Thursday, February 21, 2013

AC MILAN YAITEPETESHA BARCELONA 2-0

Timu ngumu ya Barcelona ya Uhispania jana ilitepeteshwa na vigogo wa soka wa Italia AC Milan kwa bakora 2 kwa buyu katika dimba la San Siro, huku mtanange huo ukishuhudiwa na mashabiki 75,000 akiwemo Mario Balotelli na mchumba wake pamoja na masela kibao.

Mtanange huo ulitawaliwa na Barcelona lakini walishindwa kabisa kuipenya ngome ya AC Milan waliokuwa wanalinda lango lao na kufanya mashambulizi ya kushtukiza na ya kasi. AC Milan walianza kuwazidi akili Barcelona katika dk 56 pale mzaliwa wa Ghana Kevin Prince-Boateng alipotupia kambani goli la kuongoza na kulipua nderemo na vifijo toka kwa mashabiki9 waliofurika katika dimba la San Siro.

Barcelona walihaha kusawazisha goli bila mafanikio kabla ya kutepeteshwa kwa bao la pili katika dk 80 likitupiwa kambani na Raia wa Ghana Suley Muntari.

Mchezaji mtukutu aliesajiliwa hivi karibuni na AC Milan akitokea Manchester City ambae nae pia ni mchezaji mwenye asili ya Ghana Mario Barwuah Balotelli alionekana uwanjani akiwa na mchumba wake na kundi la masela wakishangilia ushindi wa AC Milan kwa hisia kali.

Boateng na Muntari wakishangilia goli la kwanza

Nimeuaaaaaaaaaaaaaaaaa

Kazi kweli kweli Iniesta na Boateng

Mungu wangu tumetepeteshwa namna hii...

Messi akijaribu kuchanja mbuga

Kamata mwizi meeeeeeeeeeeeen!! Boateng akijaribu kumchimoka Puyol

Kulala kwenuu..Messi na Alves wakiwa chini kufuatia patashika nguo kuchanika ya mpambano huo

Muntari akiachia kombora kuandika bao la pili dk 80

Muntari na Boateng wakishangilia goli la pili
 


Balotelli na mchumba wake wakifuatilia mpambano

Wednesday, February 20, 2013

BAYERN YAISULUBU ARSENAL

Timu ya soka ya Bayern Munich ya Ujerumani imeisulubu Arsenal ya Uingereza katika mpambano wa kwanza wa klabu bingwa ya Ulaya katikla dimba la Emirates huku mashabiki wapatao 59,974 wakishuhudia fedheha ya kichapo cha mabao 3-1.

Magoli ya Bayern yalifungwa na Kroos dk 6 kabla Thomas Muller kuongeza la pili dk 20 mpaka mapumziko magbao yalikuwa 2-0. Kipindi cha pili kama Arsenal waliamka vile lakini waaap pamoja na kupata bao la kufutia machozi katika dk 54 lililotupiwa na Podolski kwa kichwa baada ya kipa wa Bayern kufanya makosa katika kudaka mpira wa kona, na dk 76 Mandzukic alipeleka kilio London kwa kutupia kamba ya tatu.


Kroos akifunga goli la kwanza


Muller akitupia la pili

Mandzukic akitupia la tatu

Wilshere na Shwerzteinger

Twendeni tumeshapigwa

Pole mzee wenger unayataka mwenyewe nyoooooo!
ARSENAL 1-3 BAYERN MUNICH

Monday, February 11, 2013

NIGERIA MABINGWA AFRIKA

Timu ya soka ya Taifa ya Nigeria imetawazwa kuwa mabingwa wapya wa Afrika baada ya kuichabanga Burkina Faso kwa bao 1-0  katika mchezo wa Fainali katika dimba la Soccer City mpambano ukihudhuriwa na mashabiki wapatao 85,000.
 Goli pekee na la ushindi lilifungwa na Sunday Mba katika dk 39.

Wachezaji wa Nigeria wakishangilia goli lililofungwa na Sunday Mba.








