Monday, September 12, 2011

SIMBA YASHIKWA SHATI NA AZAM WAKATI IKIKWEA KILELENI

SIMBA wameshindwa kulipiza kisasi kwa Azam baada ya kulazimisha suluhu iliyowapeleka kileleni mwa Ligi Kuu, huku Shirikisho la Soka TFF ikizipeleka Yanga na Simba kucheza mechi zao kwenye Uwanja wa Azam Chamazi.

Matokeo hayo yanaifanya Simba kufikisha pointi kumi kileleni moja zaidi kwa JKT Ruvu huku Azam ikifikisha pointi tano katika michezo minne na Yanga wakiwa mkiani na pointi zao tatu.

Simba waliokuwa na deni la kulipiza kisasi cha mabao 3-0 na kuchezewa samba msimu uliopita na Azam kwenye Uwanja Taifa walizidiwa ujanja na matajiri hao wa Chamazi waliotawala sehemu kubwa ya mchezo huo, lakini walikosa umakini kwenye umaliziaji.

Azam walitengeneza nafasi nyingi za kufunga langoni kwa Simba na kuwafanya mashabiki wengi wa wekundu hao wa Msimbazi waliofurika uwanjani hapo kimya muda mrefu.

Viungo wa Simba, Gervais Kago na Haruna Moshi waliingia kwenye eneo la hatari la Azam dakika ya tisa kwa kugongea pasi, lakini kipa Mwadini Ally alikuwa makini kuokoa hatari hiyo.

Simba iliendeleza mashambulizi yake dakika 20, beki Juma Nyoso aliunganisha vizuri kona ya Ulimboka Mwakingwe, lakini uhodari wa kipa Mwadini ndiyo ulioinusuru Azam.

Krosi ya Mwakingwe ilitua mguuni mwa Kago aliyepiga shuti kali lililopaa juu ya goli na kuwaacha mashabiki waliofurika uwanjani hapo wakishika vichwa.

Tofauti na mechi ya Yanga na Ruvu Shooting iliyoingiza mashabiki 6,566, mchezo wa jana watazamaji walikuwa wengi kutokana na ushindani uliopo baina ya Simba na Azam.

Kiungo Jabir Aziz wa Azam alijaribu kumtungua kipa Juma Kaseja aliyekuwa ameacha goli kwa shuti la umbali wa mita 25 hata hivyo lilipaa juu kidogo ya lango la Simba.

Mshambuliaji John Boko alipoteza nafasi tatu ikiwemo ile ya dakika 45, alipopokea pasi ya Kipre Tchetche akiwa yeye na Kaseja, lakini akapiga nje.

Azam walitawala sehemu kubwa ya kipindi cha kwanza katika kiungo wakiongozwa na Ibrahim Mwaipopo, huku Mrisho Ngassa na Tchetche walikuwa wakianzisha mashambulizi yao kutoka winga na kuifanya Simba kubaki nyuma muda mwingi.

Dakika 72, Mwaipopo nusura afunge goli baada ya mpira wake wa adhabu kugonga mwamba upande wa kulia na kurudi uwanjani.

Mwamuzi Isihaka Shirikisho alitoa kadi za njano kwa Haruna, Shija Mkina kwa Simba kwa upande wa Azam ni Ngasa, Mwaipopo na Morris.

Kocha wa Simba Moses Basena aliwashanga wengi pale alipoamua kumtoa Mkina aliyekuwa ameingia uwanjani baada ya Amri Kiemba kwa dakika kumi na nafasi yake kuchuliwa na Uhuru Selemani.

Naye Steward Hall alimpumzisha Kipre na kumwingiza Wahaba Yahya, pia Simba ilimtoa Kago na kuingia Shomari Kapombe.

SIMBA YANGA KUTUMIA UWANJA WA CHAMAZIHatimaye klabu za Yanga na Simba zimepata nafasi ya kuutumia uwanja wa Azam, Chamazi wenye uwezo wa kuchukua mashabiki 2000 kwa ajili ya mechi zao za Ligi Kuu kuanzia wiki hii.

