Monday, May 12, 2014

MAN CITY VIDUME EPL......OOOPS THEY DID IT AGAIN


Mabingwa wapya wa Uingereza 2014-2015 Manchester City.

Vijana wa Manuel Pelligrini walitawazwa mabingwa katika siku ya mwisho ya ligi kuu ya Uingereza baada ya kuilaza West Ham mabao 2-0.

Samir Nasri nahodha Vincent Kompany ndio waliomhakikishia Pelleigrini alama tatu muhimu zilizotosha kuipiku Liverpool iliyomaliza katika nafasi ya pili alama 86 mbili nyuma ya City ambao wametwaa taji lao la pili katika kipindi cha miaka mitatu.
Umati uliojaa uwanjani Etihad ulimiminika uwanjani baada ya kipenga cha mwisho.
Kocha huyo kutoka Chile alifaidika na kichapo cha Liverpool mikononi mwa Chelsea na hivyo alihitaji sare ya aina yeyote kujihakikishia ushindi.
Mancity iliititima West ham 2-0 na kutamatisha msururu wa mechi tano bila ya kushindwa .
Pelligrini, atakumbukwa kwa kuirejesha kombe Etihad baada ya Roberto Mancini kupigwa kalamu kwa kushindwa kutetea taji msimu uliopita .
Kocha huyo mwenye miaka 60 anajivunia mabao 102.
Kwa upande wao Liverpool walisajili ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Newcastle United uwanjani Anfield.
 
Mashabiki wa Man City wakishuhudia timu yao ikitwaa ubingwa wa EPL.


Samir Nasri akitupia kuihakikishia Man City ubingwa.



Nahodha wa Man City Vicent Kompany akinyanyua juuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu kombe la ligi kuu ya uingereza 2014-2015




Kocha wa Man City Manuel Pellegrini akiwa amebeba kombe la ligi kuu Uingereza 2014-2015

Wachezaji wa Man City wakiwa wamembeba kocha wao Pellegrini baada ya kunyakua kombe la ligi kuu ya UIngereza

Wednesday, April 30, 2014

RONALDO AVUNJA REKODI YA KUTUPIA UEFA

 

CHRISTIANO RONALDO

Nyota wa Real Madrid ya Uhispania Cristiano Ronaldo amevunja rekodi ya Lionel Messi ya ufungaji mabao mengi zaidi katika ligi ya mabingwa barani Uropa alipoifungia timu yake mabao mawili na kuisaidia

kuichapa Bayern Munich mabao 4-0 katika nusu fainali jana usiku.

Mreno huyo mwenye umri wa miaka , 29,alifunga bao lake la 15 na 16 msimu huu katika uwanja wa Allianz Arena.

Kufuatia ushindi huo Real Madrid ilifuzu kwa fainali ya mchuano huo kwa jumla ya mabao 5-0.

Ronaldo sasa amefunga mabao 16 katika mechi kumi za ligi hiyo ya mabingwa Barani Ulaya mbili zaidi ya Lionel Messi wa Barcelona .

Rekodi hiyo ya mabao 14 ilikuwa ikishikiliwa kwa pamoja kati ya Messi (2011-12, Barcelona), Ruud van Nistelrooy (2002-03, Manchester United) na Jose Altafini (1962-63, AC Milan).

Kwa jumla Ronaldo amefunga mabao 67 katika ligi hiyo ya mabingwa barani ulaya sawa na Messi na ni mabao manne tu nyuma ya rekodi ya idadio kubwa zaidi ya mabao yaliyofungwa na mchezaji wa zamani wa Real na Schalke Raul.

 

REAL MADRID YABOMOA UKUTA WA BERLIN, YATINGA FAINALI UEFA

Vigogo wa ligi kuu ya Uhispania Real Madrid, wamekuwa timu ya kwanza kufuzu kwa fainali ya ligi ya mabingwa barani ulaya baada ya kuinyeshea Mabingwa watetezi wa kombe hilo Bayern Munich ya Ujerumani kwa mabao manne kwa nunge na hivyo kuibuka a ushindi mkubwa wa jumla ya mabao 5-0.

Sergio Ramos alifunga mabao mawili mapema katika kipindi cha kwanza cha mechi hiyo.

  

Ramos akitupia kambani goli la kwanza

Kabla ya nyota wa Ureno na mchezaji bora duniani Christiano Ronaldo kuihakikishia Madrid fainali yao ya kwanza tangu mwaka wa 2002 na mkwaju wa wa freekick.

Bao hilo lilikuwa lake la 16 katika ligi ya mabingwa barani Uropa.

Kwa Bayern, kichapo hicho kilikuwa ni kama wembe wa kutu kwao kwani mwaka uliopita Wajerumani hao waliifunga Barcelona 7-0 katika hatua ya nusu fainali kabla ya kuilaza Borussia Dortmund na kutwaa taji lao la tano barani ulaya.