Thursday, February 7, 2013

MATOKEO MECHI ZA KIRAFIKI ZA KIMATAIFA

KIMATAIFA | MATOKEO


06 February
Honduras2 -  1   USA
06 February
Portugal2 - 3   Ecuador
06 February
France1 - 2   Germany
06 February
Republic of Ireland  2 - 0  Poland
06 February
Wales2 - 1   Austria
06 February
Belgium2 - 1   Slovakia
06 February
Scotland1 - 0   Estonia
06 February
Romania3 - 2    Australia
06 February
England2 - 1    Brazil
06 February
Greece0 - 0  Switzerland
06 February
Sweden2 - 3   Argentina
06 February
Netherlands1 - 1   Italy
06 February
Iceland0 - 2   Russia
06 February
Macedonia3 - 0  Denmark
06 February
Malta0 - 0  Northern Ireland
06 February
Turkey0 - 2  Czech Republic
06 February
Albania1 - 2    Georgia
06 February
Spain3 - 1   Uruguay
06 February
Israel2 - 1   Finland
06 February
Chile2 - 1    Egypt
06 February
Cyprus1 - 3   Serbia
 
06 February
Slovenia0 - 3   Bosnia-Herzegovina
06 February
Norway0 - 2  Ukraine
06 February
Hungary1 - 1  Belarus
06 February
Moldova1 - 3  Kazakhstan
06 February
Tanzania1 - 0  Cameroon
06 February
Azerbaijan1 - 0   Liechtenstein
06 February
Croatia4 - 0   Korea Republic
06 February
Rwanda2 - 2  Uganda
06 February
Kenya3 - 0   Libya
06 February
Zimbabwe2 - 1  Botswana
06 February
India2 - 4  Palestine
06 February
Japan3 - 0  Latvia
05 February
Luxembourg   1 - 1  Armenia
05 February
Senegal1 - 1  Guinea
02 February
Poland4 - 1   Romania

TANZANIA,UINGEREZA ZAFANYA KWELI ZAZIBANGUA CAMEROON NA BRAZIL

TAIFA Stars jana ilifanya kile kilichosubiriwa na mashabiki wa soka Tanzania baada ya kuitia ‘adabu’ Cameroon kwa kuichapa bao 1-0 katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa, shukrani kwa bao la ‘jioni’ kutoka kwa mshambuliaji wa kimataifa Mbwana Samata.

Samata anayecheza soka la kulipwa TP Mazembe ya DRC, alifunga bao hilo muhimu kwenye Uwanja wa Taifa dakika ya 89 baada ya kuusukumiza wavuni kirahisi mpira wa krosi ya Frank Domayo uliompita kipa wa Cameroon, Offala Komguep.

Bao la Samata lilikuja baada ya Stars inayoshika nafasi ya 124 kwa ubora wa viwango vya soka kufanya mashambulizi yasiyo na idadi lango kwa Cameroon.
Dakika 20 za mwisho wa kipindi cha kwanza, Cameroon haikuwa mchezo na badala yake jezi za rangi ya bluu ndizo zilizokuwa zikimili mpira.

Ni ushindi wa kwanza kwa Stars dhidi ya Cameroon, kwani matokeo mazuri waliyowahi kupata ni sare moja ya bila kufungana kwenye uwanja huohuo, na kisha kukubali kipigo cha mabao 2-1 nchini Cameroon.
Stars wangeweza kupata bao la kuongoza kipindi cha kwanza kama siyo beki Erasto Nyoni kushindwa kufunga penalti iliyochezwa na kipa.
Mechi hiyo ilianza taratibu na dakika 10 za kwanza zilionekana kama za wachezaji wa pande zote kusomana kimchezo.

Wenyeji Stars walitumia mfumo wa kushambulia pamoja na kukaba kwa pamoja kama alivyosema Kocha Poulsen kabla ya mchezo huo.
Cameroon, mabingwa wa zamani wa Mataifa ya Afrika, hawakuonekana kuwa wakali kama ambavyo mashabiki wengi waliojitokeza kushuhudia mchezo huo walitarajia.

