Tuesday, April 29, 2014

ARSENAL YAISAMBARATISHA NEWCASTLE 3-0

Arsenal ya Uingereza ilijiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu kwa mchuano wa ligi ya mabingwa mwakani baada ya kuinyuka Newcastle mabao matatu kwa nunge katika mechi ya katikati ya juma iliyochezwa katika uwanja wao wa nyumbani wa Emirate.
 
Koscielny akitupia kambani bao la kwanza
 
 
Giroud akimpongeza Koscielny baada ya kufunga goli la kwanza

Ushindi huo umeiacha Arsenal na jumla ya alama 73 nne zaidi ya wapinzani wao wa karibu Everton wenye alama 69.
Laurent Koscielny ndiye aliweka niya ya 'the Gunners' bayana alipofunga mkwaju wa Santi Cazorla kunako dakika ya 26 ya kipindi cha kwanza . Mesut Ozil naye akaongezea la pili kabla ya kukamilika kipindi cha kwanza .
Hata hivyo ni Olivier Giroud ndiye aliyemhakikishia kocha Arsene Wenger alama tatu muhimu alipohitisha kichapo hicho kwa bao la tatu kunako dakika ya 66 ya mechi hiyo.
Aidha ilikuwa ni kichapo cha 6 mfululizo kwa timu ya Newcastle na kocha Alan Pardew .
Hata hivyo mbivu na mbichi itabainika Manchester City itakapokwaruzana na Everton jumamosi ijayo.
Timu nne za kwanza ndizo zinazoshiriki mchuano huo wenye kitita kikubwa zaidi barani.
Arsenal ilikuwa imedorora kutoka nafasi ya kwanza na ilikuwa na hatari ya kukosa kushiriki ligi hiyo.
 
Ozil akishangilia kutupia bao la pili


Mshikemshike kwenye lango la Newcastle


Refa nipe penatiiiiiiii
 
ARSENAL 3-0 NEWCASTLE


Monday, April 28, 2014

5 Things Single Men Are Looking for when Dating

 5 Things Single Men Are Looking for in a Woman When Dating
Most men ask: What do women want? Contrary to popular belief, we aren't all that complicated. In fact, most of my female counterparts just want to be loved by their partner. That includes being respected, adored, supported, and appreciated. Not so bad, is it?
Men, however, are said to be simple. But are they? Do men just want a good meal, good sex, and a beer, or is there more than meets the eye? I believe so. Here are five things single men are looking for in a woman when dating

 
1. That natural chemistry
You heard me right; men want chemistry as much as women do. They want to feel that "umph," that "it" factor that is often indescribable. You don't have to look like a model. They just have to feel that energy. You either got it as a couple or you don't. Oh, and chemistry has little to do with sex.

 
2. A woman who is confident
Strut in with your head held high and men will notice. Every man that I spoke with really appreciates a woman who is confident. They love a woman who knows who she is and is comfortable in her own skin. But don't confuse confidence with arrogance. Humility is best.



3. She's her authentic self
No matter who you are or what you do for a living, you must be yourself. Men can tell when women are trying too hard. Men love women who are genuine. Again, it shows that you are comfortable in your own skin. And that's super sexy.

 
4. You can dress up and dress down
Men are visual creatures. Of course they want to find you physically appealing. Put on a dress and look gorgeous. Put on jeans and a pony tail and still look stunning? Yup. Men are looking for women who can dress up and dress down. You don't have to put on the fake lashes for bed. Let your hair down and show him you are a natural beauty.

 
5. Assertiveness is sexy.
Society expects men to court women. And so do I. A man, however, also enjoys a woman who treats him from time to time. He also likes a woman who is assertive and tells him what she wants. Like one man said to me, "I want a girl that can check me from time to time." In other words, women should also wear the pants when needed. It truly is about balancing the feminine and masculine within. Because a feminine yet assertive woman is a sexy woman.

