Thursday, June 11, 2015

SONG LA LEO-CHEGE, Mwananyamala


MTOTO WA PELE ATUA SWANSEA

  
NDREW AYEW
 
Mshambuliaji wa Ghana Andre Ayew amejiunga na kilabu ya Swansea kwa uhamisho wa bure na kuandikisha mtakataba wa miaka minne na kilabu hiyo.
Ayew mwenye umri wa miaka 25,amekuwa katika kilabu ya Marseille tangu mwaka 2006 lakini mkataba wake na kilabu hiyo ya Ligue 1 ulikamilika mwezi uliopita.
Mchezaji huyo aliyetajwa kuwa mchezaji bora na BBC mwaka huu alifunga mabao 52 katika mechi 181 katika kilabu hiyo na amelichezea taifa lake mara 62.
''Nilihisi kwamba huu ndio wakati mwafaka kwangu'',alisema Ayew. Nilihisi hamu ya kucheza katika ligi ya Uingereza na kutaka kukuwa kama mchezaji na kwamba Swansea ndio suluhu kwangu kwa njia yoyote''.
"Uaminifu na hamu ya klabu hiyo ulinifanya kujihisi kwamba ni kweli wananitaka.Wameonyesha hilo kwa kila njia''.

Wednesday, June 10, 2015

RATIBA COPA AMERICA...KIMENUKAA KAZI KWENU WAZEE WA MIKEKAA


 

Copa America 2015: Schedule
Date Time (local) Home vs. Away Stage
June 11 8:30 p.m. Chile vs. Ecuador Group Match
June 12 8:30 p.m. Mexico vs. Bolivia Group Match
June 13 4 p.m. Uruguay vs. Jamaica Group Match
June 13 6:30 p.m. Argentina vs. Paraguay Group Match
June 14 4 p.m. Colombia vs. Venezuela Group Match
June 14 6:30 p.m. Brazil vs. Peru Group Match
June 15 6 p.m. Ecuador vs. Bolivia Group Match
June 15 8:30 p.m. Chile vs. Mexico Group Match
June 16 6 p.m. Paraguay vs. Jamaica Group Match
June 16 8:30 p.m. Argentina vs. Uruguay Group Match
June 17 8:30 p.m. Brazil vs. Colombia Group Match
June 18 8:30 p.m. Peru vs. Venezuela Group Match
June 19 6 p.m. Mexico vs. Ecuador Group Match
June 19 8:30 p.m. Chile vs. Bolivia Group Match
June 20 4 p.m. Uruguay vs. Paraguay Group Match
June 20 6:30 p.m. Argentina vs. Jamaica Group Match
June 21 4 p.m. Colombia vs. Peru Group Match
June 21 6:30 p.m. Brazil vs. Venezuela Group Match
June 24 8:30 p.m. TBD vs. TBD Quarter-Final
June 25 8:30 p.m. TBD vs. TBD Quarter-Final
June 26 8:30 p.m. TBD vs. TBD Quarter-Final
June 27 6:30 p.m. TBD vs. TBD Quarter-Final
June 29 8:30 p.m. TBD vs. TBD Semi-Final
June 30 8:30 p.m. TBD vs. TBD Semi-Final
July 3 8:30 p.m. TBD vs. TBD 3rd Place
July 4 7 p.m. TBD vs. TBD Final

Friday, May 15, 2015

WALIOTAKA KUMPINDUA NKURUNZUNZA WAKWAMA

Mnamo 13 mwezi May jenerali mmoja wa jeshi alitangaza katika redio ya taifa kwamba rais wa Burundi amepinduliwa na kwamba serikali ya mpito itabuniwa.Lakini msemaji wa rais alikana habari hizo akidai kuwa kulikuwa na usaidizi mdogo katika jeshi kwa mapinduzi kutendeka.Rais Nkurunziza alidaiwa kurudi nchini Burundi kutoka Tanzania ,lakini imethibitishwa kuwa leo, alishindwa kufanya hivyo na kwamba yungali nchini Tanzania.

 Kiongozi wa kundi la kiraia linalopinga hatua ya rais Nkurunziza kuwania muhula wa tatu amewataka raia nchini humo kuendelea na maandamano kulingana na shirika la habari la AFP.
Vital Nshimiriman amesema kuwa licha ya kundi hilo kupinga jaribio hilo la mapinduzi,vile raia walivyowashangilia wanajeshi wa jaribio hilo kulionyesha kwamba kuna hamu kubwa ya mabadiliko.