Erasto Nyoni akijaribu kumtoka mlinzi wa Cameroon

Stars ikitumia mfumo wa 4-3-3, ilicheza vizuri kipindi cha kwanza, lakini hata hivyo Cameroon ndiyo walitawala mchezo, huku wakitumia mfumo wa 4-3-4.
Dakika ya 19, mpira ulisimama kwa muda baada ya kipa wa Stars Juma Kaseja kuumia kufuatia kugongana na Tchami Herve wa Cameroon.

Mabeki wa Stars,Aggrey Morris na Kelvin Yondan walifanya kazi ya ziada kuwazuia washambuliaji wa Cameroon sehemu kubwa ya kipindi cha kwanza.

Cameroon waliokuwa wakicheza bila nahodha Samuel Eto’o walikaribia kufunga bao katika dakika ya 24, baada ya Aboubakar Vincent kupiga kiki iliyotoka nje kidogo la lango la Stars. Nyoni angeweza kubadilisha ubao wa matokeo, kama siyo kushindwa kutumbukiza wavuni kiki ya penalti dakika ya 26 iliyotolewa na mwamuzi kutokana na Ngoula kuucheza mpira kwa mkono ndani ya eneo la hatari. Beki huyo wa Stars alikwenda kupiga penalti hiyo akionekana kutojiamini kabla ya shuti lake kupanguliwa na kipa Effala. Kipindi cha pili Stars ilicheza kwa nguvu na hapana shaka ndiyo walitawala sehemu kubwa, wakifanya mashambulizi mara kwa mara.



Ngasa aliyeisumbua zaidi ngome ya Cameroon alimjaribu kwa shuti la mwendo mrefu kipa Offala ambaye alifanya kazi nzuri ya kulizuia.
Kiungo chipukizi Abubakary naye alikaribia kufunga kwa Stars kama siyo shuti lake kuchezwa na kipa wa cameroon ambaye sehemu kubwa ya kipindi cha pili hakupumzika kuokoa hatari
.
Pamoja na kufanya mabadiliko mengi kipindi cha pili, Stars waliendelea kutawala mchezo na kuwafunika Cameroon sehemu ya kiungo.

Katika mchezo huo, Stars ilifanya mabadiliko kwa kumtoa Mwinyi na kuingia Thomas Ulimwengu ambaye aliongeza nguvu ya mashambulizi.

Kipa wa Cameroon Efalla akiondosha hatari langoni mwake


Patashika kwenye lango la Cameroon

Mbwana Samatta akionesha udambwidambwi wake

Samattaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa goooooooooooollll

Mbwana Samatta akishangilia goli

Uingereza yaichapa Brazil
Katika mchezo mwingine uliochezwa huko duniani kati ya Uingereza na Brazil uliopigwa katika dimba la Wembley mashabiki wa soka wameshuhudia Uingereza ikiishushia kisago Brazil cha bao 2-1.
Goli la kwanza la Uingereza lilitupiwa kambani na Wayne Rooney baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Jack Wilshere na Theo Walcott na mpira kumkuta Rooney nae bila ajizi akatupia kambani.
Katika mchezo huo Brazil walioonekana kuzidiwa sehemu ya katikati ambapo wachezaji kama Wilshere,Walcott na Cleverly walionekana kuwasumbua wabrazil sehemu ya katikati. na kuwafanya kina Ronaldhino Gaucho na Oscar kushindwa kufurukuta.

Ronaldhino alikosa penati katika mchezo huo iliyookolewa kitaalamu na kipa Joe Hart, Goli la kusawazisha la Brazil lilitupiwa kambani na Adriano kabla Frank Lampard hajatupia goli la pili na la ushindi kwa Uingereza.
Ronaldhino akicontrol mpira mbele ya Rooney


Rooney na wachezaji wenzake wakishangilia goli

Jack Wilshere akichanja mbuga

Mshikemshike Wilshere na Oscar 

Ronaldinho akijaribu kumalizia mpira wa penati uliiokolewa na Joe Hart bila mafanikio

Lampard akishangilia goli

Neymar chini ya ulinzi wa Gary Cahill

Mashabiki wa England
England 2-1 Brazil