Tuesday, May 5, 2015


21:45 - 23:45
Italy
The UEFA Champions LeagueJuventus vs Real Madrid

ARSENAL KUMILIKIWA NA TAJIRI WA AFRIKA


Aliko Dangote tajiri namba moja Afrika
Mtu tajiri barani Afrika Aliko Dangote amesema kuwa bado anataka kuinunua kilabu ya Arsenal licha ya kushindwa kufanya hivyo mwaka 2010 alipotaka kununua hisa za kilabu hiyo.
Bilionea huyo kutoka Nigeria ni tajiri mara nane ya alivyokuwa wakati alipojaribu kununua hisa za klabu hiyo na kwamba shabiki huyo wa Arsenal bado hajatupilia mbali ndoto yake ya kutaka kuinunua kilabu hiyo ya Landon Kazkazini.
''Bado nina matumaini kwamba siku moja nitainunua timu hiyo',' alisema Dangote mwenye umri wa miaka 58.''Naweza kuinunua bei ambayo wamiliki wake itakua vigumu kukataa'', huku akiongezea kuwa ''najua mpango wangu''.

La kushangaza ni kwamba Dangote ametaja hadharani kwamba Arsene Wenger anafaa kubadilisha mbinu yake akisema kuwa timu hiyo inahitaji mwelekeo mpya.
Dangote ambaye ana thamani ya dola bilioni 15 ni tajiri zaidi ya Stan Kroenke ambaye anamiliki hisa nyingi katika kilabu hiyo na Bilionea raia wa Uzbek Alisher Usmanov ambao wamekuwa wakipigania udhibiti wa kilabu hiyo katika miaka ya hivi karibuni.
 
Sehemu ya nje ya uwanja wa Emirates unaomilikiwa na Arsenal

Monday, March 30, 2015

WANYAMA KUTUA ARSENAL


Wanyama akimtoka Kisly wa Swasea katika mchezo wa Ligi kuu Uingereza

Kocha wa Arsenal Arsene Wenger anapanga kumnunua kiungo wa kati wa Southampton Mkenya Victor Wanyama na mshambuliaji wa Anderlecht Aleksandr Mitrovic kulingana na gazeti la the Sun nchini Uingereza.
Wenger amejiandaa kutoa kitita cha pauni millioni 30 kwa wachezaji hao wawili,huku Wanyama akigharimu kitita cha pauni millioni 20 naye mshambuliaji huyo wa Anderlecht Mitrovic akigharimu pauni millioni 10.
Inaaminika kuwa Wanyama ataondoka katika kilabu ya Southampton iwapo atachukuliwa na kilabu kikubwa huku naye Mitrovic akiwa amekuwa akifuatiliwa na waajiri wa Arsenal katika kipindi cha wiki chache zilizopotea.
Mitrovic amekuwa akifananishwa na Didier Drogba kutokana na mchezo wake.


Victor Wanyama

WASAMBAZA PICHA ZA NGONO KUCHEZEA NYUNDO SABA JELA

 Leo, Serikali itawasilisha bungeni muswada wa Sheria ya Makosa ya Mtandao wa mwaka 2015 kwa hati ya dharura unaoorodhesha adhabu mbalimbali, ikiwamo ya faini ya Sh50 milioni au kifungo kisichopungua miaka saba kwa mtu atakayebainika kusambaza picha za ngono mtandaoni.


Baadhi ya makosa yaliyoanishwa katika sheria hiyo  ni kutuma taarifa bila ridhaa ya mtu, kusambaza picha za ngono na za utupu, udanganyifu unaohusiana na kompyuta, makosa yanayohusiana na utambuzi, kughushi kunakohusiana na masuala ya kompyuta na kusambaza picha za utupu za watoto.
Mengine ni unyanyasaji kwa kutumia mtandao, kuchapisha taarifa yoyote ambayo itasababisha mauaji ya kimbari, uongo na matusi ya kibaguzi.
Sheria hiyo katika Kifungu cha 48 inaipa Mahakama mamlaka ya kutaifisha mali iliyopatikana kutokana na kosa lililofanywa na mhusika. Sheria hiyo pia itawataka wote watakaobainika kufanya makosa hayo kuwasilisha hati zao za kusafiria kwa mamlaka husika hadi hapo watakapolipa faini au watakapokuwa wamemaliza kutumikia vifungo.


