Monday, October 5, 2015

ARSENAL YAIKOMESHA MANCHESTER UNITED 3 KWA NUNGE

Arsenal imeichabanga Man United kwa kamba 3 kwa ubuyu katika mechi kali ndani ya Dimba la Emirates na kuacha kocha wa Arsenal, Arsene Wenger akiwa mwenye furaha teleeee.
Alexis Sanchez akishangilia goli la kwanza

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger ameeleza furaha yake baada ya klabu hiyo kupata ushindi wa 3-0 dhidi ya mahasimu wao wa jadi Manchester United katika Ligi Kuu ya Uingereza Jumapili.
Wenger amesema alifurahishwa sana na uchezaji wa timu yake na kueleza kuwa walishangaza Manchester United kuanzia mwanzo wa mechi.
“Kuanzia kwa Petr Cech hadi kwa Theo Walcott wote walicheza vyema. Nimenoa timu nyingi kali lakini hakuna hata moja iliyoweza kucheza mechi 60 katika kiwango sawa. Lazima ukubali kwamba sisi ni binadamu,” alisema.
“Tuko kwenye kinyang’anyiro (cha kushindania taji), tuko alama mbili nyuma ya viongozi Manchester City na natumai matokeo ya leo yatatupa imani ya kuendelea kupigania taji.”
Arsenal walipata ushindi kupitia mabao mawili ya nyota wa Chile Alexis Sanchez na Mjerumani Mesut Ozil, mabao yote yakifungwa kipindi cha kwanza kwenye mechi hiyo iliyochezewa uwanja wa Emirates.
 
 
Mweeee hatuamini kabisaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 Imoooooooooooo.........Sanchez akiwatengeneza Man Utd, De Gea hoiii

Kwa meneja wa Manchester United Louis Vvan Gaal, ilikuwa vigumu kukubali matokeo hayo.
„Tulianza vibaya sana, bila kuonyesha ari ya kushambulia na kutaka kushinda. Ilikuwa mara ya kwanza kwangu kushuhudia hilo katika timu yangu. Sikulitarajia hili,” amesema.
„Unapoipatia timu kama Arsenal mianya tele uwanjani ya kusakata gozi, basi unajua kwamba lazima utashindwa.”
Arsenal na Manchester United sasa zinatoshana alama ingawa Arsenal wako mbele wakishikilia nambari mbili kwenye jedwali kwa wingi wa mabao.
Timu hizo zitarudi mawindoni wiki mbili zijazo mnamo Oktoba 17, baada ya mapumziko ya wiki mbili ya mechi za kimataifa, ambako United watakutaka na Everton uwanjani Goodison Park nao Arsenal wawe ugenini Watford.



Wednesday, September 30, 2015

BARCELONA, BAYERN ZATAMBA HUKU ARSENAL,CHELSEA ZIKIANGUKIA PUA



Timu za soka ambazo ni Tishio barani ulaya Barcelona, na Bayern Munich zimeshinda katika michezo yao ya pili ya klabu bingwa ulaya.
Barcelona, waliwachapa Bayern 04 Leverkusen, kwa mabao 2-1 mabao ya Barcelona yakitupiwa kambani na Luis Suárez na Sergi Roberto, huku la Bayern likitupiwa na Kyriakos Papadopoulos.
 
Suarez akishangilia baada ya kutupia kambani goli la kwanza

Bayern munich ya Ujerumani iliifanyia ukatili timu ya Dinamo Zagreb kwa kuitatika kamba 5-0 mshambuliaji Robert Lewandowski, akizifumania nyavu mara tatu na nabao mengine yakitupiwa kambani na Douglas Costa, na Mario Gotze.
 
Muuaji wa magoli matatu Lewandowski akishangilia na wachezaji wenzake

Chelsea, wakicheza ugenini huko nchini Ureno, walipokea kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa FC Porto ya Ureno mabao yakitupiwa  kambani na Brás André na Maicon, huku lile la kufutia machozi la Chelsea, likifugwa na Mbrazil Willian.
 
Mshikemshike dimbani hatumwi mtoto gengeni mpaka kieleweke
 
 Maicon akishangilia baada ya kuitengeneza Chelsea


Bwana mdogo tulia usilete shida alaaa

""Oyaaaaah mnanitia aibuuuu"" Kocha wa Chelsea Jose Mourinho akiwahimiza vijana kufanya kweli

Washika bunduki wa London ,Arsenal wakiwa katika uwanja wao wa Emirates walitolewa nishai kwa kutandikwa mabao 3-2 na Olympiakos,
 