CHELSEA YAIVURUGA LIVERPOOL


Demba BA akifunga goli la kwanza.

Chelsea vijana wa darajani Stanford, jijini London, wamewanyamazisha vinara wa ligi kuu ya England, Liverpool baada ya kuwachakaza mabao 2-0 katika uwanja wao wa Anfield.

Liverpool ikiwa imeuanza mchezo huo kwa kasi na kwa dhamira ya kupata ushindi ilishuhudia jahazi lake likitota katika dakika ya 45 ya kipindi cha kwanza.


Ba akisujudu kuashiria kumtukuza muumba wake aliemuwezesha kutupia goli la kwanza



Jose Mourinho akishangilia ushindi

Alikuwa ni Demba Ba aliyeanza kupeleka kilio kwa majogoo wa Liverpool pale alipounasa mpira kufuatia nahodha wa Liverpool Steven Gerrard kuteleza na Ba kupata mwanya wa kumfunga kirahisi Mignolet.

Liverpool hawakukubali kusalimu amri kwa wageni,kwani waliendelea kupeleka mashumbulizi ya hatari langoni mwa wapinzani wao wakiishia kwa kosa kosa. Liverpool wanapigania ubingwa wa ligi kuu ya England kwa mara ya kwanza katika miaka 24 iliyopita.



Steven Gerrald haamini kilichotokea

Joe Allen na Luis Suarez walizidisha mashambulizi katika lango la Chelsea, kabla ya Willian aliyeingia kipindi cha pili kufunga bao la pili kwa timu yake ya Chelsea baada ya Fernando Torres bila uchoyo akiwa katika nafasi ya kufunga alimpasia Willian na kuwaachia kilio wenyeji wao Liverpool.

Chelsea katika mchezo huo ilikuwa ikipewa nafasi finyu ya kuibuka washindi. Lakini ni Jose Mourinho aliyeibuka na kicheko, huku Brendan Rodgers akiugulia kipigo cha kwanza kwa timu yake tangu kuanza kwa mwaka huu.

Kwa ushindi huo sasa, Chelsea inaachwa pointi mbili nyuma ya Liverpool ambayo inaoongoza ikiwa na pointi 80, baada ya michezo 36. Msimamo wa timu hizo ni Liverpool pointi 80, Chelsea 78, Manchester City 74, itakuwa na pointi 77 iwapo itaifunga Crystal Palace katika mchezo wao, huku Arsenal ikichukua nafasi ya nne ikiwa na pointi 70. Manchester City na Arsenal zimecheza mechi 35 kila moja huku Liverpool na Chelsea zikiwa zimecheza mchezo mmoja zaidi.


Luis Suarez chini ya ulinzi mkali


Heka heka langoni mwa Chelsea





Mashabiki chipukizi wa Liverpool hawaamini wanachokiona uwanjani


Wanaume kazini........Willian na Allen

 

 
LIVERPOOL 0-2 CHELSEA


Thursday, April 17, 2014

MELI YA WATU 400 ILIYOZAMA KOREA YA KUSINI MAWIMBI YAKWAMISHA UOKOZI

Mawimbi makali na hali mbaya ya hewa baharini imetatiza juhudi za utafutaji na uokoaji wa takriban watu mia tatu baada ya feri ya abiria kuzama katika pwani ya Korea Kusini.
Watu tisa wamethibitishwa kuaga dunia katika mkasa huo.
 
Wengi wa abiria kwenye meli hiyo walikuwa ni wanafunzi wa shule ya upili. Takriban watu mia moja sabini wameokolewa. Kapteni wa jeshi la wanamaji la Marekani Heidi C. Agle anashiriki katika operesheni ya uokoaji.
Ameiambia BBC kuwa maandalizi yanafanywa kupeleka mtambo wa kuinua chombo hicho.
Wakati huohuo Rais Park Geun-hye, amewataka waokozi kuharakisha juhudi zao za kuwatafuta manusura wa ajali hiyo.
Rais Park -- ambaye amejionea meli hiyo mwenyewe, amesema kuwa kila dakika ni muhimu katika kuhakikisha kuwa manusura wanapatikana.
Wapiga mbizi wamekuwa wakikabiliana na mawimbi makali kujaribu kukifikia chombo hicho kilichozama hapo jana.
 