Haijulikani kufikia sasa iwapo halmashauri inayoingoza klabu hiyo itachukua hatua yeyote dhidi ya kocha wa klabu hicho Pep Guardiola ambaye licha ya kuiongoza Barca kutwaa taji la Bundesliga ameshindwa kutetea hadhi ya klabu hiyo katika mchuano huu wenye kitita kikubwa zaidi.

 

Nimeuaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

 

Oyooooooo...Sergio Ramos akishangilia goli

Madrid sasa inasubiri kujua iwapo itachuana na Chelsea ya Uingereza chini ya ukufunzi wake aliyekuwa kocha wao Jose mourinho ama wapinzani wao wa mji wa Madrid , Athletico .

Mshambulizi wa Athletico Madrid Diego Costa alisema anatumai Chelsea hawata regesha basi kwenye lango lao ilhali watacheza mchezo yenye maarifa.

Timu hizo zilitoka sare tasa katika mkondo wa kwanza .

  

 

 

 

 
BAYERN MUNICH 0-4 REAL MADRID


Tuesday, April 29, 2014

ARSENAL YAISAMBARATISHA NEWCASTLE 3-0

Arsenal ya Uingereza ilijiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu kwa mchuano wa ligi ya mabingwa mwakani baada ya kuinyuka Newcastle mabao matatu kwa nunge katika mechi ya katikati ya juma iliyochezwa katika uwanja wao wa nyumbani wa Emirate.
 
Koscielny akitupia kambani bao la kwanza
 
 
Giroud akimpongeza Koscielny baada ya kufunga goli la kwanza

Ushindi huo umeiacha Arsenal na jumla ya alama 73 nne zaidi ya wapinzani wao wa karibu Everton wenye alama 69.
Laurent Koscielny ndiye aliweka niya ya 'the Gunners' bayana alipofunga mkwaju wa Santi Cazorla kunako dakika ya 26 ya kipindi cha kwanza . Mesut Ozil naye akaongezea la pili kabla ya kukamilika kipindi cha kwanza .
Hata hivyo ni Olivier Giroud ndiye aliyemhakikishia kocha Arsene Wenger alama tatu muhimu alipohitisha kichapo hicho kwa bao la tatu kunako dakika ya 66 ya mechi hiyo.
Aidha ilikuwa ni kichapo cha 6 mfululizo kwa timu ya Newcastle na kocha Alan Pardew .
Hata hivyo mbivu na mbichi itabainika Manchester City itakapokwaruzana na Everton jumamosi ijayo.
Timu nne za kwanza ndizo zinazoshiriki mchuano huo wenye kitita kikubwa zaidi barani.
Arsenal ilikuwa imedorora kutoka nafasi ya kwanza na ilikuwa na hatari ya kukosa kushiriki ligi hiyo.
 
Ozil akishangilia kutupia bao la pili


Mshikemshike kwenye lango la Newcastle


Refa nipe penatiiiiiiii
 
ARSENAL 3-0 NEWCASTLE


Monday, April 28, 2014

5 Things Single Men Are Looking for when Dating

 5 Things Single Men Are Looking for in a Woman When Dating
Most men ask: What do women want? Contrary to popular belief, we aren't all that complicated. In fact, most of my female counterparts just want to be loved by their partner. That includes being respected, adored, supported, and appreciated. Not so bad, is it?
Men, however, are said to be simple. But are they? Do men just want a good meal, good sex, and a beer, or is there more than meets the eye? I believe so. Here are five things single men are looking for in a woman when dating

 
1. That natural chemistry
You heard me right; men want chemistry as much as women do. They want to feel that "umph," that "it" factor that is often indescribable. You don't have to look like a model. They just have to feel that energy. You either got it as a couple or you don't. Oh, and chemistry has little to do with sex.

 
2. A woman who is confident
Strut in with your head held high and men will notice. Every man that I spoke with really appreciates a woman who is confident. They love a woman who knows who she is and is comfortable in her own skin. But don't confuse confidence with arrogance. Humility is best.



3. She's her authentic self
No matter who you are or what you do for a living, you must be yourself. Men can tell when women are trying too hard. Men love women who are genuine. Again, it shows that you are comfortable in your own skin. And that's super sexy.

 
4. You can dress up and dress down
Men are visual creatures. Of course they want to find you physically appealing. Put on a dress and look gorgeous. Put on jeans and a pony tail and still look stunning? Yup. Men are looking for women who can dress up and dress down. You don't have to put on the fake lashes for bed. Let your hair down and show him you are a natural beauty.

 
5. Assertiveness is sexy.
Society expects men to court women. And so do I. A man, however, also enjoys a woman who treats him from time to time. He also likes a woman who is assertive and tells him what she wants. Like one man said to me, "I want a girl that can check me from time to time." In other words, women should also wear the pants when needed. It truly is about balancing the feminine and masculine within. Because a feminine yet assertive woman is a sexy woman.

CHELSEA YAIVURUGA LIVERPOOL


Demba BA akifunga goli la kwanza.