Wachezaji wa Olympiacos wakishangilia baada ya kuiteketeza Arsenal
 
Wachezaji wa Arsenal wakiwa hawaamini kinachotokea katika Dimba la Emirates

Matokeoa mengine ya michezo ya klabu bingwa ulaya
 BATE Bor 3 – 2 Roma
Maccabi Tel Aviv 0 - 2 Dynamo Kiev
Lyon 0 – 1 Valencia
Zenit St P 2 – 1 KAA Gent

Wednesday, September 9, 2015

Ngoma kali ya leo- Ya Moto Band=Cheza kimadoido


10 Health Benefits of Honey (Faida 10 za Asali)

Health Benefits:
1. Prevent cancer and heart disease:
Honey contains flavonoids, antioxidants which help reduce the risk of some cancers and heart disease.
2. Reduce ulcers and other gastrointestinal disorders.
Recent research shows that honey treatment may help disorders such as ulcers and bacterial gastroenteritis. This may be related to the 3rd benefit…
3. Anti-bacterial, anti-fungal, anti-fungal:
“All honey is antibacterial, because the bees add an enzyme that makes hydrogen peroxide,” said Peter Molan, director of the Honey Research Unit at the University of Waikato in New Zealand.
4. Increase athletic performance.
Ancient Olympic athletes would eat honey and dried figs to enhance their performance. This has now been verified with modern studies, showing that it is superior in maintaining glycogen levels and improving recovery time than other sweeteners.
5. Reduce cough and throat irritation:
Honey helps with coughs, particularly buckwheat honey. In a study of 110 children, a single dose of buckwheat honey was just as effective as a single dose of dextromethorphan in relieving nocturnal cough and allowing proper sleep.

6. Balance the 5 elements:
Honey has been used in ayurvedic medicine in India for at least 4000 years and is considered to affect all three of the body’s primitive material imbalances positively. It is also said to be useful useful in improving eyesight, weight loss, curing impotence and premature ejaculation, urinary tract disorders, bronchial asthma, diarrhea, and nausea.
Honey is referred as “Yogavahi” since it has a quality of penetrating the deepest tissues of the body. When honey is used with other herbal preparations, it enhances the medicinal qualities of those preparations and also helps them to reach the deeper tissues.
7. Blood sugar regulation:
Even though honey contains simple sugars, it is NOT the same as white sugar or artificial sweeteners. Its exact combination of fructose and glucose actually helps the body regulate blood sugar levels. Some honeys have a low hypoglycemic index, so they don’t jolt your blood sugar. (Watch this video Sweetener Comparison where I compare stevia, brown rice syrup, honey, molasses and agave, and discuss the strengths and weaknesses of each.)
8. Heal wounds and burns:
External application of honey has been shown to be as effective as conventional treatment with silver sulfadiazene. It is speculated that the drying effect of the simple sugars and honey’s anti-bacterial nature combine to create this effect.
9. Probiotic:
Some varieties of honey possess large amounts of friendly bacteria. This includes up to 6 species of lactobacilli and 4 species of bifidobacteria. This may explain many of the “mysterious therapeutic properties of honey.”
10. Beautiful skin:
Its anti-bacterial qualities are particularly useful for the skin, and, when used with the other ingredients, can also be moisturizing and nourishing! For a powerful home beauty treatment for which you probably have all the ingredients in your kitchen already,

Monday, July 6, 2015

CHILE BINGWA COPA AMERICA

Chile yanyakua kombe la Copa America baada ya kuichabanga Argentina kwenye mikwaju ya penati baada ya kushindwa kufungana ndani ya dakika 120. Chile ilipata penati 4 na Argentina moja tuuuu.

Wachezaji wa Chile wakishangilia ubingwa wa Copa America
null
Alexis Sanchez "SANchenga" akishangilia baada ya kutupia penati ya mwisho na ya ubingwa.

null
null
Hivi ndivyo hali ilivyokuwa kwa wachezaji wa Argentina wakati Sanchez akipiga penati wa mwisho
null
Ushindi mtaaaaaamu hawa ni mashabiki wa Chile

null
Woyooooooooooooooooooooo    Vidal akishangilia ushindi

null
Wachezaji wa Argentina wakiongozwa na Messi kuvaa medali za ushindi wa pili huku wakilitazama kombe kwa "ugwadu"

 
Cheki mtanange huo hapa

Thursday, June 25, 2015

STARS MPYA YA MKWASA "MAFADHA WAPIGWA CHINI"

Kocha mkuu wa timu ya Taifa 'Taifa Stars' Charles Boniface Mkwasa (kushoto) akifafanua jambo leo wakati akitaja kikosi kipya tangu ateuliwe jana (kulia) kocha msaidizi Hemed Morocco
Kocha mkuu wa timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ Charles Boniface Mkwasa (kushoto) akifafanua jambo leo wakati akitaja kikosi kipya tangu ateuliwe jana (kulia) kocha msaidizi Hemed Morocco