 Nukuu muhimu kutoka kwa Gervais Abayeho,msemaji wa rais Pierre Nkurunziza akizungumza na kipindi cha BBC cha Newsday.''Mapinduzi hushirikisha watu wengi Kuna wanajeshi wa nyadhfa za chini ambao wamesalimu amri na ambao wanawasaidia maafisa wa poisi na uchunguzi wao,lakini ninaamini watu waliopanga mapinduzi hayo ,wale viongozi hilo ni swala jingine ni lazima washtakiwe.hakuna mgawanyiko katika jeshi.Iwapo unaweza kuwaangalia wale waliokuwa wakipanga kutekeleza mapinduzi ni wachache ...kundi dogo la jeshi'',alisema..

Majenerali wawili waliotekeleza jaribio la mapinduzi nchini Burundi dhidi ya rais Pierre Nkurunziza wamekamatwa.
Hatahivyo kiongozi wa mapinduzi hayo jenerali Godefroid Niyombare ametoroka na anasakwa kulingana na msemaji wa rais.
Awali Jenerali Niyombare alikiambia chombo cha habari cha AFP kwamba yeye na wafuasi wake watajisalimisha akiongezea kuwa ''natumai hawatatuua''.
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amesema kuwa amerudi nchini Burund na kwamba anatarajiwa kulihutubia taifa.

Thursday, May 14, 2015

WAZIRI AUWAWA KWA KUSINZIA MKUTANONI MBELE YA RAIS


Taarifa hiyo iliyotolewa bungeni imesema Hyon Yong-Chol alipigwa na kombora la kuangusha ndege mbele ya mamia ya maafisa wakuu serikalini 


Idara ya ujasusi ya Korea Kusini imesema kuwa waziri wa ulinzi wa Korea Kaskazini ameuawa kwa kutokuwa muaminifu kwa kiongozi wa nchi hiyo, Kim Jong-un.
Taarifa hiyo iliyotolewa bungeni imesema Hyon Yong-Chol alikutana na mauti yake baada ya kupigwa kwa kombora la kuangusha ndege mbele ya mamia ya maafisa wakuu serikalini mwishoni mwa mwezi Aprili.
Bwana Hyon anasemekana kuwa alisinzia katika hafla iliyokuwa ikihutubiwa na rais Kim jambo lililomuudhi sana kiongozi huyo wa kiimla.
Hata hivyo ukweli wa ripoti hiyo haujabainika kutokana na usiri wa serikali ya Korea Kaskazini.
 
Waziri Hyon Yong Cho enzi za uhai wake

Bwana Hyon alipandishwa cheo na kuwa Generali mwaka wa 2010 na kuuawa kwake kunatia shaka udhabiti wa uongozi wa rai Kim Jong -un.
Hyon alipandishwa cheo na kutangazwa kuwa waziri wa usalama wa taifa mwaka uliopita.
Mwandishi wa BBC aliyeko huko Seoul anasema mauaji hayo ya kikatili mbele ya umma ikiwa yatathibitishwa, yanaonyesha athari za uasi dhidi ya Kim Jong-un.
Mapema idara hiyo ya ujasusi ilisema viongozi wakuu katika serikali ya Korea Kaskazini wamekuwa wakiuawa kila mmoja kwa wiki.
 
Waziri Hyong Chol akikamatwa na kutolewa mkutanoni baada ya kudakwa akisinzia kwenye mkutano huo

Mara ya mwisho kwa kiongozi huyo wa korea kaskazini kuamrisha kuuawa kwa kiongozi mkuu serikalini ilikuwa ni mwaka wa 2013 alipoamrisha ami wake
Chang Song-thaek - kukamatwa na kutiwa kitanzi.
Chang alikamatwa katika mkutano wa hadhara na kupelekwa katika eneo la hadhara alikouawa mbele ya umma.

BURUNDI "KIMENUKA"



Makundi hasimu ya askari yanakabiliana katikati mwa mji mkuu wa Burundi- Bunjumbura, mahala ambapo tangazo lilitolewa jana Jumatano kuwa Rais Pierre Nkurunziza, amepinduliwa.
Makabiliano ya risasi yanaendelea kwa sasa, huku milipuko kadhaa ikisikika.
Radio na runinga ya taifa inang'ang'aniwa kwa sasa huku wanajeshi waaminifu kwa rais Nkurunziza ndio wanaoidhibiti.