Muswada huo ambao ukipitishwa utakuwa sheria, unawasilishwa bungeni katika kipindi ambacho kina matukio mengi ya watu kusambaza picha za ngono na utupu mitandaoni, kuingilia mawasiliano ya kompyuta ya watu wengine bila ridhaa yao.
Pia, kifungu hicho kinaeleza kuwa mtu atakayebainika kusambaza picha za ngono, uasherati na matusi, atatozwa faini isiyopungua Sh30 milioni au kwenda jela miaka 10, mtu atakayesambaza picha za utupu atalipa faini isiyopungua Sh20 milioni au kwenda jela miaka saba.
Inawabana pia watoa taarifa za uongo. Katika Kifungu cha 16, inasema mtu atakayetoa taarifa, takwimu au maelezo kwa njia ya picha au maandishi au aina nyingine yoyote zikiwa ni za uongo, akipatikana na hatia atalipa faini isiyopungua Sh3 milioni au kifungo kisichopungua miezi sita.
Kuhusu mauaji ya kimbari, inakataza mtu kuchapisha au kusababisha kuchapisha vitu vinavyochochea au kuhalalisha matendo yanayosababisha mauaji ya kimbari na adhabu yake ni faini ya Sh10 milioni au miaka mitatu jela .

Wednesday, February 11, 2015

MSIMAMO LIGI KUU YA UINGEREZA

# team pts P W D L GF GA +/-
1 Chelsea Chelsea 56 24 17 5 2 54 21 33
2 Manchester City Manchester City 49 24 14 7 3 47 24 23
3 Southampton Southampton 45 24 14 3 7 38 17 21
4 Arsenal Arsenal 45 25 13 6 6 47 28 19
5 Manchester United Manchester United 44 24 12 8 4 40 23 17
6 Tottenham Tottenham 43 25 13 4 8 39 34 5
7 Liverpool Liverpool 42 25 12 6 7 36 29 7
8 West Ham West Ham 37 24 10 7 7 36 28 8
9 Swansea Swansea 34 24 9 7 8 28 31 -3
10 Stoke Stoke 33 24 9 6 9 27 29 -2
11 Newcastle Newcastle 31 24 8 7 9 30 36 -6
12 Everton Everton 27 24 6 9 9 31 34 -3
13 Crystal Palace Crystal Palace 26 24 6 8 10 26 34 -8
14 Sunderland Sunderland 24 25 4 12 9 22 36 -14
15 Hull Hull 23 25 5 8 12 23 34 -11
16 West Bromwich West Bromwich 23 24 5 8 11 22 34 -12
17 QPR QPR 22 25 6 4 15 26 43 -17
18 Aston Villa Aston Villa 22 25 5 7 13 12 34 -22
19 Burnley Burnley 21 24 4 9 11 23 40 -17
20 Leicester Leicester 17 25 4 5 16 22 40 -18  






























































SONG LA LEO -AKADUMBA ya NEY WA MITEGO


Wednesday, December 31, 2014

BYE BYE 2014..WELCOME 2015

Bye Bye 2014 Welcome 2015

Oh my Dear, Forget your Fear! Oh my Dear, Forget your Fear! Let all your Dreams be Clear! Never put Tear, Please Hear! I want to tell one thing in your Ear! Wishing you a very Happy New Year. Welcome 2015!!!

Welcome January Tumblr
May The Stars Shine Upon Your Life, May Gorgeous Flowers Blossom Your Life, May The New Year Rock Your Life, And May God Bless And Protect You, All Through The Year. Bye Bye 2014 Most Welcome 2015!!

Goodbye December Welcome January
In everything there must be a season, a time to come and a time to go, I pray that this New Year 2015 brings to you happiness and joy forever and ever.. Bye Bye 2014 and welcome 2015