Taarifa ya Simba na Yanga kutumia uwanja wa Chamazi ilitolewa jana na Shirikisho la Soka nchini TFF ikiwa ni kutii maagizo ya Serikali ya kutaka Uwanja wa Taifa utumike kwa michezo miwili tu kwa wiki.

Uongozi wa Azam ambao awali ulikataa kuziruhusu klabu hizo kongwe nchini kutumia uwanja wake kutokana na kuhofia uhalibifu wa mali zake wamefanya mazungumzo na Simba na Yanga na kukubaliana.

Mechi zitakazochezwa Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Dar es Salaam; mechi namba 35- Simba vs Polisi Dodoma (Septemba 14), mechi namba 29- African Lyon v Yanga (Septemba 15), mechi namba 45- Yanga vs Villa Squad (Septemba 21), mechi namba 66- Simba vs Ruvu Shooting (Oktoba 19) na mechi namba 71- Yanga vs Oljoro JKT (Oktoba 23).

Huku Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ukitumika kwa mechi namba 39- Azam vs Yanga (Septemba 18), mechi namba 50- Simba vs Mtibwa Sugar (Septemba 25), mechi namba 52- Yanga vs Coastal Union (Septemba 28) na mechi namba 58- Yanga vs Kagera Sugar (Oktoba 13).

Nyingine ni mechi namba 62- Simba vs African Lyon (Oktoba 16), mechi namba 65- Yanga vs Toto Africans (Oktoba 20), mechi namba 72- Simba vs JKT Ruvu (Oktoba 22), mechi namba 78- Yanga vs Simba (Oktoba 29) na mechi namba 86- Moro United vs Simba (Novemba 2).
Vikosi
Azam: Mwadini Ally, Erasto Nyoni, Waziri Omari, Said Morad, aggrey Morris, Ibrahimu Mwaipopo, Mrisho Ngasa, Jabir Aziz, John Boko, Kipre Tchetche na Ramadhan Chombo.Simba: Juma Kaseja, Nassoro Said, Amir Maftah, Juma Nyoso,Victor Costa, Partick Mafisango, Amri Kiemba(Shija Mkina/ Uhuru Seleman), Jerry Santo, Gervais Kago, Haruna Moshi, Ulimboka Mwakingwe.

KIUMBE MPYA KUBAINI ASILI YETU AGUNDULIWA A.KUSINI

Mabaki ya kale ya viumbe wawili waliopatikana huko Afrika ya kusini wanaofanana na binadamu yanaweza kubadili mtazamo wetu kuhusu asili yetu.
australopithecus sediba
Babu australopithecus sediba

Mabaki hayo yanayokadiriwa kuwa yamepatikana baada ya miaka milioni 1.9 yalielezewa kwa mara ya kwanza mnamo mwaka 2010, na kupewa jina la kitaalamu Australopithecus sediba.
Tangu hapo kundi la wataalamu lililofanya ugunduzi wakati ule limerudi na uchambuzi wa kina zaidi.
Kundi hilo limelifahamisha jarida linalochapisha habari za Sayansi kua maumbile yaliyoshuhudiwa ya ubongo, miguu, mikono na mifupa ya nyongo yote yameonyesha kama viumbe hawa ni wa kwanza katika asili yetu -binadamu - ama kwa jina la kitaalamu - Homo sapiens.
Profesa Lee Berger wa Chuo kikuu cha Witwatersrand mjini Johannesburg anasema kuwa "wamechunguza sehemu muhimu za binadamu zinazoelezea umbo linalombainisha binadamu na viumbe wengine, na kuna uwezekano wa sehemu za binadamu kukuwa kwa nyakati tofauti na A.sediba anaonyesha kutimiza vigezo vya maumbile ya mwanadamu, kiongozi wa kundi la wataalamu aliifahamisha BBC.
Ni madai makubwa, na ikiwa yana ukweli, basi kuna uwezekano wa rekodi zilizokuepo kuhusu asili yetu kuwekwa kando.
Nadharia inashikilia msimamo kuwa binadamu wa sasa anaweza kudai urithi wake kutoka kwa kiumbe anayejulikana kama Homo erectus aliyeishi zaidi ya miaka milioni moja iliyopita.
homo erectus
kiumbe aliyekwenda kwa miguu miwili

