi huenda wakamsajili.