Chelsea vijana wa darajani Stanford, jijini London, wamewanyamazisha vinara wa ligi kuu ya England, Liverpool baada ya kuwachakaza mabao 2-0 katika uwanja wao wa Anfield.

Liverpool ikiwa imeuanza mchezo huo kwa kasi na kwa dhamira ya kupata ushindi ilishuhudia jahazi lake likitota katika dakika ya 45 ya kipindi cha kwanza.


Ba akisujudu kuashiria kumtukuza muumba wake aliemuwezesha kutupia goli la kwanza



Jose Mourinho akishangilia ushindi

Alikuwa ni Demba Ba aliyeanza kupeleka kilio kwa majogoo wa Liverpool pale alipounasa mpira kufuatia nahodha wa Liverpool Steven Gerrard kuteleza na Ba kupata mwanya wa kumfunga kirahisi Mignolet.

Liverpool hawakukubali kusalimu amri kwa wageni,kwani waliendelea kupeleka mashumbulizi ya hatari langoni mwa wapinzani wao wakiishia kwa kosa kosa. Liverpool wanapigania ubingwa wa ligi kuu ya England kwa mara ya kwanza katika miaka 24 iliyopita.



Steven Gerrald haamini kilichotokea

Joe Allen na Luis Suarez walizidisha mashambulizi katika lango la Chelsea, kabla ya Willian aliyeingia kipindi cha pili kufunga bao la pili kwa timu yake ya Chelsea baada ya Fernando Torres bila uchoyo akiwa katika nafasi ya kufunga alimpasia Willian na kuwaachia kilio wenyeji wao Liverpool.

Chelsea katika mchezo huo ilikuwa ikipewa nafasi finyu ya kuibuka washindi. Lakini ni Jose Mourinho aliyeibuka na kicheko, huku Brendan Rodgers akiugulia kipigo cha kwanza kwa timu yake tangu kuanza kwa mwaka huu.

Kwa ushindi huo sasa, Chelsea inaachwa pointi mbili nyuma ya Liverpool ambayo inaoongoza ikiwa na pointi 80, baada ya michezo 36. Msimamo wa timu hizo ni Liverpool pointi 80, Chelsea 78, Manchester City 74, itakuwa na pointi 77 iwapo itaifunga Crystal Palace katika mchezo wao, huku Arsenal ikichukua nafasi ya nne ikiwa na pointi 70. Manchester City na Arsenal zimecheza mechi 35 kila moja huku Liverpool na Chelsea zikiwa zimecheza mchezo mmoja zaidi.


Luis Suarez chini ya ulinzi mkali


Heka heka langoni mwa Chelsea





Mashabiki chipukizi wa Liverpool hawaamini wanachokiona uwanjani


Wanaume kazini........Willian na Allen

 

 
LIVERPOOL 0-2 CHELSEA


Thursday, April 17, 2014

MELI YA WATU 400 ILIYOZAMA KOREA YA KUSINI MAWIMBI YAKWAMISHA UOKOZI

Mawimbi makali na hali mbaya ya hewa baharini imetatiza juhudi za utafutaji na uokoaji wa takriban watu mia tatu baada ya feri ya abiria kuzama katika pwani ya Korea Kusini.
Watu tisa wamethibitishwa kuaga dunia katika mkasa huo.
 
Wengi wa abiria kwenye meli hiyo walikuwa ni wanafunzi wa shule ya upili. Takriban watu mia moja sabini wameokolewa. Kapteni wa jeshi la wanamaji la Marekani Heidi C. Agle anashiriki katika operesheni ya uokoaji.
Ameiambia BBC kuwa maandalizi yanafanywa kupeleka mtambo wa kuinua chombo hicho.
Wakati huohuo Rais Park Geun-hye, amewataka waokozi kuharakisha juhudi zao za kuwatafuta manusura wa ajali hiyo.
Rais Park -- ambaye amejionea meli hiyo mwenyewe, amesema kuwa kila dakika ni muhimu katika kuhakikisha kuwa manusura wanapatikana.
Wapiga mbizi wamekuwa wakikabiliana na mawimbi makali kujaribu kukifikia chombo hicho kilichozama hapo jana.
 
Duru zinasema kuwa meli hiyo ilipoteza mwelekeo huku baadhi ya familia za waathriwa zikihoji mwenendo wa nahodha wa meli.
Hata hivyo nahodha huyo Lee Joon-seok aliomba msamaha na kusema ana majuto tele na kuwa hata hajui la kusema.
Dauru zinseama kuwa miongoni mwa wliofariki ni wanafunzi wanne wenye umri wa miaka 17 na mwaliamu wao mwenye umri wa miaka 25 pamoja na mfnyakazi mmoja wa meli hiyo.
Wengine wlaiofariki bado hawajatajwa.
Takwimu za hivi karibuni zinasema kuwa wtu 475 walikuwa kwenye meli hiyo huku 287 wakiwa bado hawajapatikana.