Wednesday, August 28, 2013

BURUDANI YA LEO-KUKERE DANCE

SIMBA YATAKATA YANGA YAVUTWA SHATI NA COASTAL UNION

Kikosi cha Yanga

Ligi kuu Tanzania bara imeendelea tena leo, Watani wa wajadi wakishuka katika viwanja tofauti kuwania pointi tatu muhimu. Yanga walikuwa katika dimba kuu la Taifa wakikipiga na Coastal Union ya Tanga,katika mpambano huo timu zote zilitoka sare ya 1-1 baada ya dakika 90 kumalizika.
Yanga walikuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 15 likitupiwa kambani na Jerryson Tegete na Coastal walijitoa kimasomaso kwa kuchomoa katika dakika ya 16 na Abdi Banda.

Simba walikipiga na JKT Oljoro na kuibuka na ushindi wa bao 1-0 bao likitupiwa kambani na Chanongo.

Tuesday, August 27, 2013

PATA BURUDANI-VIDEO YA STEVE R&B (RADIO)

MSHINDI WA BIGBROTHER AFRICA 2013 DILISH WA NAMIBIA AKIMWAGA RADHI



Mshindi wa Bigbrother africa 2013 Dilish akioga bila chenga. Dilish kutoka Namibia amefanikiwa kuibuka kidedea katika kinyang'anyiro hicho kilichodumu kwa siku 90 na kuondoka na kitita cha dola 300,000. usipimee....

Dilish

MAN U CHELSEA ZATOSHANA NGUVU

Man Utd & Chelsea fail to find breakthrough
Rooney akijaribu kumhadaa Lampard katika mtanange huo
Rooney akijaribu kufunga bia mafanikio.

Klabu za Chelsea na Manchester United zimeminyana uwanjani Old Trafford. Pande zote mbili zimekosa kufunga bao, na hivyo kutoka sare ya bila kwa bila.
Matokeo hayo yanamaanisha kwamba mabingwa wa ligi kuu ya Uingereza, wote wamepoteza pointi katika siku kumi na sita za kwanza wa msimu huu, na zinaifuata Manchester City iliyopoteza pointi pia kufuatia mechi dhidi ya Cardiff.
Meneja wa Chelsea Jose Mourinho aliiambia BBC Sport " Hakuna Upande uliostahili kushinda na kushindwa vile vile, unataka kushinda lakini pande zote zilikua na ulinzi mkali. Na kwa mashabiki najua angalau bao moja lingewafurahisha, iwapo ungekuwa mchuano mzuri''.
Naye meneja wa Manchester United, David Moyes alisema, alivunjika moyo kwa sababu hawakuzoa pointi yoyote, lakini ndivyo ilivyo na hawana budi kujifunza kutokana na hali hiyo.
Chelsea kwa sasa inaongoza ligi kuu kwa pointi saba, ikifuatwa kwa karibu sana na Liverpool na Tottenham, zote zikiwa na pointi sita. Machester United inashikilia nafasi ya nne ikiwa na pointi nne.

Wednesday, August 14, 2013

HAPPY BIRTHDAY ENNA

Leo ni siku nzuri ya kuzaliwa mtoto wa rafiki yangu mpenzi Maria Kitenge. Enna ambaye pia ni kipenzi changu "mchumba" alizaliwa mwezi na tarehe kama ya leo. Yangu machache kwake ni haya;


Monday, August 12, 2013

MAN U YATWAA NGAO YA HISANI, MOYES AUANZA MSIMU VYEMA

Timu ya soka ya Manchester United ya Uingereza imetwaa ngao ya hisani ikiwa ni ishara ya ufunguzi mwema wa msimu huu kwa kuitandika timu ya Wigan kwa bakora 2-0 katika dimba la Wembley.
Ushindi huo ni wa kwanza kwa kocha mpya wa Man U Moyes ambaye amepokea mikoba ya aliekuwa kocha wa Man U kwa miaka mingi Sir Alex Furguson , na hii ni kiashirio kizuri kwa Moyes.
Katika mpambano huo wa Ngao ya hisani sio mwingine alieipatia ushindi Man U bali ni ile ile LULU waliyoiokota Emirates,Robin Van Persie aliepachika mabao yote mawili katika mpambano huo.
 
Umati wa mashabiki ukielekea katika dimba la Wembley kushuhudia mpambano wa ngao ya hisani kati ya Man UNITED na Wigan Athletics.
 
Man U 2-0 wIGAN

Van Persie akipiga kichwa kutupia bao la kwanza la Man United.
 
Van Persie akijaribu kuwatoka walinzi wa Wigan Athletic

Van Persie na wenzake wakishangilia goli

Kocha wa Man United David Moyes akifurahia ngao ya hisani

Robin Van Persie akiwa na furaha tele baada ya kuiwezesha Man U kutwaa ngao ya hisani