Mnyama huyu, kwa mujibu wa wataalamu wa anthropolojia, huenda naye alikua na asili ya aina ya kiumbe ambaye hakustaarabika ajulikanaye kama hominin, mfano ni Homo habilis au Homo rudolfensis.
Jambo la kuridhisha kuhusu madai juu ya A. sediba ni kwamba ingawa ni wa kale kuliko wenzake , baadhi ya maumbile yake na uwezo wake yanaonyesha kuwa alikuwa na uwezo zaidi kuliko wenzake wa baadaye.
Kwa kifupi inaaminika A.sediba yuko karibu zaidi na babu wa mwanadamu Homo erectus.
babu wa miguu miwili
homo erectus

Mabaki ya sediba yalifukuliwa huko Malapa katika eneo maarufu la asili ya mwanadamu , nje kidogo na kaskazini magharibi mwa Johanesburg.
Viumbe hawa waliotambuliwa kama mwanamke my mzima na mvulana kijana, wametambuliwa kuwa mama na mwana. Kilichobainika ni kuwa walifariki kwa pamoja kufuatia ajali iliyowasababisha kudondoka ndani ya mfumo huo wa shimo kuu au walikwama humo ndani.
Baada ya kufariki, miili yao ilisukumwa ndani ya shimo lenye tope na kuganda humo kwa mda mrefu kama mabaki ya wanyama wengine yaliyokwama humo.

AJALI YA MELI ZANZIBAR YAUA MAMIA YA WATU

Watu wasiopungua 197 wamekufa baada ya meli iliyokuwa imezidisha mizigo kuzama katika pwani ya kisiwa cha Zanzibar ikiwa na watu takriban 800.
Msemaji wa serikali amesema watu 620 walionusurika wameokolewa. Serikali imetangaza siku tatu za maombolezo.
Inadhaniwa kuwa meli hiyo ilizama baada ya injini yake kukosa nguvu.
Shughuli za uokoaji zilikwazwa kwa kuwa meli hiyo ilizama usiku.
Zanzibar
Meli iliyozama

Zaidi ya watu 100 bado hawajulikani walipo, lakini watu 325 walionusurika wameokolewa, kwa mujibu wa waziri wa masuala ya dharura wa Zanzibar.
Meli hiyo, MV Spice Islander ilikuwa ikisafiri kati ya Kisiwa kikuu cha Unguja kuelekea Pemba.
Meli hiyo ilikuwa ikirejesha watu baada ya kumalizika kwa mfungo wa Ramadhani.

Msaada

Serikali ya Zanzibar imeunda kituo cha uokoaji na kutoa wito kwa taasisi zote kusaidia katika shughuli za uokozi. Serikali hiyo pia imeomba msaada kutoka nchi nyingine za nje, kama vile Kenya na Afrika Kusini.
Walionusurika walichukuliwa na boti za kibinafsi na kupelekwa katika bandari ya Zanzibar, amekaririwa kamishna wa polisi wa Zanzibar Mussa Hamis.
ZNZ
Watu walionusurika wakipelekwa hospitali

Miili ya watu imekuwa ikisukumwa katika pwani ya Zanzibar na mawimbi. Mpaka sasa miili ya watu 100 wamepatikana, amesema mwandishi wa BBC Ali Saleh akiwa Zanzibar.
Maelfu ya ndugu na jamaa wanasubiri kusikia taarifa za ndugu zao ambao walikuwa ndani ya meli hiyo, anasema mwandishi wetu.
Mohhamed Aboud, waziri wa masuala ya dharura wa Zanzibar anasema watu 259 walionusurika wameokolewa lakini 40 kati yao wamejeruhiwa sana.
"Boti yetu imechelewa kwa sababu wanatumia vyombo vyote vya baharini kuokoa watu"Anasema Catherine Purvis