Kocha wa timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ Charles Boniface Mkwasa Jana ametangaza kikosi kipya cha timu hiyo ambacho kitaingia kambini hivi karibuni kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa marudiano wa kufuzu kucheza fainali za michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani (CHAN) utakaopigwa kwenye uwanja wa Namboole, Kampala Uganda.
Mbali na kutangaza kikosi cha wachezaji 26, Mkwasa ametaja vipaombele vyake kwenye timu hiyo ambavyo amezingatia katika kuteua majina hayo. Amesema kitu pekee ambacho wameangalia ni uwezo wa mchezaji na nidhamu ndani na nje ya uwanja ili kuweza kujenga timu imara ambayo itakuwa na uwezo wa kupambana kwa kuwawakilisha watanzania.
Ametaja pia benchi la ufundi ambalo atashirikiana nalo katika kuhakikisha wanatekeleza majukumu ya kuinoa Stars mpya, waliotajwa kwenye benchi la ufundi ni pamoja na kocha msaidizi Hemed Morocco, kocha wa makipa Peter Manyika, madaktari wa timu watakuwa wawili watatangazwa baada ya kuwasiliana na idara ya tiba, mtunza vifaa Hussein Sued ‘Gaga’ Mshauri wa timu Abdallah Kibadeni ‘King Kibadeni Mputa’, mratibu wa timu Alhaj Ahmed Idd Mgoyi na meneja wa timu ni Juma Mgunda.
Mkwasa pia ameomba ushirikiano kutoka kwenye vilabu vyote vya Tanzania na pindi watakapoliona benchi la ufundi la Stars kwenye vilabu vyao watoe ushirikiano kwani watakuwa wakitembelea vilabuni ili kufuatilia kwa karibu maendeleo ya wachezaji ili kuendelea kukiimarisha kikosi chao.
Ameishukuru kamati ya utendaji ya TFF kwa kumuamini na kumpa majukumu ya kuifundisha timu ya Taifa huku akikiri kuwa kazi hiyo siyo nyepesi kwasababu timu imeshapoteza mchezo wake wa nyumbani kwa idadi kubwa ya magoli lakini akakiri kuwa kwenye mpira chochote kinaweza kikatokea. Mbali na kuishukuru TFF, ameushukuru pia uongozi wa klabu yake ya Yanga kwa kumruhusu kwenda kuifundisha timu ya Taifa.
Lakini Mkwasa ameonya kuwa, wachezaji ambao wameitwa kwenye kikosi cha Taifa wanatakiwa kuendelea kufanya vizuri kwenye kikosi cha Stars na vilabu vyao. Mchezaji yeyote ambaye hatopata nafasi ya kucheza kwenye klabu yake hatoitwa kwenye kikosi cha Taifa hata kama anacheza nje ya nchi kama mchezaji nwa kulipwa.
Kikosi kipya cha Stars ni;
Mudathir Khamis (KMKM), Mwadini Ali (Azam FC) na Ally Mustafa ‘Barthez’ (Yanga). Mabeki ni Shomary Kapombe (Azam), Michael Aidan (Ruvu Shooting), Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ (Simba SC), Mwinyi Hajji Mngwali (KMKM), Nadir Haroub ‘Cannavaro’ (Yanga SC), Kevin Yondan (Yanga SC), Hassan Isihaka (Simba SC), Aggrey Morris (Azam FC).
Viungo ni Jonas Mkude (Simba SC), Abdi Banda (Simba SC), Salum Telelea (Yanga SC), Frank Domayo (Azam FC), Simon Msuva (Yanga SC), Said Ndemla (Simba SC), John Bocco (Azam FC), Ramadhani Singano ‘Messi’ Simba SC na Deus Kaseke (Mbeya City). Washambuliaji ni Atupele Green (Kagera Sugar), Rashid Mandawa (Kagera Sugar), Ame Ali (Mtibwa Sugar), wakati wengine ambao wamewekwa akiba ni Juma Abdul wa Yanga SC, Mudathir Yahya wa Azam FC na Samuel Kamuntu wa JKT Ruvu.  Leo benchi la Ufundi la Stars litakutana na wachezaji wote walioteuliwa katika hoteli ya Tansoma, eneo la Gerezani, Dar es Salaam ili kuzungumza nao juu ya uzalendo na Mkwasa amesema Jumamosi timu itaenda kuweka kambi nje ya mji.
Mwisho, amewaomba wapenzi na mashabiki wa Stars wasahau yote yaliyopita kwasababu timu ipo mikononi mwao nao wanaamini watafanya vizuri. Amewaomba watanzania kuiunga mkono timu yao kama ilivyokuwa zamani na kuacha vitendo vya kuwadhihaki wachezaji ikiwa ni pamoja na kuwapiga mawe