Wednesday, April 2, 2014

ROBO FAINALI UEFA MAN UTD YAIDINDIA BAYERN OT, ATLETICO YAIVIMBIA BARCELONA

 
 
Vidic akiifungia Manchester bao dhidi ya Bayern
  
Tulia weweeeeee

Kulikuwa na mechi mbili za mkondo wa kwanza wa robo fainali ya ligi kuu ya mabingwa barani Ulaya iliyochezwa Jumanne usiku, Manchester United ya Uingereza ikikabana koo na mabingwa watetezi waligi hiyo Bayern Munich ya Ujerumani.
Nayo Barcelona ya Uhispania ikikabiliana na Athletico Madrid vilevile ya Uhispania.

 
Wachezaji wa Man U wakishangilia bao

Licha ya kuwa Bayern Munich ilikuwa imepigiwa upatu kutamba dhidi ya Manchester United vijana wa pep Gardiola walikabiliwa na ukuta mrefu wa Manchester uwanjani Old Traford.
Na walipopata fursa nahodha wa Manchester Nemanja Vidic alifunga bao maridadi la kichwa baada ya kuunganisha vizuri kona kutoka kwa Wayne Rooney kunako dakika ya 58 ya kipindi cha pili.

Gonga gonga ya Wajerumani ilikosa kuzaa matunda lakini bao la Bastian Schweinsteiger kunako dakika ya 66 iliwatunuku mabingwa hao wao watetezi bao muhimu la ugenini kabla ya mkondo wa pili utakaochezwa huko Ujerumani .
Bila shaka mashabiki na watani wa kocha David Moyes watakubaliana naye kuwa United itajutia fursa aliopoteza Danny Welbeck alipokuwa ni yeye pekee dhidi ya kipa wa Bayern Manuel Neuer .

United vilevile itamshukuru kipa David de Gea aliyefanya kazi ya ziada kuzuia mashambulizi haswa kutoka kwa Arjen Robben.
Kutokana na sare hiyo sasa mkufunzi Pep Guardiola ana kibarua kigumu pale Man United itakapozuru uwanja wa Allianz Arena wiki ijayo.
Mechi nyingine 2 zimeratibiwa kuchezwa baadaye Jumatano, Real Madrid ya Uhispania ikivaana na Borussia Dortmund kutoka Ujerumani nayo Paris st Germain ikiikaribisha wawakilishi wengine wa Uingereza Chelsea ya Uingereza Katika uwanja wa Parc des Princes. 


ATLETICO YAIVIMBIA BARCA
 
Messi akijaribu kumhadaa Gabi

Messi akikokota kijiji

Vita vya mahasimu wa nyumbani Atletico Madrid na Barcelona viliishia sare ya nne msimu huu timu hizo mbili za Uhispania zilipotoka sare ya moa kwa moja katika mkondo wa kwanza wa
ligi kuu ya mabingwa barani Ulaya iliyochezwa katika uwanja wa Camp nou.
Atletico inayoongoza katika dimba la nyumbani ya la Liga sasa imejipatia bao muhimu la ugenini licha ya kuwa ilifuzu kuingia katika robo fainali hizo kwa mara ya kwanza tangu mwaka wa 1997.
Licha ya barcelona kupigiwa upatu kushinda taji hilo ni Atletico iliyofunga ya kwanza kupitia kwa kiungo Diego aliyekuwa ameingia kuchukua nafasi yake Diego Costa aliyelazimika kuondolewa uwanjani 
 

 
Neymar akishangilia goli

baada ya kupata jeraha katika dakika ya 30.
Barca ilijifurukuta na kufunga baada ya Andre Iniesta kupenyeza pasi safi katikati ya ulinzi mkali wa Atletico iliyopokelewa na Neymar aliyesawazisha zikiwa zimesalia dakika 20 mechi hiyo kukamilika.
Juhudi za Barcelona za kutafuta bao la Ushindi ziliambulia patupu ngome ya ulinzi ya Atletico ilipoimarishwa na mambo yakasalia kuwa sare .
Athletico inaongoza ligi ya nyumbani kwa alama moja zaidi ya Barca.

Wednesday, March 26, 2014

SHABIKI WA MAN U AKIMPA ''MAKAVU LIVE'' DAVID MOYES


Hii ilikuwa katika mechi dhidi ya Man City..shabiki uzalendo ulipomshinda na kuanza kumporomoshea mitus kocha wa Man United 'The Chosen One'' David Moyes.

MAN UNITED MDEBWEDO YANYOLEWA 3 NA CITY

 
 

 Edwin Dzeko akishangilia


Manchester City iliendelea kujiimarisha na kuikosesha amani klabu ya Manchester United katika ligi kuu ya premier.
Sio hilo tu bali Man City wanaongeza shinikizo kali kwa Chelsea walio juu kwenye jedwali la ponti katika ligi hiyo.
Man Uinted walipata kichapo cha mbwa cha mabao matatu bila nyumbani Old Trafford.
Edin Dzeko alitupia mabao mawili katika kila kipindi kwa City hapo jana huku Yaya Toure akizidisha machungu kwa bao la tatu mwishoni mwa mechi bila jibu kutoka kwa Man United.
Sasa vijana hao wa City wanashikilia nafasi ya pili nyuma ya Chelsea.

 
Kocha wa United Moyes akilia kwa uchungu


 Kambaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

 
Hapa kazi tuu

Fellaini akijaribu kumwaga majaro

Niache bhanaaaa mbona shoboo

 
MAN UTD 0-3 MAN CITY

Friday, March 21, 2014

Affiliate Program ”Get Money from your Website”

REAL MADRID INAONGOZA KUNYAKUA KOMBE LA UEFA CHAMPIONS LEAGUE

UEFA Champions League

Wakati draw ya kutafuta timu zitakazopambana katika hatua ya robo fainali ya UEFA itakayochezeshwa majira ya saa 8 mchana kwa saa za Afrika ya mashariki huko jijini Nyon,Switzerland. Real Madrid mpaka sasa inaongoza kwa kulibeba kombe hilo kwa kulinyakua mara 9. 
Ifuatayo ni orodha ya timu zilizokwisha jitishwa ndoo hiyo. Real Madrid (9), Bayern Munich (5), Barcelona (4), Manchester united (3), wakati Chelsea na Borussia Dortmund mara 1 kila moja.

  • Atletico Madrid imetinga robo fainali baada ya miaka 17 kwa kuichabanga AC Milan jumla ya mabao 5-1.
  • Kwa mwaka wa pili mfululizo Spain imeingiza timu nyingi katika hatua ya robo fainali ikifuatiwa na Uingereza 2,Ujerumani 2,France 1.
  •  
Baada ya draw kuchezeshwa leo mechi za robo fainali zitachezwa April 1 na 2. Marudio April 8 na 9.