Catherine Purvis, mtalii kutoka Uingereza aliyepo Zanzibar, akisubiri boti ya kwenda Dar es Salaam amesema ameshuhudia miili ya watu wengi ikitolewa ndani ya maji.
"Nimesimama katika bandari ya Zanzibar nikiwa na watalii wengine kama 10 wa Marekani na Uingereza.
"Boti yetu imechelewa kwa sababu wanatumia vyombo vyote vya baharini kuokoa watu".
Rubani mmoja wa helikopta Kapteni Neels van Eijk alipita juu ya eneo la tukio.
"Tuliona walionusurika wakiwa wameshikilia magodoro na majokofu au chochote kile kinachoweza kuelea. Ni vigumu kusema idadi kamili, lakini naweza kusema walikuwepo zaidi ya watu 200 walionusurika ndani ya maji na miili ya watu pia," ameiambia BBC.
znz
Shughuli za uokoaji pwani ya Zanzibar

"Wakati huo, kulikuwa na boti chache zilizofika katika eneo hilo. Walikuwa wakitafuta walionusurika, ingawa bahari haikuwa imechafuka sana, mawimbi walikuwa makubwa, kwa hiyo ilikuwa vugumu kuona walionusurika.
"Tulirusha ndege yetu na kuziongoza boti hadi kwa watu walionusurika ili waweze kuwachukua. Kulikuwa na miili kadhaa ndaniya maji."
Meli hiyo iliondoka Unguja takriban saa tatu usiku saa za Afrika Mashariki na inadhaniwa kuwa ilizama majira ya saa saba usiku.
Ilikuwa imebeba abiria wengi kiasi kwamba baadhi ya abiria waligoma kupanda, amekaririwa abiria mmoja aliyenusurika Abdullah daid, akizungumza na shirika la habari la AP.

Thursday, September 8, 2011

7 Things to Expect from Kenny Dalglish's Team Next Season

7: Pass and Move

Two football legends, Xavi and Scholes 

The best team in the world, Barcelona, is the best because of its quality of players and its style of play.  Xavi, Iniesta, and Messi are the kings of the pass and move style of play.  Johann Cruyff had a tremendous effect on Barcelona's style, and Guardiola has taken over the reigns.
Dalglish knows that to win consistently you need to control games; counter-attacking can only go so far.  If your team only gets a few chances at goal, then you need to have the best players in the world to capitalize on those chances.  This is why Manchester United and Real Madrid would have beaten any team in the world, except Barcelona.  United and Madrid players are incredible, but Barcelona dominates games because opponents have so few chances to score that they cannot win.
Dalglish understands how to play pass and move football very well, and he will ensure that Liverpool play that way this season.

6: Spreading the Field and Relying on Wingers

Downing is essential for Liverpool's success 
Dalglish got his man in the form of Stewart Downing.  Downing will allow Liverpool to spread the field, which is one thing that Liverpool has lacked for quite awhile.  Downing could be the most important signing for Liverpool this summer, no matter who else joins.  His ability opens up the option for Carroll to score many goals (and after the last friendly maybe Agger too)!
Downing's success is closely tied to Liverpool's success.  Liverpool signed him because he is hitting his prime, he works incredibly hard, and has a lot of experience in the Premier League.  Dalglish will rely on Downing to widen the pitch, which will open up space in the middle for Suarez and Carroll to cause trouble.



5: Liverpool Will Score a Many Goals

Carroll will score plenty for Liverpool

Dalglish signed Carroll in January because he is the type of striker that only comes around once a generation.  His aerial ability and powerful shot make a lethal combination.  The 'Giant Geordie' has nearly endless potential, and with Downing, Henderson, Johnson, Suarez, and Adam providing him opportunities he will score plenty of goals this season.
That is not even including the goal-scoring ability of Luis Suarez, who set the Copa America alight this summer. If Suarez returns to Liverpool playing at that level then the Carroll and Suarez strike partnership will be unstoppable.


