Tuesday, March 26, 2013

WEMA WA WEMA WAMRUDISHA KAJALA URAIANI


Kajala akimkumbatia Wema Sepetu kwa machozi ya furaha baada ya kumtolea faini ya milioni 13 na kumuepusha na kifungo cha miaka 8 jela baada ya kupatikana na hatia ya kula njama ya kubadilisha umiliki wa nyumba na kosa jingine la kushiriki kusafisha pesa chafu ambacho ni kinyume cha sheria.


Kajala na Wema nje ya mahakama.

Kajala akiwa na Lulu akizungumza na waandishi wa habari.

Kajala na Dk Cheni nje ya mahakama baada ya hukumu.


Thursday, February 21, 2013

AC MILAN YAITEPETESHA BARCELONA 2-0

Timu ngumu ya Barcelona ya Uhispania jana ilitepeteshwa na vigogo wa soka wa Italia AC Milan kwa bakora 2 kwa buyu katika dimba la San Siro, huku mtanange huo ukishuhudiwa na mashabiki 75,000 akiwemo Mario Balotelli na mchumba wake pamoja na masela kibao.

Mtanange huo ulitawaliwa na Barcelona lakini walishindwa kabisa kuipenya ngome ya AC Milan waliokuwa wanalinda lango lao na kufanya mashambulizi ya kushtukiza na ya kasi. AC Milan walianza kuwazidi akili Barcelona katika dk 56 pale mzaliwa wa Ghana Kevin Prince-Boateng alipotupia kambani goli la kuongoza na kulipua nderemo na vifijo toka kwa mashabiki9 waliofurika katika dimba la San Siro.

Barcelona walihaha kusawazisha goli bila mafanikio kabla ya kutepeteshwa kwa bao la pili katika dk 80 likitupiwa kambani na Raia wa Ghana Suley Muntari.

Mchezaji mtukutu aliesajiliwa hivi karibuni na AC Milan akitokea Manchester City ambae nae pia ni mchezaji mwenye asili ya Ghana Mario Barwuah Balotelli alionekana uwanjani akiwa na mchumba wake na kundi la masela wakishangilia ushindi wa AC Milan kwa hisia kali.

Boateng na Muntari wakishangilia goli la kwanza

Nimeuaaaaaaaaaaaaaaaaa

Kazi kweli kweli Iniesta na Boateng

Mungu wangu tumetepeteshwa namna hii...

Messi akijaribu kuchanja mbuga

Kamata mwizi meeeeeeeeeeeeen!! Boateng akijaribu kumchimoka Puyol

Kulala kwenuu..Messi na Alves wakiwa chini kufuatia patashika nguo kuchanika ya mpambano huo

Muntari akiachia kombora kuandika bao la pili dk 80

Muntari na Boateng wakishangilia goli la pili
 


Balotelli na mchumba wake wakifuatilia mpambano

Wednesday, February 20, 2013

BAYERN YAISULUBU ARSENAL

Timu ya soka ya Bayern Munich ya Ujerumani imeisulubu Arsenal ya Uingereza katika mpambano wa kwanza wa klabu bingwa ya Ulaya katikla dimba la Emirates huku mashabiki wapatao 59,974 wakishuhudia fedheha ya kichapo cha mabao 3-1.

Magoli ya Bayern yalifungwa na Kroos dk 6 kabla Thomas Muller kuongeza la pili dk 20 mpaka mapumziko magbao yalikuwa 2-0. Kipindi cha pili kama Arsenal waliamka vile lakini waaap pamoja na kupata bao la kufutia machozi katika dk 54 lililotupiwa na Podolski kwa kichwa baada ya kipa wa Bayern kufanya makosa katika kudaka mpira wa kona, na dk 76 Mandzukic alipeleka kilio London kwa kutupia kamba ya tatu.


Kroos akifunga goli la kwanza


Muller akitupia la pili

Mandzukic akitupia la tatu

Wilshere na Shwerzteinger

Twendeni tumeshapigwa

Pole mzee wenger unayataka mwenyewe nyoooooo!
ARSENAL 1-3 BAYERN MUNICH

Monday, February 11, 2013

NIGERIA MABINGWA AFRIKA

Timu ya soka ya Taifa ya Nigeria imetawazwa kuwa mabingwa wapya wa Afrika baada ya kuichabanga Burkina Faso kwa bao 1-0  katika mchezo wa Fainali katika dimba la Soccer City mpambano ukihudhuriwa na mashabiki wapatao 85,000.
 Goli pekee na la ushindi lilifungwa na Sunday Mba katika dk 39.

Wachezaji wa Nigeria wakishangilia goli lililofungwa na Sunday Mba.








Thursday, February 7, 2013

MATOKEO MECHI ZA KIRAFIKI ZA KIMATAIFA

KIMATAIFA | MATOKEO


06 February
Honduras2 -  1   USA
06 February
Portugal2 - 3   Ecuador
06 February
France1 - 2   Germany
06 February
Republic of Ireland  2 - 0  Poland
06 February
Wales2 - 1   Austria
06 February
Belgium2 - 1   Slovakia
06 February
Scotland1 - 0   Estonia
06 February
Romania3 - 2    Australia
06 February
England2 - 1    Brazil
06 February
Greece0 - 0  Switzerland
06 February
Sweden2 - 3   Argentina
06 February
Netherlands1 - 1   Italy
06 February
Iceland0 - 2   Russia
06 February
Macedonia3 - 0  Denmark
06 February
Malta0 - 0  Northern Ireland
06 February
Turkey0 - 2  Czech Republic
06 February
Albania1 - 2    Georgia
06 February
Spain3 - 1   Uruguay
06 February
Israel2 - 1   Finland
06 February
Chile2 - 1    Egypt
06 February
Cyprus1 - 3   Serbia
 
06 February
Slovenia0 - 3   Bosnia-Herzegovina
06 February
Norway0 - 2  Ukraine
06 February
Hungary1 - 1  Belarus
06 February
Moldova1 - 3  Kazakhstan
06 February
Tanzania1 - 0  Cameroon
06 February
Azerbaijan1 - 0   Liechtenstein
06 February
Croatia4 - 0   Korea Republic
06 February
Rwanda2 - 2  Uganda
06 February
Kenya3 - 0   Libya
06 February
Zimbabwe2 - 1  Botswana
06 February
India2 - 4  Palestine
06 February
Japan3 - 0  Latvia
05 February
Luxembourg   1 - 1  Armenia
05 February
Senegal1 - 1  Guinea
02 February
Poland4 - 1   Romania