Duru zinasema kuwa meli hiyo ilipoteza mwelekeo huku baadhi ya familia za waathriwa zikihoji mwenendo wa nahodha wa meli.
Hata hivyo nahodha huyo Lee Joon-seok aliomba msamaha na kusema ana majuto tele na kuwa hata hajui la kusema.
Dauru zinseama kuwa miongoni mwa wliofariki ni wanafunzi wanne wenye umri wa miaka 17 na mwaliamu wao mwenye umri wa miaka 25 pamoja na mfnyakazi mmoja wa meli hiyo.
Wengine wlaiofariki bado hawajatajwa.
Takwimu za hivi karibuni zinasema kuwa wtu 475 walikuwa kwenye meli hiyo huku 287 wakiwa bado hawajapatikana.
 












 


REAL MADRID YATWAA KOMBE LA MFALME..BARCELONA YELEEEEWIII

Timu ya Real Madrid Wamefanikiwa kutwaa kombe la Copa del Rey 2014/2015 .

Madrid waliwacharaza wapinzani wao wa jadi katika ligi ya nyumbani La liga Barcelona mabao 2 kwa 1 katika fainali iliyochezwa jana mbele ya mfalme wa Uhispania .
Kocha wa Madrid Carlo Ancelotti alikuwa anajikuna kichwa kwani mshambulizi wake nyota Cristiano Ronaldo hakuwa uwanjani kutokana na jeraha la mguu na hivyo ikambidi kumchezesha mshambulizi aliyegharimu kitita kikubwa
zaidi msimu huu Gareth Bale .
Na alidhibitisha udedea wake alipofuma bao la ushindi zikiwa zimesalia dakika tano tu mechi hiyo kukamilika na hivyo kuisadia kutwaa taji lake la 19 la Kombe hilo la mfalme la Copa del rey.
Real Madrid ilidhibitisha niya yao mapema kwa bao la dakika ya 11 Angel Di Maria .

 
 
Bale akishangilia goli la pili lililoipa ubingwa Madrid
 

Modric akioneshana kazi na Iniesta

Lakini ikasawazishwa na bao la Bartra katikadakika ya 68 ya kipindi cha pili.
Bao la ushindi lilifungwa na Gareth Bale dakika tano tu kabla ya mechi hiyo kukamilika .
Bale alitimuka mbio na kumpiku mlinzi wa Barca Marc Bartra katikati ya kiwanja na akafululiza hadi akampiga chenga kipa machachari Jose Manuel Pinto na kuihakikishia Madrid ushindi.
Real Madrid bado iko mbioni kuwania kombe la ligi ya Uhispania, ambapo inashikilia nafasi ya pili na alama 79 alama tatu nyuma ya wakinzani wao Athletico Madrid.
Barcelona ambayo imekuwa ikishuhudia msururu wa matokeo yasiyo ya kuridhisha katika siku za hivi punde inafunga orodha ya tatu bora ikiwa na alama 78.
Madrid sasa inamuda wa kutoka kujiandaa kwa mechi ya nusu fainali ya kombe la mabingwa barani Ulaya dhidi ya mabingwa watetezi Bayern Munich ya Ujerumani.
Mechi nyingine ya nusu fainali ya kombe la mabingwa barani Ulaya itakuwa kati ya Chelsea ya Uingereza dhidi ya Atletico Madrid.
Nusu fainali hizo zitachezwa juma lijalo.
 
Ubabe na undava kama kawa kama dawa




Mwaka wa shetani..duuu hatuambilii chochote
 
BARCELONA 1-2 MADRID