4: Dalglish Will Rotate His Squad Often

KUALA LUMPUR, MALAYSIA - JULY 16: Liverpool lines up during the pre-match ceremony during the pre-season friendly match between Malaysia and Liverpool at the Bukit Jalil National Stadium on July 16, 2011 in Kuala Lumpur, Malaysia. (Photo by Stanley Chou/G
Although Liverpool will not play in Europe this season, the club will still play in three competitions throughout the season.  This means that Dalglish must rotate the squad constantly to make sure every player is 100% for the game he is playing.  This is one thing that Liverpool coaches have not done very well recently, but this needs to happen for Liverpool to succeed.
Dalglish knows the ability of the academy and reserve players better than anyone, so he will know when they are ready to play for the first team.  In addition, his summer signings provide a lot of depth (especially at midfield).  He will need to rotate these players to keep them happy and hungry for wins.


3: Luis Suarez Will Be in Contention for Premier League Player of the Season

LIVERPOOL, ENGLAND - MAY 01:  Luis Suarez of Liverpool in action during the Barclays Premier League match between Liverpool  and Newcastle United at Anfield on May 1, 2011 in Liverpool, England.  (Photo by Clive Brunskill/Getty Images) 
Liverpool will miss Suarez for the first few days of the campaign, but when he gets back he will be unstoppable.  He proved last season and during the Copa America that he is quickly becoming one of the best strikers in the world.  Liverpool will miss his passing and vision, as well as his incredible work rate.
Many compared Suarez to Dalglish, and if Suarez stays healthy he should be in the running for Premier League Player of the Season.  He will score plenty of goals, but the number of goals he will create for other players is where he really shines.


2: Liverpool Will Beat Mid-Table Teams

Competition for places will ensure hungry players
Liverpool has struggled recently to get wins against weaker teams.  It is hard to say whether this comes from a lack of passion when playing against weaker opponents, or whether the squad is so confident in a victory that they relax.  I'm sure it is a combination of both.  Alex Ferguson recognized this years ago, and the result is that he rarely plays with the same squad from week to week.  Dalglish is an excellent coach as well, and he will ensure these losses will not happen.
Dalglish has signed top players who will want to prove themselves, as will the established players from last season.  The competition for places among the veterans and the youngsters coming up from the reserves will ensure that the squad will be hungry for a win each week.

1: Liverpool Will Finish in the Top Four

Henry and Werner want more European Cups
When FSG bought Liverpool last year, Henry and Werner stated their desire to win titles.  They have proven their desire by supplying Dalglish with funds to sign top players.  Everyone at the club has one goal, which is to get back into the Champions League.
Dalglish will ensure that this happens.  He has already brought in the perfect players for Liverpool, and he will ensure that the players focus on the game in front of them.  Through just focusing on one game at a time, the squad will not overlook any games and will win enough matches to finish in the top four.

SIMBA DOZI NZITO YANGA HOI BIN TAABAN

MABINGWA watetezi Yanga wameendelea kung'ang'ania mkiani mwa Ligi Kuu huku mahasimu wao Simba wakipata ushindi wa tatu mfululizo kwenye ligi hiyo katika mechi zilizofanyika jana kwenye viwanja vya Jamhuri, Morogoro na Mkwakwani, Tanga.

Yanga walishuka kwenye Uwanja wa Jamhuri wakiwa na matumaini ya kupata pointi tatu, lakini walijikuta wakilazimishwa suluhu na Mtibwa Sugar, wakati Gervas Kago alifunga bao lake la kwanza tangu aanze kuichezea Simba na kuiwezesha timu hiyo kuilaza Villa Squad bao 1-0, huku Polisi Dodoma wakitoka suluhu na Ruvu Shooting.

Kwa matokeo hayo Simba imefikisha pointi tisa na kupanda hadi nafasi ya pili nyuma ya kinara wa ligi JKT Ruvu kwa tofauti ya mabao.Mabingwa wa Kombe la Kagame Yanga waliokusanya pointi mbili katika michezo mitatu ya ligi waliyocheza mpaka sasa walilazimika kubaki ndani ya uwanja wa Jamhuri kwa dakika tano na kuondolewa na ulinzi mkali wa polisi FFU baada ya mashabiki wao wenye hasira kuanza kurushia mawe basi lililobeba wachezaji hao.

