Wednesday, June 24, 2015

TAZAMA GOMA JIPYA LA CHAMELEONE-BWERERE


LIVERPOOL YANASA SAINI YA MBRAZIL FIRMINO


Firmino akiwa katika uzi wa Brazil


Firmino akiwa na uzi wa Hoffenheim

Klabu ya Liverpool imefanikiwa kumnasa Mbrazil Firmino aliekuwa akikipiga nchini Ujerumani na klabu ya Hoffenheim na kumsainisha mkataba wa ''Nyundo'' tano unaogharimu paundi za Uingereza Milioni 29 kuitumikia Liverpool.
Mkataba huo utakamilika sambamba na ukaguzi wa matibabu baada ya Firmino kurudi toka Chile ambako anaitumikia timu yake ya taifa ya Brazil katika michuano ya Copa Amerika.

Firmino akiwa ametikisa nyavu mara 47 katika mechi 151 alizokipiga na klabu ya Hoffenheim katika ligi ya Bundesliga nchini Ujerumani anakuwa mchezaji wa pili ghali katika klabu ya Liverpool baada ya Andy Caroll kunyakuliwa kwa kitita cha paundi za Uingereza milioni 35 mwaka 2011 akitokea Newcastle United.

Thursday, June 11, 2015

SONG LA LEO-CHEGE, Mwananyamala


MTOTO WA PELE ATUA SWANSEA

  
NDREW AYEW
 
Mshambuliaji wa Ghana Andre Ayew amejiunga na kilabu ya Swansea kwa uhamisho wa bure na kuandikisha mtakataba wa miaka minne na kilabu hiyo.
Ayew mwenye umri wa miaka 25,amekuwa katika kilabu ya Marseille tangu mwaka 2006 lakini mkataba wake na kilabu hiyo ya Ligue 1 ulikamilika mwezi uliopita.
Mchezaji huyo aliyetajwa kuwa mchezaji bora na BBC mwaka huu alifunga mabao 52 katika mechi 181 katika kilabu hiyo na amelichezea taifa lake mara 62.
''Nilihisi kwamba huu ndio wakati mwafaka kwangu'',alisema Ayew. Nilihisi hamu ya kucheza katika ligi ya Uingereza na kutaka kukuwa kama mchezaji na kwamba Swansea ndio suluhu kwangu kwa njia yoyote''.
"Uaminifu na hamu ya klabu hiyo ulinifanya kujihisi kwamba ni kweli wananitaka.Wameonyesha hilo kwa kila njia''.