Kocha Sam Timbe akizungumzia pambano hilo alisema vijana wake walishindwa kutumia nafasi walizopata kwenye mchezo huo.

Mkenya Tom Olaba aliyeiwezesha Mtibwa Sugar kufikisha pointi nane mpaka sasa aliwapongeza wachezaji wake kwa kucheza vizuri na kutawala sehemu ya kiungo, lakini walipoteza nafasi chake walizopata.Mtibwa ilianza mchezo huo kwa kasi na katika dakika ya 17, kipa Yaw Berko alifanya kazi ya ziada kuokoa shuti la Said Mkopi.

Yanga ikicheza bila ya nahodha wake,  Shadrack Nsajigwa ilionekana kupwaya katika kiungo na kuruhusu mashambulizi mengi golini kwake shukrani kwa juhudi binafsi za kipa Berko.

Mshambuliaji Thomas Mourice wa Mtibwa Sugar alipoteza nafasi ya kufunga katika dakika ya 40 kwa kushindwa kuunganisha vema krosi ya upande wa kushoto iliyopigwa na Said Bahanunzi.

Washambuliaji wa Yanga, Davis Mwape na  Jerryson Tegete walikosa mabao katika dakika ya 29 na 42 waliposhindwa kutumia nafasi zilizotengenezwa na winga Julius Mrope.

Mshambuliaji wa Ghana, Kenneth Asamoah alishindwa kumalizia mpira wa kona uliopigwa na Rashid Gumbo na kutemwa na kipa Munishi katika dakika ya 70.

Tanga; Mabingwa wa Ngao ya Jamii, Simba wamedhamiria kurudia rekodi yao ya msimu wa 2009/10 waliotwaa ubingwa bila ya kupoteza mchezo wowote baada ya kuichapa Villa Squad bao 1-0.

Mshambuliaji wa kimataifa wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Kago alifunga bao lake la kwanza Ligi Kuu ya Tanzania katika dakika ya 7 akipokea krosi ya Haruna Moshi na kuipa Simba ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Villa Squad.

Katika mchezo huo beki Victor Costa alifanya kazi ya ziada kuokoa bao lililotaka kufungwa na Mohamed Kijuso katika dakika za mwisho kwa mpira wa kichwa uliompotea kipa Juma Kaseja.

Pia winga wa Simba, Ulimboka Mwakingwe alipewa kadi ya njano kwa kujiangusha kwenye eneo la penalti, huku Amri Ramadhan wa Villa Squad akipewa kadi ya njano kwa kuushika mpira kwa makusudi.

VIKOSI

Yanga: Yaw Berko, Godfrey Taita, Oscar Joshua, Bakari Mbegu, Chacha Marwa, Nurdin Bakari, Julius Mrope, Rashid Gumbo, Jerryson Tegete (Kenneth Asamoah), Davis Mwape, Kigi Makassi (Idrissa Rashid).
Mtibwa Sugar: Deogartius Munishi, Juma  Abdul, Issa Rashid, Salvatory Ntebe, Salum Sued, Shabaan Nditi, Said Mkopi, Masoud Ali, Said Bahanunzi, Thomas Mourice na Ali Mohamed.
Simba: Juma Kaseja, Nasoro Chollo, Amir Maftah, Juma Nyoso, Victor Costa, Jerry Santo, Shija Mkina, Amri Kiemba, Gervas Kago, Haruna Moshi na Ulimboka Mwakingwe.
Villa Squad: Abbas Nassoro, Haruna Shamte, Yassin Majota, Shai Mpala, Menard Mbugunza, Zuberi Dadi, Lameck Mbonde, Mussa Nampaka, Mohamed Kijuso, Mohamed Binslum na Nsa Job.

SITA WASHIKILIWA KWA MAUAJI YA SHABIKI WEMBLEY

Shabiki wa soka wa Wales aliyekufa kabla ya pambano dhidi ya England katika uwanja wa Wembley, ametajwa na mashabiki wenzake kuwa ni Mike Dye, na watu sita wanashikiliwa na polisi kutokana na kifo chake.
Polisi uwanja wa Wembley wakichunguza mauaji
Polisi uwanja wa Wembley wakichunguza mauaji


Dye mwenye umri wa miaka 44 alipelekwa hospitali akiwa na majeraha kichwani baada ya kupatwa na maradhi ya moyo nje ya uwanja.
Salamu za rambirambi kwa shabiki huyo wa soka wa klabu ya Cardiff City, aliyefariki dunia usiku wa saa tatu zilitolewa kupitia mtandao wa soka.
Watu hao sita waliokamatwa inaaminika ni mashabiki wa Wales na polisi hawaamini kama kuna shabiki yeyote wa England alihusika na kifo hicho.
Katika taarifa kupitia mtandao wake klabu ya Cardiff City imesema: "Usiku wa Jumanne taarifa zilitufikia kuhusiana na msiba huu ambapo shabiki wa Wales na Cardiff City amekufa katika mechi baina ya England na Wales.
Msemaji wa polisi amesema: "Maafisa wa polisi na wa Huduma za gari la Wagonjwa walimhudumia shabiki huyo. Mtu huyo anayeaminika kuwa na umri miaka 40 alipelekwa hospitalini kaskazini mwa London akiwa na majeraha kichwani. Alitangazwa amekufa saa mbili na dakika hamsini.
England katika mechi hiyo ya kuwania kufuzu katika Ubingwa wa Ulaya, ilishinda kwa bao 1-0.

NIGER YAKANA KUMPA HIFADHI GADAFFI

Serikali ya Niger imesema kuwa itaamua jinsi ya kumshughulikia Kanali Muamar Gaddafi iwapo ataingia nchini humo kuomba hifadhi ya kisiasa.
Kanali Gadaffi
Kanali Gadaffi

Ripoti kutoka eneo hilo zinasema kuwa maafisa wa vyeo vya juu katika Serikali iliyotimuliwa wamewasili nchini Niger na kuna habari kuwa huenda Kanali Gaddafi akajiunga nao.
Baraza la Kitaifa la Mpito la Libya limetoa wito kwa Serikali ya Niger isimpe hifadhi Kanali Gaddafi.
Mwandishi wa Habari wa BBC nchini Libya anasema kuwa ombi hilo limeweka Niger katika hali ya kutatanisha kwa sababu tayari imetambua serikali ya mpito lakini haiwezi kumfukuza Kanali Gaddafi kwa sababu ya uhusiano wa karibu waliokuwa nao viongozi hao wa Niger.
Kiongozi wa Baraza la mpito nchini Libya
Kiongozi wa Baraza la mpito nchini Libya

Wakati huo huo Kanali Gadafi amepuuza madai kwamba ametorokea nchi jirani ya Niger na kuyataja madai hayo kama uongo na vita vya kiakili.
Matamshi ya Gadaffi yamepeperushwa na kituo kimoja cha televisheni nchini Syria, kilichodai kuwa Gadaffi baado yuko nchini Libya.
Gadafi ameapa kuwashinda wapiganaji wa upinzani wanaoungwa mkono na majeshi ya muungano wa NATO.
Huu ndio ujumbe wake wa kwanza katika kipindi kirefu.
Ripoti zinasema katika muda wa siku 10 zilizopita, maafisa wakuu wa uliokuwa utawala wa gadaffi wamekuwa wakiwasili nchini Niger na kuibua fununu kuwa Kanali Gadaffi huenda akajaribu kujumuika nao.
Baraza la kitaifa la mpito nchini Libya limetoa wito kwa Niger kutompa hifadhi. Serikali ya Niger imesema kwamba itaamua jinsi itakavyomshughulikia Kanali muammar gadaffi ikiwa ataingia nchini humo na kuomba hifadhi.